“Tuchukulie Kama Wanadamu”

Ubaguzi dhidi ya Wafanyabiashara wa Ngono, Walio wachache Kijinsia na Wanaotumia Dawa za Kulevya nchini Tanzania

“Tuchukulie Kama Wanadamu”

Ubaguzi dhidi ya Wafanyabiashara wa Ngono, Walio wachache Kijinsia na Wanaotumia Dawa za Kulevya nchini Tanzania

Faharasa
Istilahi Zinazohusiana na Mwelekeo wa kingono na Utambulisho wa Kijinsia
Istilahi Zingine Zimetumiwa Katika Ripoti Hii
Ramani ya Tanzania
Muhtasari
Dhuluma Kutoka kwa Polisi
Ukiukaji Katika Sekta ya Afya
Makundi Yaliyoko Katika Hatari Zaidi (MARPs)/ Makundi Maalum
Wahalifu katika Muktadha wa Sheria
Watoto
Mafanikio Madogo
Mkabala Jumlifu wa Haki Kuhusu VVU/ UKIMWI
Mapendekezo Muhimu
Kwa Rais Kikwete
Kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Kwa Mabunge ya Tanzania na Zanzibar
Kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Jamhuri ya Tanzania, Wizara ya Afya ya Zanzibar, na Asasi Zote za Serikali Zinazohusika na Masuala ya VVU/UKIMWI
Kwa Polisi ya Tanzania na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma
Kwa Serikali na Asasi Zinazofadhili Programu za VVU/UKIMWI ama Haki za Binadamu nchini Tanzania
Mbinu
I. Historia
VVU Tanzania: Kiwango cha Juu cha Maambukizi Miongoni mwa Makundi Maalum
Mazingira ya Sheria na Sera
Upatikanaji wa Taarifa
Ujamaa na Utengwaji
II. Muktadha wa Jamii na Sheria kwa Dhuluma Dhidi ya Wana LGBTI , Wafanyabiashara wa Ngono, na Watumiaji wa Dawa za Kulevya
Watu Wenye Jinsia Tofauti na Asili na Watu Wenye Jinsia Mbili (“Huntha”)
KISA CHA SAIDI W
Kazi ya Ngono na Unyonyaji Katika Biashara ya Ngono
Biashara ya Unyonyaji ya Kingono kwa Watoto
KISA  CHA ROSEMARY I.
Watumiaji wa Dawa za Kulevya
KISA CHA JANUARY H.
III. Dhuluma, Vitisho na Unyang’aji wa Polisi
Mateso na Maonevu
Ushambulizi  na Unyanyasaji  wa Kingono kutoka kwa Polisi
Ubakaji na Hujuma kwa Watoto kutoka kwa Polisi
Unyang’anyi wa Pesa
Kukamatwa Kiholela
IV. Polisi Jamii, Sungu Sungu na Makundi  Mengine ya Wanamgambo
Sungu Sungu
Polisi Jamii
V. Ukosefu wa Haki kwa Waathiriwa wa Uhalifu  katika Makundi Yaliotengwa
VI.Ubaguzi katika Sekta ya Afya
Kunyimwa Huduma za Afya
Matusi, Unyanyasaji, na Ukiukaji wa Usiri
Mahitaji ya Kuwasilisha Fomu ya Polisi Nambari 3 (PF3) kabla ya Matibabu
Mahitaji ya “Mlete Mpenzi Wako”
Ukosefu wa Vilainisho
VII. Sheria ya Tanzania, ya Ukanda, na ya Kimataifa
Ngono ya Hiari Baina ya Wapenzi wa Jinsia Moja
Kazi ya Ngono
Unyonyaji wa Kingono
Utumiaji  Binafsi wa Dawa za Kulevya
Haki ya Kutoteswa
Haki ya Kupata Huduma Ya Kiwango cha Juu cha Afya
Haki ya Usalama na Uadilifu wa Kimwili
Ufisadi
VIII. Jibu kutoka kwa Serikali ya Tanzania
IX. Mapendekezo Kamili
Kwa Rais Kikwete na Serikali ya Tanzania
Kwa Mabunge ya Tanzania na Zanzibar
Kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Jamhuri ya Tanzania, Wizara ya Afya ya Zanzibar, na Asasi Zote za Serikali Zinazohusika na Masuala ya VVU/UKIMWI
Kwa Wizara ya Katiba na Sheria ya Jamhuri ya Tanzania na Tume ya Mabadiliko ya Katiba
Kwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ya Jamhuri ya Tanzania na Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto ya Zanzibar
Kwa Polisi ya Tanzania na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma.
Kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG)
Kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa (TAKUKURU)
Kwa Tume za Kuratibu Udhabiti wa Dawa za Kulevya za Tanzania na Zanzibar
Kwa Asasi za Umoja wa Mataifa Zinazofanya Kazi Nchini Tanzania, ikiwa ni pamoja na UNAIDS, UNDP, UNFPA, UNICEF, na UN Women
Kwa Serikali na Asasi Fadhili Zinazosaidia Mipango ya VVU/UKIMWI au Haki za Binadamu nchini Tanzania
X. Shukrani

Faharasa

Istilahi Zinazohusiana na Mwelekeo wa kingono na Utambulisho wa Kijinsia

Biashara ya unyonyaji wa kingono: Kazi ya ngono kwa watoto imeharamishwa vikali chini ya sheria za kimataifa na ni namna moja ya unyonyaji wa kingono. Watoto wanaojihusisha katika biashara ya ngono, hata hivyo, hawafai kuchukuliwa kama wahalifu, lakini wana haki ya kupata ulinzi kutoka kwa serikali dhidi ya unyonyaji kama huo na kupewa usaidizi mwafaka.

Dhuluma za kijinsia: Dhuluma inayoolekezwa kwa mtu fulani kwa mujibu wa jinsia au uana wake. Dhuluma za kijinsia hujumuisha: dhuluma za ngono, dhuluma za familia, dhuluma za kisaikolojia, tamaduni za kudhuru, na mazoea ya kubagua kwa misingi ya uana.

“Gay”: Istilahi ya kingereza inatumiwa kwa kutambulisha mtu  kimsingi mvuto wake wa kingono na kimapenzi ni kwa watu wa jinsia yake. Istilahi hii inatumiwa muda kwa muda katika lugha ya Kiswahili kama istilahi yasiyo ya kudharau kwa niaba ya “msenge” au “shoga.”  Inatumiwa mara nyingi katika lugha ya Kiswahili] kutambulisha wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume.

Jinsia: Kanuni za jamii na desturi (kinyume cha uana wa kibayolojia) zinazotumiwa kutofautisha kile ambacho jamii inachukulia kuwa mienendo ya “kiume” na “kike.”

LGBTI: lesbian, gay, bisexual, transgender and intersex katika kiingereza. Maana yake ni: Wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake, wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, wanovutiwa kimapenzi na jinsia zote mbili, watu wenye jinsia tofauti na asili, na walio na jinsia zote mbili, kiume na kike (“huntha”); istilahi jumuishi inayorejelea makundi ambayo wakati mwingine hurejelewa kama “walio wachache kijinsia.”

Mfanyabiashara wa Ngono: Istilahi hii imetumika hapa kurejelea mtu mzima, mke ama mume, ambaye hutoa huduma za ngono kwa ajili ya kupewa pesa.

Msagaji: Mwelekeo wa kingono wa mwanamke ambaye kimsingi mvuto wake wa kingono na kimapenzi ni kwa wanawake wengine. Istilahi hii imetumiwa muda kwa muda kwa ajili ya kudharau.

Msenge: Istilahi kwa mwanaume anayefanya ngono na wanaume. Istilahi hii imetumiwa sana kwa ajili ya kudharau

“MSM” (Man Who Has Sex With Men) ama Mwanaume anayefanya Mapenzi na Wanaume: Mwanaume anayefanya mapenzi na watu wa jinsia moja, lakini ambaye huenda akajitambua au akakosa kujitambua kama “shoga” ama “gay.” “MSM” inaweza kutumiwa kwa jumla ya umoja au jumla ya wingi. Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume waweza pia kuwa au kutokuwa na mahusiano ya kingono na wanawake.

Mwelekeo wa kingono: Jinsi hamu za mtu za ngono na mapenzi zilivyoelekea. Istilahi hii inaeleza ikiwa mtu anavutiwa kimsingi kwa watu wa jinsia moja, jinsia tofauti, au zote kwa pamoja. Kiswahili, lugha ya taifa ya Tanzania, ina istilahi kadhaa zinazodharau za kurejelea watu ambao mwenendo wao wa kingono si wa mapenzi ya jinsia tofauti. Istilahi hizo zinajumuisha shoga, na msenge (ambazo hutumika kurejelea wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao) na msagaji (inayorejelea wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake). Istilahi hizi hutumiwa wakati mwingine na wana LGBTI wenyewe kwa namna isiyoudhi kujirejelea au kuwarejelea wanachama wa makundi yao. “Mtu mwenye uhusiano wa jinsia moja” ni namna isiyoudhi ya kumrejelea mtu aliye na mahusiano ya kingono na jinsia yake. 

Mtu Mwenye Jinsia Tofauti na Asili: Utambulisho wa mtu ambaye jinsia yake ya kuzaliwa (ambayo alipewa alipozaliwa) hauwiani na jinsia anayoishi au jinsia anayoidhania (jinsia ambayo anaridhia zaidi kujitambulisha kwayo au angependa kujitambulisha angepewa fursa hiyo). Mtu anayetamani kubadili jinsia yake kwa kawaida huchukua au angependa kuchukua utambulisho wa kijinsia unaowiana na jinsia anayoipendelea, lakini angetamani au hapana  kubadilisha mwili yake maalum  ili ulingane na jinsia anayetamani kuchukua.

Mtu Mwenye Jinsia Zote Mbili (“Huntha”): Mtu aliyezaliwa na viungo vya uzazi ambavyo havionekani kuwiana kikamilifu na uanishaji wa “uke” au “uume”; kwa  mfano, anaweza kuwa na viungo vya uzazi vinavyowiana na jinsia zote mbili.

Shoga: Istilahi kwa mwanaume anayefanya ngono na wanaume.  Istilahi hii imetumiwa sana  kwa ajili  ya kudharau.

Ushoga: Mwelekeo wa kingono wa mtu ambaye kimsingi mvuto wake wa kingono na kimapenzi ni kwa watu wa jinsia moja.

Utambulisho wa Kijinsia: Hisia za ndani za mtu zinazomfanya kujitambulisha kama mwanamke au mwanamume, jinsia zote mbili, au hali yoyote nyingine kando na uke au uume. Utambulisho wa kijinsia si lazima uwiane na uana wa kibayolojia aliozaliwa nao mtu.

Walio Wachache Kijinsia: Istilahi jumuishi ambayo inajumuisha watu wote walio na utambulisho wa kingono na kijinsia usiofuata kaida zilizopo, kama vile LGBTI, wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (na ambao huenda wasijitambulishe kama LGBTI) na wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake.

 “WSW” (Woman Who Has Sex with Women”) ama Mwanamke Anayefanya: Ni wanawake ambao huenda wasijitambulishe kama “wasagaji”; wengine waweza kuwa na mahusiano ya kingono na wanaume pia. “WSW” inaweza kutumiwa kwa jumla ya umoja au jumla ya wingi.

Istilahi Zingine Zimetumiwa Katika Ripoti Hii

Fomu Nambari 3 ya Polisi (PF3): Fomu ambayo lazima polisi waijaze kabla ya hospitali nyingi za Tanzania kukubali kuwatibu waathiriwa wa mashambulizi.

Makundi Maalum (Key Populations) / Makundi Maalum Yaliyo Katika Hatari Kubwa ya Kuambukizwa VVU: Watu walio na uwezekano mkubwa wa kuambukizwa Virusi Vya UKIMWI (VVU) au kuvisambaza. Katika miktadha mingi, wale walio katika hatari kubwa zaidi ya VVU hujumuisha wanaume wafanyao mapenzi na wanaume, watu wenye jinsia tofauti na asili, wanaojidunga dawa za kulevya, wafanyabiashara wa ngono na wateja wao, na wapenzi wasio na VVU ilhali mchumba mwingine anavyo VVU. Kila taifa linapaswa kuainisha makundi mahsusi yaliyo katika hatari kubwa zaidi na mikakati inayowiana na mukhtadha wa janga na jamii husika.[1]

Makundi Yaliyo Katika Hatari Kubwa Zaidi (Most At Risk Populations, MARPs): Istilahi inayotumiwa na wahudumu katika sekta ya afya ya umma kurejelea makundi ambayo yana uwezekano mkubwa wa kuambukizwa VVU au kuvieneza VVU. Ripoti hii inatumia istilahi “Makundi  Maalum” na “Makundi Yaliyo Katika Hatari Kubwa Zaidi” kama visawe. Pia inatumia istilahi “makundi yaliyotengwa” na “makundi yaliyoko katika mazingira magumu” kurejelea kwa pamoja walio wachache kijinsia, wafanyakazi wa ngono, na watumiaji wa dawa za kulevya.

Polisi Jamii: Makundi ya wananchi wa kawaida katika Tanzania bara na Zanzibar ambayo hutoa habari kwa polisi na wakati mwingine yenyewe kupiga doria.

Sungu Sungu: Awali, istilahi hii ilitumika kurejelea kundi la kujihami lililoundwa kukabiliana na wizi wa ng”ombe katika magharibi ya Tanzania katika miaka ya themanini; hivi karibuni, istilahi hii imekuja kutumiwa kurejelea kundi lolote la wanamgambo lipatikanalo katika janibu zote. (Pia ni “Sungusungu.”) 

Ramani ya Tanzania

© 2013 Human Rights Watch

Muhtasari

Mnamo Disemba mwaka wa 2010, polisi walimkamata Saidi W., mwanamume mwenye umri wa miaka kumi na minane aliyejitambuslisha kama “gay” (mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume) jijini Dar es Salaam, Tanzania. Askari mmoja alimwekea bunduki kichwani akamlazimisha kuwapigia simu rafiki zake watano, ambao pia ni wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume na kuwaambia wakutane nao katika baa moja. Walipowasili, polisi waliwakamata wote wakawavua nguo katika baa hiyo wakawachapa na wakawapeleka katika stesheni ya polisi ya Central. Kule katika stesheni, wanaume wale walibakwa mara kadhaa na wafungwa wenzao. Saidi na rafiki zake walipoomba usaidizi kutoka kwa polisi, polisi walisema, “Hili ndilo mlilotaka.” Mamake Saidi alilazimika kutoa hongo ya shilingi laki nne za Tanzania (takriban dola za Marekani 250) ili mwanawe na rafiki zake waachiliwe.

Katika mwaka wa 2012, Mwamini K., mfanyabiashara wa ngono wa kike, alibakwa huku akitishwa kupigwa risasi na mteja aliyekasirika alipomtaka atumie kondomu. Kwa kukosa imani kwa polisi na hospitali, mwanamke huyo alihofia kutafuta usaidizi: mnamo mwaka wa 2011, alipokuwa katika mitaa ya Dar es Salaam akiwatafuta wateja, maafisa watatu wa polisi walimkamata, wakamwita “mbwa” na “nguruwe”, na wakamchapa kwa takriban dakika kumi kabla ya kumwacha barabarani. Katika tukio hilo, Mwamini alienda hospitalini kwa matibabu, lakini akawaambia wafanyakazi wa hospitali kuwa alikuwa ameanguka kwenye ngazi za nyumba, akiogopa kuwa angenyimwa huduma ikiwa angesema ukweli kuhusu jinsi alivyochapwa. Alikuwa pia amewahi kuwa na matatizo na hospitali katika nyakati zilizopita: katika hospitali moja, wahudumu walikataa kumtibu alipowaambia kuwa alikuwa ameambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa sababu ya kazi yake ya ngono.

*  * *

Mnamo Disemba mwaka wa 2011, polisi wa Dar es Salaam walimkamata na kumtesa Suleiman R., ambaye hutumia heroini, katika juhudi za kumlazimisha akiri wizi ambao hakuwa ameutekeleza. Walimpiga kwa vyuma na kuuchoma mkono wake kwa pasi. Polisi walimzuia Suleiman usiku kucha na kumlazimisha mamaye alipe shilingi laki mbili za Tanzania (dola za Marekani 125) ili kumwachilia Suleiman siku iliyofuata. Alipoachiliwa, Suleiman aliwaomba polisi wale Fomu Nambari 3 ya Polisi (PF-3), ambayo hospitali za umma huhitaji kabla ya kuwatibu waliovamiwa. Polisi walikataa wakisema, ikiwa angepewa PF3, angeshtaki polisi mahakamani. Suleiman alilazimika kupata matibabu ghali katika hospitali ya binafsi.

*  * *

Saidi W., Mwamini K., na Suleiman R., wana mambo mawili yanayofanana. Kwanza, wote wamo katika kile ambacho wataalamu wa afya ya umma wanaoushughulikia maenezi ya VVU/UKIMWI wanarejelea kama “kundi la watu walio katika hatari kubwa zaidi” au “makundi maalum.” Ingawa kiwango cha maambukizo ya virusi vya Ukimwi (VVU) miongoni mwa umma kwa jumla kimepungua Tanzania, data iliyopo inadhihirisha kuwa kiwango hicho kimeongezeka miongoni mwa watu katika kundi hili maalum, wakiwemo wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wafanyabiashara wa ngono, na wanaojidunga dawa za kulevya.

Watu hawa wa aina tatu pia wana sifa nyingine ya bahati mbaya kwa kuwa sheria za Tanzania zinawatambua wote kama wahalifu. Hali inayowafanya kwenda mafichoni. Hivyo basi kuwafanya kuwa walengwa wepesi wa ukiukaji wa haki za binadamu na maafisa wanaolinda sheria; kuhalalisha unyanyapaa dhidi yao kutoka kwa wengi na kuyapa mashirika ya serikali kisingizio cha kutowazingatia au kutowashughulikia vilivyo.

Ripoti hii imetokana na utafiti uliofanywa na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rihts Watch pamoja na shirika la “Wake Up and Step Forward Network” (WASO), lililoko Dar es Salaam ambalo ni mtandao wa makundi yanayowakilisha wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, kati ya Mei 2012 na Aprili 2013. Ripoti inarekodi ukiukaji wa haki za binadamu unaowahusu wafanyabiashara wa ngono; wanaojidunga dawa za kulevya; na LGBTI (wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake, wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, wanaovutiwa kimapenzi na jinsia zote mbili, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watu wenye jinsia mbili: kiume na kike (huntha) ama “lesbian, gay, bisexual, transgender and intersex kwa lugha ya kiingereza. Pia inafichua hali ya kusikitisha ya unyanyasaji wa ngono kwa watoto wanaoshiriki biashara ya ngono. Ripoti vile vile inamulika aina mbili kuu za ukiukaji wa haki za binadamu: ukiukaji unaowahusu maafisa watekelezaji wa sheria kama walaumiwa wa kimsingi na ule wa sekta ya afya. 

Dhuluma Kutoka kwa Polisi

Utafiti huu umerekodi visa kadhaa vya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaotekelezwa na polisi, vikiwemo mateso na ubakaji, uvamizi, kuwakamata watu kiholela, na kudai hongo, pamoja na kutokubali kupokea malalamishi kutoka kwa wale walioko hatarini ambao vile vile ni waathiriwa wa uhalifu.  Katika kisa kimoja cha kutisha sana, polisi walimkamata John Elias, anayetumia heroini, katika msako wa mihadarati katika eneo la Kigamboni kule Dar es Salaam mnamo Februari 18, mwaka wa 2010. Katika kituo cha polisi, afisa wa polisi aliyadunga macho yake yote kwa sirinji iliyojaa kiowevu. Elias alipoenda hospitalini wiki moja baadaye, aligundua kuwa kiowevu kile kilikuwa ni asidi. Leo hii, Elias ana mashimo badala ya macho.

Makundi yanayodumisha amani ingawa si rasmi sana hasa Sungu Sungu yamelaumiwa kwa kuzua vurugu dhidi ya makundi yaliyo hatarini kwa kuwalazimisha kubadilisha vitendo, mara nyingi kwa kutumia nguvu. Ukiukaji wao unajumuisha uvamizi kwa Mwanahamisi K., karibu na njia ya reli kule Tandika, Dar es Salaam, mnamo Mei mwaka wa 2012, ambapo alikuwa ameenda kuvuta heroini. Aliliambia shirika la Human Rights Watch: “Sita kati yao walinilazimisha kufanya ngono nao. Hawakutumia kondomu. Ubakaji huo ulichukua saa moja au mbili. Nilikuwa na mtoto wangu. Mtoto huyo wa kiume alikuwa akilala ardhini kando nilipokuwa nikibakwa. Baada ya kunibaka, waliniambia, ‘Usizurure usiku.’”

Kusisitiza zaidi hadhi ya chini ya kutoheshimiwa kwa kundi hili la wale walio hatarini, polisi hukataa wakati mwingine kukubali malalamishi wakati wafanyakazi wa ngono, wanapojidunga dawa za kulevya au wana LGBTI ni waathiriwa wa uhalifu, ama kutoka kwa vikosi vya usalama vyenyewe au kutoka kwa wananchi wengine. Kama alivyoeleza mfanyakazi wa afya ya umma kutoka Mwanza, “Wafanyakazi wa ngono hawana nafasi ya kuzungumza dhidi ya ukiukaji wa haki dhidi yao. Hata polisi wanaweza kuwanyanyasa ikiwa wataenda kupiga ripoti. Ikiwa wataenda kwa polisi, basi polisi wanageuka kuwa wateja wao kwa usiku huo."

Ukiukaji wote huu wa haki za binadamu unaendeleza unyanyapaa na kuchangia mazingira ambapo wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, wafanyakazi wa ngono na wanaojidunga dawa za kulevya, huishia kuzidi kutengwa na kupoteza imani kwa serikali, hivyo kudhoofisha miradi ya afya ya umma inayotegemea ushirikiano na ubia baina ya serikali na watu walio katika hatari ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI.

Miongoni mwa makundi matatu maalum, utafiti wetu unakisia kuwa wale walio katika hatari kubwa zaidi ya kudhulumiwa na polisi wanatoka katika matabaka ya chini ya kijamii na kiuchumi. Katika visa vyote vilivyoangaziwa hapa, maafisa wa serikali na mawakala wao wanahudumu bila hofu ya kuadhibiwa kisheria.

Ukiukaji Katika Sekta ya Afya

Ukiukaji wa haki za binadamu katika sekta ya afya unajumuisha kunyimwa huduma, kudhulumiwa kwa maneno na kutusiwa pamoja na kukiuka faragha zao. Visa kama hivyo vinajumuisha tukio la mwaka wa 2011 katika hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam ambapo mhudumu alikataa kutumia anestezia alipokuwa akimshona mtumiaji wa dawa za kulevya baada ya kuvamiwa na kundi la watu, na kisa cha Machi, mwaka wa 2012 ambapo daktari katika hospitali ya Mnazi Mmoja huko Zanzibar alikataa kumtibu mwanamume anayefanya ngono wa wanaume kisonono akidai, “Tayari unafirwa na wanaume, sasa unakuja hapa kutuletea shida. Ondoka.”

Ripoti hiyo pia ina rekodi za mahitaji magumu kuyatimiza katika sekta ya afya ambayo, ingawa hayajakusudiwa kubagua, huweka vikwazo fulani kwa upatikanaji wa huduma za afya kwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wafanyakazi wa ngono, na wanaojidunga dawa za kulevya. Kwa mfano, Jamila H., mfanyakazi wa ngono, alibakwa na genge mnamo Februari mwaka wa 2012 na akaenda katika hospitali ya umma, lakini aliambiwa kuwa alihitajika kujaziwa fomu ya uvamizi na polisi kabla ya kupewa matibabu. “Walisema kuwa ilinibidi kwenda kwa polisi, lakini singeweza kwa sababu nilikuwa mfanyakazi wa ngono,” alisema. Wawili kati ya waliombaka hawakutumia kondomu, lakini bila huduma za hospitali, hakupimwa virusi vya UKIMWI. Halima Y., pia mfanyakazi wa ngono, alisema kuwa wafanyakazi wa afya katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam walikataa kumtibu ugonjwa wa zinaa kwa sababu hangeweza kuandamana na mwenziwe wa ngono hadi hospitalini ili kupimwa na kutibiwa.

Matibabu yanayotolewa kwa njia ya ubaguzi, yakijumuishwa na ukosefu wa maagizo dhahiri kutoka serikalini kuwa hakuna yeyote atakayekamatwa au kuteswa kwa kutafuta huduma, inasababisha watu kususia huduma za afya. Polisi au makundi yale ya kudumisha usalama wakiwadhulumu au kuwakamata kiholela wanachama wa kundi lolote lililotengwa, au wahudumu wa sekta ya afya wakiwawanyima huduma, matendo yao yanakiuka kanuni dhahiri za kimataifa kuhusu haki za binadamu, na pia hukiuka sheria za Tanzania.

Makundi Yaliyoko Katika Hatari Zaidi (MARPs)/ Makundi Maalum

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Tanzania, kama wizara nyingi za afya kote duniani, imetambua kuwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume wengine (MSM), wafanyabiashara wa ngono, na wanaojidunga dawa za kulevya ni washirika muhimu katika vita dhidi ya VVU.

Mkakati wa Pili wa Taifa Kudhibiti UKIMWI, 2008-2012(National Multi-sectoral Strategic Framework II on HIV and AIDS, 2008-2012), ulitambua kuwa unyanyapaa huzuia utafutaji wa huduma. (Mkakati wa sasa kwa kipindi cha mwaka wa 2013 hadi 2017 ulikuwa ukitayarishwa ripoti hii ilipokuwa ikiandikwa). Mkakati huu ulibainisha mikakati kadhaa inayolenga kupunguza maambukizi baina ya makundi yaliyo katika hatari kubwa zaidi, wakiwemo wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, wafanyabiashara wa ngono, na wanaojidunga dawa za kulevya. Mkakati huu unajumuisha mikakati mitatu muhimu. Kwa kunukuu mkakati ule:   

  • Kuhimiza upatikanaji rahisi wa taarifa za kinga na huduma za VVU (vipeperushi, upatikanaji wa mipira, elimu rika, upimaji rafiki, ushauri rafiki na huduma za maradhi ya ngono) kwa walio katika hatari ya kuambukizwa zaidi.)
  • Kujenga ubia kati ya serikali na asasi za kijamii pamoja na taasisi nyingine zinazofanya kazi na jamii zilizo katika hatari zaidi ili kushawishi kujengewa uwezo na kupatiwa ulinzi, vilevile kuwezesha uwekaji wa kumbukumbu na ubadilishanaji wa taarifa.)
  •  Kukubali kuwa wafanyabiashara wa ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao wako katika hatari zaidi hivyo kuhimiza wapatiwe taarifa za VVU na huduma na pia kutodharau shughuli zao.

Kwa sababu ambazo hazijulikana kwa Human Rights Watch na WASO, mkakati huu wa tatu ni tofauti katika toleo la Kiingereza ya Mkakati wa Pili wa Taifa Kudhibiti UKIMWI. Unasomwa katika Kiingereza: “Kukubali kuwa wafanyabiashara wa ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao wako katika hatari zaidi na kutetea haki zao za kupata taarifa na huduma kuhusu kinga dhidi ya UKIMWI, na kutetea kuondoa uharamishaji wa shughuli zao.”Hatua muhimu ya uharamishaji wa shughuli wa makundi maalum inakosa katika toleo la Kiswahili.

Huko Zanzibar –jimbo linalodumisha muungano wa siasa na Tanzania, lakini lina bunge lake na Rais wake – Mkakati wa Pili wa Taifa wa UKIMWI Zanzibar (2011-2016) haubainishi uhalalishaji wa biashara ya ngono au ngono ya hiari baina ya wanaume, lakini unapendekeza kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha kuwepo kwa stahamala kwa makundi maalum. Pia inahimiza kuwepo kwa hatua nyinginezo endelevu, zikiwemo ubadilishanaji wa sirinji kwa wanaojidunga dawa za kulevya, na kutolewa kwa kondomu na vilainisho vya majimaji kwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume.

Kwa bahati mbaya, sheria iliyopo, ikijumuishwa na nyendo za kudhulumu za maafisa wanaotekeleza sheria na wale wa afya, huzorotesha mikakatiyote hii, katika Tanzania bara na pia Zanzibar.

Wahalifu katika Muktadha wa Sheria

Sheria za Tanzania huharamisha tendo la ngono ya hiari baina ya wanaume wazima na adhabu ya kifungo cha kati ya miaka thelathini hadi maisha gerezeni, mojawapo ya zile adhabu kali zaidi ulimwenguni kwa kosa la mapenzi ya jinsia moja. Zanzibar ina sheria tofauti kidogo lakini imeharamisha mapenzi ya jinsia moja kati ya wanaume na kati ya wanawake. Katika maeneo yote mawili, hakujatokea mashtaka yanayolenga tendo la mapenzi ya jinsia moja katika miaka ya hivi karibuni, lakini sheria hii – na jinsi inavyotekelezwa vibaya – inawabagua wapenzi wa jinsia moja, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watu wenye jinsia mbili (kiume na kike). Hii pia huwatia katika hatari zaidi ya kukumbana na unafiki na kudaiwa hongo na polisi wanapoazimia kudumisha hadhi yao ya kisiri.

Sheria ya Tanzania pia huharamisha biashara ya ngono: adhabu ya kuzurura kwa lengo la kutekeleza ukahaba ni kifungo cha miezi mitatu gerezani katika Tanzania bara, na kufanya ngono kwa lengo la kujipa pesa ni ya miaka mitatu gerezani huko Zanzibar.

Matumizi ya kibinafsi ya aina yoyote ya dawa za kulevya au dawa zozote za kusisimua akili huadhibiwa kwa kifungo cha miaka kumi gerezani katika Tanzania bara, faini ya shilingi milioni moja za Tanzania, au zote mbili. Huko Zanzibar, kosa hili huadhibiwa kwa kifungo cha hadi miaka saba gerezani.

Watoto

Matumizi, utoaji, ununuzi, au kuwapeleka watoto wa chini ya miaka kumi na minane ili kuhudumu katika biashara ya ngono ni aina ya unyonyaji katika biashara ya ngono unaharamishwa chini ya sheria za Tanzania hali kadhalika zile za kimataifa. Watoto wanaojihusisha katika biashara ya ngono, au namna yoyote hunyanyaswa kingono hawapaswi kushtakiwa au kuadhibiwa kwa kushiriki katika biashara haramu ya ngono, lakini wanapaswa kusaidiwa vilivyo.  Wale wanaotekeleza uhalifu wa unyonyaji wa kingono wanafaa kushtakiwa. Hata hivyo, unyonyaji wa kingono wa watoto – hasa wasichana – hutokea mara nyingi Tanzania na kwa kawaida, hauadhibiwi. Isitoshe, watoto wanaoshiriki katika biashara ya ngono, ambao tulizungumza nao, mara nyingi hudhulumiwa na polisi na hawana suluhisho dhidi ya dhuluma kutoka kwa raia. Baadhi ya visa vibaya zaidi vya ukiukaji wa haki za binadamu tulivyorekodi vilihusu polisi kuwabaka watoto wanaoshiriki katika biashara ya ngono. Kwa mfano, Rosemary I., mtoto aliyeshiriki katika biashara ya ngono huko Mbeya, alituambia kuwa polisi walikuwa wamembaka “takriban mara saba”, mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka kumi na miwili tu. Kwa mujibu wa Wizara ya Maswala ya Nchi za Kigeni ya Marekani, hakuna mtu aliyeshtakiwa nchini Tanzania katika mwaka wa 2012 kwa kuwadhulumu watoto kimapenzi.

Mafanikio Madogo

Kiasi fulani cha mafanikio kimeafikiwa chini ya Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (Tanzania bara), na Mkakati wa Taifa wa  UKIMWI (Zanzibar), huku hospitali chache za serikali na mashirika yasiyo ya serikali kote nchini yakitoa huduma nzuri kwa makundi yaliyo hatarini. Serikali pia, kupitia kwa mashirika yake ya afya, iliunga mkono na miradi kadhaa ya uhamasishaji iliyotekelezwa na mashirika ya kitaifa na ya kimataifa ambayo hulenga makundi maalum. Hata hivyo, wahudumu wa afya wanaendelea kuwabagua wagonjwa kwa misingi ya hisia zao za kimapenzi, kushiriki katika biashara ya ngono, au utumiaji wa dawa ya kulevya, hivyo basi kutatiza haki yao ya kupata huduma bora za afya iwezekanavyo.

Tabia za maafisa wa serikali ya Tanzania huathiri kwa njia taratibu mfumo huu wa kimkakati, ikiwemo ahadi ya “kuhimiza upatikanaji rahisi wa taarifa za kinga na huduma za VVU,” pamoja na “upimaji rafiki,” kwa makundi yaliyo hatarini. Watu wengi waliohojiwa kwa ajili ya ripoti hii walisema kuwa ubaguzi bado ni kikwazo kikubwa kwa upimaji na matibabu.  Kuhusu upatikanaji wa taarifa, makundi yaliyobaguliwa, hasa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, mara nyingi hawalengwi katika kampeni za uhamasishaji kuhusu VVU/UKIMWI.

Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI unaahidi  “kujenga ubia kati ya serikali na asasi za kijamii pamoja na taasisi nyingine zinazofanya kazi na jamii zilizo katika hatari zaidi ili kushawishi kujengewa uwezo na kupatiwa ulinzi.” Serikali kupitia mashirika yake ya afya, imeunga mkono miradi kadhaa ya uhamasishaji iliyotekelezwa na mashirika ya umma, pamoja na mashirika mengine yasiyo ya serikali, na kuyalenga makundi maalum. Lakini wawakilishi bora zaidi wa maslahi ya makundi yaliyo hatarini ni mashirika yenye wanachama wa kutoka kwenye vikundi vile vyenyewe–na katika muktadha ambapo wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, wafanyakazi wa ngono, na watumiaji wa dawa za kulevya wanakabiliwa na tishio la kila mara la uvamizi mikononi mwa polisi na maafisa wengine wa serikali, ikiwemo kuteswa na kubakwa, ni vigumu kuzungumzia ubia kati ya makundi haya na serikali.

Wanaharakati wa kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja na wafanyakazi wa ngono walituambia kuwa hawakuwa na habari yoyote kuhusu juhudi zozote za mashirika ya afya ya serikali za kutetea uhalalishaji wa tendo la mapenzi ya jinsia moja au biashara ya ngono, tangu kuchapishwa kwa Mkakati wa Kudhibiti UKIMWI licha ya ahadi ya “kukubali kuwa wafanyibiashara wa ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao wako katika hatari zaidi hivyo kuhimiza wapewe taarifa za VVU na huduma na pia kutodharau shughuli zao” ama katika toleo la Kiingereza, “kutetea uhalalishaji kwa shughuli zao.” Mapema mwaka wa 2013, afisa wa afya serikalini aliliambia shirika la Human Rights Watch kwamba shirika lake lilikuwa limeanza kuwasiliana na polisi, kwa lengo la kuanzisha mjadala kuhusu uhalalishaji. Lakini hakuna juhudi zozote thabiti zaidi – ambazo mwishowe zingewahusisha wabunge, bali si polisi peke yao – zilikuwa zimechukuliwa.  

Mkabala Jumlifu wa Haki Kuhusu VVU/ UKIMWI

Ikiwa kweli Tanzania imejitolea kushughulikia VVU/UKIMWI miongoni mwa makundi maalum, ni lazima ifanye hivyo kwa namna jumlifu. Taasisi zinazoingiliana na umma mara kwa mara, kama vile polisi na sekta ya afya, zinapaswa kutoa ulinzi na matibabu kwa makundi yaliyo hatarini, ili ziwe mfano bora kwa Watanzania wengine, badala ya kuweka mfano wa chuki na itikadi kali.

Sheria za Tanzania na desturi zao kwa wanaume wanaofanya ngono wa wanaume, wafanyakazi wa ngono, na watumiaji wa dawa za kulevya hazitatizi tu utekelezaji kamili wa dhamira ya Tanzania ya kutokomeza VVU, lakini pia hukiuka sheria za kimataifa. Uharamishaji wa mahusiano hiari ya kimapenzi baina ya watu wazima hauambatani na haki kadhaa za binadamu zinazotambuliwa kimataifa, ikiwemo haki ya kutoingiliwa na kutobaguliwa. Uharamishaji wa kufanya ngono kwa hiari, ili kupata fedha kama vile wafanyakazi wa ngono kwa hiari miongoni mwa watu wazima, pia ni kinyume cha haki ya kutoingiliwa, ikiwemo uhuru wa mtu binafsi. Ukiukaji wa haki za binadamu pia mara nyingi huambatana na utekelezaji wa seti zote za sheria za jinai, na utekelezaji wa sheria za jinai dhidi ya matumizi na umilikaji wa dawa za kulevya kwa matumizi ya kibinafsi.

Mashirika ya Human Rights Watch na WASO yanatoa mwito kwa Tanzania kuunga mkono haki za binadamu kwa watu wote yakiwemo makundi yaliyotengwa. Kanuni ya Adhabu inahitaji kudhihirisha misingi ya usawa, badala ya kuimarisha ubaguzi katika sheria.  Matendo ya maafisa wa serikali yanahitaji kila wakati kudhihirisha ufahamu kwamba wana LGBTI (hasa wanaumewanaofanya mapenzi na wanaume), wafanyakazi wa ngono, na wanaotumia dawa za kulevya wanafaa kupewa haki zote walizopewa Watanzania wengine.

Kuna uhusiano thabiti kati ya haki za binadamu na jambo la kimsingi linalohitajika kwa dharura kuboresha afya ya jamii kupunguza maambukizi ya VVU na kuwatibu walioambukizwa. Kukomesha ubaguzi na unyanyasaji dhidi ya makundi maalum ni lazima kwa afya ya umma, na suala la heshima ya kimsingi ya binadamu.

Mapendekezo Muhimu

Kwa Rais Kikwete

  • Atoe amri kwa taasisi za serikali hadharani  wakomeshe dhuluma ya polisi, ubaguzi katika sekta ya afya, na aina zote za  ubaguzi dhidi ya  wafanyakazi wa ngono, watumiaji wa dawa za kulevya, wapenzi wa jinsia moja, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watu wenye jinsia zote mbili.

Kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania  

  • Ibuni halmashauri huru ya raia isimamie kikosi polisi na ipewe mamlaka ya kupokea malalamishi yanayohusu mwenendo mbaya katika polisi, ifanye uchunguzi na kuyapeleka malalamiko yale kwa waendesha mashtaka.

Kwa Mabunge ya Tanzania na Zanzibar

  • Yaanze michakato ya kuhalalisha ngono ya hiari kati ya watu wazima, pamoja na ngono kati ya watu wa jinsia sawa, na biashara ya ngono ya hiari. Pia yarekebishe sheria zilizopo juu ya matumizi ya kibinafsi ya dawa za kulevya na kuwa na dawa za kulevya ili kuhakiksha kwamba zinaambatana na  kanuni za  afya ya umma na haki za binadamu.

Kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Jamhuri ya Tanzania, Wizara ya Afya ya Zanzibar, na Asasi Zote za Serikali Zinazohusika na Masuala ya VVU/UKIMWI

  • Zitoe amri kwa wafanyakazi wa afya kwamba ubaguzi dhidi ya wanachama wa makundi yaliyotengwa hautakubaliwa kamwe na zitoe mafunzo na zifanye ukaguzi kuhakikisha kwamba sheria hii inatimizwa.

Kwa Polisi ya Tanzania na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma

  • Zitoe amri kwa polisi wote kwamba hakuna mwathiriwa yeyote atakayenyimwa usaidizi, ama kukamatwa, ama kuteswa kwa msingi ya mwenendo wake wa kingono au utambulisho wa kijinsia, au hali yake kama mfanyakazi wa ngono au mtumiaji wa dawa za kulevya. Zitangaze hadharani kwamba watu walio katika  hatari kubwa zaidi wanaweza kuripoti uhalifu bila hatari ya kukamatwa na zianzishe maafisa ushirikiano kwa ajili ya makundi haya.

Kwa Serikali na Asasi Zinazofadhili Programu za VVU/UKIMWI ama Haki za Binadamu nchini Tanzania

  • Ziimarishe maendeleo ya mashirika ya wafanyakazi wa ngono, wana LGBTI, na watu wanaotumia dawa za kulevya, ili wawe na mashirika yanayoheshimiwa na yanayowakilisha matakwa yao.
  • Zihakikishe kwamba ufadhili unaoelekezwa kwa VVU/UKIMWI nchini Tanzania unajumuisha fedha ambazo zimetengwa mahususi kwa matumizi katika mahitaji ya afya ya makundi maalum.

Mbinu

Ripoti hii ni ushirikiano kati ya shirika linalotetea haki za binadamu la “Human Rights Watch” na “Wake Up and Step Forward Coalition” (WASO), ambao ni muungano wa mashirika yanayowahudumia wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume jijini Dar es Salaam. Aidha, mashirika ya “Tanzania Gender Networking Program” (TGNP) na lile la “Nyerere Centre for Human Rights,” yote yanayopatikana Dar es Salaam, yalisaidia pia kutunga na kutafiti ripoti hii.

Kati ya Mei 2012, na Aprili 2013, Human Rights Watch na WASO yalifanya utafiti wa nyanjani huko Dar es Salaam, Zanzibar, Tanga, Arusha, na Mwanza. Human Rights Watch lilifanya utafiti wa ziada Mbeya na Chunya likisaidiwa na “Population Services International” (PSI), shirika lisilo la serikali la kimataifa linaloangazia afya ya uzazi na jinsia.

Watafiti wawili wa Human Rights Watch, na wawili wa WASO waliwahoji watafitiwa 254 kwa ajili ya ripoti hii, wakiwemo watu 121 walioko katika makundi maalum:

  • Wanaume 47 wanaofanya mapenzi na wanaume (14 kati yao wakiwa pia wafanyakazi wa ngono wa mara kwa mara au wanaoifanya kama kazi yao ya kudumu);
  • Watu 3 wenye jinsia tofauti na asili (wawili kutoka ya kiume hadi ya kike, na mmoja kutoka ya kike hadi ya kiume);
  • Wanawake wazima 39 ambao ni wafanyakazi wa ngono;
  • Wasichana 13 wenye umri wa chini ya miaka 18 wanaofanya kazi ya ngono;
  • Wanaojidunga dawa za kulevya 19, 5 kati yao wakiwa wanawake.

Watafiti waliwauliza watu wanaofanya kazi ya ngono umri wao ili kuamua ni wepi kati yao ni watoto. Nchini Tanzania, wengi hawana vyeti vya kuzaliwa hivyo basi kubaini umri kamili kunaweza kuwa kugumu.

Pia tulizungumza na wanachama wengine wa wakazi wanaoishi katika mazingira magumu ijapokuwa hawachukuliwi kuwa katika hatari kubwa zaidi, wakiwemo wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake tisa, mmoja wao ambaye alikuwa pia mfanyakazi wa ngono, na mmoja wao aliyejitambulisha kama mwenye jinsia mbili; watu 13 wanaotumia dawa za kulevya zisizo za kujidunga, na watu 12 watumiaji wa zamani wa dawa za kulevya.

Wahojiwa wengi walifikiwa kwa usaidizi wa mashirika yasiyo ya serikali ya kitaifa au ya kimataifa. Wakati mwingine ambapo tusingepata shirika lolote linalofanya kazi na wafanyakazi wa ngono wa kike, tuliwaendea wafanyakazi wa ngono wa kike katika baa au mitaani na kuomba kuwahoji.

Katika maeneo yaliyoko nje ya Dar es Salaam na Zanzibar, ilikuwa ni vigumu kuwatambua na kuwahoji wale walio katika makundi maalum, kwingine kwa sababu ya kukosekana kwa mashirika ya wenyeji yanayoshirikiana nao. Ziara zetu za siku mbili hadi nne katika miji ya wastani, ambapo mapenzi ya jinsia moja na masuala mengine tata ya kijamii hujadiliwa kwa nadra hadharani, hazikuturuhusu muda wa kutosha kupata uaminifu wa idadi kubwa ya wana LGBTI, wafanyakazi wa ngono, na watumiaji wa dawa za kulevya. Kutokana na upungufu huu na kiasi kikubwa cha wakati tuliotumia kufanya mahojiano jijini Dar es Salaam, ripoti hii inajumuisha mifano mingi zaidi kutoka Dar es Salaam ikilinganishwa na maeneo mengine ya nchi. Utafiti zaidi katika hali maalum zinazowakabili walioko katika makundi maalum katika maeneo mengine ya nchi utakuwa wenye manufaa kwa wadau wanaonuia kuendeleza miradi inayoshughulikia mahitaji yao.

Katika kila eneo, tulizungumza na mashirika yasiyo ya serikali ya mitaa na ya kimataifa, hasa yale yanayohusika katika masuala kama vile elimu ya VVU na juhudi za kuwafikia waathiriwa nje ya vituo, usawa wa kijinsia, na kupunguza madhara.

Tuliwahoji pia  maafisa kutoka serikalini, wakiwemo maafisa wa polisi; Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii; Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto; na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, hali kadhalika wanachama wa tume za serikali zinazoshughulikia haki za binadamu, VVU/UKIMWI, na dawa za kulevya. Pia tuliwahoji wasomi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kile cha Muhimbili ambao wanafanya utafiti juu ya VVU miongoni mwa makundi maalum.

Mahojiano yaliendeshwa katika lugha za Kiingereza na Kiswahili na kuongozwa na watafiti na mshauri mwenye ufasaha katika lugha hizo. Wahojiwa waliosafiri kukutana nasi, kwa kawaida kwa mabasi ya umma, walifidiwa hela za usafiri na chakula cha mchana, hadi shilingi 5,000 hela za Tanzania (kama dola 3 za Marekani) kulingana na umbali wa safari. Wahojiwa wote walikubali kushiriki katika mahojiano yetu, ambayo walijulishwa yangejumuishwa katika ripoti ya haki za kibinadamu.

Majina ya wahojiwa wengi kutoka makundi maalum yamewekwa siri ili kuhakikisha kwamba hawajulikani. Kila mmoja amepewa jina la kwanza kwa vifupisho visivyo na uhusiano wowote na majina yao halisi.

I. Historia

VVU Tanzania: Kiwango cha Juu cha Maambukizi Miongoni mwa Makundi Maalum

TAREHE MUHIMU

1983

Kisa cha kwanza cha UKIMWI kilirekodiwa Tanzania bara. [2]

1980- mapema miaka ya 1990

Maambukizi ya UKIMWI yaongezeka kwa kasi.

1996    

Janga la UKIMWI lafika asilimia lake la juu: 8.4 ya watu wenye umri wa 15-49 waambukizwa VVU.[3]

1988

Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (National AIDS Control Programme) waundwa ili kuratibu shughuli za kukabiliana na VVU/ UKIMWI.

2001

Tanzania yaunda sera ya taifa kuhusu UKIMWI, yazindua Tume ya Kudhibiti UKIMWI (Tanzania Commission for AIDS-TACAIDS) kuratibu mbinu jumlifu ya kukabiliana na UKIMWI. Viwango vya maambukizo vyaanza kushuka.[4]

2007

Kiwango cha maambukizo chapungua hadi alisimia 5.8.[5]

2007-2012

Maendeleo yakwama.

TACAIDS yakadiria kiwango cha maambukizo kuwa asilimia 5.[6]

Ripoti ya hivi punde iliyotolewa na wanauchumi wa Benki ya Dunia imepata kuwa:

Tanzania iko nyuma ya nchi nyingine za eneo hili katika kupunguza vifo vinavyohusishwa na UKIMWI… Ukweli kwamba Watanzania wengi bado wanakufa kutokana na UKIMWI, licha ya kuwepo kwa matibabu, inaashiria kuwa mfumo wa afya wa nchi hiyo hauwafikii wale wanaohitaji kupimwa VVU na kutibiwa.[7]

Leo hii Tanzania inashikilia nafasi ya nne ulimwenguni kwa mujibu wa idadi ya vifo vitokanavyo na UKIMWI.

Kukwama kwa juhudi za kupunguza viwango vya maambukizo hakudhihirishi ukosefu wa uwekezaji wa Tanzania na washirika wake katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI. Kati ya mwaka wa 2004 na 2012, Mfuko wa Kimataifa ya Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (The Global Fund to Fight AIDS, Tuberculosis and Malaria) ilitoa zaidi ya dola za Marekani milioni 400 kwa matumizi ya VVU/UKIMWI.[8] Na kati ya mwaka wa 2009 na 2011, Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (United States President’s Emergency Plan for AIDS Relief-PEPFAR) uliipa Tanzania zaidi ya dola za Marekani bilioni 1 kwa kinga na tiba ya VVU/UKIMWI, na kuandikisha mkataba wa miaka mitano na serikali ya Tanzania kupunguza maambukizi mapya ya VVU na vifo vinavyohusishwa na UKIMWI.[9] Kwa mujibu wa PEPFAR, serikali ya Tanzania imeongeza kwa njia thabiti hela za kugharamia shughuli zinazohusu VVU/UKIMWI, na kumekuwepo na maendelea yanayoonekana katika ufahamu wa umma, upimaji, na upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya VVU (antiretroviral therapy, ART).[10]

Lakini kukwama huku katika kupunguza kiwango cha maambukizi kunaashiria kwamba baadhi ya makundi hayafikiwi. Miongoni mwa yale makundi magumu kufikiwa ni wale walio katika kile ambacho mashirika ya afya yametambua kama “makundi maalum” (“key populations, KP”) au “makundi yaliyo katika hatari kubwa zaidi” (“most at-risk populations,” MARPs). Makundi haya – yakijumuisha wanaume wanaofanya ngono na wanaume (MSM), watu wenye jinsia tofauti na asili, wanaojidunga dawa za kulevya, na wafanyakazi wa biashara ya ngono – wana uwezekano mkubwa wa kukabiliana na VVU au kuvieneza virusi hivyo.[11]

Kwa hakika, huku kiwango cha jumla cha maambukizi ya VVU vikiwa karibu na asilimia 5 katika Tanzania bara, baadhi ya tafiti zinaonesha kuwa viwango vya maambukizi viko juu miongoni mwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wafanyakazi wa ngono, na wanaojidunga dawa za kulevya. Takwimu za nchi nzima zinazoweza kutegemewa hazipo. Hata hivyo:

  • Viwango vya maambukizi vilikuwa asilimia 31 miongoni mwa wafanyikazi wa ngono wa kike jijini Dar es Salaam ikilinganishwa na asilimia 10 miongoni mwa wanawake wengine kiujumla, kwa mujibu wa utafiti wa NACP (Mpango wa Kudhibiti UKIMWI) wa 2010;[12]
  • Kiwango kikubwa cha asilimia 70 cha wanawake wafanyakazi wa ngono katika Mbeya walikuwa na VVU, kwa mujibu wa utafiti wa 2001;[13]
  • Kiwango cha maambukizi ya VVU miongoni mwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume kiko juu kwa asilimia 40, kwa mujibu wa matokeo ya awali ya utafiti wa hivi punde;[14]
  • Takriban asilimia 35 ya watu wanaojidunga dawa za kulevya jijini Dar es Salaam wana VVU.[15]

Katika kisiwa kinachojitawala cha Zanzibar,[16]kiwango cha maambukizi ya VVU miongoni mwa jamii kwa kijumla kilibaki chini – kwa takriban asilimia 0.6 mnamo mwaka wa 2008 – tangu kuripotiwa kwa kisa cha kwanza cha UKIMWI mnamo mwaka wa 1986.[17] Lakini Zanzibar inakabiliwa na janga lililokolea katika makundi haya maalum. Kwa mujibu wa makadirio ya serikali, asilimia 12.8 ya wanawake wafanyakazi wa ngono, asilimia 10.8 ya wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, na asilimia 16 ya wanaojidunga dawa za kulevya wana VVU.[18]

Mazingira ya Sheria na Sera

Wataalamu wa afya wametoa wito kwa serikali zitambue kuwa uhusiano baina ya haki za binadamu na jambo la kimsingi linalohitajika kwa dharura kuboresha afya ya jamii kupunguza maambukizi ya VVU na kuwatibu walioambukizwa tayari. Kama linavyotetea Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), uharamishaji na ubaguzi huyasukuma makundi maalum mbali na huduma muhimu:

Uharamishaji wa watu walio katika hatari kubwa ya kuambukizwa, kama vile wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wafanyakazi wa ngono, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watumiaji wa dawa za kulevya huwafukuza mafichoni, mbali na huduma za VVU. Hii huongeza hatari yao ya kuambukizwa VVU, pia unyanyapaa, ubaguzi, kutengwa na uvamizi. [19]

Tume ya Kimataifa kuhusu VVU na Sheria (Global Commission on HIV and the Law), ni tume ya wataalam iliyoanzishwa na idara ya Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) mwaka wa 2010, pia inatoa mwito wa kuhalalisha biashara ya ngono na mahusiano ya jinsia moja. [20] Hata Mkakati wa Pili wa Taifa wa UKIMWI Zanzibar unatambua vikwazo vinavyozuka kutokana na sheria na sera zinazobagua:

Sheria zinazobagua,sera zisizosaidia na mifumo ya udhibiti zinayaathiri makundi maalum na kuwazuia wasifi kie huduma au mara nyingi kuzipata huduma zisizo bora.[21]

Hata hivyo, Tanzania inaharamisha shughuli za makundi maalum yote matatu. Mapenzi ya hiari ya “kumuingilia mtu yeyote kinyume cha maumbile” huadhibiwa Tanzania bara kwa adhabu ya kifungo cha kati ya miaka 30 au maisha, [22] ilhali “matendo ya aibu baina ya wanaume” yanaadhibiwa kwa kifungo cha miaka mitano gerezani. [23] Huko Zanzibar, sheria inaharamisha mahusiano ya kimapenzi ya hiari baina ya wanaume (kwa adhabu ya kifungo cha miaka 14) na baina ya wanawake (kwa adhabu ya kifungo cha miaka 5).[24] Zanzibar pia imeharamisha mahusiano yasiyodhahiri baina ya wenzi wa jinsia moja.[25] Sheria zinazoharamisha mienendo ya mapenzi ya jinsia moja hazitekelezwi mara nyingi, lakini hutumika kuwasukuma mafichoni wapenzi wa jinsia moja, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watu wenye jinsia mbili.

Kushiriki katika biashara ya ngono ni haramu nchini Tanzania bara sawia na Zanzibar, na wafanyakazi wa ngono hukamatwa mara nyingi katika maeneo yote mawili. Sheria ya Tanzania huadhibu kwa miezi mitatu gerezani “kuzurura au kushawishi mahali popote pa hadhara kwa ajili ya kufanya umalaya.”[26] Sheria ya Zanzibar ni kali zaidi, na inasema kwamba mtu yeyote ambaye hujiuza kwa ajili ya kufanya ngono hufanya kosa na akipatikana na hatia ataadhibiwa kwa kifungo cha miaka mitatu.[27]

Matumizi ya kibinafsi ya dawa za kulevya na dawa za kusisimua akili ni marufuku bara na Zanzibar, na huadhibiwa kwa hukumu ya kati ya miaka saba hadi kumi.[28] Sheria ya mwaka wa 2009 ya Zanzibar inayotumika kama hukumu mbadala kwa wahalifu wa mara ya kwanza wanaopatikana na hatia ya kumiliki kiasi kidogo cha dawa za kulevya kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi wanaweza kuhukumiwa kifungo cha miezi sita katika kituo cha elimu na kufuatiwa na tiba katika kituo cha kurekebisha tabia.[29] Sheria hiyo ilikarabatiwa mnamo mwaka wa 2011, na badala ya kupelekwa katika kituo cha elimu sasa mtu hufungwa gerezani kwa miezi sita.[30]

Mkakati wa Pili wa Taifa Kudhibiti UKIMWI wa Tanzania unaorodhesha kama mkakati mmoja wa kupunguza kiwango cha maambukizi miongoni mwa makundi yaliyo hatarini, “Kukubali kuwa wafanyabiashara wa ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao wako katika hatari zaidi hivyo kuhimiza wapatiwe taarifa za VVU na huduma na pia kutokudharau shughuli zao”[31] – ama, katika toleo la Kiingereza la mkakati huu, “Kukubali kuwa wafanyibiashara wa ngono na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao wako katika hatari zaidi na kutetea haki zao ya kupata taarifa na huduma kuhusu kinga dhidi ya UKIMWI, na kutetea kuondoa uharamishaji wa shughuli zao.”[32]Lakini wabunge wa Tanzania hawajashirikisha mjadala muhimu kuhusu uhalalishaji wa mwenendo wa mapenzi ya jinsia moja au kazi ya ngono.

Afisa wa afya wa zamani mjini Arusha, kaskazini mwa Tanzania, alithibitisha kuwa kuharamishwa kwa mapenzi ya jinsia moja kulifanya iwe vigumu zaidi kuwafikia wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM) katika kampeni za afya za umma:

Hakuna mpango maalum hapa kwa makundi yaliyo katika hatari kubwa ni vigumu sana kwa maafisa wa afya kuwapata. Tunajua wapo, lakini ni kwa jinsi gani   unaweza kuwafikia ikiwa haramu? Ingekuwa shughuli halali, labda isingekuwa  vigumu.[33]

Uharamishaji pia unatatiza juhudi za kufikiwa na mashirika yasiyo ya serikali. Mwakilishi wa shirika moja lenye makao yake Arusha ambalo hufanya uhamasishaji juu ya VVU na ngono salama aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO kwamba yeye alikuwa amefikiria kuhusu kujaribu kuwafikia wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, lakini alikuwa na hofu ya kufanya hivyo, akifikiri kwamba ilikuwa kinyume cha sheria kuendesha warsha kwa ajili yao na kwamba angeweza kuingia katika matatizo na serikali.[34]

Kutowaamini maafisa wa serikali – kwa sababu ya sheria za jinai na mienendo ya kudhulumu – ni kikwazo kwa kazi ya uhamasishaji. Katika Zanzibar, mwakilishi wa shirika la VVU / UKIMWI, ZAYEDESA, alieleza:

Polisi ni tatizo. Katika kazi yetu ya kuzuia VVU tulilazimika kuyashawishi (makundi maalum) kwamba sisi hatukuwa tumekuja na polisi kuwakamata.[35]

Huko Mwanza, mwakilishi wa shirika la VVU / UKIMWI linalofanya kazi na watu wanaotumia dawa za kulevya aliliambia shirika la Human Rights Watch, "Tunahitajika kujenga imani kwao, na kueleza kwamba sisi hatufanyi kazi serikalini.”[36] Vile vile, mwakilishi wa shirika la kimataifa lisilo la serikali lililotaka kufanya uhamasishaji kuhusu VVU kwa wafanyabiashara wa ngono mjini Mwanza alisema, “Kuna haja ya kukaa na kushughulikia baadhi ya masuala muhimu kwao. Wanahitaji kukujua, kujenga uaminifu. Wanaweza kufikiria kwamba tunataka kuwafukuza kutoka mji huu.”[37]

Dkt. Joyce Nyoni, mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anayetafiti miongoni mwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, aliliambia shirika la Human Rights Watch kuwa uharamishaji unatatiza utafiti wa kitaaluma kuhusu makundi maalum:

Kwa sababu [mwenendo wa mapenzi ya jinsia moja] ni haramu, ni vigumu zaidi kwetu kufanya uhamasishaji na elimu. Ingekuwa rahisi kupata jukwaa la kufanya hivyo ingekuwa halali. Watu wanaogopa kuja kwetu. Kwa ajili ya kufanya utafiti huu tu, nilikuwa na ofisi nje ya chuo kikuu. Tulilazimika kufanya mambo kichinichini, na haturuhusu vikundi vya watu kuja.
Changamoto kubwa ni, tutawafikia vipi? Ni vigumu zaidi sasa ambapo kadi za simu zinasajiliwa. Wao [watu wa serikali] wanaweza kuwafuatilia watu. Tulikuwa tukitoa ujumbe kwa simu tamba kuhusu VVU/UKIMWI na matumizi ya kondomu, kusahihisha taarifa potofu. Baadhi yao walidhani kuwa kondomu hazizuii VVU/UKIMWI, au kwamba ngono ya mkundu hainezi VVU/UKIMWI. Inaweza kuwa vigumu kuutekeleza mradi huu sasa hivi.[38]

Uharamishaji pia hutoa kisingizio kwa mashirika mengine ya serikali kutokuwa makini katika kuyashughulikia makundi maalum. Afisa katika Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (Commission on Human Rights and Good Governance, CHRAGG), taasisi ya kitaifa ya haki za binadamu nchini Tanzania, aliliambia shirika la Human Rights Watch kuwa tume haishughulikii ukiukaji wa haki dhidi ya wana LGBTI. Kulingana na afisa huyo, “Swala hili ni nyeti, hakuna anayetaka kulizungumzia. Kama taasisi ya serikali, hatuwezi kuifanya. Itakuwa ni kinyume na mfumo uliopo. Ni kesi ya jinai.”[39]

Licha ya kutofanya utafiti juu ya swala hili, afisa huyo wa CHRAGG hata hivyo alilihakikishia shirika la Human Rights Watch kuwa makundi maalum “hayadhulumiwi wala kubaghuliwa.”[40]

Upatikanaji wa Taarifa

Kampeni za afya ya umma kuhusu VVU nchini Tanzania kwa kiasi kikubwa huwalenga wapenzi wa jinsia tofauti. Katika utafiti juu ya matumizi ya kondomu miongoni mwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM), watafiti wakuu walibainisha kuwa, “Ni kama hakuna vitabu, mabango na kadhalika kuhusu kinga dhidi ya VVU nchini Tanzania vilivyoandikwa na vinawataja MSM.... Kuna haja kubwa ya vitabu, mabango na kadhalika juu ya kuzuia VVU yanayowalenga MSM.” Watafiti wanaelekeza lawama ya pengo hili la taarifa kwa sheria inayoharamisha ngono kati ya wanaume, sawia na mazingira ya kijamii “ambapo MSM hudharauliwa na karibu wote.”[41]

Pengo la taarifa linachangia ujinga kwa upande wa baadhi ya watu walio katika hatari kubwa ya kupata VVU. Dkt. M.T. Leshabari, profesa wa afya ya umma katika Chuo Kikuu cha Muhimbili, alisema yeye alikumbana na imani nyingi potofu kuhusu VVU miongoni mwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume:

Baadhi ya [MSM] wanaamini kuwa ngono ya mkundu si njia ya maambukizo, kwa   sababu katika kampeni maarufu za uhamasishaji nchini Tanzania, mapenzi kati ya mwanaume na mwanamke ndiyo yaliyooneshwa kama njia ya maambukizo. Baadhi yao huamini mkundu ni moto na unaweza kuviua virusi, nao wengine wanaamini wanaweza kukimwaga nje baadaye. Hakuna chochote maalum kwa ajili ya uhamasishaji wa MSM kwa mujibu wa kampeni za uhamasishaji umma.[42]

Utafiti wa mashirika ya Human Rights Watch na WASO pia ulithibisha kuwepo kwa fikra hizi potovu. Daudi L., mwanaume anayefanya ngono na wanaume katika mkoa wa Mwanza, aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO kwamba hakujua VVU vinaweza kuenezwa kupitia kwa ngono ya mkundu.[43] Kashif M. alituambia yeye hajichukulii kama MSM, lakini aliwahi kufanya ngono ya mkundu na mwanamume mara moja, na hakuwa na ufahamu kuhusu hatari iliyokuwepo:

Mimi nilifanya ngono na mwanaume hivi majuzi. Yeye alinitaka kufanya ngono naye, kwa hivyo nami nikafanya hivyo. Sikutumia kondomu. Sikujua unaweza kupata UKIMWI kupitia kwa ngono ya mkundu. [44]

Mkakati wa Pili wa Taifa Kudhibiti UKIMWI unatoa mwito kuwepo kwa ushirikiano kati ya serikali na mashirika ya umma yanayoyawakilisha makundi maalum, lakini wanaume wanaofanya ngono na wanaume, watumiaji wa dawa za kulevya, na wafanyabiashara wa ngono wana mashirika machache ambayo huwawakilisha moja kwa moja, na mara nyingi hutengwa katika mijadala ya umma kuhusu masuala ambayo yanawahusu moja kwa moja.

Kwa mujibu wa yale ambayo yangeweza kuthibitishwa na mashirika ya Human Rights Watch na WASO, mashirika ya LGBTI yanapatikana Dar es Salaam na Zanzibar pekee. Mashirika haya hayawezi kufanya kazi kwa njia iliyo wazi kabisa, kwani yanahofia kufungwa na serikali, lakini yana uhusiano wa kikazi na taasisi za afya za serikali kama vile TACAIDS na Tume ya UKIMWI ya Zanzibar. Hakuna programu za kupunguza madhara kwa watu ambao wanatumia dawa za kulevya nje ya Dar es Salaam. Kwa sasa hakuna shirika la aina yoyote linalofanya kazi na wafanyakazi wa ngono katika mkoa wa Arusha, kitovu cha utalii, licha ya idadi kubwa ya wafanyakazi wa ngono walioko huko. [45] Huku mashirika ya wafanyakazi wa ngono yakiwepo Dar es Salaam, hakuna hata moja lililojaribu kujiandikisha na serikali.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, baadhi ya mashirika ya kijumla ya haki za binadamu huchelea kuyafikia makundi maalum kwa hofu kwamba kufanya programu za makundi haya yaliyotengwa kunaweza kuwa kinyume na sheria. Kuharamishwa kwa Makundi maalum kunaleta changamoto kwa watetezi wa haki za binadamu. Kwa jamii ndogo ingawa inayokua ya watetezi wa haki za binadamu waliojitolea wenyewe nchini Tanzania, ukosefu wa uwazi kuhusu uhalali wa kazi na wana LGBTI na  wafanyakazi wa ngono – ikijumuishwa na mitazamo ya kutovumilia ya baadhi ya watetezi wa haki za binadamu — kunaleta kikwazo kwa ushirikiano kati ya makundi ya wanaharakati wa LGBTI na wafanyakazi wa ngono, na mashirika ya kijumla ya haki za binadamu. Mmoja wa wanaharakati wa haki za binadamu aliliambia shirika la Human Rights Watch kuwa kama serikali ingeonyesha uvumilivu zaidi kwa wana LGBTI na wafanyabiashara wa ngono, mtandao wake ungejisikia salama kuyafikia  makundi yaliyotengwa na kushirikiana nao katika kushughulikia haki za kimsingi za binadamu, zikiwemo kukamatwa kiholela, mateso, na kunyimwa huduma za afya na haki. [46]

Ujamaa na Utengwaji

Chini ya rais wa kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere (1961-1985), Tanzania ilikuza itikadi ya kipekee ya Usoshalisti wa Kiafrika, inayojulikana kama Ujamaa. Ujamaa wa Nyerere ulikuwa falsafa ya kisoshalisti ya maendeleo, inayosemekana kwamba imejikita katika misingi ya uhuru, usawa, na umoja. Nyerere alikifanya Kiswahili kuwa lugha ya taifa ili kukuza utambulisho wa itaifa na kuzuia migogoro ya ukabila. Katiba ya Tanzania inajumuisha kauli kali kuhusu kutobaguliwa, heshima kwa binadamu na kuangamizwa kwa aina zote za ubaguzi na dhuluma (tazama sehemu ya VII kwa nukuu).

Kielelezo hiki cha umoja wa taifa na kutobagua kimekuwa na ufanisi kwa namna nyingi. Tanzania ni nchi ya pekee katika Afrika Mashariki ambayo haijakumbwa na ghasia za kila mara za ukabila na siasa. Kwa nchi yenye idadi kubwa ya Wakristo na Waislamu, ghasia zinazochochewa kidini ni nadra, ingawa hivi karibuni kushambuliwa kwa makanisa kumezua wasiwasi[47].

Lakini Tanzania haijaepuka ubaguzi wa kijamii. Kutokana na sifa zao zisizobadilika au hadhi yao ya kijumla ya kijamii, kumekuwa siku zote na waliotengwa nchini Tanzania. Katika miongo ya hivi karibuni, "waliotengwa" wamejumuishwa makundi kama vile watu wenye ulemavu wa ngozi (zeruzeru), wakimbizi, na watoto wa mitaani[48].

Aidha, msisitizo uliozidi kwa mshikamano wa jamii haujakuwa jambo zuri kila wakati kwa ajili ya haki za binadamu nchini Tanzania. Mbunge mmoja wa chama tawala alimwambia mwandishi wa habari katika mwaka wa 2012 kufuatia wimbi la maandamano ya upinzani, ambayo mengi yao yalizimwa na polisi kuwa, "Nchi hii ni pahali ambapo makubaliano yanathaminiwa – utulivu na amani ni suala nyeti. Wanaotekeleza sheria wanahitaji pengine kujifunza njia ya kukabiliana na aina hii [mpya] ya kujieleza. [49]

Chini ya umoja huu wa kulazimisha, majadiliano kuhusu haki za binadamu yanaweza kuonekana kama uchokozi. Mwanaharakati mmoja kutoka Dar es Salaam alielezea, "Hakukuwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu hapo awali kwa sababu ya mfumo wa jamii. Tulipoanza kuzungumzia haki za binadamu, kwa wengi nchini Tanzania, lilikuwa jambo geni." [50] Majadiliano kuhusu haki za makundi yaliyotengwa, kama vile wana LGBTI, wafanyakazi wa ngono, au watumiaji wa dawa za kulevya, hasa yanachukuliwa kuwa nyeti. [51] Mgogoro wa VVU kwa kiasi fulani umeyafanya makundi haya kuangaziwa, huku wizara za serikali kwa mara ya kwanza zikiyatambua kama makundi yaliyo katika hatari ya kuambukizwa VVU na hasa kama makundi yaliyotengwa katika jamii ya Watanzania. Lakini mjadala mkubwa kuhusu makundi maalum nchini Tanzania umelenga upatikanaji wa huduma za VVU na huduma ya afya pekee.

II. Muktadha wa Jamii na Sheria kwa Dhuluma Dhidi ya Wana LGBTI , Wafanyabiashara wa Ngono, na Watumiaji wa Dawa za Kulevya

Makundi haya matatu maalumyanayoshughulikiwa katika ripoti hii hukabiliana na aina sawa ya ukiukwaji wa haki za binadamu. Sehemu hii inatoa maelezo kwa jumla ya njia mahususi ambazo sheria, matumizi ya sheria kwa njia ya ubaguzi, na unyanyapaa wa kijamii huungana kuimarisha kutengwa kwa kila kundi. Hadithi tatu zilizoonyeshwa katika visanduku vya matini zinadhihirisha jinsi wanachama wa makundi yaliyotengwa ni waathiriwa wa mchanganyiko wa aina mbalimbali za ukiukaji mwingi.

Wapenzi Wa Jinsia Moja, Wenye Jinsia Tofauti na Asili, na Walio na Jinsia Zote Mbili  (LGBTI)

Tanzania ina mojawapo ya sheria kali zaidi kuhusu ushoga kote ulimwenguni, huku adhabu ya miaka 30 hadi kifungu cha maisha jela ikitolewa Tanzania bara kwa kosa la kufanya mapenzi kwa hiari kati ya wanaume. [52] Masharti ya kisheria yanayoharamisha ngono ya jinsia moja yamejikita katika msingi wa sheria za kikoloni ya Uingereza, ambayo ilitoa hukumu ya kifungo cha miaka 14 gerezani kwa ajili ya “kumuingilia mtu yeyote kinyume cha maumbile.” [53] Hukumu hii iliratibiwa upya mnamo mwaka wa 1998 na tena katika mwaka wa 2002, na sasa ni ya pili katika kutumia ubabe mkubwa zaidi kupambana na ushoga katika Afrika Mashariki baada ya sheria ya Uganda, ambayo inaamrisha kifungo cha maisha dhidi ya kosa la mwenendo wa ngono ya jinsia moja. [54] Sheria ya Zanzibar, kama ilivyoelezwa, haiharamishi tu mahusiano ya kingono, lakini pia mahusiano yasiyodhahiri kati ya washirika wa jinsia moja.

Hali ya wana LGBTI nchini Tanzania ilijadiliwa nadra sana hadharani hadi kufikia mwongo uliopita, na hatua ya kuanzishwa kwa mjadala wa umma kuhusu suala hili imekashifiwa sana. Katika mwaka wa 2003, takriban Watanzania 300 walipinga ziara ya Dar es Salaam iliyopangwa na kundi la mashoga kutoka Marekani [55] . Ziara hiyo hatimaye ilifutiliwa mbali. Katika mwaka wa 2007, Askofu mmoja wa Tanzania alikashifiwa vikali kwa kupendekeza mjadala zaidi kuhusu ushoga katika jamii na kanisa [56] . Mnamo Septemba 2011, Tamasha la Jinsia – hafla inayowaleta pamoja wanaharakati wa masuala ya kijinsia kutoka kote Afrika tangu mwaka 1996 na iliyopangwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (Tanzania Gender Networking Programme-TGNP) na Feminist Activist Coalition (FemAct), mashirika mawili ya Tanzania yasiyo ya serikali – lilikuwa jukwaa la mjadala mkali kuhusu haki za kingono na ikiwa mwenendo wa ngono ya jinsia moja ni "tendo asilia kimaumbile." Washiriki waliojitambulisha kama wana LGBTI walifukuzwa na vyombo vya habari na kulazimishwa kukimbia kutoka mahala pale, na kisha kushambuliwa na wananchi. [57] Kulingana na mshiriki mmoja MSM, "Genge la watu lilikuwa limekusanyika huko likisema lilitaka kuwaua mashoga. Nilikuwa ninapanda daladala [basi la abiria] na kondakta akaanza kunipiga. Kisha kila mtu akaanza kunipiga." Mwanahabari mmoja maarufu wa runinga alimwokoa na kumpeleka hospitalini. [58]

Tukio hilo lilichangia kuongezeka kwa upinzani kutoka kwa vyombo fulani vya habari na mitandao ya kijamii, na uoneshaji bila kupenda kwao wa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM) kuliathiri mahusiano yao na familia, waajiri na wamiliki wa nyumba za kukodisha. Washiriki waliiambia Human Rights Watch kuwa angalau MSM sita walipoteza kazi zao au walilazimika kuhama baada ya tamasha, wengine kwa sababu walikuwa wameonekana kwenye televisheni, wengine kwa sababu tu mjadala huo uliochochewa na Tamasha la Jinsia ulisababisha msako wa kiuonevu ambapo watuhumiwa wa ushoga wakashifiwa hadharani na jamaa, majirani, na waajiri. [59]

Mnamo Oktoba 2011, Baraza la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu lilifanya Mfumo wa Kimataifa Wa Mapito Wa Haki Za Binadamu (Universal Periodic Review) li. te a yao halisikwa wa Tanzania. [60] Wakati wa uhakiki huo, Tanzania ilikataa kukubali mapendekezo yote matatu kutoka kwa wanachama wenzake wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na haki za kingono: kuchukua hatua za kulinda haki za watu wote bila kujali mwenendo wao wa kingono, kupitisha sheria ya kupambana na ubaguzi, na kutoharamisha ngono hiari ya jinsia moja. [61]

Mnamo Novemba 2011, maafisa wa Tanzania walijibu kwa kina maoni ya Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron kuwa rekodi ya nchi kuhusu haki za wana LGBTI ingechangia kuafikiwa kwa uamuzi wa Uingereza kutoa misaada ya kigeni. Huku hatua za nchi wafadhili kushirikisha haki za binadamu na misaada ikiwa si dhana mpya, kuainishwa kipekee kwa haki za binadamu kwa wana LGBTI kulikashifiwa vikali. Gazeti moja linalotolewa kila siku Tanzania lilimripoti Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, akisema, "Msimamo wetu juu ya jambo hili ni wazi kabisa. Maadili na utamaduni wetu daima utatawala hata kama tutabaki maskini." [62] Gazeti hilo lilitoa maoni yake, likisema kuwa ushoga ni

…dhambi kuu ambayo hunuka hadi juu Mbinguni na ambayo inaweza tu kutokea katika dunia yenye kichaa ambapo wanaume wendawazimu na wanawake malaya hawana aibu kuvunja kanuni imara za desturi za kijamii au  kumchukiza Mwenyezi Mungu. [63]

Katika muktadha huu, kukamatwa, dhuluma, na unyanyasaji wa wana LGBTI ni mambo ya kawaida, hasa kwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM). [64] Mifano ya ubaguzi katika sekta ya elimu, makazi, na ajira pia umeripotiwa na huathiri wasagaji na wanawake wanaovutiwa kingono na wanaume na wanawake, halikadhalika mashoga na wanaume wanaovutiwa kingono na jinsia zote mbili. [65]

Ubaguzi dhidi ya walio wachache kingono na kijinsia kwa kiasi fulani unatokana na kutoelewa kuwa ushoga ni “jambo ambalo mtu hufanya” bali si “jinsi mtu alivyo”. Mwakilishi mmoja wa shirika lisilo la kiserikali katika mkoa wa Tanga, huku akisisitiza umuhimu wa kutoa huduma kwa wana LGBTI, alisema kuwa MSM ni “biashara,” akifananisha ushoga wa kiume na kazi ya ngono – na kudhihirisha dhana ya kawaida kote nchini Tanzania. [66] Imani hii inachangia hofu ya ushoga hata miongoni mwa wale wanaofanya kazi katika sekta kama za afya ya umma na haki za kibinadamu: katika mahojiano na Human Rights Watch, meneja wa kanda wa shirika moja la kimataifa la afya lenye hadhi kubwa alitoa mwito wa "kuuawa kwa mashoga" ili kuwazuia wengine “kuwa wanachama.” [67]

Huku ubaguzi ukitokea katika ngazi nyingi, MSM mmoja alilaumu ukosefu wa uongozi mzuri katika ngazi ya juu zaidi serikalini: "Rais haungi mkono haki za wana LGBTI. Akifanya hivyo – siku moja wakati yeye mwenyewe atasema 'Watu hawa wana haki sawa' – watu wataacha kutudhulumu." [68] Abdalla J., MSM mmoja mwenye umri wa miaka 32 ambaye babake alimfukuza nyumbani baada ya kuhudhuria Tamasha la Jinsia la mwaka wa 2011, alilaumu sheria ya Tanzania dhidi ya ushoga: "Unapaswa kuiambia serikali ituhalalishe. Kile ninachokifanya ni maisha yangu ya kibinafsi. Sijui ni nani anayeathirika ila mimi." [69] Mwanamume mmoja gay mjini Tanga alitoa rai moja: "Mimi nataka tu serikali ituchukulie kama binadamu.” [70]

Watu Wenye Jinsia Tofauti na Asili na Watu Wenye Jinsia Mbili (“Huntha”)   

Mashirika ya wana LGBTI yanayofanya kazi nchini Tanzania yalifahamu visa vichache tu vya watu wanaojitambulisha kama wenye jinsia tofauti na aili au wanaowasilisha hadharani utambulisho wa kijinsia usio wa kawaida. Kati ya Watanzania watatu wenye jinsia tofauti na asili ambao Human Rights Watch na WASO waliweza kuwatambua na kuwahoji wakati wa utafiti huu, wawili kati yao walikuwa wamekumbana na dhuluma za ukiukaji wa haki za kibinadamu mikononi mwa polisi, kama ilivyorekodiwa katika sehemu ya III. [71]

Human Rights Watch lilimhoji mtu mmoja mwenye jinsia mbili nchini Tanzania (taz. Faharasa). Dhana ya “kuwa wa jinsia mbili” ama “huntha” inaeleweka kidogo hata zaidi nchini Tanzania kuliko ile ya kubadilisha jinsia, na inawezekana kuwa mtu mwenye jinsia mbili wengi huchukuliwa kama mwenye jinsia moja au nyingine. Hata hivyo, visa vingi vilivyorekodiwa kuhusu ubaguzi kwa misingi ya mwelekeo wa kingono katika idara ya afya ya Tanzania vinaashiria kuwa wenye jinsia mbili wanaweza vilevile kukumbana na ubaguzi.

Hakuna utafiti uliowahi kuchapishwa kuhusu hali ya VVU ya watu wenye jinsia tofauti na asili au wenye jinsia mbili nchini Tanzania. Katika mataifa mengine, unyanyapaa dhidi ya watu wenye jinsia tofauti na asili na watu wenye jinsia mbili umegunduliwa kutatiza juhudi za kinga na tiba. [72]

KISA CHA SAIDI W .

Saidi W., mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume, na mwanafunzi wa chuo kikuu aliye na umri wa miaka 20 ambaye wakati mwingine hufanya kazi ya ngono ili kujikimu, alisimulia kisa kifuatacho:

Mnamo Disemba [2010], nilikuwa mahali ambapo mimi huwatafuta wateja. Nilikutana na mteja, lakini [iligeuka kuwa] hakuwa mtu wa kawaida, alikuwa polisi. Tulikwenda katika nyumba ya wageni. Mteja akasema, "Vua nguo zako." Nilivua  nguo zangu na ghafla mtu huyo akaelekeza bastola kwangu. Ghafla akawa na kinasa sauti na kamera ya video. Alisema,"Wewe utakuwa mfano kwa wengine. Mimi ninatoka CID [Idara ya Upelelezi wa Jinai] na ninatafuta watu kama wewe."Alinipeleka katika stesheni ya polisi ya Central na kunifungia huko.
Polisi huko waliniambia, "Waite mashoga wenzako. Sisi tunakwenda baa." Walikuwa wakiulizia mashoga kwa kijumla, si tu wafanyakizi wa ngono. Walikuwa polisi watano. Walinipa simu yao na kusema, "Waite rafiki zako, waambie kuna karamu hapa, hivyo kuna vinywaji vingi." Walikuwa wakitishia kunipiga risasi kama nisingewaita rafiki zangu. Walikuwa na bunduki za aina ya SMG. Walizielekeza bunduki zao kwangu, wakisema, "Kama huwaiti rafiki zako, tutakupiga risasi."
Tulienda pamoja hadi Kilabu cha Sun Cillo huko Sinza. Polisi wakanunua  vinywaji vingi. Niliwaita marafiki watano. Wote walifika. Baadhi yao walikuwa wamevaa sketi, baadhi walikuwa wamejikwatua. Polisi walikuja na kuwaweka katika Defender [gari la polisi]. Wakasema, "Sisi tunawakamata nyinyi kwa sababu nyie  ni mashoga na mnatuaibisha. Nchi yetu hairuhusu wasenge. Sheria zetu na dini yetu na desturi zetu haziruhusu jambo hili."
Walitupiga sana sisi sote katika baa. Walitupiga kwa mishipi yetu. Mmiliki wa baa na watu wengine hawakutusaidia—walicheka, walifurahi kwamba haya yalikuwa yanatokea. Polisi walituvua nguo na kuanza kutupiga kwa viboko. Walitupiga kila mahali mwilini. Walitupeleka rumande katika Stesheni ya Polisi ya Central huku wakituita mashoga. "Nyinyi ni mashoga, mbona mnauza miili yenu?"
Tulikuwa katika stesheni cha polisi kwa siku nne. Wafungwa wengine walitusumbua. Siku ya nne, wanaume hao waliamua kutubaka. Hawakutumia kondomu. Sisi tulikataa, lakini walikuwa wakubwa na wenye umri mkubwa kuliko sisi na hivyo walitumia nguvu. Tuliwaita polisi kwa kupiga mayowe kuomba msaada, tukisema, "Hawa wanaume wanatulazimisha kufanya ngono nao." Lakini polisi walisema, "Hivyo ni vyema, hayo ndiyo mnayotaka." Hivyo polisi walikuwa wakiwatia motisha wanaume hao. Kulikuwa na wafungwa wengine takriban hamsini. Watano kati yao walikuwa wakitubaka. Watatu kati yao walinibaka mimi binafsi. Nilipata maumivu mengi.

Siku iliyofuatia, wanaume hao watano walipelekwa katika kituo cha polisi cha Sitakishari. Afisa wa polisi wa kike aliwahoji. Aliwahurumia waliposema kuwa walikuwa wamebakwa: “Alisema, ‘Subiri hadi kesho, tutaweza kwenda hospitalini.’ Alitupa simu yake ili tuwapigie jamaa zetu waje kwa ajili ya dhamana.” Saidi alimpigia mamake, ambaye alikuja kukutana na afisa huyo. Hata hivyo, licha ya hurumu ya afisa yule, alitaka hongo:

Afisa alitaka fedha kama rushwa ili kutuachilia na kumaliza kesi yetu. Polisi walikuwa wakitaka shilingi 500,000 kwa ajili ya sote watano. Mama yangu alilia sana, akisema, "Sina fedha." Nikasema, "Mama, kesi hii ni mbaya sana." Mama yangu aliweza kukopa shilingi 400,000 baada ya siku tatu zaidi kutoka kwa mtu anayekopesha fedha. Baada ya kuwahonga polisi, tuliachiliwa. Ilimchukua mamangu muda mrefu kulipa deni hilo.

Saidi alihitimisha: "Ninapokumbuka hali ile, mimi hutaka kulia." [73]

Kazi ya Ngono na Unyonyaji Katika Biashara ya Ngono

Ingawa kazi ya ngono ni haramu nchini Tanzania, hufanyika wazi wazi katika majiji na miji mingi huku wafanyabiashara wa ngono wakikukusanyika katika maeneo yanayojulikana vyema. Ingawa wakati mwingine hufunguliwa mashtaka na kutumikia adhabu gerezani, wafanyakazi wa ngono mara nyingi hupigwa na kubakwa na polisi kisha hurudi barabarani kama ilivyorekodiwa katika Sehemu ya III.

Utafiti wa hivi majuzi uliofadhiliwa na Benki ya Dunia umeonesha kama “kushughulikia dhuluma, unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya wafanyikazi wa ngono” ni “uhitaji wa kimsingi wa haki za binadamu unaohitajika kwa dharura.” [74]   Kwa mujibu wa utafiti huo:

Uharamishwaji unawawezesha polisi kuendeleza dhuluma na unyanyasaji, kutaka ngono kwa nguvu na bila malipo, na kulazimisha walipwe faini kutoka kwa wafanyakazi bila malipizi. Imeachawaathiriwa wa fujo pamoja na dhuluma nyinginezo za ukiukaji wa haki na nafasi kidogo yaya kupata sheria. Kwa kuwalazimisha wafanyakazi wa ngono kwenda mafichoni, uharamishaji pia unarudisha nyuma juhudi za uhamasishaji wa jamii ili kuimarisha haki za wafanyakazi wa ngono, na kuendeleza ujitawala wao. [75]  

Madhara haya ya uharamishaji ni dhahiri nchini Tanzania. Wafanyabiashara wa ngono ambao huathiriwa na dhuluma, mikononi mwa Polisi na wananchi, huripoti uhalifu dhidi yao kwa nadra sana. Utafiti kuhusu wafanyabiashara wa ngono uliofanywa na Programu ya Kitaifa ya Kudhibiti UKIMWI (National AIDS Control Programme—NACP) jijini Dar es Salaam ulibaini kuwa asilimia 33.3 kati yao waliripoti kupigwa na wateja wao. [76] Mwakilishi wa shirika la kimataifa la afya ya umma mjini Mwanza alieleza, “Wafanyakazi wa ngono hawana pa kulalamikia dhidi ya hali ya kukosekana kwa haki iliyowakabili na polisi wanaweza kuwatumia vibaya kama wataenda kupiga ripoti. Ikiwa wataenda kwa polisi, polisi hao hugeuka na kuwa wateja wao kwa usiku huo.” [77]

Watu wazima na watoto wanaofanya kazi ya ngono hulazimishwa mara kwa mara kufanya ngono bila kondomu, ikiwa ni pamoja na maafisa wa polisi. Kama mfanyakazi wa ngono katika kijiji kidogo chenye migodi alisema: “Baadhi ya wanaume wana visu, na kama unataka kutumia kondomu, wao hutishia kukuua. Jambo hili lilinipata hapa Itumbi. Niliamua kufanya ngono bila kondomu kwa sababu nilikuwa na hofu. Wanaume wote hapa hubeba visu.” [78] Jijini Dar es Salaam, ingawa NACP ilitambua kiwango kikubwa cha matumizi ya kondomu miongoni mwa wafanyakazi wa ngono, pia iligundua kwamba “kiwango kikubwa cha unyanyasaji wa kingono na kimwili na washirika kunaonyesha kwamba wafanyakazi wa ngono wa kike (FSWs) huenda wasiwe na uwezo wa kufanya maamuzi kuhusu kinga.” [79]

Wafanyakazi wengi wa ngono hawana imani na hospitali za umma, ambapo wana hatari ya kunyimwa huduma au kukumbana na unyanyapaa, kama inavyoonekana hapa chini.

NACP ilitambua kuwa ingawa wafanyakazi wa ngono wengi wa kike katika utafiti huu walikuwa wamepimwa VVU angalau mara moja, “Harakati za kufikia huduma na upimaji wa VVU hazikuwa za kila wakati au hazikutokea kwa kiasi kinachopendekezwa kwa wanachama wa makundi yaliyo katika hatari kubwa. [80]  

Biashara ya Unyonyaji ya Kingono kwa Watoto

Kundi ambalo hasa limo katika mazingira magumu sana linajumuisha watoto wanaonyanyaswa kingono kupitia kazi ya ngono. Wasichana wanaoshiriki katika kazi ya ngono, au wanaonyanyaswa kingono, wana uwezekano mkubwa wa kukabiliana na dhuluma za kingono, kimwili, na kihisia, kulingana na utafiti wa kitaifa kuhusu dhuluma dhidi ya watoto nchini Tanzania. [81]

Sheria ya kimataifa inakataza vikali unyanyasaji wa watoto kwa njia ya biashara ya ngono. [82] Mtoto yeyote ambaye anashiriki katika kazi ya ngono au amepatikana katika biashara ya unyonyaji wa kingono, hapaswi kushitakiwa wala kuadhibiwa kwa kushiriki katika kazi haramu ya ngono lakini lazima apewe usaidizi wote utakikanao. Matumizi ya watoto katika kazi ya ngono huadhibiwa kwa kifungo cha hadi miaka 20 chini ya sheria ya Tanzania. [83] Hata hivyo katika visa kadhaa ambavyo Human Rights Watch na WASO yalirekodi, polisi waliwadhulumu kimwili na kingono watoto walioshiriki katika kazi ya ngono, badala ya kuwalinda. Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, hakuna mtu aliyefunguliwa mashitaka nchini Tanzania katika mwaka wa 2012 kwa unyanyasaji wa watoto kingono. [84]

KISA  CHA ROSEMARY I.

Rosemary I., yatima, alianza kazi ya ukahaba alipokuwa na umri wa miaka 10. Alipohojiwa na shirika la Human Rights Watch  kule Mbeya, alikuwa na umri wa miaka 14 na alikuwa na mtoto mwenye umri wa mwaka 1. Alifukuzwa shule akiwa katika kidato cha 3 baada ya kushika mimba. [85] Rosemary ana matumaini madogo ya kupata riziki kwa njia nyingine isipokuwa kazi ya ngono.

Rosemary ni mtoto kulingana na sheria za kimataifa na zile za Tanzania, lakini kwa polisi wa Tanzania, yeye ni mhalifu pia pamoja na kuwa windo rahisi kwa wawindaji ngono katika jeshi la polisi. Alisema kuwa amewahi kubakwa na polisi “takriban mara saba.” Alieleza,

Wanapokukamata, hawakupeleki katika stesheni ya polisi. Popote wanapokutana nawe, wangeweza kukupeleka vyooni katika kilabu, au ikiwa wamekutana nawe barabarani, wao hutafuta mahali pa faragha tu na kufanya ngono nawe hapo. Hawatumii kondomu – wao daima hukataa.

Kukataa kufanya mapenzi na polisi si chaguo kwa wafanyakazi wengi wa ngono tuliowahoji. Mnamo Disemba 2010, Rosemary alipokuwa na umri wa miaka 12, alikamatwa akifanya kazi huko Tunduma, karibu na mpaka wa Zambia. Polisi alitaka ngono, naye akakataa. Aliliambia shirika la Human Rights Watch kuwa:

Wakati mmoja nilikataa na wakanituma katika stesheni ya polisi ya Tunduma. Niliomba msamaha nilipofika katika stesheni. Walikuwa askari wanne au watano. Wakasema, “Kama unataka msamaha, ni lazima ufanye mapenzi nasi.” Kwa hiyo mimi nilifanya mapenzi na wao wote, kwa sababu wote walitaka. Baada ya kulala nao wote, waliniachilia.

Mwezi huo, Rosemary alipigwa na kubakwa na kundi jingine la maafisa wa polisi, tena katika stesheni ya polisi ya Tunduma:

Siku moja niliwahi kupigwa barabarani na kupelekwa katika stesheni ya polisi. Walikuwa wananipiga kwa vijiti vikubwa wanavyobeba. Walinipiga kichwani, mikononi. Nilipofika kituoni, nilikuwa nahisi maumivu na kutokwa damu puani. Polisi wengine wakasema, “Lazima tufanye mapenzi nawe kama unataka kuachiliwa.”

Katika mwezi wa Aprili 2011, Rosemary aliwekewa dawa na mteja huko Mbeya. Baadaye aligundua kuwa mteja huyo alikuwa amemchukua hadi kwenye nyumba ya wageni na kumbaka na kumlawiti akiwa amepoteza fahamu, na kumwacha uchi nje ya nyumba ya wageni. Kwa kauli yake Rosemary:

Niliamka asubuhi na nikajikuta nje, nikitokwa na damu kutoka sehemu zangu za siri. Watu walinipata na wakataka kunipeleka hospitalini, lakini nilikataa kwa sababu nilikuwa na hofu. Ningejieleza vipi?
Niliogopa pia kwenda kwa polisi kwa sababu huenda polisi wangetaka tu pesa, na sikuwa na pesa. Pia, nisingeeleza kwamba nilikuwa ninajiuza kwani hiyo ingeweza kuwa kesi dhidi yangu. [86]

Watumiaji wa Dawa za Kulevya

Katika sehemu za Tanzania, ikiwa ni pamoja na Dar es Salaam, Zanzibar na Arusha, kuna viwango vya juu vya utumiaji wa dawa za kulevya, hasa kwa watumiaji  mihadarati ya kujidunga. Takriban watu 25,000 hadi 50,000 hujidunga mihadarati nchini Tanzania. [87] Wengi hujidunga heroini, ambayo ilienea katika miaka ya 1990 wakati ambapo walanguzi wa mihadarati walibadilisha njia za jadi za usafiri wa ardhini kutoka Asia hadi Ulaya, badala yake wakipendelea usafiri katika Bahari Hindi. Zanzibar na Dar es Salaam zikawa bandari za kuingiza dawa za kulevya. [88]

Watu ambao hujidunga mihadarati (people who inject drugs, PWID) hasa huwa katika hatari kubwa ya kuambukizwa VVU / UKIMWI, hasa kwa sababu ya watu zaidi ya mmoja kutumia sindano moja. Utafiti unaonyesha kuwa maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa PWID nchini Tanzania yanaongezeka. [89]

Kushughulikia viwango vya juu vya maambukizi ya VVU, shirika la “Médecins du Monde”, shirika lisilo la serikali la kimataifa, limeanzisha programu ya kupunguza madhara miongoni mwa watumiaji mihadarati ya kujidunga katika eneo la Temeke, wilaya maskini zaidi Dar es Salaam. Shirika la MdM linaendesha mpango wa sindano na sirinji, na limetoa mafunzo kwa maafisa wa polisi wasiopungua 150 jijini Dar es Salaam kuhusu  umuhimu wa upatikanaji wa sindano na sirinji safi. [90] Pia limerekodi visa vya ukiukaji wa haki za binadamu miongoni mwa walengwa wake, na kufanya kazi na makamanda wa polisi ili kushughulikia visa husika kwa utaratibu. Hakuna mipango ya sindano na sirinji nchini Tanzania nje ya Dar es Salaam, ingawa mipango hiyo imezingatiwa huko Zanzibar [91] .

Maafisa wa afya ya umma nchini Tanzania wameanzisha pia matibabu ya methadone kwa watumiaji wa heroini. [92] Kliniki ya methadone katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam, ambayo ilianzishwa mwaka wa 2011 kutokana na ufadhili wa PEPFAR, ni kliniki ya pili ya aina hiyo katika Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara. [93] Kliniki ya pili ya methadone ilifunguliwa katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam mnamo mwaka wa 2012.

Kule Zanzibar, serikali imeanza kutambua kwamba matumizi ya heroini yamesambaa sana, na njia bora ya kuyashughulikia si kupitia kwa hatua za adhabu. Rais wa Zanzibar ametamka hadharani kuhusu haja ya kuwasaidia watu wanaotumia dawa za kulevya na kuwapa huduma; kwa mujibu wa wanachama wa Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya ya Zanzibar, kauli ya rais imechangia pakubwa katika kupunguza unyanyapaa kwa kuanzisha mbinu zisizo za kuadhibu katika mijadala ya umma. [94]

Hata hivyo, watumiaji mihadarati nchini Tanzania bado wanakumbwa kwa kiwango kikubwa na unyanyapaa pamoja na unyanyasaji. Watu kadhaa waliohojiwa na Human Rights Watch na WASO walielezea kunyanyaswa kimwili katika mikono ya polisi, vikundi vya wanamgambo, na majirani. Wengi wao walituambia kwamba watu wanaotumia dawa za kulevya kwa ujumla huonekana kama "wezi," bila kujali kama kweli wameiba chochote.

KISA CHA JANUARY H.

January H. anaishi katika Wilaya ya Temeke na anatumia heroini. Katika mwaka wa 2011, alishambuliwa na wanachama wa Sungu Sungu—kundi la wanamgambo, maelezo mengi yanapatikana chini —ambao walimtuhumu kuwa wizi. Walimkokota hadi uwanja wa shule iliyokuwa karibu, ambapo walimkata kichwani na usoni kwa panga. Januari alijiokoa kutoka kwa genge hilo na kukimbia hadi katika kituo cha polisi cha Mashini ya Maji, ambapo alipoteza fahamu. Alisema kwamba, fahamu zilipomrejea:

Nikasikia polisi akisema [wakiambia Sungu Sungu], "Kwa nini hamkumwua? Mlimleta hapa kwa nini?" Kisha afisa wa polisi mwenye cheo cha juu akauliza "Aliiba kutoka kwa nani?” na hakuna aliyejibu.
Polisi walinipeleka katika stesheni ya polisi ya Mtongani. Waliuliza ni nani aliyekuwa mlalamishi na nambari ya usajili katika R.B. (kitabu cha kusajili), lakini hakukuwepo. Mlalamishi alipokosekana, polisi wa Mtongani waliwaita polisi wa Chang'ombe. Walikuja wakanipeleka hospitalini.

January alidhani kuwa taabu zake zimekwisha, lakini wahudumu wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke ambao walimtibu waliiharibu hali yake hata zaidi. Alieleza:

Daktari alinichunguza, akaandika vitu, na kunituma Wodi nambari 10 kushonwa. Hapo, walianza kunishona bila kudungwa sindano yoyote [anestezia]. Nikaiulizia muuguzi akasema, "Hatuna haja ya kuitumia. Tutakushona bila anestezia. Tungeweza kukudunga sindano ya sumu badala ya anestezia." Niliwasikia [wafanyakazi wa hospitali] wakisema, "Huyo ni mwizi." Basi walinishona kila mahali bila ya anestezia.

January aliporuhusiwa kutoka hospitalini, alidhamiria kufungua mashtaka dhidi ya washambuliaji wake kwa polisi, lakini akachelea: "[Kwa] wengi wetu vijana tunaotumia dawa za kulevya, polisi huzua vikwazo kwetu dhidi ya kufungua kesi. Wanaweza kuendelea kukwambia usubiri. Na kisha wakufungulie mashtaka ya uongo [ulaghai] na kukupeleka gerezani."

Aliongezea, kuhusu Sungu Sungu, “Najua ukweli ni kwamba siku moja wataniua.” [95]

III. Dhuluma, Vitisho na Unyang’aji wa Polisi

Vurugu, chuki bila sababu, na unyang’anyi wa polisi huchangia sana kutoaminiana kati ya makundi maalum na taasisi za serikali. Kwa Watanzania wengi, polisi ndio wawakilishi wa Serikali ya Tanzania wanaokumbana nao mara kwa mara. Kwa makundi maalum, maingiliano hayo si mazuri. Human Rights Watch na WASO yalirekodi visa vya mashambulizi makali ya polisi dhidi ya makundi yote matatu yaliyoangaziwa katika ripoti hii: wana LGBTI, watumiaji wa dawa za kulevya, na wafanyakazi wa ngono. Polisi pia waliwalenga watoto walioathiriwa kutokana na unyonyaji wa kingono. Kati ya wale ambao hawakuwa wamekumbana na mashambulizi ya polisi, karibu kila mmoja alikuwa amenyang’anywa hela na polisi, amenyanyaswa kingono, au yote mawili.

Kati ya makundi haya matatu maalum, utafiti wetu unaonyesha kwamba wale ambao wamo katika hatari zaidi ya unyanyasaji wa polisi wanatoka katika matabaka ya chini ya kijamii na kiuchumi. Wanaume wanaofanya ngono na wanaume, watumiaji wa dawa za kulevya, na wafanyabiashara wa ngono kutoka katika matabaka ya juu kiuchumi mara nyingi huweza kuepuka polisi. Mtumiaji wa heroini kutoka familia ya tabaka la kati aliliambia Human Rights Watch kuwa hakuwahi kukamatwa kamwe na polisi kwa sababu alitumia mihadarati katika faragha ya nyumba yake mwenyewe. [96] Vile vile, kundi la wafanyakazi wa ngono kutoka mjini Arusha lilisema kwamba kwa sababu walikuwa wakifanya kazi katika baa ambayo wateja wake ni wa tabaka la kati, kwa kiasi walikuwa wamelindwa kutokana na unyanyasaji wa polisi, ilhali wenzao ambao walifanya kazi mitaani walikuwa wakikamatwa na kupigwa mara nyingi zaidi. [97] Huku dhuluma za polisi kwa wafanyakazi wa ngono wa kiume zikiwa za kawaida, Human Rights Watch na WASO hayakusikia kisa chochote cha polisi kuwakamata au kuwatesa wateja wao, ambao kwa ujumla walikuwa wanaume matajiri. Uwezo wa matajiri kulipa hongo kuliwasaidia pia, katika baadhi ya visa, kuepuka kuwekwa kizuizini na kudhulumiwa.

Si makundi yaliyotengwa pekee ndiyo hukabiliwa na dhuluma na ukiukaji katika mikono ya polisi wa Tanzania. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre, LHRC), shirika lisilo la serikali, liliripoti kwamba polisi wa Tanzania waliwaua kinyume na sheria takriban watu 11 katika mwaka wa 2012. [98] LHRC lilitaja desturi ya kutojali sheria na ukosefu wa taasisi zilizoundwa kando na huru za usimamizi kama sababu ya dhuluma ya hali ya juu ya polisi dhidi ya raia. [99]

Ufisadi wa polisi pia ni tatizo lililoenea sana Tanzania. [100] Kulingana na mwakilishi wa shirika la misaada ya kigeni linaloshirikiana na polisi wa Tanzania, "Polisi ni wafisadi zaidi kuliko taasisi nyingine. Inaweza pia kuwa taasisi mbaya zaidi katika haki za binadamu." [101] Mara kwa mara polisi wa Tanzania huwasumbua wananchi kwa ajili ya rushwa. Hii ni pamoja na madereva, kwa mfano, ikiwa wamevunja au hawajavunja sheria; waathiriwa wa uhalifu ambao wanatafuta msaada wa polisi na wanaambiwa kuwa msaada huja tu kwa gharama fulani; wakimbizi au wanaotafuta hifadhi ambao hukamatwa kwa kukosa stakabadhi zinazohitajika; au watu wanaoshiriki katika matendo haramu ya kingono au matumizi ya dawa za kulevya. [102] Polisi wanajua kwamba kundi la mwisho ni windo jepesi, kwani ni haba kwa wanachama wa makundi yaliyotengwa kuwasilisha malalamiko.

Kiasi fulani cha juhudi zimekuwa zikifanywa kupambana na ufisadi wa polisi. Polisi ililiambia Human Rights Watch kuwa maafisa 47 walifukuzwa kazi kutokana na ufisadi katika miezi sita ya kwanza ya mwaka wa 2012. [103] Hata hivyo, kuna uwezekano finyu wa makundi ya waliotengwa kuwaripoti polisi wafisadi au wenye vurugu, kama inavyodhihirika katika hadithi ifuatayo.

Mateso na Maonevu

Human Rights Watch na WASO yaliwahoji wanachama kadhaa wa makundi maalum waliokuwa wameteswa, kubakwa, kudhulumiwa, au kulazimishwa na polisi kutoa hongo katika miaka kadhaa iliyopita. Katika visa hivi vyote, hakuna hata kimoja ambapo polisi walilazimishwa kuwajibikia ukiukaji huo.

Huko Temeke, wilaya ya Dar es Salaam yenye kiasi cha juu cha matumizi ya dawa za kulevya, waathiriwa mara nyingi walimrejelea afisa wa polisi kwa jina la utani "Tyson,"

anayefanya kazi katika Stesheni ya Polisi ya Chang'ombe, ambaye kwa ushahidi wote alionekana kufurahia kuwashambulia na kuwadhalilisha watumiaji wa dawa za kulevya. Katika kisa kimoja, Suleiman R. alikamatwa mnamo tarehe 31 Disemba, 2011, na kupelekwa katika Stesheni ya Polisi ya Chang'ombe. Kulikuwa kumetokea visa vitatu vya ujambazi wiki iliyotangulia, na kwa sababu Suleiman alikuwa anajulikana kwa kutumia mihadarati ya kujidunga, polisi walimshuku kwa ujambazi huo. Alisema,

Walinipeleka katika chumba maalum kunitesa ili nikiri kuwa nilitenda visa hivyo vya ujambazi.... Kwanza walinipiga kwa vyuma kwenye mkono wa kulia. Kisha wakachukua pasi ya nguo na kunipiga pasi mkononi. Walinipiga pasi mara mbili. Mmoja wao alikuwa Tyson, ambaye pia anajulikana kama Adnan. [104]

Human Rights Watch liliona alama za kuchomwa kwenye mkono wa Suleiman zinazofanana na zile zinazoachwa na pasi. Siku iliyofuatia, wazazi wa Suleiman walilipa hongo ya shilingi 200,000 ili aachiliwe.

Zeitoun Y. alikamatwa Januari 2009 mara tu baada ya kuvuta heroini katika maskani yake. [105] Alijaribu kukimbia; wakati polisi walipomkamata, alisema, "Nilifungwa shingoni kwa kamba. Nilibururwa kwa umbali wa mita 200. Tyson alinifunga kwa kamba na kuniburura mwenyewe." Zeitoun  alipelekwa katika Stesheni ya Polisi ya Chang'ombe. [106]

Mwajuma P. aliripoti kuwa katika mwaka wa 2011, Tyson aliwapiga na kudhalilisha kundi la wanawake ambao hutumia dawa za kulevya:

Alikuja katika maskani yetu na polisi wengine wawili, akatukamata, na kutulazimisha tuombe.... alituambia tuweke mikono yetu juu ya vichwa vyetu. Kisha alitulazimisha kutembea hadi kwa polisi huku tukuiimba nyimbo: "Sisi, sisi ni watumiaji wa dawa za kulevya. Sisi, sisi ni wezi wa simu." Tyson alianza kututenda kama ng'ombe, akitupiga kwa paipu nzito ya plastiki yenye urefu wa futi tano. Yeye ndiye aliyekuja nayo. Alinipiga mgongoni, na miguuni. [107]

Kwa mujibu wa Mwajuma, Tyson aliwalazimisha wanawake hao kutembea zaidi ya kilomita nne katika jua kali la adhuhuri. Katika Stesheni ya Chang'ombe, polisi walirekodi taarifa zao. Mwajuma aliachiliwa baada ya siku mbili bila kushtakiwa, shemeji yake alipolipa shilingi 20,000.

Ally H., ambaye anatumia heroini, alisema kuwa polisi kutoka Chang'ombe walimpiga yeye na mke wake mnamo Agosti 2012:

Polisi walikuja kutoka Chang'ombe mwendo wa saa mbili usiku. Walivunja mlango kwa nguvu. Waliingia na kuanza kunipiga mimi na mke wangu.... Walikuwa wakitushuku kuwa walanguzi wa mihadarati. Hawakuwa na kibali chochote. Walikuwa saba.
Mimi nilipigwa kwa rungu magotini, mikononi na mgongoni. Bado nina maumivu magotini. Walinipiga mgongoni kwa fimbo iliyokuwa kama jiti nene. [108]

Ally alisema kuwa kituoni, afisa wa uchunguzi alimwamuru kulala chini sakafuni na polisi mwingine tofauti akampiga. Hata baada ya Ally kulipa hongo ya shilingi 40,000, alisema, “Polisi waliendelea kutupiga kwa viboko wakitufukuza kutoka katika stesheni ya polisi. Ilikuwa alasiri na maafisa wengine wote wa polisi waliona.” [109] Takriban mwezi mmoja baada ya kuachiliwa, mtafiti wa Human Rights Watch aliona alama za kipigo mgongoni mwa Ally zilizofanana na kupigwa kwa viboko.

Waathiriwa kadhaa pia walitaja mifano ya polisi kutoka Stesheni ya Polisi ya Oysterbay, jijini Dar es Salaam waliohusika na mashambulizi, unyanyasaji wa kingono, na unyang’anyi. Fazila Y. alisema kuwa polisi kutoka Stesheni ya Polisi ya Oysterbay walimpiga barabarani alipopatikana katika maskani yake akitumia dawa za kulevya na marafiki zake mnamo Oktoba 2011:

Wapita njia na wenye maduka walitazama huku polisi wakinipiga, wakinitusi na kunirarulia nguo. Waliridhika kuwa nilikuwa nimeumia kama walivyopenda, waliniburura hadi ndani ya gari la polisi.[110]

Alipoulizwa kama alifikiria kuwasilisha malalamiko dhidi ya maafisa ambao walimpiga, Fazila alisema, "Sioni haja ya kulalamika kuhusu dhuluma tunazozipokea kutoka kwa polisi. Nini kitabadilika? Nani atasikiliza?" [111]

Sajenti wa polisi alimtia mbaroni na kumpiga Mickdad J., huko Tandika, Dar es Salaam, mnamo Juni 2012 kwa sababu alikuwa amebeba sirinji ambazo hazikuwa zimetumika kutoka kwa “Médecins du Monde”  chini ya programu yao ya kupunguza madhara:

Mimi nilikuwa natoka MdM nikiwa na sirinji, visanduku vya njano [vya kutupa vifaa vyenye makali], vitu nivitumiavyo kujidunga sindano. Nilikuwa nje ya nyumba yangu nikipanga vitu hivyo. Sajenti akaniona, akasimama na kunikamata. Nilitaka kuwapigia MdM, lakini [sajenti huyo] alinipeleka katika kituo cha polisi cha Mamboleyo. Huko, alinipiga mwenyewe kwa mikono yake, kwa kiboko na pia kwa viatu vyake vikubwa vya polisi (buti). [112]

Mamake Mickdad alikuja katika kituo cha polisi na kulipa shilingi 30,000 ili aachiliwe, lakini kisa hicho kilikuwa na madhara ya kudumu kutokana na afya yake mbaya. Mickdad alisema, "Hata sasa mimi huwa na maumivu katika uti wa mgongo wangu na uratibu wangu si mzuri. Nina VVU, hivyo basi wakati watu hunipiga huwa ni tatizo. " [113]

Kisa kimoja cha kutisha hasa cha madai ya unyanyasaji wa polisi kinamhusu John Elias (jina lake halisi), mtumiaji wa heroini katika eneo la Kigamboni, Dar es Salaam. Mnamo Februari 18, 2010, alikamatwa katika kitongoji cha Kurasini wakati wa msako wa dawa za kulevya. Kulingana na Elias, mmoja wa maafisa wa polisi waliohusika katika kukamatwa kwake alikuwa na tatizo la kibinafsi naye: afisa huyo aliamini Elias alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wake. Inaonekana kuwa afisa huyo alitumia msako ule wa dawa za kulevya, na hali mbaya na hatari ya Elias, kama fursa ya kulipiza kisasi.

Elias aliliambia Human Rights Watch kuwa polisi walimvamia ndani ya nyumba saa kumi alasiri na wakadai kuwa walikuwa wakiendesha operesheni ya kusaka dawa za kulevya:

Walitafuta lakini hawakupata chochote. Waliwakamata watatu kati yetu. Mimi nilikamatwa na polisi aitwaye James ambaye alinishuku kumnyemelea mpenzi wake. Yeye alinijua kutoka zamani. Alinituhumu kuwa mtumiaji wa dawa za kulevya, lakini pia kumnyemelea mwanamke wake. Wengine wawili walikamatwa kwa sababu walikuwa watumiaji wa dawa ya kulevya. [114]

Wote watatu walipelekwa katika Stesheni ya Polisi ya Kilwa Road. Polisi walianza kuchukua taarifa kutoka kwa marafiki za Elias, lakini Elias alisema afisa Kamanda wa Wilaya (Officer Commanding District, OCD) – mkubwa wa James na wengine waliokuwepo – waliagiza apelekwe katika kituo cha polisi tofauti.

Niliwekwa ndani ya gari huku nikiwa nimefungwa pingu kwenye mikono na miguu. Hawakuniambia sababu ya kufanya hivyo. Kisha James alisema, "Tunakupeleka Chang'ombe kuvunja mguu wako." Lakini walikuwa wakidanganya – walinipeleka katika kituo cha Minazini.
Walinitia pingu mikononi na miguuni na kuniangusha. Niliona sirinji iliyokuwa na kioevu. James alikuwa ameishika. Alisema, "Leo ni siku yako ya mwisho ya kuona, Bw. John." Kwanza alinidunga jicho langu la kulia, kisha la kushoto. Nilikuwa nimelala sakafuni. Takriban polisi watano walikuwa hapo. Walikuwa wakininyakua, kunishika, kunikanyaga kwa viatu vyao vikubwa.... Nilihisi kama macho yangu yalikuwa yakichomeka. Kulikuwa na joto jingi. [115]

Karibu saa moja jioni, Elias alisema polisi walimrudisha katika Stesheni ya Polisi ya Kilwa Road na kumtia rumande na marafiki zake. Polisi walimpeleka mahakamani moja kwa moja asubuhi. Ingawa aliwaambia maafisa wa mahakama kile alichotendewa na polisi, alichukuliwa gerezani moja kwa moja wala hakupelekwa hospitalini mpaka baada ya wiki. [116] Huko, aligundua kwamba polisi walikuwa wamemdunga machoni kwa asidi.

Leo hii, Elias ana mashimo matupu mahali ambapo macho yake yanafaa kuwa.

The Nyerere Centre for Human Rights, shirika la nchini lisilo la serikali lenye makao yake wilayani Temeke, limekuwa likifuatia kesi hiyo tangu 2010. Edward Nsajigwa wa Nyerere Centre aliliambia Human Rights Watch, "Yeye alienda kufungua kesi katika Stesheni ya Polisi, lakini hawakumsaidia. Alikwenda kwa katibu mkuu katika Wizara ya Mambo ya Ndani, lakini katibu mkuu alisema macho yake yalitobolewa na genge la kujichukulia sheria mkononi." [117] Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), taasisi ya kitaifa ya Tanzania ya haki za binadamu, imezuru nyumbani mwake Elias kuchunguza kesi hiyo. Mwezi wa Aprili 2013, afisa wa CHRAGG aliliambia shirika la Human Rights Watch kwamba faili ya kesi hiyo bado inachunguzwa katika CHRAGG, bali hakutoa maelezo zaidi. [118]

Mateso ya polisi na dhuluma kwa watu wanaotumia dawa za kulevya si jambo lililojikita katika jiji la Dar es Salaam pekee. Katika mkoa wa Mbeya, Musa E., kijana ambaye amekuwa yatima tangu alipokuwa na umri wa miaka minane na ambaye alikuwa akitumia heroini, anasema kuwa alikubali kusafirisha gunia la heroini mpakani kutoka Zambia ili kugharamia mihadarati. Polisi wa Tanzania walimtia mbaroni katika mji wa Tunduma ulioko mpakani na wakamtesa ili kujua ni nani alikuwa akimfanyia kazi. Musa alisema polisi walifinya kucha zake za mikononi na miguuni kwa chamburo; wakampiga kumbo kwenye taya, na kusababisha kinywa chake kutokwa na usaha kwa mwezi kutokana na maambukizi yaliyosababishwa na kipigo, na kukanyagwa vifundoni kwa viatu vikubwa, mpaka alipofichua jina la mwajiri wake. [119]

Huko Zanzibar, waliokuwa watumiaji wa dawa za kulevya waliliambia Human Rights Watch kuwa mengi ya malalamiko yao yalikuwa na polisi jamii (tazama Sehemu ya IV hapo chini). Mashirika ya mitaani yameandaa mafunzo na mijadala ya kuhamasisha polisi wa kawaida kuhusu umuhimu wa matibabu badala ya adhabu. Haya yamekuwa kwa kiasi kikubwa yenye mafanikio. Lakini baadhi ya visa vya unyanyasaji wa polisi bado hutokea. Polisi walimshika Omary Q. katika mtaa wake akiwa na heroini mnamo mwishoni mwa mwaka wa 2011. Omary alisema,

Waliikamata shingo yangu na kunipiga ngumi mapafuni na kunipiga teke kiasi cha kuniangusha chini. Kisha walinitia pingu na kunipeleka katika stesheni. Waliniuliza, "Unaweza kulipa pesa ngapi [ili uachiliwe]?" Nikasema, "Sina hela yoyote, lakini kama tunaweza kwenda mahali fulani naweza kupata kiasi." Niliondoka na wawili wao. Tukakwenda kwa kaka yangu. Kakangu aliwahonga kwa shilingi 50,000 na wakaniachilia huru.
Huwezi kwenda kwa polisi na kutoa malalamiko kama umedhulumiwa nao. Hatuwezi kuwaamini. Watatushtaki kwa  kwenda kinyume na sheria. [120]

Mtumiaji mmoja wa zamani wa heroini aliliambia Human Rights Watch kuhusu udhalilishwaji aliokumbana nao chini ya kizuizi cha polisi huko Zanzibar:

Wakati mmoja nilikuwa kizuizini na nilikuwa na dalili za kujitenga na dawa za kulevya–kuendesha, kutapika. Polisi hawakujali, waliniacha katika seli ya kawaida. Nilikuwa nikilia, "Nipelekeni msalani!" Wangeweza kuniruhusu kwenda msalani mara moja tu kwa usiku. Hivyo nililazimika kujisaidia katika seli. [121]

Wanawake kadhaa waliohojiwa katika kituo cha kuwatibu watumiaji wa dawa za kulevya huko Zanzibar walisema kuwa walikuwa pia wamewahi kupigwa na polisi. Sharifa Z. alipigwa alipokuwa amezuiliwa na polisi katika kituo cha polisi cha Ngambo mwaka wa 2011, kama adhabu kwa kutapika kama sehemu ya dalili yake ya kujitenga na dawa za kulevya: "Nilikuwa nikitapika kwa sababu ya kujitenga na dawa za kulevya, hivyo walikasirika na kunipiga kidogo." [122] Polisi walimpiga Suhayla F., mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka 23, katikati ya mwaka wa 2012 kwa kutumia heroini. Suhayla alikumbuka, "Polisi mmoja aliwaambia wenzake 'Yeye ni mjamzito, usimpige,' lakini mwenzake alinipiga mgongoni." [123]

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM) pia wanakabiliwa na vurugu kutoka kwa polisi, hasa jijini Dar es Salaam, ambapo wao huwa wazi kidogo zaidi na hivyo kutambulika. Saidi A. ambaye kisa chake kimeelezwa katika Sehemu ya II, hapo juu, alitishiwa na polisi kwamba angempiga risasi na kulazimishwa kuita marafiki zake MSM. Polisi waliwapiga kwa mikanda, wakavuliwa nguo na kuwadhalilisha huku wakibakwa mara kadhaa wakiwa katika stesheni ya polisi.

Collins A., mwanamume gay huko Tandika, alikamatwa na kupigwa kwa kujaribu kuandaa semina juu ya masuala ya afya kwa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM), ambayo alitumaini ingekuwa hatua ya kwanza katika kuanzisha shirika la MSM katika ujirani wake:

Nilimwomba Msimamizi [warden] wa Tandika ruhusa ya kuandaa semina. Tulijitokeza wazi, kuomba kuandaa semina kwa MSM. Msimamizi aliwaita polisi. Polisi walikuja na kunikamata katika ofisi ya Msimamizi. Walinipiga makofi usoni na kunipeleka katika seli ya polisi. Walinizuilia kwa siku mbili katika Stesheni ya Polisi ya Chang’ombe. Waliniambia, “Tunakukamata kwa sababu wewe ni wa jinsia moja." Hawakuniambia haki zangu. Walinitusi walipokuwa wakinihoji, kwa kusema, "Hatuwahitaji nyie watu, hatutaki nyinyi mwishi, hiyo ndiyo sababu tunapigana dhidi yenu." Walinirarulia nguo. Waliichapa miguu yangu kwa kirungu. Nilipata shida ya kutembea baadaye. [124]

Rafiki yake alileta shilingi 12,000 kuwahonga polisi ili wamwachilie Collins. Alipoenda hospitalini kwa kipigo alichopigwa, Collins alikabiliwa na kikwazo kingine:

Nilikwenda hospitalini baadaye kwa sababu nilikuwa katika maumivu kutokana na kipigo. Lakini hospitali ilisema kuwa nilihitaji fomu ya PF3. Nilikwenda katika stesheni kuiulizia, lakini polisi walikataa kunipa fomu ile. Hivyo nililazimika kumhonga daktari ili kutibiwa…. Nilipoteza matumaini kwa wazo la kuunda ushirika. [125]

Huko Arusha, Lester F. mwanamume gay mwenye umri wa miaka 18, alielezea kukamatwa kwake mnamo mwezi wa Oktoba mwaka wa 2012. Alikuwa amefanya kosa la kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume aliyeoa, ambaye mkewe aligundua uhusiano huo:

Tulikuwa katika baa. Mke wake akaja katika baa hiyo akiandamana na kaka yake, ambaye alikuwa polisi na wakatupata hapo. Aliwaita polisi wengine na takriban wanne wakaja na kunikamata.
Walinipiga njia yote kutoka baa hadi garini na hadi katika stesheni ya polisi. Walinipiga kwa virungu na mikanda. Hata waliniambia huenda angenipiga risasi. Nilikuwa na alama za viganja usoni na alama za mikanda mikononi ambapo walinipiga. Nililia sana. [126]

Polisi walimpeleka Lester katika stesheni, ambapo, kwenye ukumbi, polisi wengine waliuliza mbona alikuwa amekamatwa. Walipojulishwa kuwa Lester alikuwa gay, alikumbuka, "Basi, polisi wote walianza kunipiga. Kila polisi ambaye aliyekuwapo alikuwa akinipiga. Baadhi yao walinitusi. Wengine walinisukuma." [127] Lester F. aliachiliwa alipompigia simu mwanajeshi mmoja, ambaye kwa mujibu wa maelezo aliyotoa kwa Human Rights Watch, alikuwa mpenzi wake, ambaye alikuja kituoni na kuingilia kati.

Mariam H., mfanyakazi wa ngono, alisema polisi katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam walimweka kizuizini na kumpiga mapema mwaka wa 2012 baada ya kumshika mitaani. Yeye alilipa hongo ya shilingi 30,000 ili kuachiliwa. Siku kadhaa baadaye, aliamua kuripoti kupigwa kwake katika stesheni ya polisi ya karibu:

Nilijaribu kwenda na kuwaripoti. Ilikuwa siku mbili baadaye, wakati nilihisi nguvu za kutosha kuondoka nyumbani. Polisi walidanganya na walisema kwamba nilikuwa nimepigwa na watu [raia]. Walisingizia kuwa nawezakana kwamba ni kwa sababu mimi ni mwizi au mfanyakazi wa ngono. Walikuwa wameniumiza kimwili, na hakuna popote ambapo ni halali kisheria kwa polisi kuwadhulumu kimwili “wahalifu.” [128]

Ushambulizi  na Unyanyasaji   wa Kingono kutoka kwa Polisi

Aina moja maalum ya dhuluma ambazo polisi walitekeleza dhidi ya makundi maalum ni dhuluma za kingono, ambazo zinaweza kuwa aina ya mateso au ukatili, unyama na matendo ya udhalilishaji.

Walid A., MSM mwenye umri wa miaka 19 kutoka Zanzibar ambaye wakati mwingine hufanya kazi ya ngono, alibakwa na polisi pamoja na polisi Jamii akiwa njiani kuelekea nyumbani kutoka kilabuni katika mwaka wa 2011. Alisema,

Wana paipu za maji na nyaya za umeme. Walinipiga kwazo. Walinilazimisha kufanya ngono nao. Watano au sita kati yao walikuja [kunikamata] na wawili kunibaka. Walikuwa na mikongojo na paipu na walinipiga katika nyayo zangu. Sikuweza kutembea baadaye. Sikwenda hospitalini baadaye kwa sababu wao hunyanyasa watu huko. [129]

Human Rights Watch liliona makovu kwenye miguu ya Walid yaliyowiana na kupigwa na nyaya za umeme.

Alex N., mwanaume aliyebadili jinsia yake, alidhulumiwa kingono na polisi katika Stesheni ya Polisi ya Buguruni jijini Dar es Salaam mnamo mwaka wa 2009 alipokuwa na umri wa miaka 18. Meneja katika baa ambapo alifanya kazi na ambaye alimtuhumu kuwa msagaji na mwenye "mwelekeo mbaya," alimpeleka kwa polisi. Alex alisema kuwa wakati alipowasili katika stesheni ya polisi, polisi walimwambia avue nguo zake na wakashika matiti na uke wake. Walimpiga mikononi na mgongoni kisha wakamlazimisha kuvaa mavazi ya wanawake na kusafisha stesheni ya polisi. Aliachiliwa baada ya siku sita na kusema, "Sikuwasilisha malalamiko. Nilikuwa na hofu." [130]

Jessie L., mfanyakazi wa ngono na mwanamke aliyebadilisha jinsia yake, ambaye kibayolojia ni mwanamume lakini huonekana kama mwanamke alisema alikuwa amekamatwa na polisi zaidi ya mara 10 kwa ajili ya kazi ya ngono. Na mara moja au zaidi, polisi walimdhulumu kingono:

Mimi kawaida huwaambia ukweli. Kwa hiyo polisi hushangaa. "Wewe ni shoga? Hapana, wewe ni mwanamke." Kwa hiyo hawanipigi. Wao hunichukua katika chumba maalum na kunichunguza. Wao huniweka katika chumba maalum bila wanawake wala wanaume. Wao huwaita watu wote kuja kuniona—maafisa wa polisi wa kike na wa kiume. Wao huitana, “Njoo, njoo! Mwaangalie shoga huyu!” Nao huniuliza maswali zaidi. "Ulianza vipi kufanya ngono ya mkundu? Wewe huhisi vipi unapofirwa?" Kwa kawaida wao hunilazimisha kuvua nguo zangu nami huwa sina budi, hivyo hukubaliana nao.
Polisi kamwe hawakunilazimisha kufanya ngono nao ili kuniachilia. Lakini waliwahi kunishikashika, wakinitania na kufinya matiti yangu ya bandia. Walisema "Tuonyeshe jinsi wewe humshughulikia mpenzi wako, wakati unafanya ngono, huwaje." Nilikataa. Lakini walikuwa wakinishika, "Je, kweli wewe ni mwanamke?" Walinishika kila mahali. Waliniuliza, "Je una uke?" na wakashika uume wangu. [131]

Kati ya watu 66 tuliowahoji ambao walikuwa katika au awali waliwahi kushiriki katika biashara ya ngono – wanaume, wanawake na watoto – angalau 23 walisema polisi walikuwa wamewalazimisha kufanya ngono nao. Watano kati ya waathiriwa hao walikuwa watoto. Wanawake ambao hutumia dawa za kulevya pia walisema walilazimishwa kufanya ngono na polisi ili kuachiliwa kutoka kizuizini. Baadhi ya polisi wanakataa kutumia kondomu na kuwafanya polisi kuwa na uwezekano wa njia ya  maambukizi ya VVU na magonjwa mengine ya zinaa. Matendo yote ya ngono ya kulazimishwa hujumuisha ubakaji.

Halima Y. alibakwa na genge la maafisa wa polisi wanane mnamo Machi 2013. Alieleza,

Ki ukweli, kufanya ngono na polisi, mara nyingi, hata sikumbuki…. Ananikamata, anataka hela, hela sina kwa hiyo ananiforce [ananilazimisha]. Sikukuu ya pasaka [2013], polisi watatu walinikamata, wakataka hela. Hela nilikuwa sina. Nikawapa rushwa ya ngono. Wakaja watatu tena wengine, nikawapa rushwa ya ngono. Wakaja wengine wawili, nikawapa ngono. Niliumwa… nikapata UTI juu hadi na gono [kisonono] nilipata. Hapa natumia dawa. [132]

Amanda Z., mfanyakazi wa ngono wa kike jijini Dar es Salaam, alisema polisi walikuwa wamemlazimisha kufanya ngono nao bila kondomu mara mbili, kisa cha hivi karibuni kikiwa mapema mwaka wa 2013:

[Katika visa vyote viwili,] hawatumii condom na mi sikuwaambia chochote kwa sababu nilitaka kuachiliwa na kwenda nyumbani kwa watoto wangu. Kama lazima nifanye ngono isiyo salama ili niachiliwe basi mimi hufanya hivyo, natoka. [133]

Ramazani H., mfanyakazi wa ngono wa kiume mwenye umri wa miaka 22 jijini Dar es Salaam, alikamatwa mitaani angalau mara nne. Mara mbili za kwanza, polisi walimpiga kwa viboko na  kumwitisha rushwa. Mara ya tatu, alisema,

Polisi wawili walinikamata huko Kariakoo. Walinipiga tena na kunipeleka katika Stesheni ya Polisi. Nilishinda usiku mmoja huko. Walinilazimisha kufanya ngono nao, lakini nilikataa, kwa hivyo wakasema "Kama umekataa, basi nyonya mboo zetu." Kwa hiyo nilinyonya mboo zao nje ya stesheni ya polisi.

Bado Ramazani alilazimika kulipa shilingi 30,000 ili kuachiliwa huru. [134]

Wilson N., mfanyakazi wa ngono wa zamani jijini Dar es Salaam, alisema kuwa kwenye matukio mawili, katika mwaka wa 2009 na 2011, polisi walimtia mbaroni wakati alikuwa akifanya kazi ya ngono na kumlazimisha kufanya ngono nao. Mara ya kwanza, maafisa wawili wa polisi walimpeleka katika Kituo cha Polisi cha Keko na kusisitiza kufanya ngono nao bila kondomu, kisha wakamlazimisha kulala katika jela usiku huo. Katika tukio la pili, Wilson alikumbuka:

Nilipita karibu na Kituo cha polisi cha Tandika na afisa wa polisi akaniita. Nilikuwa nimevalia nguo za wanawake. Alisema, "Wewe unazurura na kutafuta wateja. Kama unataka nikuachilie huru, huna budi kufanya ngono nami." Niliamua kufanya ngono naye. Alitumia kondomu na kilainisho cha mafuta. Alitaka kufanya haraka kwa sababu alikuwa na hofu ya maafisa wengine wa polisi kuja…. Tulifanya tendo hilo katika choo cha kituo cha polisi.[135]

Ubakaji na Hujuma kwa Watoto kutoka kwa Polisi

Baadhi ya kesi mbaya zaidi za dhuluma zinazofanywa na polisi dhidi ya makundi maalum zinawahusu watoto, haswa watoto wale wanaoshiriki katika biashara ya ngono. Polisi wanawabaka, wanawadhulumu kingono na kuwapiga watoto wanaoshiriki katika biashara ya ngono bila kujali sheria. Dhuluma kingono dhidi ya watoto ni hatia mbaya sana katika nchi ya Tanzania, kwa hiyo polisi wanapaswa kuchunguzwa na kushtakiwa.Watoto wale wanaoshiriki katika biashara ya ngono kamwe hawapaswi kukamatwa na kushtakiwa kwa kushiriki katika biashara ya ngono, bali wanapaswa kusaidiwa vilivyo.

Kama ilivyoelezwa katika Sehemu ya 1, maafisa wengi wa polisi kule Tunduma walimbaka Rosemary I. mara mbili alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili. Maafisa wa polisi watatu vilevile walimbaka msichana mwengine kwa jina Alamisi V. aliyehusika katika biashara ya ngono, baada ya kumkamata katika kituo cha malori cha Magorofani kule Mbeya wakati wa Pasaka katika mwaka wa 2011. Alikuwa na umri wa miaka 14. [136]

Mnamo Julai 2012, polisi wawili walimzuilia Jenifer A. kwa kuhusika na biashara ya ngono kule Mbeya. Alikuwa na umri wa miaka 16. Walimpeleka katika Stesheni ya Polisi ya CCM, wakambaka, wakampiga mateke akilala chini nje ya stesheni. Alisema kwamba walipokuwa wakimpiga “Waliniambia kwamba sipaswi kuenda kwenye baa kufanya mapenzi.” [137]

Kufanya mapenzi na polisi hakutamzuia mtu kushikwa na polisi. Khadija J. mwenye umri wa miaka 16 alioko Mbeya, amebakwa na polisi mara nane au zaidi katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu alipokuwa akifanya biashara ya ngono. Mara mbili polisi walimpeleka makwao na wakamlazimisha kukaa nao usiku mzima. Lakini, alisema, “Mara hizo mbili walifanya mapenzi nami na baadaye asubuhi wakanipeleka katika Stesheni ya Polisi ya Central. Ilinibidi ningojee hadi niwapigie marafiki zangu na wakalipa hela ili niachiliwe. Walilazimika kutoa shilingi 30,000 au 40,000.” [138]

Wakati mwingine, Khadija alijaribu kumkataza polisi mmoja kufanya mapenzi naye bila mafanikio: “Baada ya kunipiga ngumi kwenye jicho na kunipiga kofi, ilikuwa lazima nikubali.” [139]

Kwa sababu biashara ya ngono ni haramu, watoto na watu wazima kwa jumla wanalazimika kufanya mapenzi na polisi wakikamatwa hata kama hawafanyi kazi ya ngono wanapokamatwa, hasa katika miji midogo zaidi ambapo wafanyakazi wa ngono wanajulikana kwa urahisi. Adimu S., msichana mwenye umri wa miaka 16 na anayeishi Mbeya, alieleza, “Wakati mwingine, wakikukamata kwa mara ya kwanza, wanafanya mapenzi nawe au unawapa pesa. Halafu wanakujua na wanakutumia tena kwa ngono, hata wasipokukamata ukifanya kazi ya ngono. Wanakutisha kwamba watakupeleka kwenye stesheni. [140] Hali hii inaelezea sababu inayowafanya watoto wanaodhulumiwa katika kazi ya ngono pamoja na watu wazima, hawataki kupeleka malalamiko yao kwa polisi, hata kama mkosaji ni raia (maelezo zaidi katika Sehemu VI); watatambuliwa na wataweza kudhulumiwa katika siku zijazo.

Pamoja na kukiukwa kingono, polisi vilevile waliwadhulumu watoto kimwili. Rosemary I. alisema kwamba alipokuwa na umri wa miaka 13, afisa wa polisi alimchoma mkononi kwa kiberiti [cha chuma], akimwuliza, “Unajiuza kwa nini?” [141]

Ruby C., msichana mwenye umri wa miaka 17 na anayefanya kazi ya ngono katika mji wa Mwanza mnamo Oktoba 2012 aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO kwamba alipigwa na polisi katika wiki iliyotangulia nje ya hoteli moja iitwayo Villa:

Kulikuwa na maafisi wa polisi watatu walionishtaki kwa kujiuza. Polisi walinilazimisha kupiga magoti na wakaanza kunipiga. Walinipiga mateke kwa viatu vyao vikubwa. Walinipiga mgongoni kwa rungu zao ambazo wao hubeba kwa kawaida. Nilikuwa na maumivu – nilifura. Sikuenda hospitalini nilipotoka kwa sababu sikuwa na pesa. Sikuenda kuripoti kwa sababu niliogopa kwamba polisi wangenipiga tena. [142]

Mtoto mwengine anayerandaranda mitaani na anayehusika katika biashara ya ngono kwa jina Bishara A. mwenye umri wa miaka 16, alisema kuwa maafisa wa polisi watatu walimsimamisha barabarani na wakampiga kule Mwanza katika mwaka wa 2011.

Polisi waliniuliza, “Unafanya nini?”, kwa sababu ilikuwa usiku. Niliwaambia, “Ninalala hapa.” Walianza kudai  kwamba mimi ni mfanyabiashara wa ngono na wakanipiga. Walinipeleka katika Stesheni ya Polisi ya Kati. Katika stesheni walinichapa kwa tyubu iliyotengenezwa kwa mpira kutoka kwenye tairi ya gari. Waliniambia kuwa nilale chini na wakanichapa kwenye makalio.

Polisi walimlazimisha awape hongo ya shilingi 30,000 ili kumwachilia. Kwa kuwa Bishara hangeweza kumudu kiasi hiki cha fedha, afisa wa kike aliyesimamia stesheni hii, aliamuru aachiliwe siku mbili baadaye. [143]

Unyang’anyi wa Pesa

Polisi wakikosa kudai ngono kutoka kwa makundi haya ya watu walioko katika hatari, mara nyingi hudai pesa. Harun Z., mwanaume anayetumia heroini kule Temeke, aliongea kuhusu kulazimishwa kutoa pesa na polisi kama jambo la kawaida katika maisha ya kila siku:

Nimekumbana nalo sana katika vituo vidogo vya polisi, Kilimahewa, Vianiza, Tandika. Wanaomba kiasi cha pesa kulingana na jinsi unavyoonekana. Ukivaa kifahari wanaomba shilingi 50,000 la sivyo  wanaomba shilingi 10,000 ama 20,000 ama 30,000.[144]

Ilham K., mfanyabiashara wa ngono Dar es Salaam, alienda na mteja katika nyumba ya wageni katika mwaka wa 2011. Mteja yule alikataa kutumia kondomu. Aliposisitiza kwamba ni lazima atumie kondomu, mteja alianza kumsukuma kwa fujo. Ilham aliomba usaidizi na wafanyakazi wa nyumba ile wakaja chumbani. Mteja yule alidai kuwa amemwibia kisha akampeleka katika Stesheni ya Polisi ya Oysterbay. Polisi walimhurumia Ilham baada ya kuwasimulia kisa chake, ila bado walimzuilia na wakalazimisha kuhongwa: kulingana na Ilham, dadake alipokuja katika stesheni asubuhi, “Polisi walimwambia, “Tunajua kuwa dadako hajafanya chochote, lakini mwanaume huyu anashinikiza, kwa hiyo tutasubiri mpaka mwanaume huyu aende halafu wewe na dadako mnaweza kuenda, lakini ni lazima ulipe shilingi 20,000. [145]

Evelyn D. alikamatwa karibu na mwisho wa mwaka wa 2011 akijiandaa kujidunga heroini. Alisema, “Katika stesheni ya polisi nilitukanwa na polisi hasa maanake nilikuwa mwanamke. Walisema maneno kama, ‘Wewe ni mwanamke mjinga. Wewe ni malaya!’” Evelyn aliachiliwa usiku ule ule baada ya mpenzi wake wa kuwaletea polisi shilingi 20,000 hela za Tanzania. [146]

Edwin J., mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume (MSM), alilazimika kutoa hongo ya shilingi 30,000 kwa maafisa kutoka katika Kituo cha Polisi cha Kongwe katika Dar es Salaam mnamo Jan. 2012, baada ya mhudumu katika nyumba ya wageni kuwapigia polisi na kuripoti kuwa kulikuwa na “mashoga” katika chumba kimoja. [147]

Kulazimishwa kutoa pesa ama kulazimishwa kufanya mapenzi, hufanyika hata kama watu walioko katika makundi maalum hawajihusishi katika shughuli yoyote haramu. Henry O., mwanaume katika mji wa Mwanza anayetumia madawa ya kulevya, alifafanua: “Polisi hawa, wananijua vyema sana na nimekuwa mtu wa kutoa hela kwao. Kawaida mimi huwapa kati ya shilingi 10,000 na 20,000 kutegemea siku. Wakati mwingine wao hunipiga na wakati mwingine hawanipigi.” [148]

Kulazimishwa kutoa pesa au kufanya mapenzi si uhalifu tu. Inasababisha kukosa imani kati ya wale walioko katika makundi maalum na maafisa wa usalama. Kulingana na Ilham K., mfanyabiashara wa ngono kule Dar es Salaam:

Shida ya polisi ni pesa. Wanataka tu pesa na wanajua kwamba wafanyabiashara wa ngono wana pesa. Kwa hiyo hakuna urafiki hapo. (Urafiki) ungekuwa, tungewaomba usaidizi na tungeenda kwao tukikosewa. Lakini tunawaogopa na tunakimbia kutoka kwao.[149]

Kukamatwa Kiholela

Wafanyabiashara wa ngono, wana LGBTI na watumiaji wa dawa za kulevya wote waliripoti kuwa polisi wa Tanzania walikuwa wamewahi kuwakamata. Kundi la Umoja wa Mataifa Kuhusu Kukamatwa Kiholela [UN Working Group on Arbitrary Detention] limepitisha kuwa kukamatwa kwenye msingi wa ngono kati ya watu ya jinsia moja tu ni ya kiholela. [150] Polisi wakiwakamata watu kwa sababu ya biashara ya ngono au utumiaji wa dawa za kulevya, ni wazi kuwa kesi nyingi pia ni za kiholela, zinafanyika bila ushahidi wowote wa matendo yoyote ya kiuhalifu. Katika baadhi ya kukamatwa huku  kunahusu polisi kuwalazimisha waathiriwa kutoa pesa au kufanya mapenzi.

Mohammed R. na rafiki yake walikamatwa kule Dar es Salaam na wakazuiliwa na polisi “kwa kutembea kama wanawake”:

Wakati mmoja nilikuwa sokoni nikinunua vitu na rafiki yangu na kwa ghafla watu walianza kupiga kelele kwa kuwa rafiki yangu alionekana msenge sana. Kwa hiyo tulikimbia kwenye duka la mwanamke mmoja. [Lakini] aliwaita polisi na walitukamata na wakatupeleka katika Stesheni ya Polisi ya Buguruni. Tuliwauliza polisi sababu ya kutushika, lakini polisi walikuwa wakali na wapumbavu. Walituzuilia na wakatuambia kuwa hatia yetu ilikuwa kutembea kama wanawake. Polisi walinipiga baada ya kujaribu kubishana nao na kujitetea, nikisema kuwa sikuhusika katika uhalifu wowote.   

Polisi mmoja alipendekeza asubuhi kuwa Mohammed atoe hela au ngono ili tuachiliwe. Mohammed alikataa kufanya mapenzi naye, lakini akalipa shilingi 30,000 na tukaachiliwa. [151]

Victor G., mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume Dar es Salaam, alisema kuwa alikuwa amezuiliwa mara mbili kwa sababu ya mwenendo wake wa kingono:

Mara ya kwanza ilikuwa katika mwaka wa 2009. Nilikuwa na watu watatu, wote MSM. Tulienda kwenye hosteli ya wanafunzi kumtembelea rafiki. Tulikosana na mwenye hosteli, kwa sababu alikataa kutukubalia kuingia. Aliwaita polisi na akaturipoti kama mashoga. Walikuja na wakatufunga pingu. [Mwenye hosteli] aliwaambia tu kuwa sisi ni mashoga, hakutushtaki kwa uhalifu mwingine wowote. Polisi mmoja wa kike alituhurumia, kwa sababu tulikuwa wadogo na tulikuwa na vitambulisho vya chuo. Tuliondoka bila kutoa hongo.

Wakati mwingine, Victor alisema kuwa polisi walimkamata na marafiki zake barabarani walipokuwa wakirudi nyumbani saa tano unusu usiku kutoka baa na wakawapeleka katika Stesheni Kuu ya Polisi ya Magomeni. Kulingana na Victor, “Walitushtaki kwa ‘uhuni’ kwa sababu tu kuwa MSM. Tulikaa katika stesheni usiku mzima. Shangazi yangu alikuja asubuhi iliyofuata na akawahonga kwa shilling 150,000 ili kunitoa.”[152]

Joseph S. alikamatwa kwa kumbusu mpenzi wake wa kiume barabarani wakitembea wakielekea nyumbani kutoka baa katika mwaka wa 2010. Polisi waliwalazimisha Joseph na mpenzi wake kuingia ndani ya gari la polisi. Wakiwa ndani ya gari,

Walitupiga, walitupiga mateke, walisema kwamba wangetupiga picha na tuliogopa kwamba wangetuweka katika ukurasa wa mbele kwenye magazeti. Lakini hawakupiga picha. Walikuwa wakitutusi, wakituita “mbwa jike.”[153]

Polisi walimlazimisha Joseph na mpenzi wake kulipa shilingi 10,000kama hongo ili kuachiliwa.

Hussein M. alipelekwa kwa polisi na familia yake alipokuwa na umri wa miaka 16 katika mwaka wa 2007, familia yake ilipogundua kwamba alikuwa gay. Mjomba wake alimpiga kisha akampeleka katika Stesheni ya Polisi ya Minazini katika jiji la Dar es Salaam. Hussein hana hakika kuhusu kile mjomba wake aliwaambia polisi, lakini aliachiliwa bila kuhojiwa baada ya kuzuiliwa kwa siku mbili. Aliporejea nyumbani, wazazi wake walisema kuwa hawangelimlipia karo tena hatua iliyokuwa kama adhabu kwa ushoga wake, kwa hiyo Hussein kwa upande wake, alienda kwa polisi kuwaripoti wazazi wake kwa kutomjali.

Polisi waliwaita kwenye stesheni wazazi wa Hussein, lakini ni mjomba wake ndiye alienda kujadiliana na polisi juu ya kesi ile. Kwa mujibu wa Hussein,

Wakati huu mjomba wangu alimwambia [afisa wa polisi], “Jamaa huyu         anafanya mapenzi na wanaume wengine.” Halafu polisi yule alianza kumwunga mkono mjomba wangu. Polisi yule alianza kulalamika, “Kwa nini usiache kufanya hii?” Alinichapa kwa fimbo mara tano kwenye mapaja. Halafu aliniachilia na akamwambia mjomba wangu, “Nenda naye na umchunguze kwa siku mbili. Akiendelea kufanya mapenzi na wanaume, umrudishe tena kwenye stesheni ya polisi.”

Hussein alienda nyumbani, lakini familia yake ilimfukuza baada ya wiki moja. Alisema, “Mpaka wa leo ninaishi na marafiki, na wazazi wangu wamekataa kunilipia karo maanake mimi ni MSM. [154]

Polisi kule Zanzibar walimzuilia Hamisi K. katika mwaka wa 2009 na wakajaribu kumwangalia kwenye mkundu “kuthibitisha” kuwa alifanya mapenzi na wanaume. Hamisi alielezea:

Tulikuwa kwenye karamu. Polisi walipata taarifa na wakaja. Walisema wanaume walikuwa wanaolewa.  Walifikiria kuwa ilikuwa harusi, ila ilikuwa karamu tu. Hata walitupeleka katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kutupima kwa ngono ya mkundu, kutuchunguza kwenye mkundu. Lakini daktari alikataa kutupima [155] .

Hayat E. ni mtu mwenye jinsia mbili na anayejitambulisha kama mwanamke. Anaishi Dar es Salaam. Amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume kwa wanawake, lakini amewahi kudhulumiwa mara nyingi na wapenzi wake wa kiume baada ya kugundua kwamba ana sehemu za siri za kiume na kike. Kwa bahati mbaya, alipojaribu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke, alizuiliwa kiholela:

Mnamo Machi [2012], nilikuwa nikiishi na mwanamke. Nilimhamisha hadi kwangu katika chumba changu nilichokodi na tulifurahi pamoja. Mwakilishi wa serikali ya mtaa aligundua kwamba nilikuwa nikiiishi na mwengine wa kike na walikasirika sana. Mwakilishi yule alienda katika stesheni ya polisi kunisema. Ya kutisha ni kwamba, polisi walilichukulia jambo lile kwa makini sana. Waliniambia kwamba nitoe hongo ya shilingi 350,000 [kama dola 210] ili kuitupilia mbali kesi ile. Polisi pia walitaka nivue nguo zangu na niwaonyeshe mwili wangu ili waone jinsi nilivyoonekana. Hii ilinisumbua sana na niliamua kuhama kutoka chumba kile nilichokuwa nikikodi. Tangu wakati ule, nimeamua kutojaribu kuishi na mtu mwengine yeyote. [156]

Mwajuma P., mwanamke anayejidunga heroini, alikamatwa kwa kuwa na sirinji ambazo hazikuwa zimetumika. Alisaidiwa na mashirika ya kupunguza madhara na yale ya haki za binadamu katika Temeke:

Nilikamatwa na Sungu Sungu wakiwa pamoja na polisi, kama miezi sita iliyopita. Walinishika nyumbani nikiwa na sirinji. Walibisha na nikafungua. Hawakuwa na kibali cha kutafuta. Waliingia na wakapata maboksi matano ya sirinji. Sungu Sungu walinipiga makofi, kwa sababu walinipata tu na maboksi yale. Walinipeleka kwa polisi. Nilituma ujumbe kwa shirika la MDM lililotuma ujumbe kwa Nyerere Centre [for Human Rights] kunitolea dhamana nayo kesi iliishia pale. [157]

IV. Polisi Jamii, Sungu Sungu na Makundi Mengine ya Wanamgambo

Tanzania ina mashirika mengi ya polisi jamii na makundi ya kiusalama yaliyorasmi katika viwango mbali mbali. Lengo la maafisa wa kutekeleza sheria nchini Tanzania ni kushirikiana na makundi ya kiusalama ama wanamgambo kukabiliana na uhalifu. Lakini wanachama katika makundi haya, sawa na polisi wenyewe, wakati mwingine wanatumia dhuluma ya kimwili na kingono pamoja na unyang’anyi dhidi ya wale wanaokabiliwa na tuhuma katika shughuli ya uhalifu.

Baadhi ya makundi haya yamebuniwa kisheria na yana utaratibu rasmi wa mawasiliano na taasisi za nchi zinazotekeleza sheria. [158] Moja kati ya makundi yale ni “Polisi Jamii.”  Kupitia kwa programu rasmi ya kulinda jamii, vikundi hushika doria mtaani mwao na hutoa ripoti kila siku kwa polisi rasmi wa Tanzania. Katika baadhi ya maeneo nchini Tanzania, wakaaji walipongeza kazi yao. Hata hivyo, polisi jamii waliripotiwa kuhusika na idadi kubwa ya ukiukaji wa haki za binadamu katika Zanzibar. [159]

Sungu Sungu

Kundi lenye utata mwingi kabisa ni lile la “Sungu Sungu.” “Sungu Sungu” awali lilirejelea kundi la wanamgambo lililobuniwa ili kukabiliana na wizi wa ng’ombe katika magharibi ya Tanzania katika miaka ya 1980. Kundi hili baadaye lilielekeza nguvu zake katika kukabiliana na “uchawi,” iliyokuwa ishara ya mapema ya uwezo hatari wa kundi hilo kuhudumu kama aina ya polisi ya maadili mema. [160] Katika miaka ya hivi karibuni, jina lile limetumiwa kulirejelea kundi la wanamgambo  lolote linalohudumu mitaani.

Kinadharia, Sungu Sungu linafanya kazi chini ya uongozi wa serikali ya mitaa na polisi, lakini katika maeneo mengine linaonekana kufanya kazi kivyao. Sheria ya Jeshi la Wanamgambo [The People’s Militia Act] ya mwaka wa 1973, iliyobadilishwa katika mwaka wa 1989 ili kulirejelea waziwazi Sungu Sungu, inawapa mamlaka ya kukamata. [161] Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, “Wanachama wa Sungu Sungu hawaruhusiwi kubeba bunduki au panga, ila wanabeba fimbo au marungu.” [162] Lakini utafiti wa Human Rights Watch uligundua kwamba Sungu Sungu mara nyingi wanajihami kwa panga.

Maafisa wengine Dar es Salaam hata wanakanusha kuwa kundi la Sungu Sungu liko. [163] Wakaaji wa Temeke, wilaya yenye watu maskini kabisa Dar es Salaam, wanajua vinginevyo. Katika mitaa yenye umaskini mwingi na iliyoko kando kando au mbali na mji, wanachama wa Sungu Sungu – wasiolipwa vizuri, wasio na ujuzi wowote na kulingana na wakaaji hata wana rekodi ya uhalifu – hushika doria mitaani usiku wakiwa na panga na rungu na hivyo vyote kwa pamoja vinaweza kuchochea ukiukaji wa haki za binadamu. [164] Pamoja na kuzuia uhalifu kamili wakati mwingine pia wanachukua jukumu la kuangalia maadili wakiwalenga hasa wanaofanya kazi ya ngono na watumizi wa dawa za kulevya.

Wakaaji wa Temeke wanasema kuwa wanachama wa Sungu Sungu walimwua Abdallah Yunus (jina lake kamili), mwenye umri wa miaka 34 almaarufu “Dula,” na mwanaume mwengine aliyejulikana kama Abdallah pia mnamo Aprili mwaka wa 2012. Kulingana na majirani zao Dula na Abdallah wote walitumia heroini. Dula alikuwa akiishi kwa Abdallah. Mwanamke aliyeishi nao anakumbuka alivyoamshwa usiku wa manane na umati.

Walisema “Mwizi! Mwizi!” Walipigapiga milango wakiuliza, “Dula yuko wapi?” Sijui kama waliwataka Abdallah wote wawili au mmoja wao. Nilijua kwamba walikuwa Sungu Sungu kwa sababu walikuwa zaidi ya 50 na hakuna kama wao. Watu hawakuchukua hatua yoyote ili kuwakomesha. [165]

Mwengine aliyeshuhudia Dula akipigwa na watu waliojihami kwa mawe, panga na matofali ya saruji. Alielezea,

Kuna Sungu Sungu kutoka katika maeneo mawili. Sungu Sungu kutoka eneo hili walienda wakasema, “Mnawadhulumu watu hawa kwa nini?” Wale wengine kutoka eneo tofauti walikuwa watu 50, ilhali wanaotoka katika eneo hili walikuwa 7 au 8 tu. Ninajua kwamba wao ni Sungu Sungu kwa sababu wao hushika doria mara nyingi katika vikundi vya watu 40 au 50. Wao  hushika doria kila usiku.
Walikuja na watu wawili. Walitupa mmoja pale. Wote wawili walikuwa hai, ingawa mmoja alikuwa amepigwa. Alianguka. Alikuwa amepigwa kwa na mawe, na alikufa. Sikuona akipigwa, kwa sababu walikuwa wametoka pembeni. Wa pili alikimbia. Walimkimbiza, wakamkamata, wakampiga kwa mawe, fimbo na panga.
Baadaye walisimamisha pikipiki…. wakaizingira kwa panga. Walifungua paipu kutoka kwenye tangi na wakatia petroli kwenye chupa ya maji. Kisha wakatia tairi kwenye vifua vya wanaume wale wawili. Wakawamwagia petroli na kuwachoma. Tayari walikuwa wanaonekana kama wameaga.

Shahidi yule alisema kuwa polisi walikuja kama saa tisa usiku:

Walikuwa na mmoja ndani ya gari aliyekuwa amekamatwa [kuhusiana na kesi tofauti]. Walimwambia aiweke mili ile katika gari. Sijui walikuwa wametoka katika stesheni gani. Ni lazima polisi walikuwa amefahamishwa juu ya kilichotokea. Hawakurudi kufanya uchunguzi. Hawakuwauliza wakaaji juu ya kisa kile. [166]

Kulingana na mamake Dula:

Baada ya siku tatu familia yetu ilienda kuuliza katika Stesheni ya Polisi ya Chang’ombe juu ya uchunguzi, lakini afisa anayesimamia upelelezi alikataa kutupokea. Alisema, “Unasema kwamba walikuwa Sungu Sungu, lakini walikuwa magaidi utajuaje?” Kaka yake Dula aliuliza, “Kama walikuwa magaidi, mbona huwakamatwi?” Polisi walisema, “Unatusumbua”…. Tulipokosa kupata usaidizi kutoka kwa polisi, tulikata tamaa. [167]

Ingawa iliripotiwa kwamba Sungu Sungu walipiga mayowe wakisema, “Mwizi! Mwizi!” walipokuwa wakimteka Dula, mamake hakujua kuhusu kesi yoyote maalum ambayo Dula alishtakiwa kwa wizi:

Sielewi sababu yao yakumwua. Sijawahi kupata habari kwamba aliiba chochote. Wote Abdallah na Dula walikuwa wakitumia madawa ya kulevya.  Dula alikuwa mpole na hakupigana na watu; labda dawa za kulevya tu ndiyo  ilikuwa shida. [168]

Disemba mwaka wa 2012, shirika la Human Rights Watch lilipokea taarifa kutoka kwa wafanyakazi wa shirika la Médecins du Monde wanaoenda nje la kituo  kuwa mwanaume anayejulikana kama Maliki alikuwa ameuawa na Sungu Sungu katika Temeke. Kwa mujibu wa wafanyakazi wa MdM, kuna watu walioshuhudia Sungu Sungu wakimteka Maliki kutoka katika maskani aliyotumia dawa za kulevya na kumkata kwa panga hadi akafa. [169]

Rashid E. alikamatwa Temeke na Sungu Sungu walipokuwa wakipita naye alikuwa ameketi nje mtaani akila chipsi, kama Disemba 2011:

Nafikiri wanajua kwamba ninatumia dawa za kulevya maanake wanatoka katika eneo sawa na mimi. Walikuja tu na kunishika na wakaanza kunipiga. Walinipiga kwa panga, vyuma vya dirisha na fimbo. Nina kidole kisichoweza kukunjika toka siku ile walinipiga mikononi kwa vyuma. Kidole kilifura na kuwa cheusi.

Sungu Sungu walimpeleka Rashid katika Kituo cha Polisi cha Vyaniza, ambapo polisi alimshtaki kwa kuwa mwizi. Siku iliyofuata, rafiki yake alikuja kulipa hongo ya shilingi 7,000 na Rashid aliachiliwa. [170]

Sungu Sungu walimbaka Mwanahamisi K. mnamo Mei 2012 karibu na maskani ambapo alihojiwa na shirika la Human Rights Watch.

Nilikuwa nimekuja hapa kuvuta [heroini]. Nilikuwa nikirudi nyumbani nilipokutana na Sungu Sungu kwenye reli. Ilikuwa saa sita au saba usiku. Waliuliza, “Unatoka wapi, na unaenda wapi?” Niliwaambia, lakini walikataa kuelewa. Walikuwa na panga. Nilipiga nduru lakini sikusaidiwa na yeyote. Ilikuwa usiku, kwa hiyo hakuna aliyepitia pale.
Sita kati yao walinilazimu kufanya mapenzi nao. Wote sita walinibaka wakaniacha kule. Hawakutumia kondomu. Ubakaji ulichukua muda wa saa moja au mbili. Nilikuwa na mtoto wangu. Mwanangu alikuwa akilala chini kando nikibakwa. Baada ya kinibaka, waliniambia “Usizurure usiku.” [171]

Asubuhi, Mwanahamisi alienda kwenye Kituo cha Polisi cha Mashini ya Maji kulalamika, lakini polisi walikataa kumsaidia ila kama angewalipa shillingi 10,000, kwa hiyo alienda nyumbani. [172]

Wafanyakazi wa ngono katika Dar es Salaam vilevile waliripoti kuwa Sungu Sungu waliwafanyia dhuluma ya kimwili na ya kingono. Mfanyabiashara wa ngono mmoja katika Wilaya ya Kinondoni alisema, “Tunalazimika kujificha kutoka kwao. Wakijua kwamba fulani anafanya biashara ya ngono, wanawapiga.” [173] Kwa mujibu wa mfanyabiashara wa ngono mwengine wa kike,

Sungu Sungu katika eneo ninaloishi ni wakali. Wakikuona ukirejea kutoka kazini au ukifanya kazi usiku wa manane wanakulazimu kushika doria nao. Shida moja tu katika jambo hili ni kuwa wanahisi kwamba wana haki ya kukushika wakati wowote wanapotaka. [174]

Vile vile iliripotiwa kuwa Sungu Sungu wapo katika maeneo ya Mbeya na Arusha. Katika Mbeya, wanafanyakazi wa ngono watatu waliliambia shirika la Human Rights kuwa walikuwa wamepigwa na Sungu Sungu. [175] Katika Arusha, mwanaharakati wa kijamii anayefanya kazi ya kuwarekebisha watumiaji wa madawa ya kulevya alisema kuwa Sungu Sungu wanatumia vurugu hata wakati hakuna uhalifu ambao umetokea, kwa kisingizio kuwa hii kuzuia uhalifu: “Usiku, wanazunguka. Wakikutana na watumiaji wa dawa za kulevya wanawapiga kwa sababu wanafikiria kuwa wataiba kitu. [176]

Polisi Jamii

Kama ilivyotajwa hapo awali, polisi jamii ni kitengo rasmi katika miradi ya ulinzi wa jamii. Baadhi ya Watanzania walisema mambo mazuri juu ya polisi jamii. Kwa Mwanza, mwakilishi wa shirika moja lisilo ka serikali lifanyalo kazi Mwanza, aliyaambia mashirika la Human Rights Watch na WASO kuwa polisi jamii waliyasaidia mashirika yasiyo ya serikali katika kazi zao na watoto wanaozurura mitaani. Waliwapeleka watoto wale katika mashirika yasiyo ya serikali yanayowasaidia. [177]

Katika Zanzibar, hata hivyo, polisi jamii walikashifiwa vikali mara nyingi. Mfanyakazi mmoja wa kituo cha kuwarekebisha watumiaji wa dawa za kulevya aliyetumwa nje ya kituo, aliliambia Human Rights Watch kwamba polisi jamii—ambao husafiri katika kundi pamoja na polisi rasmi mmoja – walikuwa changamoto kwa  kazi yao nje ya kituo.

Tukienda mahali kujaribu kuwashauri watu, tunafika pahali na watu wakatoweka kwa sababu polisi jamii wanakuja na kuwapiga. Wakikushika ukivuta (heroini), wanakupeleka kwa polisi au wanakupiga. Hata wakati mwingine wanawaumiza vibaya. Wanatumia mijeledi, mikanda, au mkia wa taa. Wakati mwingine wanawapiga bila kujua watu walio na VVU au kifua kikuu au hepatitisi. Imeripotiwa mara nyingi. [178]

Mwenzake aliongezea kuwa, “Wanafikiria kwamba wako juu ya sheria.” [179]

Idris Z. ni miongoni mwa wale waliowahi kukumbana na unyama mikononi mwa polisi jamii, wakishirikiana na polisi wa kawaida. Alielezea jinsi karibu na mwisho wa 2011, polisi jamii walimkamata akilala nje ya pahali watumiaji wa dawa za kulevya walipenda kuzuru wakampeleka katika Stesheni ya Polisi ya Jangombe.

Polisi jamii walisema, “Tulimkamata kwa sababu analala nje kila mara na yeye huiba.” Polisi jamii [waliwaambia] polisi wa kawaida, “Tupe watu hawa.” Polisi wa kawaida walikubali.
Polisi jamii waliturudisha mtaani. Wakatupeleka uwanjani wakatupiga. Wakachukua upupu wakatupaka ili mili yetu ituwashe. Baadaye walituambia tuende nyumbani. Walicheka kwa sababu walifurahi kumtesa mtu haswa teja. [180]

Mwanaharakati mmoja wa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume alilalamika kuwa alikuwa amepigwa na polisi jamii katika jiji la Dar es Salaam – hata hivyo haikuwa wazi kama waliotenda kosa lile walikuwa wana polisi jamii au Sungu Sungu:

Mwaka jana mimi na mpenzi wangu wa kiume tulikuwa tumeketi mahali tukiongea. Polisi jamii walikuja, wanawasaidia polisi. Tulikuwa tukidhani ni Sungu Sungu. Walisema, “Unafanya nini hapa na huyu bwana? Mnafanya mapenzi?” Tulisema, “Hapana, tunaongea tu.” [Mmoja wao] alisema, “Sawa, wapeleke wafungwe.”
Mpenzi wangu alipata nafasi akatoroka mbio. Walinifunga mikono kwa kamba nyuma yangu. Sikuweza kufanya chochote. Walinipeleka mahali wakanifungua mikono wakanilazimu kuinama. Wakaanza kunipiga kwa waya, waya wa umeme. Waliniumiza vibaya. Walinipiga kwenye mgongo na makalio. Nilipiga kite kwa kusema  “Mnaniumiza,  tafadhali.” [181]

Mwanaharakati yule mwishowe aliweza kutoroka akaenda kwa polisi wa kawaida kuripoti kisa kile, lakini hakukuwa na ufuatiliaji uliofanywa na polisi licha ya ahadi zao za kufanya uchunguzi. Alihitimisha, “Walionipiga wanawachukia wasenge – hiyo ndiyo sababu walinipiga. [182]

Kwa kukosa kuchunguza uhalifu kama ule au kwa kuutia moyo, kama katika kesi ya Idris iliyoelezwa hapo awali, polisi wa kawaida mara nyingi wanakula njama katika ukiukaji unaofanywa na polisi jamiina makundi ya usalama. Mtu mmoja aliripoti kuwa polisi walijaribu kuzuia ukiukaji wa polisi jamii. Ally H. alikamatwa nyumbani mwake mnamo Septemba 2012 kwa tuhuma za kuuza dawa za kulevya na polisi sita kutoka Kituo cha Polisi cha Kilimahewa wakiwa pamoja na mpelelezi  mmoja kutoka polisi jamii:

Polisi jamii alianza kunipiga. Polisi halali walimwambia akome. Na pia mpelelezi  yule alichukua baadhi ya sirinji na maboksi kutoka kwangu, lakini polisi halali walimwambia, “Acha kuchukua hizo, kwa sababu zinatoka pahali pengine [shirika lisilo la serikali].” [183]

Hata hivyo polisi bado walimnyang’anya Ally shilingi 5,000 ili kumwachilia. [184]

V. Ukosefu wa Haki kwa Waathiriwa wa Uhalifu katika Makundi Yaliotengwa

Kama wanachama wa makundi yaliyoko katika hatari wakidhulumiwa na raia wenzao, wanahisi kwamba hawana pa kwenda ili kupata haki, kwa sababu wao wenyewe watachukuliwa kama wahalifu.

Wengi wa wafanyakazi wa ngono waliohojiwa na shirika la Human Rights Watch na WASO wamedhulumiwa na wateja wao lakini katika karibu kesi zote, walisema kuwa hawawezi kupeleka mashtaka makahamani au kwenye polisi. Asha W., msichana mwenye umri wa miaka 15 anayefanya kazi  ya ngono Mbeya alitiliwa dawa na mteja wake kisha akabakwa kwenye uke na mkundu akiwa amepoteza ufahamu. Alikuwa na maumivu kwa siku nyingi. Asha alieleza sababu zake za kutopeleka malalamiko kwa polisi: “Niliogopa, kwa sababu kama ningalienda kwa polisi, ningalilazimika kusema kwamba nilikuwa nikijiuza, na polisi wangesema kuwa nilikuwa nimekubali, na kesi ingishia hapo.” [185]

Mwamini K., anayefanya kazi ya ngono kule Dar es Salaam, alilazimishwa kwa bunduki kufanya ngono na mteja bila kondomu.

Nilisema kwamba sikutaka kuifanya bila kondomu. Ghafla alitoa bunduki na akaielekeza kwangu. Niliendelea kukataa. Mwishowe niliamua kufanya mapenzi bila kondomu…. Nisingeweza kwenda kwa polisi. [186]

Polisi wakati mwingine wanakataa dhahiri kuwasaidia watu walioko katika makundi maalum wakidhulumiwa. Kwa mujibu wa Louisa T., mfanyakazi wa ngono kule Mwanza:

Hatuna haki zozote. Mnamo Septemba nilikuwa nikitoka katika nyumba moja ya wageni. Nilikutana na wanaume wawili barabarani. Mmoja alinishika na akanibeba. Alinibeba huku nikipiga mayowe. Polisi walikuwako. Waliona lakini hawakufanya lolote kwa sababu walijua  nilikuwa mfanyakazi  wa ngono. [187]

Katika kesi nyingine, polisi waliwadhulumu zaidi waathiriwa. Mickdad J. alisema kwamba katika mwezi wa Februari 2012, alipigwa na umati mpaka karibu afe kwa tuhuma za utumiaji wa dawa za kulevya na wizi.

Nilikuwa nikitoka kwa dadangu saa kumi na moja alfajiri. Kulikuwa na sehemu ambako kulichezwa muziki wa kiasili. Kisa kimoja kilitokea ambako mtu aliiba simu. Kwa hiyo walinishuku. Walinizunguka kwa sababu ninatumia dawa za kulevya. Walisema, “Huyo ni yeye,” na walianza kunipiga. Walinipiga kwa mawe kichwani, mgongoni, katika sehemu mbalimbali mwilini. Kisha, walitaka kunichoma kwa tairi. Wengine walienda kuleta mafuta taa ilhali wengine kuleta tairi. Niliyasikia haya na nikapata nguvu kutoka kwa Mungu na nikaanza kukimbia mwenyewe kuelekea Kituo cha Polisi cha Mamboleo.

Nilipofika kule, polisi walikuwa wananijua. Walinijua kama mtumiaji wa dawa za kulevya. Kwa hiyo waliamini kuwa nilikuwa nimeichukua simu ile na wakaanza kunipiga…. Mmoja wao alikuwa akinishika shingoni  kutoka nyuma, mwengine alichukua mshipi akaanza kunipiga. Ulikuwa  mshipi wa mashine ya kusaga [wa kuzungusha mota] —uliniacha na alama yenye upana wa inchi moja. Alinipiga katika sehemu mbalimbali – kichwani, makalio, mguuni – hakuchagua. Nilipigwa hadi nikafura machoni. Nililala katika seli.

Asubuhi, mamake Mickdad aliwahonga polisi ili wamwachilie baadaye aliiripoti kesi kwa shirika la “Médecins du Monde”.  Walimtuma na mwanaharakati wa haki za binadamu kutoka katika Nyerere Centre for Human Rights kuandikisha malalamiko, lakini walipata tu polisi jamii katika stesheni. Alisema;

Tuliuliza kuhusu polisi waliokuwa kazini usiku. Lakini mtu mwengine aliwapigia polisi wale na kusema “Msije, kuna mtumiaji wa dawa za  kulevya hapa pamoja na watu wengine.” Tulirudi saa kumi alasiri na hawakuwa katika stesheni.

Baadaye nilibaki na maumivu kutokana na kupigwa na nikanyamazishwa. Polisi walishindwa kunisaidia. [188]

Watende A. alishtakiwa kwa wizi katika mtaa anaoishi mnamo Machi 2012. Alifuatwa na umati wenye hasira hadi kwenye ofisi ya shirika la “Médecins du Monde”, na wafanyakazi wa shirika MdM waliweza kutuliza ghadhabu yao. [189] Hata hivyo, Watende alisema kuwa siku mbili baadaye, raia walimpata katika maskani akijitayarisha kutumia dawa za kulevya.

Walianza kunipiga kwa panga na fimbo. [Walinipeleka] kwa polisi. Polisi   walisema, “Kwa nini mlimleta akiwa hai? Huyu ndiye mwizi mlikuwa mkiongea juu yake? Mngemwua tu na tungechukua mwili.” [190]

Polisi ndiyo walimpa Watende A. Fomu ya Polisi Number 3 (PF3), inayohitajika na hospitali ya umma waathiriwa wa dhuluma wapate kuwatibu. Hata hivyo, hawakuchukua hatua zozote ili kuwakamata au kuwachunguza waliomdhulumu. Human Rights Watch lilipokutana na Watende miezi mitatu baada ya kisa kile alikuwa na makovu kifuani na mgongoni yaliyofanana na yale ya kukatwa kwa panga.

Ni jambo la kawaida kwa polisi wa Tanzania kudai rushwa kutoka kwa waathiriwa wa uhalifu ili kuwasaidia. Lakini makundi yaliyotengwa haswa yako katika hali ya hatari zaidi. Jamal P., mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume (MSM) katika Zanzibar, alisema kuwa majirani zake wanne walimpiga barabarani mwezi wa Disemba mwaka wa 2011, wakimtusi kwa matusi ya kidharau kwa  ushoga. Walimkata kwenye sehemu ya juu ya pua na kichwani kwa upanga, na wakamwacha akilala chini barabarani. Jamal aliweza kwenda hadi Hospitali ya Mnazi Moja kwa matibabu kisha akairipoti kisa kile kwa polisi:

Niliwaambia polisi majina ya wale walionipiga, lakini polisi wakanidharau – wanajua kuwa ninafanya mapenzi na wanaume. Waliandika taarifa yangu  pamoja na majina. Ingawa hawakufuatilia. Nilirudi kwao mara mbili kuona kilichokuwa kikiendelea kuhusu kesi ile, lakini hawakuwa wakifanya chochote, kwa hiyo nilikata tamaa. Wakati mmoja nilipojaribu kufuatilia, polisi mmoja aliniomba pesa, na nikakataa. Halafu alisema, “Kama huna pesa, tufanye mapenzi.” Niliendelea kukataa. [191]

Abdalla J. alishambuliwa katika mwaka wa 2011 kule Dar es Salaam katika kituo kimoja cha mabasi na mwanaume aliyemwaibisha kwa kumwita kwa jina la kidharau la shoga, akampiga, na akamwibia simu. Abdalla aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO:

Singeweza kuenda kwa polisi. Ningalisema kuwa nilipigwa, wangaliniuliza kwa nini. Tulikuwa tukienda kwa polisi zamani. Lakini polisi wangetutambua kama mashoga. Tungejaribu kudanganya kuhusu sababu yetu ya kupigwa na tungesema, “Niliibiwa,” ama kitu kama hicho. Bali mtu angejitokeza na kusema, “Yeye ni shoga,” kisha wangekataa kutusaidia. [192]

Rahim R., mwanaume anayefanya mapenzi na wanaume (MSM) aliyepigwa na akakatwa tumboni kwa kisu katika mwaka wa 2008 baada ya kucheza densi na wanaume wengine katika karamu, vilevile alikuwa na hofu kama hizo. “Sikuenda kwa polisi. Ningesema nini? Ningewaelezaje polisi kitu kilichosababisha kupigwa kwangu?” [193]

Ramazani H., mwanaume mwenye umri wa miaka 22 na anayefanya kazi ya ngono kule Dar es Salaam, aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO kwamba ameshapigwa na majirani zaidi ya mara 10 isipokuwa hajawahi kuenda kwa polisi. Alieleza, “Nimeogopa kuenda kwa polisi kwa sababu labda wataniambia kuwa sina haki. Labda watasema ‘Hatushughuliki na kesi za mashoga, nenda zako.’” [194]

Wilson N., mfanyakazi wa ngono wa zamani katika wilaya ya Temeke kule Dar es Salaam, alisema kuwa majambazi mara nyingi walimkabili njiani akielekea nyumbani baada ya kazi ya ngono na kumpiga, kumwibia, na kumbaka. Hata hivyo, Wilson aliogopa kuenda kwa polisi: “Naogopa kushutumiwa na polisi. Siwezi kuenda kuripoti kuwa nilibakwa, kwa sababu sheria hairuhusu ngono ya mkundu, kwa hiyo nahofia kukamatwa.” [195]

Kesi ya mwanamume mwengine anayefanya kazi ya ngono, Ismail P., inaonyesha kuwa woga huu unatokana na hali halisi. Ismail aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO,

Ninaporejea kutoka kazi ya ngono, nimewahi kukutana na vijana wanaozurura mitaani usiku. Walichukua simu zangu, hela, wakanibaka, na kunipiga. Sikumbuki ni mara ngapi – nimebakwa mara nyingi mno kushinda  kuweza kukumbuka. Inafanyika kwenye vichochoro nikirudi nyumbani.

Nimeenda kwa polisi kuhusu jambo hili, lakini nilipofika kule walikataa kunisikiliza na kusema, “Nenda zako, hatuna wakati wa kusikiliza kesi yako. Hatuwezi kusikiliza kesi ya mashoga.” Kwa hiyo nilikufa moyo kuhusu kuripoti kesi kwa polisi. [196]

Kutoka mwaka wa 2011, polisi wameweka Madawati ya Jinsia na Watoto katika stesheni nyingi za polisi, na inapanga mwishowe kuwa na madawati hayo katika kila stesheni ya polisi nchini Tanzania. [197] Madawati yatasimamiwa na maafisa wa  polisi wenye ujuzi maalum ili waweze kuzishughulikia kesi za dhuluma za kingono na kijinsia na ukiukaji wa watoto. Madawati mengi ya Jinsia hayafanyi kazi kabisa, na kwa sababu wafanyakazi wanaobadilishwa kila mara, ni ngumu kubaki au kuwa na maafisa waliohitimu. Idadi kubwa ya wafanyakazi wa ngono na wana LGBTI waliohojiwa na mashirika Human Rights Watch na WASO hawakuwa wamepeleka malalamiko yao kwa Madawati ya Jinsia na Watoto. Sababu moja ni kuwa Madawati yale bado ni sehemu ya idara ile ile ya polisi inayowadhulumu na kuwanyanyasa wana LGBTI, wafanyakazi wa ngono na watumiaji wa dawa za kulevya.

VI.Ubaguzi katika Sekta ya Afya

Mnamo Septemba mwaka wa 2012, afisa mmoja katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii aliliambia Human Rights Watch,

Sera ni wazi. Hakuna yeyote atakayenyimwa huduma za afya, hata mwengine akifananisha [tabia zao] na kile kisichokubalika kisheria. Kukiharamisha hakumaanishi kuwa mtu anaweza kunyimwa huduma za afya. Upande wa huduma haipaswi kutegemea msimamo wa kisheria ya nchi. [198]

Licha ya kujitolea kwa serikali kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya kwa kiwango sawa kwa wote, walioko katika makundi maalum hupitia ukiukaji mwingi wa haki zao dhidi ya upatikanaji wa hali ya juu kabisa ya afya iwezekanavyo. Huwa ni pamoja na kunyimwa wazi huduma, kutukanwa na kutishiwa, na mahitaji mazito yanayoathiri kupita kiasi makundi yaliyotengwa. Hali hii kwa mfano hutokea hospitali zikihitaji kuwa wanaopimwa magonjwa ya zinaa waandamane na wapenzi wao wakienda hospitalini, masharti ambayo wafanyakazi wa ngono na wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume hawawezi kutimiza kwa urahisi, maanake hata wakiwashawishi wapenzi wao kuandamana nao hadi hospitalini, kuna uwezekano wa wao kukumbana na stigma.Hali hii hutokea pia hospital zikihitaji kwamba waathiriwa wa uvamizi wachukue fomu kutoka kwa polisi kabla ya kutibiwa, hata kama waathiriwa walikuwa wamevamiwa na polisi wenyewe.

Hivi karibuni taasisi za serikali na mashirika yasiyo ya serikali yamechukua hatua za kuwahamasisha wahudumu wa afya kuhusu mahitaji ya makundi maalum. Katika Zanzibar kwa mfano, Tume ya UKIMWI pamoja na Mpango wa Kudhibiti UKIMWI Zanzibar (Zanzibar AIDS Control Programme – ZACP) yamechukua  mbinu muafaka kuhusu VVU kwa kutoa mafunzo juu ya makundi yaliyoko katika hatari kubwa kwa wahudumu wa afya, polisi na polisi jamii. [199] Mwanaharakati mmoja wa wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume (MSM) jijini Dar es Salaam aliliambia shirika la Human Rights Watch kwamba kama sehemu ya mradi uliofadhiliwa na serikali, Mpango wa Kitaifa wa Kudhibiti UKIMWI  (Tanzania AIDS Prevention Program, TAPP):

Tunajaribu kushirikiana na Muhimbili [Hospitali ya Kitaifa] kutoa kondomu, vilianisho, na elimu rika. Katika zahanati nyingine za afya, unadanganya ili  upimwe – wanakuuliza ni lini ulifanya mapenzi mara ya mwisho na mahali mpenzi wako wa kike yupo. Kuna vituo vya Angaza [Vituo vya ushauri nasaha na upimaji, VCTs] wilayani. Nilitembelea kituo kimoja na mwanamke alianza kunihubiria dhidi ya kufanya mapenzi na wanaume. Niliondoka nikaenda pahali pengine. Tunahitaji pahali rafiki zaidi pa kupimwa. [200]

Wafanyakazi wa TAPP wanaotumwa nje ya vituo katika maeneo mbalimbali pia wanafanya kazi na hospitali za serikali ili kuboresha usikivu wao kwa MSM. Vilevile mashirika yasiyo ya serikali matatu yafuatayo Engender Health, PSI na T-Marc yameunganisha juhudi zao katika Mradi wa Husika (Husika Project) unaolenga kuwafikia MSM na wafanyakazi wa ngono na mambo juu ya VVU pamoja na kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya wa serikali ili kupunguza stigma. [201] Shirika la “Médecins du Monde”  limetekeleza mtaala wa mafunzo kwa wahudumu wa afya katika Temeke ili kuwahamasisha kuhusu utumiaji na watumiaji wa dawa za kulevya. Mpaka sasa zaidi ya wafanyakazi 100 wanaofanya katika hospitali mbalimbali, kliniki na zahanati wameyapokea mafunzo yale. [202]

Hata bila mafunzo maalum, wataalam wengine wa afya Tanzania wanafanya kazi yao bila upendeleo. Christian B., mwanaume gay, alienda katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya alipokuwa na kisonono ya mkundu. Aliliambia Human Rights Watch, “Waliuangalia mwili wangu pamoja na mkundu wangu. Hawakunishutumu. Walinipa tu dawa na nikaondoka.”[203] Hospitali ya Mt. Meru inajulikana katika mji wa Arusha kwa kuwashughulikia vilivyo watumiaji wa dawa za kulevya.[204] Hata hivyo, ushuhuda ufautao unaonyesha kuwa kesi hizi ni za kipekee na wala si hali halisi ya kawaida na kwamba mafunzo na uwajibikaji unahitajika miongoni mwa wahudumu wa afya.

Hospitali za umma zisipopatikana kwa urahisi, mashirika yasiyo ya serikali mara nyingi huingilia kati na kuuziba mwanya huo. Shirika lisilo la serikali la kimataifa lenye ofisi kule Mwanza, AMREF, limetoa mafunzo kwa wahudumu katika kituo cha Angaza [VCTs] ili wawe makini kwa mahitaji ya wafanyakazi wa ngono wa kike. AMREF linawashauri wafanyakazi wa ngono kuwa wanaweza kutembelea vituo vya Angaza hivi ili kupata huduma rafiki.[205] Katika wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, kliniki moja inayosimamiwa na kanisa katoliki kwa jina PASADA, ni kliniki rafiki na ni wazi kwa wale walioko katika makundi maalum.[206] Katika Zanzibar, ZAYEDESA ina VCT rafiki kwa walioko katika makundi maalum.

Hata hivyo idadi kubwa ya Watanzania bado wanategemea zahanati na hospitali za umma kwa mahitaji yao ya kimsingi ya afya na katika taasisi hizi licha ya mafanikio madogo katika miaka ya hivi karibuni, bado kuna vizuizi vingi dhidi ya haki ya afya.

Kunyimwa Huduma za Afya

Baadhi ya wale walioko katika makundi maalum hunyimwa hadharani huduma za afya. Mwanaume gay Dar es Salaam aitwaye Collins A., alifukuzwa kutoka katika zahanati moja ya serikali katika mtaa wa Tandika, Dar es Salaam, mnamo Disemba mwaka wa 2011. Collins aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO, “Wauguzi walisema, “Hatuwezi kukuhudumia hapa. Hatuwezi kumtibu mtu kama wewe. Hata umma hautaki kukuona.”[207]

Alex N., mwanaume aliyebadilisha jinsia yake, alipoenda kwenye zahanati moja katika jiji la Dar es Salaam kwa matibabu kwa ugonjwa wa zinaa, daktari alimwambia, “Haiwezekani. Wewe ni mtu wa aina gani?” na alikataa kumtibu. Baada ya kuwaomba ushauri marafiki zake, Alex alirejea kwa daktari tofauti aliyejulikana kuwa wazi kupokea mambo mapya na aliyemhudumia.[208]

Ukosefu wa huduma unaweza kusababisha madhara mabaya mno hata kifo. Human Rights Watch na WASO yalimhoji rafiki wa MSM mmoja aliyeaga dunia mwaka wa 2011 baada ya kuhudumiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke. Alituambia:

Mimi ndimi nilikuwa nikimwangalia na nikampeleka hospitalini. Alikuwa na malaria na joto jingi. Katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke, kulikuwa na daktari mmoja katika eneo la mapokezi aliyejua kwamba tulikuwa MSM. Alisema “Ondokeni hapa! Hakuna huduma kwa watu kama nyinyi.” Kwa hiyo tulienda PASADA (kliniki ya afya inayosimamiwa na Kanisa Katoliki). Alipimwa kwa VVU kule. Walisema, “Njoo juma lijalo kwa matokeo yako.” Hawana vitanda vya hospitali, ni VCT peke yake. Lakini katika kipindi cha wiki moja baadaye alikuwa amekufa kabla ya kupata matokeo yake. Hakuna mtu aliyeenda kuchukua matokeo yake.[209]

Hivi majuzi, wanaharakati wanaowasaidia jamaa ya MSM katika eneo la Temeke walikutana na maafisa wa hospitali wilayani ili kuwahamasisha juu ya maswala ya afya ya wana MSM. Wanaharakati walielezea hisia zao vizuri kwamba matibabu huenda yakaimarike kutokana na hatua ile.[210]

Jamal P., MSM mwenye umri wa miaka 28 kule Zanzibar, aliliambia Human Rights Watch kwamba mnamo Machi 2012, alienda katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kutibiwa ugonjwa wa zinaa. Jamal alisema:

Daktari aliniangalia na akaniambia kuwa ulikuwa kisonono, lakini alikataa kunitibu. Alisema “Tayari unafanya mapenzi na wanaume, na sasa unakuja hapa kutuletea shida – ondoka.” Aliniambia kwamba hangenitibu kwa sababu mimi ndiye MSM. Nilirudi nyumbani na mamangu alinipeleka katika hospitali ya kibinafsi.[211]

Mwezi uliofuata, hata hivyo, Hospitali ya Mnazi Mmoja ilizindua mradi mpya ambapo daktari maalum wa kuyashughulikia mahitaji ya makundi maalum aliwekwa ili awahudumia siku mbili kwa wiki.[212] Wanaharakati wa haki za wana LGBTI Zanzibar walikuwa na matumaini kwa huduma bora chini ya mradi huu.[213] Wafanyakazi wa Mnazi Mmoja wamewafahamisha vilivyo makundi maalum juu ya huduma zipatikanazo: walipogundua kwamba ni wachache ndio walitumia huduma zao, walianza kuwatuma nje wana elimu rika na kwa ushirikiano na mashirika ya jamii ili wapeleke huduma nje ya vituo, mfano ambao unaweza kuigwa katika sehemu nyingine Zanzibar na Tanzania bara.[214]

Matusi, Unyanyasaji, na Ukiukaji wa Usiri

Mahirika la Human Rights Watch na WASO lilirekodi kesi nyingi ambazo wahudumu wa afya waliwatusi kwa maneno na kuwadhulumu watu, hatua iliyowazuia kuenda kupata huduma baadaye. Lester F., mwanaume gay mwenye umri wa miaka 18 kule Arusha, huonekana kama mwanamke na wakati mwingine hupaka vipodozi, na mara nyingi hutambuliwa kama shoga. Aliyaambia mashirika ya Human Rights Watch na WASO,

Nilibaguliwa mara moja nilipoenda kupimwa VVU. Nilienda Angaza [VCT] kama kawaida. Baada ya kupimwa, nilikuwa nikingojea matokeo. Matokeo yalipokuja, daktari aliniangalia na kusema, “Ninajua unachofanya. Acha unachofanya, ni kibaya sana.” Niliyachukua matokeo tu nikasema, “Asante,” nikaondoka kuepukana na shida.[215]

Carlos B. alipata ugonjwa wa zinaa kwenye mkundu na akaenda katika Hospitali ya Mwanayamala (inayojulikana pia kama Hospitali ya Wilaya ya Kinondoni) kule Dar es Salaam. Licha ya juhudi zake Carlos za kuficha mwenendo wake wa kingono, daktari alimtusi:

Niliogopa kumwelezea daktari kuhusu mwelekeo  wangu wa kingono kwa sababu ya stigma na ubaguzi katika jamii, kwa hiyo nilibuni hadithi bandia ili kumshawishi daktari anisikilize. Nilisema, “Siku tatu zilizopita, nililewa, nikazirai pahali pengine na watu walinibaka. Kwa hiyo nafikiri niliambukizwa ugonjwa wa zinaa kwenye mkundu.” Daktari alianza kunitusi, akisema, “Wewe ni mwanaume, unafanya hivi kwa nini? Si sawa kwa mwanaume kamili kufanya kitendo kama hiki.” Nilisema “Mimi si shoga, halikuwa kosa langu, ilitokea tu.” Daktari alisema, “Wakati mwingine, usifanye kitendo kama hicho, wewe ni mwanaume, hupaswi kunywa pombe kupindukia mpaka uruhusu kitendo kama hiki, lazima uwe na kiwango.” [216]

Matibabu hutofautiana sana kutoka kwa mtaalamu mmoja wa afya hadi mwengine. Ismail P., mfanyakazi wa ngono, aliyaambia Human Rights Watch na WASO kuwa yeye hupata magonjwa ya zinaa kila mara, sababu moja ikiwa ni idadi kubwa ya wateja wanaokataa kutumia kondomu. Alisema,

Nilipopata magonjwa ya zinaa na kuenda hospitalini, madaktari wengine walinihudumia vizuri, nao wengine walinihudumia vibaya – inawategemea madaktari walioko siku fulani. Wengine hunihudumia kama mgonjwa mwengine yeyote. Wengine husema, “Sisikii starehe kukutibu, acha nimwite daktari mwengine.” Wengine husema, “Unajua, dini yangu hairuhusu hii,” au “Sheria ya nchi hairuhusu hii.” [217]

Wana LGBTI wengi huamua kulipa gharama za juu katika hospitali za kibinafsi ili kuepukana na ubaguzi katika hospitali za umma. Mohamed R. alisema,

Nilikuwa na ugonjwa wa zinaa kwenye mkundu wakati mmoja. Nilienda Hospitali ya Wilaya ya Temeke, nilitendewa vibaya na hata sikuangaliwa. Lakini nilihudumiwa vyema katika hospitali ya kibinafsi, hata nikamleta mpenzi wangu naye akatibiwa pia. [218]

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume vilevile hukabiliana na unyanyasaji na ukiukaji wakienda kutibiwa kwa magonjwa mengine kando na yale ya zinaa. Peter E. alienda hospitalini baada ya kupigwa kwa sababu ya mwenendo wake wa kingono. Alimweleza daktari hali ile ambayo alishambuliwa. Alisema, “Nilipomwelezea daktari juu ya mwenendo wangu wa kingono, daktari alianza kuwaita wenzake akisema ‘Aisee daktari, njoo hapa!’ akawaambia kwamba nilikuwa shoga…. Hujioni kama binadamu kuwa pale.” [219]

Ismail P., aliambia Human Rights Watch na WASO kwamba alishambuliwa barabarani, kwa kuonekana kama mwanamke. Alipigwa hadi akapoteza fahamu na aliamka hospitalini. Kule hospitalini alihudumiwa kwa njia mbalimbali:

Madaktari wengine walinihudumia vizuri, lakini wengine walinidhulumu, walinitusi, wakisema, “Watu hawa, ilikuwa kosa lake, anapaswa kupigwa. Hupaswi kumtibu, achana naye tu. Kwa nini wanaume wanakuja na kufanya vitendo kama hivi? Yeye ni shoga kwa nini? Ni kwa nini aliamua kuwa shoga? Ni kosa lake. Ni vyema kwa watu kumpiga.” Na wengine walisema, “Hapana hii si sawa, huyu pia ni binadamu, hapaswi kupigwa.” [220]

Hayat E., mtu aliyezaliwa na sehemu zote za siri za mwanaume na mwanamke, aliliambia Human Rights Watch kwamba katika hospitali za umma, “Wanaanza kukunyooshea vidole, na unaweza kuwasikia wakiongea. Huitana kuniona, halafu wagonjwa wengine nao wanaanza kustaajabu juu yangu…. Naogopa kwenda hospitalini.” [221]

Watumiaji wa dawa za kulevya pia wanadhalilishwa na kutendwa vibaya na wataalamu wa tiba kwa sababu kwa kiwango kikubwa wanachukuliwa kuwa “wezi.” Kama ilivyoelezwa katika Sehemu ya II hapo juu, baada ya January H. kuvamiwa katika jiji la Dar es Salaam na umati wa Sungu Sungu waliomkata usoni kwa panga, wahudumu katika Hospitali ya Temeke walimwita “mwizi” na wakakataa kutumia anestezia walipomshona.

Mwajuma P. alisema kuwa aliamini kwamba wanawake wanaotumia dawa za kulevya hasa walikabiliwa na unyanyapaa:

Katika Hospitali za Temeke na Muhimbili, nimekabiliwa na unyanyapaa. Watumiaji wa dawa za kulevya katika nchi hii, haswa wanawake hawathaminiwi. Katika Muhimbili wakati mwingine wauguzi husema, “Hawa ni watumiaji wa dawa za kulevya,” halafu wanawaita wengine. Katika Temeke pia wanafanya vilevile.” [222]

Katika Dar es Salaam  na Tanga miradi ya tiba dhidi ya dawa za kulevya inayotolewa na mashirika yasiyo ya serikali inawapa wanaopokea tiba kadi maalum inayowatambua kama washiriki katika miradi ya tiba, inayowasaidia kupata huduma hospitalini. Walioshiriki katika miradi hii waliripoti viwango vya chini vya stigma. [223] Mwakilishi wa CBO moja kule Tanga alielezea, “Bila kadi, ni vigumu kuhudumiwa, kwa sababu ya stigma kutoka kwa wahudumu. Wahudumu wanafikiria kuwa labda wataiba kitu, au hawapendi tu jinsi wanavyoonekana. [224]

Mahitaji ya Kuwasilisha Fomu ya Polisi Nambari 3 (PF3) kabla ya Matibabu

Hospitali za Tanzania zinahitaji kwamba waathiriwa kutokana na dhuluma watoe fomu inayojulikana kama Police Form Number 3 (PF3) kabla ya kutibiwa. [225] Nia ya fomu hii ni kuhakikisha kwamba polisi wana rekodi ya visa vyote vya dhuluma na uhalifu unaweza kuchunguzwa na wahusika washtakiwa. [226] Wakati mwingine hospitali humlaza mgonjwa bila PF3 ikiwa hali yake imeamuliwa kuwa ya dharura, lakini wakati mwingine, wagonjwa wasiokuwa na PF3 wanatumwa kwenye stesheni ya polisi kabla ya kutibiwa. [227]

Waathiriwa waliyaambia Human Rights Watch na WASO kwamba hospitali za binafsi zilikuwa na uwezekano mkubwa wa kumhudumia mtu bila PF3 kuliko zile za umma, lakini Watanzania wengi hawawezi kuzimudu gharama katika hospitali za binafsi.

Matakwa ya kutaka PF3 yanatatiza upatikanaji wa huduma za afya. Kwa wale ambao wamedhulumiwa na polisi wenyewe au wanasitasita kwenda kwa polisi kwa woga wa kukumbana na madhara kwa sababu ya hali yao, hawapati matibabu, kwa sababu polisi wanakataa waziwazi kuwapa PF3 au waathiriwa wanaogopa kuiomba. Huduma za afya baada ya dhuluma yoyote, ikijumuisha dhuluma ya kingono, haipaswi kuhusishwa na hatua za kisheria. Waathiriwa wanapaswa kuwa na afya, bila kutegemea kama wameamua kuripoti uhalifu ule.

Suleiman R., alituhumiwa kwa wizi kwa sababu ya yeye kutumia dawa za kulevya, alidhulumiwa kwa pasi moto na afisa wa polisi katika wilaya ya Temeke mnamo Disemba 2011(angalia Sehemu ya III, juu). Baada ya kuachiliwa na polisi, alienda katika Stesheni ya Polisi ya Chang’ombe pamoja na mamake kuchukua fomu ya PF3 na baadaye kwenda kutibiwa:

Mamangu alieleza, “Alipigwa na polisi kwa hiyo anahitaji kwenda hospitalini.” Koplo mmoja katika stesheni alikataa na akasema: “Tukikupa PF3, utashtaki polisi kortini.”

Suleiman alilazimika kwenda katika hospitali ya kibinafsi, ambapo alilipa shilingi 35,000 kwa matibabu. [228]

Susan N., mfanyakazi wa ngono, alienda kwenye hospitali ya umma katika mwaka wa 2011 baada ya kulazimishwa na mteja kufanya ngono ya mkundu, bali hangeweza kutibiwa bila kujaza ripoti ya polisi:

Nilipoenda hospitalini usiku ule na mkundu uliovilia walikataa kunitibu hadi niripoti kwa polisi kwanza. Hali hii ilinifanya nirudi nyumbani hadi siku iliyofuata nikaenda katika hospitali ya kibinafsi. Ilinigharimu hela nyingi lakini nilipata huduma niliyohitaji. [229]

Baadhi ya wale walioko katika makundi maalum huwadanganya polisi au wahudumu hospitalini ili kupata PF3 au kuepukana na masharti yale ya kuwa na fomu hii. Kuna uwezekano wa hatua hii kuchangia kutotibiwa vilivyo: kama wagonjwa hawawezi kusema ukweli kuhusu vyanzo vya majeraha yao, wahudumu wa afya labda hawatajua ni nini wanapaswa kuangalia. Walter S. ametunga visa mbalimbali ili kupata PF3 mara kadha kwamba amepigwa na majirani zake kwa sababu ya utumiaji wa dawa za kulevya: “Wakati mwingine unabuni hadithi bandia kwa polisi kwamba ulianguka au kitu kama hicho ili upate ile fomu ya PF3. Hutaki kuwaambia kuwa ulipigwa kwa kuwa wewe ni mtumiaji wa dawa za kulevya. Kwa hiyo unasema, ‘Nilipata ajali kwa pikipiki.’” [230]

Mwamini K., mfanyakazi wa ngono Dar es Salaam, aliwadanganya wahudumu hospitalini ili kutibiwa baada ya kupigwa na maafisa wa polisi katika wilaya ya Kinondoni mnamo mwaka wa 2011.

Walikuwa maafisa wa polisi watatu. Walinipiga kwa mikoni na mateke. Walikuwa wakisema, “Unafanya nini hapa, wewe ni kahaba, mbwa, wewe ni nguruwe”…. Nilienda hospitalini kwa sababu walikuwa wameniumiza vibaya. Nilikuwa na jeraha kwenye ngozi. Mwili wangu wote uliuma. Nilimwambia daktari kwamba nilianguka kwenye ngazi. Ningewaambia ukweli juu ya kilichotendeka, wangehitaji PF3. Niliogopa kuenda kwa polisi kuchukua fomu maanake wangeniuliza maswali mengi na wangetaka kumkamata aliyenipiga na kama polisi wale wangekamatwa wangesema kwamba nilikuwa mfanyakazi wa ngono. [231]

Wengine hujitibu wenyewe au hawapati matibabu ya aina yoyote kwa sababu ya mahitaji ya fomu ile ya PF3. Jamila H., mfanyakazi wa ngono, alibakwa na genge moja mwezi wa Februari 2012 na akaenda katika hospitali ya umma, lakini aliambiwa kwamba alihitaji PF3. Aliliambia Human Rights Watch, “Walisema kwamba ninapaswa kuenda kwa polisi, lakini nisingeweza kwa sababu nilifanya kazi ya ngono.” Wawili wa wale waliombaka hawakutumia kondomu, lakini kwa sababu ya kukosekana kwa huduma za afya, hakupimwa VVU.” [232] Kwa kunyimwa tiba ya hospitali, Jamila alinunua dawa za kawaida katika duka la dawa.

Baadhi ya polisi hutumia kwa manufaa yao wenyewe hali ya hatari ya makundi maalum ili kuwalazimisha kutoa hela ili wawape PF3. Maureen B., mfanyakazi wa ngono Dar es Salaam, alipigwa na mteja wake katika mwaka wa 2010:

Nilipelekwa hospitalini na msichana mwengine, lakini kwanza walitaka PF3. Tulilazimika kwenda katika stesheni ya polisi kuchukua stabadhi ile na kwa sababu walibaini kwamba nilikuwa mfanyakazi wa ngono, walitulipisha shilingi 20,000. [233]

Wengine waliwahonga maafisa wa afya badala ya polisi. Dalili S., mfanyakazi wa  ngono, alisema, “Nikiumia nikifanya kazi, ni lazima niwahonge baadhi ya wale madaktari wanaofanya kazi usiku ili nihudumiwe bila kufuata njia ile ya kupata PF3.” [234]

Disemba 2011, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ilizindua mwongozo wa kitaifa kuhusu dhuluma ya kijinsia ambayo ingewaruhusu waathiriwa wa dhuluma ya kingono na kijinsia kupata matibabu kabla ya kuchukua PF3 kutoka katika stesheni ya polisi. [235] Mwongozo kama huu ni ari nzuri mno, lakini matukio kama ya Jamila H., hapa juu, yanadokeza kwamba mwongozo huu hautekelezwi kwa njia ya sawa. Aidha kwa sababu ulitumika tu katika visa vya dhuluma za kingono na kijinsia, ulikuwa wenye manufaa kwa kiwango kidogo tu: waathiriwa walioteswa na polisi au wale walioshambuliwa na umati wenye ghadhabu kwa sababu ya mwenendo wao wa kingono ama utumiaji wa dawa za kulevya hawakunufaika kutokana na mwongozo huu mpya.

Mahitaji ya “Mlete Mpenzi Wako”

Baadhi ya wahudumu wa afya wa Tanzania wanakataa kuwatibu wanaougua magonjwa ya zinaa hadi wawalete wapenzi wao. Mashirika ya Human Rights Watch na WASO hayakuweza kubainisha kama mahitaji haya yalijikita kwenye msingi wa sera ama sheria rasmi na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii haikujibu barua zetu juu ya utaratibu wa mahitaji haya. Ingawa mahitaji kama haya labda yanatokana na hamu ya kuhakikisha tiba kwa wote walioambukizwa au athiriwa na VVU na magonjwa mengine ya zinaa, hayawasaidii wafanyakazi wa ngono na wana LGBTI ambao pengine hawawezi kuwashawishi wapenzi wao kwenda kutibiwa, hata kama wao wenyewe wananuia kufanya hivyo na badala yake inawafanya wagonjwa wajifiche. Mwamini K., mfanyakazi wa ngono katika Dar es Salaam, alisimulia kisa chake alipotembelea Hospitali ya Mwananyamala ili kupata matibabu kwa kuvu:

Kawaida wanakuambia umlete mpenzi wako. Niliwaambia ukweli, “Sina mpenzi. Mimi ni mfanyakazi wa ngono, na niliambukizwa ugonjwa katika kazi yangu.” Nesi yule alikataa kunitibu. Alisema “Siwezi kukutibu bila kumleta mpenzi wako.” Niliondoka na nikaenda kwenye hospitali ya kibinafsi. [236]

Pili M., alikumbana na hali kama ii hii katika Hospitali ya Sinza katika Dar es Salaam. Alipoenda kupata matibabu kwa ajili ya ugonjwa wa zinaa na akasema kuwa hangeweza kumleta mpenzi wake, kwa mujibu wa Pili,

Nesi yule alisema “Unafanya kazi ya ngono au nini? Wewe ni mwongo. Kwa sababu ugonjwa huu wa zinaa ni hatari sana.” Alikataa kunitibu, akisema, “Siwezi kukutibu hadi umlete mpenzi wako.” [237]

Mahitaji haya si sawa. Kulingana na Melissa L., mfanyakazi wa ngono katika mji wa Arusha, “Ni sawa tukielezea kwamba hatuwezi kuwaleta wapenzi wetu. Hata katika hospitali za serikali, wanaelewa. Hawatulaumu, lakini wanatushauri kwamba tutumie kondomu. [238] Katika Zanzibar, mashirika yanayofanya kazi na wafanyakazi wa ngono walisema kwamba upimaji haujajikita katika masharti ya  kumleta mpenzi. [239]

Mifano hii inapaswa kuigwa kote Tanzania, kwa sababu bila kufanya hivi,  walioko kwenye hatari zaidi hawatapimwa wala kutibiwa.

Ukosefu wa Vilainisho

Utumiaji wa vilainisho vya maji  ni hatua muhimu ya kujikinga wakati wa ngono ya mkundu. Kuna uwezekano mkubwa wa kondomu kuraruka wapenzi wa ngono wakifanya ngono ya mkundu bila kilainisho au wakitumia vilainisho vya mafuta kama Vaseline. Kwa bahati mbaya, vilainisho vya maji maji havipatikani katika sehemu nyingi Tanzania ama ni ghali mno. Karibu wanaume wote wanaofanya mapenzi na wanaume waliohojiwa na Human Rights Watch na WASO walisema kuwa hawakujua pahali ambapo vilainisho vya maji maji vinapatikana au hawangeweza kumudu bei yake; wengi hawakujua umuhimu wa vilainisho vya maji maji au hata hawakujua vilanisho ni nini. Wachache waliokuwa na vilainisho vya maji maji walitegemea mashirika ya VVU/UKIMWI yaliyoko Dar es Salaam na yaliyowahudumia MSM, ambayo pia wakati mwingine havipatikani kwa njia inayoweza kutegemewa.

Upatikanajiwa vilainisho vya maji  ni ngumu sana nje ya jiji la Dar es Salaam. Kulingana na Lester F. katika Arusha, “Ni rahisi kupata kondomu, lakini si kilainisho. Labda unaweza kwenda kwenye maduka matano ukiulizia KY bila mafanikio. Kwa hiyo natumia Vaseline.” [240] Lester alijua kuwa Vaseline ilikuwa na uwezo wa kuziharibu kondomu, lakini aliona hana budi.

Katika Mbeya, Christian B., mfanyakazi wa ngono, aliliambia shirika la Human Rights Watch kwamba alikuwa amejaribu kilainisho cha maji maji mara moja tu, mteja wake alipokileta kutoka Dar es Salaam. Nyakati nyingine alitumia kilainisho cha mafuta. Christian B. anajua kwamba anahatarisha maisha yake lakini hajawahi kupimwa VVU. Alisema kuwa anahofia kujua hali yake kwa sababu hajui atapata usaidizi kutoka wapi  akigundua kwamba ana VVU. [241]

MSM mmoja mwenye umri wa miaka 19 anayeishi Tanga na wakati mwingine hufanya biashara ya ngono aliyaambia Human Rights Watch na WASO kwamba hakuwahi kusikia juu ya kilainisho cha maji au mafuta; alitumia mate peke yake kulainisha wakati wa ngono ya mkundu. [242]

VII. Sheria ya Tanzania, ya Ukanda, na ya Kimataifa

Ripoti hii inaangazia aina tatu za mienendo – ngono kwa hiari kati ya watu wa jinsia moja, kazi ya ngono, na utumiaji wa dawa za kulevya – ambayo sheria ya kimataifa haishughulikii kwa njia sawa.

Hata hivyo, ulinzi wa haki za binadamu unahitajika katika kesi zote tatu. Polisi au makundi ya usalama yaliyo rasmi kidogo huwatendea vibaya au kuwakamata kiholela walioko katika makundi yaliyo hatarini, au wahudumu wa afya wakiwanyima huduma, matendo yao hukiuka kanuni za kimataifa kuhusu haki za binadamu.Vilevile, wanavunja mara  nyingi sheria za Tanzania.

Tanzania imeanzisha utaratibu wa kubadilisha katiba, hatua inayotoa fursa ya kujumuisha haki za binadamu. Wanaoiandika katiba wanapaswa kuzingatia kujumuisha Muswada wa Haki; kujumuisha makala kali dhidi ya ubaguzi; na kufafanua umuhimu wa  mikataba ya kimataifa iliyotiwa saini na Tanzania.

Ngono ya Hiari Baina ya Wapenzi wa Jinsia Moja

Kuharamisha ngono ya jinsia moja kati ya watu wazima waliokubaliana kunakiuka haki ya watu ya faragha  na ile ya uhuru wa kutobaguliwa, ambazo zote zinahakikishwa katika Mkataba wa Kimataifa wa Haki ya Kiraia na Kisiasa (International Covenant on Civil and Political Rights, ICCPR) uliosainiwa na Tanzania. [243] Kumkamata mtu kwa kufanya ngono kwa hiari kati ya wale wa jinsia moja ni ukiukaji wa sheria inayopiga marufuku kuzuiliwa kiholela. [244]

Tume ya Afrika kuhusu Haki za Watu na Binadamu imetetea kuwa ubaguzi kwenye msingi ya mwelekeo wa kingono ni ukiukaji wa sheria zinazoharamisha ubaguzi katika Mkataba wa Afrika wa Haki za Watu na Binadamu (African Charter on Human and Peoples’ Rights). [245] Katiba ya Tanzania aidha inapiga marufuku ubaguzi. Ibara ya 9, “Ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea” inasema hivi:

… Mamlaka ya Nchi na Vyombo Vyake Vyote Vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha…kuamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na kudumushwa kwa kufuata kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu Haki za Binadamu… (na) kwamba aina zote za dhuluma vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini. [246]

Zaidi ya hayo, Ibara ya 13 inhakikisha usawa mbele ya sheria na kukataza Jamhuri ya Muungano kupitisha sheria zinazobagua. [247] Ibara ya 16 inalinda haki ya faragha. [248]

Hakuna mtu yeyote aliyewahi kuleta kesi mbele ya korti ya Tanzania inayohusiana na ibara hizi ili kuona zinavyotekelezwa katika muktadha wa mwelekeo wa kingono au utambulisho wa kijinsia, lakini korti ingeweza kugundua kuwa sheria zinazopiga marufuku ngono ya jinsia moja si ya kikatiba.

Kazi ya Ngono

Human Rights Watch linaamini kuwa kuharamisha ngono ya hiari kwa sababu za kifedha kati ya watu wazima, kwa mfano kazi ya ngono kati ya watu wazima waliokubaliana, kunakiuka haki ya faragha, pamoja na uhuru wa kibinafsi, unaolindwa na Mkataba wa Kimataifa wa Haki ya Kiraia na Kisiasa (ICCPR). [249]

Pamoja na hayo, kukamatwa kwa sababu ya jinsi mtu anavyojulikana kama inavyofanyika mara kwa mara nchini Tanzania – tabia ya polisi kumkamata mtu kwa sababu anajulikana kama “mfanyakazi wa ngono” – kunakiuka marufuku juu ya kukamatwa kiholela kama ilivyo katika Ibara ya 9 ya ICCPR na Ibara za 4 na 6 za Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Watu na Binadamu (ACHPR). [250] Katiba ya Tanzania vilevile inapiga marufuku kuwakamata watu kiholela. [251]

Unyonyaji wa Kingono

Biashara ya unyonyaji wa watoto kingono imepigwa marufuku kabisa katika sheria za kitaifa na kimataifa. [252] Katika kesi hizi zote, anayemnyanyasa mtoto – si mtoto mwenyewe – anapaswa kuhukumiwa. Mpango Kazi wa Pili wa Taifa wa Huduma kwa Watoto Walio Katika Mazingira Hatarishi (National Costed Plan of Action for Most Vulnerable Children) inawatambua na kuwalenga “Watoto wanaohusika katika aina mbaya kabisa za ajira kwa watoto,” kama “unyanyasaji kingono.” [253] Mpango huu ukitekelezwa, utachangia ongezeko la rasilimali za kuwalinda na kuwarekebisha watoto wanaohusika katika kazi ya ngono.

Utumiaji  Binafsi wa Dawa za Kulevya

Mataifa yanapaswa kulinda haki za binadamu za wote bila kujali kama matendo yao yanakiuka sheria za kitaifa. Kwa kuwakamata kiholela wanaotuhumiwa kwa utumiaji wa dawa za kulevya kwenye msingi wa “hali” yao kama watumiaji wa dawa za kulevya tu, bila ushahidi wa kutosha kwamba wanatumia dawa za kulevya wakati wa kukamatwa, polisi wa Tanzania wanakiuka Ibara ya 9 katika ICCPR na zile za 4 na 6 katika ACHPR, zinazowalinda watu wote dhidi ya kukamatwa kiholela. [254]

Tanzania inapaswa kupitia tena na kubadilisha sheria zilizopo zinazoharamisha utumiaji binafsi wa dawa za kulevya pamoja na kuwa na dawa za kulevya kwa matumizi ya kibinafsi, ili kuhakikisha kwamba haki za binadamu za wale wanaotumia dawa za kulevya zinalindwa na sheria kuhusu dawa za kulevya haziongezi hatari za maambukizi ya VVU wala hazitatizi upatikanaji wa kinga dhidi ya VVU, huduma au matibabu.

Haki ya Kutoteswa

Sheria ya kimataifa inapiga marufuku kabisa mateso. Marufuku hii inaelezwa katika Ibara ya 5 katika ACHPR na Ibara za 7 na 10 katika ICCPR. [255] Tanzania ni miongoni mwa nchi chache ambazo hazijatia saini Mkataba Dhidi ya Mateso na Adhabu au Matendo Mengine ya Kikatili, yasiyo ya Kibinadamu au ya Kiudhalilishaji (Convention against Torture and Other Cruel, Inhuman or Degrading Treatment or Punishment) inayoainisha marufuku juu ya mateso na maonevu na unalazimisha utaratibu wa majukumu mengi kwa mataifa unaonuiwa kuzuia mateso na kuyashughulikia yakitokea. [256] Kupigwa na ngono ya lazima ambayo Watanzania wengi wamelazimika kukumbana nayo wakiwa mikononi mwa polisi zinakiuka waziwazi marufuku juu ya mateso.

Katiba ya Tanzania inasema kuwa “Ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa  adhabu zinazomtezwa  au kumdhalilisha hakuna mtu yeyote atakayeteswa au atakayetendewa unyama au atakayeadhibiwa au atakayehudumiwa kwa njia ya kudhalilisha.” [257] Zaidi ya hayo, “Kwa ajili ya kuhifadhi haki ya usawa wa binadamu, heshima ya mtu itatunzwa katika shughulu zote zinazohusu upelelezi na uendeshaji wa mambo mtu anakuwa chini ya ulinzi bila uhuru, au katika kuhakikisha utekelezaji wa adhabu.” [258]

Ili kudhihirisha kujitolea kwake kwa haki za binadamu na heshima za binadamu, Tanzania inapaswa kusaini Mkataba wa kimataifa Dhidi ya Mateso, na kuhakikisha kwamba mateso ni uhalifu unaoweza kuchukulia hatua za kisheria chini ya Kanuni ya Adhabu na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Haki ya Kupata Huduma Ya Kiwango cha Juu cha Afya

Haki ya kupata huduma ya kiwango cha juu cha afya inahakikishwa katika  Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Watu na Binadamu na Watu, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (International Covenant on Economic, Social and Cultural Rights, ICESCR), na Mkataba Kimataifa wa Kukomesha Aina Zote  ya Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (U.N. Convention on the Elimination of all Forms of Discrimination Against Women, CEDAW). [259] La muhimu kwa walioko katika makundi maalum, ni upatikanaji wa haki ya afya bila ubaguzi. Ubaguzi kwa msingi ya mwelekeo wa kingono na utambuzi wa kijinsia umepigwa marufuku wazi na sheria ya kimataifa. [260]

Haki hii inalazimisha mataifa kuchukua hatua zinazohitajika za kuzuia, kutibu, nakudhibiti magonjwa ya maradhi  na magonjwa mengine. Katika kutimiza jukumu hili, mataifa “yanapaswa kuhakikisha kwamba bidhaa, huduma na taarifa zinazofaa katika kuzuia na kutibu magonjwa ya zinaa, yakiwemo VVU/ UKIMWI, zipo na zinapatikana.” [261] Kwa watumiaji wa dawa za kulevya, kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya kiwango cha juu cha afya inapaswa kujumuisha kupanua miradi ya kupunguza madhara. [262] Kwa makundi yote maalum, haki hii inapaswa kujumuisha kuhakikishaupatikanaji wa kondomu na  vilainisho vya maji.

Kama eneo, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imeanza kuchukua hatua za kulinda haki ya afya, haswa kuhusu VVU/ UKIMWI. Bunge la Afrika Mashariki (East Africa Legislative Assembly) linalojumuisha wawakilishi kutoka Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda, lilipitisha Muswada wa Kudhibiti na Kuzuia VVU/UKIMWI Afrika Mashariki mnamo Aprili 2012, [263] ingawa  bado haujatiwa saini na marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ili iwe sheria. Ukisainiwa, utawalinda kwa kiwango fulani wafanyakazi wa ngono, wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume, na wanaojidunga dawa za kulevya: unatoa wito kwa serikali kukabiliana na unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya wale walioko katika hali ya hatari zaidi [264] ; kutekeleza mikakati ya kukuza na kulinda afya yao [265] ; na kuhakikisha kuwa mbinu za kujikinga zinazotambulika zinapatikana kwa walioko katika hatari zaidi. [266]

Itifaki ya Maputo juu ya Haki za Wanawake katika Afrika, ambayo Tanzania ni nchi mwanachama, inasema  kuwa mataifa lazima yahakikishe “haki ya kujilinda na kulindwa dhidi ya magonjwa ya zinaa ukiwemo VVU/ UKIM WI”. [267]

Haki ya Usalama na Uadilifu wa Kimwili

Tanzania imepewa jukumu la kuwalinda watu wote dhidi ya dhuluma, wakiwemo wale walioko kwenye makundi yaliyotengwa. Nchi ina jukumu lake la kuchunguza na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya dhuluma bila kujali kama ilitekelezwa na wawakilishi wake au la. [268]

Tanzania pia ni nchi mwanachama katika Itifaki ya Maputo iliyotoa masharti kwa nchi kuratibu na kutekeleza hatua zinazofaa ili “kuhakikisha ulinzi wa haki ya kila mwanamke ya kuheshimu hadhi yake na ulinzi wa wanawake dhidi ya aina zote za dhuluma, haswa ya kingono na ya kimaneno.” [269] Mataifa wanachama katika Itifaki ya Maputo yanaahidi pia “kubuni na kutekeleza sheria zinazoharamisha aina zote za dhuluma dhidi ya wanawake zikiwemo ngono ya lazima bila kujali kama dhuluma ilitekelezwa kwa faragha au hadharani” [270] na “kuwaadhibu   wahusika wa unyanyasaji dhidi ya wanawake  pamoja na kutekeleza miradi ya kuwarekebisha wanawake waathiriwa.” [271]

Dhuluma ya kingono – hata mwaathiriwa akifanya kazi ya ngono, na hata kama walioitekeleza ni polisi – ni uhalifu mbaya sana katika sheria ya Tanzania. Ubakaji unaadhibiwa kwa adhabu ya juu kuwa ya kifungo cha maisha. [272]

Kanuni ya Adhabu kwa wakati huu hauadhibu ubakaji wa wanaume na wavulana, ambao, inavyooneshwa katika ripoti hii, wakati mwingine ni waathiriwa wa ubakaji, baadhi ya visa vikifanywa na maafisa wa polisi. Kanuni zote mbili za adhabu kwa wakati huu zinafafanua ubakaji hivi “Ni kosa kwa mtu wa jinsia ya kiume kumbaka msichana au mwanamke.” [273]

Wanaotunga sheria wakijitahidi kutoa ibara zile zinazoharamisha ngono ya hiari kati ya watu wa jinsia moja, wanapaswa kizibadilisha na zile zinazoharamisha ubakaji wa wavulana na wanaume.

Ufisadi

Sheria ya Tanzania inaharamisha vikali ufisadi, ikiwemo kulazimishwa kutoa hela au ngono. Ni haramu kwa afisa wa umma kuomba fadhila ya ngono kulingana na sehemu  25 ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana Na Rushwa ya mwaka wa 2007. [274] Mwakilishi mmoja wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa aliliambia Human Rights Watch, “Ni hatia hata kama waathiriwa ni wafanyakazi ya ngono.” Afisa yule alisema kuwa sheria ile inawalinda wanaofichua ufisadi, kwamba wafanyakazi wa ngono, wana LGBTI, na watumiaji wa dawa za kulevya hawawezi kushtakiwa kwa taarifa wanazotoa kwa taasisi. [275]

VIII. Jibu kutoka kwa Serikali ya Tanzania

Serikali ya Tanzania imechukua hatua kiasi za kupunguza ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya wale walioko katika makundi maalum, zaidi kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya serikali yanayohusika na kupunguza madhara na huduma za VVU kwa makundi ya waliotengwa. Hata hivyo bado kuna mengi ya kufanya.

Wakati wa utafiti wa ripoti hii, shirika la Human Rights Watch lilikutana na polisi, Wizara ya Afya na Usitiwai wa Jamii, na ile ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, pamoja na wanachama wa tume za serikali zinazosimamia haki ya binadamu, VVU, ufisadi na sera zinazohusu dawa za kulevya. Maafisa wa serikali walitoa habari kwa urahisi, na walikubaliana na hali mbaya iliyodhihirika katika ripoti ya mwanzo ya shirika la Human Rights Watch.

Baadhi ya ukiukaji mbaya kabisa wa haki za binadamu zilizopo katika ripoti hii, zinajumuisha mateso, ubakaji uliotendwa na polisi. Elice Mapunda, mkuu wa Maendeleo na Mafunzo katika polisi ya Tanzania na mwanzilishi wa Mtandao wa Polisi Wanawake Tanzania  alihakikishia Human Rights Watch kwamba atasambaza nakala za ripoti hii katika maeneo yote 42 ya makamanda wa polisi na atawahimiza wahakikishe uwajibikaji katika ukiukaji uliofanywa na polisi.

Mapunda alisema kuwa alitumaini kwamba Madawati ya Jinsia yataweza kushughulikia uhasama ulioko kati ya makundi maalum na polisi, lakini akaongezea kwamba wale wanaosimamia Madawati ya Jinsia wanahitaji mafunzo zaidi. Alikiri haja maalum ya kuwawezesha polisi katika kushughulikia maswala ya wana LGBTI. Mapunda alitetea matakwa yanayowataka waathiriwa wa dhuluma kuchukua ile fomu ya PF3 kutoka kwa polisi, akisema kuwa inahitajika maana yake itawawezesha polisi kutambua uhalifu na kuufanyia uchunguzi, kauli ambayo Human Rights Watch na WASO yanashikilia kuwa ni kikwazo kwa haki ya kupata tiba. [276]

Maafisa wa serikali katika taasisi za afya, ikiwemo Tume ya UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Programu ya Kudhibiti UKIMWI Zanzibar, waliliambia Human Rights Watch kuwa wanajitahidi kuhakikisha kwamba hudumu za VVU ni rafiki na zinapatikana kwa wote walioko katika makundi maalum. Mwanzo wa 2013, TACAIDS ilibuni “Jopo kazi kwa ajili ya makundi maalum” (“Key Populations Task Force”) lililojumuisha wanachama wa makundi yaliyotengwa. Jopo hili limewapa wale walioko katika makundi maalum nafasi ya kuchangia sera za serikali zinazowalenga. Kulingana na Dkt. William Kafura wa TACAIDS, polisi imealikwa kumtuma mwakilishi wao mmoja kwenye jopo ili waweze kuelewa kwa kina zaidi masuala ya afya na haki za binadamu yanayoyahurusu makundi maalum. Kafura alisema kuwa alitumai hatua hii itaboresha jinsi polisi wanavyowahudumia watu na kupunguza kukamatwa. [277]

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imefanya kazi kidogo kuhusiana na ulinzi wa haki za wafanyakazi wa ngono, kando na kushirikiana na mashirika ya umma kama KIWOHEDE  linalowapa njia mbadala ya kuchuma riziki. Kwa mujibu wa Naibu wa Katibu Mkuu Anna Maembe, “Tunajua kwamba wafanyakazi wa ngono wanadhulumiwa na polisi pamoja na wateja wao, lakini  hatufuatilii sana maswala haya – ni idara ya polisi ndiyo inapaswa kufanya ufuatiliaji.” Maembe alielezea kuwa maafisa wa wizara wanahusika na kutoa mafunzo kwa polisi wanaosimamia Madawati ya Jinsia; lakini hawajawaelimisha polisi kuhusu namna ya kuwahudumia wafanyakazi wa ngono. Maembe alisema kwamba wizara yake iko tayari kuhusu wazo la kuangazia mambo ya wafanyikazi wa ngono katika mafunzo yao na polisi. Wizara mpaka sasa haijafanya kazi yoyote katika mambo yanayowahusu wanawake wanaofanya mapenzi na wanawake (WSW). [278]

Tanzania haijachukua hatua imara ili kukabiliana na ufisadi, ikiwemo ikiwemo utumiaji wa nguvu na mabavu unaofanywa na polisi kudai pesa na ngono. Katika uchunguzi uliofanywa na Afrobarometer, shirika huru la utafiti wa uchunguzi linaloongozwa na Waafrika, Watanzania waliwachukulia polisi kama wafisadi zaidi katika mwaka wa 2012 ikilinganishwa na 2008. [279] Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  ilibuniwa ili kukidhi haja ya chombo huru cha kuchunguza na kupeleka kortini kesi, hata  na zile zinazohusu kikosi cha polisi, lakini kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, watuhumiwa walikuwa na hatia kortini katika asilimia 1 tu ya kesi ya madai ya ufisadi zilizoletwa kwa TAKAKURU katika miaka saba iliyopita. [280] Aidha kesi nyingi za unyang’anyi haziripotiwi kwa TAKUKURU. Afisa mmoja wa TAKUKURU aliliambia Human Rights Watch kwamba wale walioko katika makundi yaliyotengwa wanapaswa kujisikia huru na wajitokeze wawasilishe malalamiko yao, lakini taasisi hii haijajaribu kuwafikia waliotengwa ili kujenga uaminifu. [281]

Nia njema dhahiriya maafisa wengi wa serikali katika kushughulikia haki za binadamu na upatikanaji wa huduma za afya kwa makundi maalum inasambaratishwa na maafisa wa serikali wakitoa matamshi yasiyokuza stahamala, labda kwa sababu za kuimarika kisiasa. Mnamo machi mwaka wa 2013, afisa mmoja wa serikali ya Zanzibar alitoa wito hadharani kwa wananchi kuungana pamoja dhidi ya wapenzi wa jinsia moja. Kulingana na afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa, katika muktadha ambao fujo ya umma ni jambo la kawaida, matamshi kama hayo yanaweza kuchochea vurugu. [282] Hata hivyo, matamshi yanayotolewa hadharani na maafisa wa serikali juu ya kupunguza madhara kwa wanaotumia dawa za kulevya yamekuwa ya manufaa. Kwa mfano, mnamo Machi 2013, Rais Kikwete alizuru kliniki ya Methadone katika hospitali ya Muhimbili na akaiunga mkono hadharani. [283]

Kuhakikisha kuwa nchi ya Tanzania inatimiza malengo yake ya kuyalinda makundi waliotengwa dhidi ya kuenea kwa VVU, na kuzilinda haki za kimsingi za Watanzania wote, nia njema pekee haitoshi. Hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa kubadilisha sheria na matendo yanayobagua; kuhakikisha uwajibikaji wa wawakilishi wa serikali wanaokiuka haki; na kuwapa mafunzo polisi, wahudumu wa afya, maafisa wa mahakama na wengine kuhusu kuzitekeleza haki za binadamu za wana LGBTI, wafanyabiashara wa ngono na watumiaji wa dawa za kulevya.

IX. Mapendekezo Kamili

Kwa Rais Kikwete na Serikali ya Tanzania

  • Waamrishe polisi hadharani  wakomeshe dhuluma dhidi ya  wafanyabiashara ya ngono, watumiaji wa dawa za kulevya, wapenzi wa jinsia moja, watu wenye jinsia tofauti na asili, na watu wenye jinsia zote mbili.
  • Waibuni  halmashauri huru ya raia isimamie kikosi polisi na ipewe mamlaka ya kupokea malalamishi yanayohusu mwenendo mbaya katika polisi, ifanye uchunguzi na kuyapeleka malalamiko yale kwa waendesha mashtaka.
  • Wahakikishe kwamba mashirika yanayowakilisha watu walio katika makundi yaliyotengwa, wakiwemo wana  LGBTI na wafanyakazi wa ngono, wana uwezo wa kusajiliwa kufuatana na sheria za nchi ya Tanzania.
  • Waridhie Mkataba dhidi ya Mateso.
  • Watenge rasilimali za kutosha katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuimarisha mfumo wa kulinda watoto Tanzania, ikiwa ni pamoja na kupitia utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Huduma kwa Yatima na Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi.

Kwa Mabunge ya Tanzania na Zanzibar

  • Yaanze mchakato wa kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja ya hiari kwa kuandaa marekebisho ambayo yataondoa Ibara ya 154 na 157 kutoka katika Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, marekebisho ya Ibara  150 na 153 kutoka katika Sheria ya Makosa ya Jinai ya Zanzibar, na pia kusisitiza kuondolewa kwa Ibara ya 158 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ya Zanzibar, ambavyo huzuia "muungano" wa wanaouhusiano wa jinsia moja, ambayo inakiuka uhuru wa kujumuika.
  • Yaanze mchakato wa kuhalalisha kazi ya ngono kwa hiairi ya watu wazima na kuandaa rasimu ya muswada wa kurekebisha au kuondoa ibara ya 176(a) cha Kanuni ya Adhabu ya Tanzania na 181(a) ya Sheria ya Makosa ya Jinai ya Zanzibar ambayo inaharamisha biashara ya ngono, pamoja na sheria nyingine zinazohusiana na biashara ya ngono na ambazo zinaingilia haki za kibinadamu pamoja na sheria zinazohusu “kuruhusu au kukubali kwa makusudi makahaba wa kawaida kukusanyika na kubaki katika jengo lake kwa ajili ya ukahaba” na “kuishi kwa kutegemea mapato kutokana na ukahaba.”
  • Yafanye majukumu ya usimamizi wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (Tanzania) na Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala Bora (Zanzibar) na kwa kuchunguza dhuluma ya polisi dhidi ya makundi yaliyotengwa.
  • Kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI (Tanzania), yafanye uchunguzi kuhusu matukio ya kunyimwa huduma na ubaguzi dhidi ya makundi maalum katika upatikanaji wa huduma za VVU/UKIMWI.
  • Yaratibishe na yarekebishe sheria zilizopo ambazo zinaharamisha utumiaji na kuwa na dawa za kulevya kwa matumizi binafsi na yahakikishe kuwa haki za binadamu za watu wanaotumia dawa za kulevya zinalindwa na kuwa sheria zinazohusika na dawa za kulevya haziongezi hatari ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kwa wanaotumia dawa hizo ama kuwatatiza watu hao kupata huduma za kujikinga na matibabu. Pia yaanzishe marekebisho ya Kanuni za Adhabu zote mbili ili ziharamishe ubakaji wa wanaume na wavulana; na zihakikishe kwamba tabia yoyote ya ubakaji ni marufuku.

Kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Jamhuri ya Tanzania, Wizara ya Afya ya Zanzibar, na Asasi Zote za Serikali Zinazohusika na Masuala ya VVU/ UKIMWI

  • Kulingana na mapendekezo ya Mkakati wa Pili wa Taifa Kudhibiti UKIMWI wa Tanzania, zitoe wito hadharani wa kuondoa sheria zinazoharamisha ngono ya watu wa jinsia moja na kazi ya ngono ya hiari kwa watu wazima.
  • Zitoe amri kwa wafanyakazi wa afya kwamba ubaguzi dhidi ya wanachama wa makundi yaliyotengwa, ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa ngono, watu wanaotumia dawa za kulevya, na wana LGBTI, hautakubaliwa kamwe.
  • Zikague vituo vya afya ili kuhakikisha kuwa wanachama wa makundi yaliyotengwa hawanyimwi huduma wala kubaguliwa.
  • Zibuni utaratibu wa malalamishi kwa njia ambayo wanachama wa makundi yaliyotengwa wanaweza kuripoti kesi za kunyimwa huduma au ubaguzi.
  • Zitoe mafunzo kwa wafanyakazi wote wa afya juu ya makundi maalum ikiwa ni pamoja na mafunzo kuhusu haki za binadamu kama vile mafunzo kuhusu mahitaji maalum ya afya ya makundi haya. Mafunzo yafanyike kwa kushirikiana na mashirika ya kiraia yanayowakilisha makundi maalum.
  • Zihakikishe kwamba Mkakati wa Tatu wa  wa Kudhibiti UKIMWI una vifungu vinavyobainisha kwamba vituo vya afya na vituo vya ushauri nasaha na upimaji  (VCT) vipatikane kwa urahisi na makundi maalum, na hutoa mipango madhubuti kwa ajili ya mafunzo ya wafanyikazi wa afya.
  • Zihakikishe kwamba Mkakati wa Tatu wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWIunajumuisha pamoja na masharti juu ya ulinzi wa haki za binadamu za makundi maalum.
  • Zihakikishe kuwa  kondomu na vilainishi vya maji vinapatikana kwa bei  nafuu na  urahisi kwa  walio katika makundi maalum, ama kwa njia ya utoaji wa moja kwa moja na Wizara ya Afya, au kuwezesha mashirika yasiyo ya serikali kuzisambaza.
  • Zipanue upatikanaji wa matibabu yenye huruma na ufanisi kwa ajili ya walioathhiriwa na  utumiaji wa dawa za kulevya.
  • Ziondolee mbali mahitaji ya kwamba waathiriwa wa unyanyasaji walete fomu za PF3 zilizo na sahihi ya polisi kabla ya kupokea matibabu.
  • Zitekeleze Mpango wa Taifa wa Huduma kwa Yatima na Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi ambao unahusisha watoto walioathiriwa na unyonyaji wa kingono. Mpango huo una lengo la kuimarisha uwezo wa jamii na watendaji wa serikali za mitaa kuwalinda watoto wanaoishi katika mazingira magumu, na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya, elimu na huduma nyingine za kuwalinda watoto.
  • Zitoe mafunzo kwa vyombo vya habari vya Tanzania kuboresha maarifa na uelewaji wao wa makundi maalum na uwezo wao wa kuripoti bila kuegemea upande wowote na kujali masuala yanayowahusu walio katika haya makundi maalum.

Kwa Wizara ya Katiba na Sheria ya Jamhuri ya Tanzania na Tume ya Mabadiliko ya Katiba

  • Zihakikishe kwamba marekebisho ya rasimu ya Katiba yanajumuisha kwa undani maswala ya usawa na yasiyo na ubaguzi.
  • Zihakikishe kujumuishwa kwa makundi yaliyotengwa katika mijadala ya kikatiba.

Kwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ya Jamhuri ya Tanzania na Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto ya Zanzibar

  • Zichukue hatua kamili za kulinda haki za watu wazima wanaofanya biashara ya ngono, ikiwa ni pamoja na kuanzisha ubia na mashirika yanayowawakilisha.
  • Zichukue hatua za kukomesha unyonyaji wa kingono kwa watoto na kuwasaidia waathiriwa, kama sehemu ya juhudi za kuendeleza na kutekeleza Mpango wa Taifa wa Kukabiliana na Ukatili Dhidi ya Watoto. Haswa, ni pamoja na shughuli za msaada wa kisheria, huduma za afya na ushauri nasaha na upatikanaji wa elimu, mafunzo ya ufundi, au hatua nyingine za kijamii kuwaunganisha walioathiriwa na jamii. Shughuli lazima pia zijumuishe mafunzo kwa polisi.

Kwa Polisi ya Tanzania na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma.

  • Zitoe amri kwa polisi wote kwamba hakuna mwathiriwa yeyote atakayenyimwa usaidizi, ama kukamatwa, ama kuteswa kwa msingi ya mwenedo wake wa kingono au utambulisho wa kijinsia au hali yake kama mfanyakazi wa ngono au mtumiajiwa dawa za kulevya. Zitangaze hadharani kwamba watu walio katika kundi hili  na walio katika hatari kubwa zaidi wanaweza kuripoti uhalifu bila hatari ya kukamatwa.
  • Zihakikishe kuwepo kwa maafisa ushirikiano wa polisi (police liaisons) kwa kila kikundi cha watu walio katika hatari kubwa zaidi walioangaziwa katika ripoti hii. Maafisa ushirikiano wanafaa wawe polisi wenye rekodi ya uadilifu na wa kuaminika na makundi haya maalum. Wanapaswa kuwa na mamlaka ya kushirikiana na makundi maalum katika kujenga uaminifu na makundi haya, bila ya kutumia taarifa wanazozipata katika kutekeleza majukumu yao dhidi ya wanachama wa makundi hayo.
  • Zichunguze vituo vya polisi na maafisa wa polisi ambao wametajwa katika ripoti hii kuambatana na ukiukaji wa haki za binadamu na panapofaa wafunguliwe mashtaka na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.
  • Zitoe amri kwa polisi kwamba hakuna mtu anapaswa kukamatwa kwa kumiliki vifaa vya kupunguza madhara, kama vile sirinji au sindano safi na jik (bleach) kwa kuzisafisha hizo sindano.
  • Zitoe mafunzo kwa maafisa wanaosimamia “Madawati ya Jinsia” katika vituo vya polisi juu ya mwendendo wa kingono, utambulisho wa kijinsia, na haki za binadamu za wafanyakazi wa ngono na watoto wanaoshiriki katika kazi ya ngono.
  • Ziwatie nguvuni na kuwafunguliwa mashtaka washiriki wa Polisi Jamii, Sungu Sungu na makundi mengine ya kudhibiti usalama katika jamii ambayo hukiuka sheria.
  • Ziimarishe usimamizi wa  vikundi vya kudhibiti usalama katika jamii, ikiwemo kuhakikisha kwamba havibebi bunduki na havitumii nguvu.
  • Zihakikishe kwamba kila mtu anayemtumia, anayemtoa, anayemwingiza, ama anayemnunua mtoto kwa ajili ya unyonyaji wa kingono ashtakiwe, hata akiwa afisa wa polisi ama mfanyakazi wa serikali.
  • Zihakikishe kwamba watoto wanaonyanyaswa kingono ama wanaohusika na biashara ya ngono hawashtakiwi ama kuadhibiwa kisheria kwa kuhusika na biashara haramu  ya ngono.
  • Zihakikishe kwamba mafunzo ya polisi kuhusu haki za binadamu yanafanyika mara kwa mara na vilivyo, na kwamba ni pamoja na mafunzo juu ya haki chini ya sheria ya kimataifa ya wana LGBTI, wafanyabiashara wa ngono na wanaotumia dawa za kulevya.

Kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG)

  • Iwahimize hadharani wana LGBTI, wafanyabiashara wa ngono, na wanaotumia dawa za kulevya kuripoti kesi yoyote ya ubaguzi au unyanyasaji dhidi yao kwa CHRAGG na ichukue hatua mwafaka kuhusu ripoti hizo.
  • Itoe mafunzo kwa wafanyakazi wote kuhusu uvumilivu, na kutobagua, na kuyajali mahitaji ya makundi yaliyotengwa. Mafunzo hayo lazima yafanywe kwa pamoja na wanachama wa makundi haya maalum.
  • Iteue kamishna mmoja ambaye atachukua jukumu la kushugulikia kesi za ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya wanachama wa makundi maalum.
  • Ifanye utafiti wa nchi nzima kuhusu ubaguzi dhidi ya makundi maalum ikijumuika na mashirika ya kijamii yanayo yanawakilisha.

Kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa (TAKUKURU)

  • Iwape maafisa jamii (outreach officers) uwezo wa kushirikiana na wafanyabiashara wa ngono, wanaotumia dawa za kulevya, na wana LGBTI ili wapate taarifa  kuhusu rushwa, ikiwemo rushwa ya ngono inayoathiri jamii hiyo.
  • Iwachukulie hatua za kisheria maafisa wa polisi ambao wanapatikana wakiitisha pesa ama ngono kutoka kwa wanachama wa makundi yaliyotengwa.

Kwa Tume za Kuratibu Udhabiti wa Dawa za Kulevya za Tanzania na Zanzibar

  • Zipitie sheria zilizopo zinazoharamisha kupatikana na dawa za kulevya kwa lengo la kuyatumia mwenyewe, kwa kushauriana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na Ukimwi (UNAIDS)na wataalamu wengine ili kuhakikisha kwamba sheria za dawa za kulevya zinaambatana na malengo ya kuzuia ueneaji wa VVU na kulinda haki za binadamu.

Kwa Asasi za Umoja wa Mataifa Zinazofanya Kazi Nchini Tanzania, ikiwa ni pamoja na UNAIDS, UNDP, UNFPA, UNICEF, na UN Women

  • Yashiriki katika utetezi hadharani na faragha na serikali ya Tanzania kuhusu haki za watu waliomo katika makundi yaliyotengwa, chini ya sheria za kimataifa.
  • Yapange mazungumzo na maafisa wa serikali kuhusu chapisho za hivi karibuni ikiwemo utafiti wa Umoja wa Mataifa ambazo zinaangazia kwamba uharamishaji  wa biashara ya ngono na uhusiano wa jinsia moja unatia vikwazo kwa  uzuiaji  na matibabu ya VVU.
  • Yarekodi ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya wafanyakazi wa ngono, wana LGBTI, na watu wanaotumia dawa za kulevya. Yaripoti ukiukaji huo kwa serikali ya Tanzania na katika mazingira mengine yanayofaa kama vile Mfumo wa Kimataifa wa Mapitio ya Haki za Binadamu (Universal Periodic Review, UPR) katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.
  • Yaendeshe mafunzo kwa vyombo vya habari vya Tanzania kuboresha maarifa na uelewaji wao wa makundi maalum na uwezo wao wa kuripoti bila kuegemea upande wowote na kujali masuala yanayowahusu walio katika makundi haya maalum.
  • Yahakikishe kwamba mafunzo yanayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa maafisa wa polisi, maafisa wa haki serikalini na maafisa wa afya yanajumuisha maswala ya haki za binadamu za makundi yaliyotengwa.
  • Kwa Serikali na Asasi Fadhili Zinazosaidia Mipango ya VVU/UKIMWI au Haki za Binadamu nchini Tanzania

    • Ziimarishe maendeleo ya mashirika ya wafanyakazi wa ngono, wana LGBTI, na watu wanaotumia dawa za kulevya, ili wawe na mashirika yanayoheshimiwa na yanawakilisha matakwa yao.
    • Zihakikishe kwamba ufadhili unaoelekezwa kwa VVU/UKIMWI nchini Tanzania unajumuisha fedha ambazo zimetengwa mahususi kwa matumizi katika mahitaji ya makundi maalum, na pia zihakikishe uwajibikaji katika matumizi ya fedha hizo.
    • Zihakikishe kwamba mashirika yanayotetea haki zote za binadamu ambayo hupokea ufadhili, yanatetea pia kwa makini haki za wafanyabiashara wa ngono, wana LGBTI na watu wanotumia dawa za kulevya.
    • Zifadhili mipango maalum ambayo huwasaidia watoto walioathiriwa na unyanyasaji wa kingono ukiwemo Mpango wa Taifa wa Huduma kwa Yatima na Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatarishi na  Mpango  wa Taifa wa Kukabiliana na Ukatili Dhidi ya Watoto
    • Zishiriki katika utetezi hadharani na faragha na serikali ya Tanzania kuhusu haki za watu waliomo katika makundi yaliyotengwa, chini ya sheria za kimataifa.
    • Zihakikishe  kwamba mafunzo yanayofadhiliwa na wafadhili kwa maafisa wa polisi, maafisa wa haki serikalini na maafisa wa afya yanajumuisha maswala ya haki za binadamu za makundi yaliyotengwa.

    X. Shukrani

    Ripoti hii ilifanyiwa utafiti na Neela Ghoshal, mtafiti katika Programu ya Haki za LGBT katika shirika la Human Rights Watch; Elula Kibona, mshauri kwa Programu ya Haki za LGBT katika shirika la Human Rights Watch; Abdilah Diwani, Katibu Mtendaji wa Muungano wa WASO; na Geoffrey Mashala, mwanachama wa Muungano wa WASO. Ally Semsella na Peter Celestine, vile vile wa Muungano wa WASO, na Edward Nsajigwa, mkurugenzi wa Nyerere Centre for Human Rights, walisaidia kufanya baadhi ya mahojiano.

    Ripoti hii iliandikwa na Neela Ghoshal. Ilihaririwa na Graeme Reid, mkurugenzi wa Programu ya Haki za LGBT katika Human Rights Watch; Rona Peligal, kaimu mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika; Juliane Kippenberg, mtafiti mwandamizi katika Kitengo cha Haki za Watoto; Liesl Gerntholtz, mkurugenzi wa Kitengo cha Haki za Wanawake; Joe Amon, mkurugenzi wa Kitengo cha Afya na Haki za Binadamu; Aisling Reidy, mshauri mwandamizi wa kisheria; na Danielle Haas, mhariri mwandamizi katika Ofisi ya Programu. José Luis Hernandez, mshiriki katika Programu ya Haki za LGBT katika Human Rights Watch, aliratibu uhariri na uzalishaji pamoja na kuisanifisha. Usaidizi zaidi katika uzalishaji ulitolewa na Grace Choi, mkurugenzi wa uchapishaji, na Fitzroy Hepkins, meneja wa barua. Ripoti hii ilitafsiriwa katika lugha ya Kiswahili na Oloo Ochieng’, Naomi Ogutu, Willy Buloso na Neela Ghoshal.

    Watu wengi Tanzania walichangia kwa kiasi kikubwa kutoa mwongozo wa utafiti huu kama John Kashiha wa Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation; Pade Edmund wa Stay Awake Network Activities; Oliver Ndalu wa Young Women Solidarity Organization; Sophia Lugilahe wa Warembo Forum; Habiba Hashimu wa KBH Sisters; Dr. Emmanuel Kandusi wa Centre for Human Rights Promotion (CHRP); Sylvester Mapinduzi na Elizabeth Tobias wa Population Services International (PSI); Usu Mallya wa Tanzania Gender Network Programme (TGNP); Sandrine Pont na Ancella Voets wa “Médecins du Monde”; Suleiman Mauly wa ICAP; Amandine Oleffe wa UNAIDS; Dr. William Kafura wa Tume ya UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Onesmo Paul Kasale Olengurumwa wa Tanzania Human Rights Defenders Coalition.



[1] Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupamabana na UKIMWI (UNAIDS), “Monitoring and evaluation of key populations at higher risk for HIV,” http://www.unaids.org/en/dataanalysis/datacollectionandanalysisguidance/monitoringandevaluationofkeypopulationsathigherriskforhiv/ (ilisomwa Mei 8, 2013).

[2]Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), “VVU / UKIMWI Tanzania,” http://www.tacaids.go.tz/tacaids_sw/ (ilisomwa Juni 14, 2013).

[3]Jacques Morisset, Waly Wane na Isis Gaddis, “HIV/Aids: Still Claiming Too Many Lives,” imeandikwa katikaAfrica Can … End Poverty (blogu), Februari 12, 2013, http://blogs.worldbank.org/africacan/hivaids-still-claiming-too-many-lives (ilisomwa Aprili 3, 2013).

[4]Mpango wa Kudhibiti Ukimwi (NACP),“VVU na UKIMWI nchiniTanzania: Taarifa kuhusu Udhibiti wa VVU na UKIMWI nchini . http://www.tanzania.go.tz/pdf/serayaukimwi.pdf (ilisomwa Aprili 3, 2013).

[5] Morisset, Wane na Gaddis, “HIV/Aids: Still Claiming Too Many Lives.”

[6]TACAIDS et. al, “Tanzania: Matokeo ya Utafi ti wa Viashiria vya VVU/UKIMWI na Malaria Tanzania 2011-2012,” Machi 2013, http://www.measuredhs.com/pubs/pdf/MF8/MF8.Kiswahili.pdf (ilisomwa Juni 14, 2013).

[7] Morisset, Wane, and Gaddis, “HIV/Aids: Still Claiming Too Many Lives.” Makala asilia katika lugha ya kingereza ilitafsiriwa kwa Kiswahili na Human Rights Watch.

[8]Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI Kifua Kikuu na Malaria, “Tanzania,” http://www.tacaids.go.tz/tacaids_sw/projects/global-fund.html (ilisomwa Juni 14, 2013). Utoaji wa Mfuko wa Kimataifa unakwenda kwa serikali ya Tanzania, NGOs na mashirika ya kiraia enye  kushughulikia na VVU / UKIMWI.

[9] PEPFAR, “Partnership to Fight HIV/AIDS in Tanzania,” http://www.pepfar.gov/countries/tanzania/ (ilisomwa Aprili 3, 2013)

[10]PEPFAR, “Five-Year Partnership Framework in Support of the Tanzanian National Response to HIV and AIDS, 2009‐ - 2013, Between The Government of the United Republic of Tanzania and the Government of the United States of America,” Machi 4, 2010, http://www.pepfar.gov/documents/organization/138931.pdf, pp. 6-7. Hata hivyo,  ni idadi ya 40% tu ya watu ambao wanapatikana na hali ya juu ya UKIMWI wanapata ART, ikilinganishwa na 82%  Zambia, 72% Kenya, 67%  Malawi, na 54%  Uganda. Soma Morisset, Wane na Gaddis, “HIV/Aids: Still Claiming Too Many Lives.”

[11]Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), “Monitoring and evaluation of key populations at risk for HIV,” http://www.unaids.org/en/dataanalysis/datacollectionandanalysisguidance/monitoringandevaluationofkeypopulationsathigherriskforhiv/ (ilisomwa Aprili 3, 2013). Sio tu makundi maalum  yanayoshughulikiwa katika ripoti hii  ambayo ni ngumu kufikia; makundi mengine pia yanahitaji tahadhari katika jitihada  ya Tanzania kupiganisha VVU / UKIMWI, ikiwemo wa mama waja uzito wenye kuwa na UKIMWI vijijini, ambao wana kiwango cha chini cha kupata huduma ya afya kwa ajili ya kuzuia maambukizi kutokea mama kwa mtoto. Mkakati wa mpya wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI Tanzania kwa miaka 2013-2017 umeunda mikakati ya kushughulikia haya makundi mengine ambayo ni ngumu kwa kufikia pamoja na makundi maalum.

[12]National AIDS Control Programme, “HIV Behavioral and Biological Surveillance Survey Among Female Sex Workers in Dar es Salaam, 2010,” 2012, kwenye faili  ya Human Rights Watch.

[13] Kulingana na Shirika la  Umoja wa Mataifa la kupambana na  Ukimwi pamoja  (UNAIDS)  na Shirika la Afya Duniani  (WHO), maambukizi ya UKIMWI miongoni mwa wafanyabiashara wa ngono waliopimwa imeongezeka kutoka asilimia 29 mwaka 1986 na kufika asilimia 49.5 mwaka 1993. Mwaka 2001, karibu asilimia 70 ya wafanyabiashara wa ngono ambao walipimwa Mbeya walikuwa na UKIMWI. UNAIDS/WHO Epidemiological Fact Sheet –2004 update , http://data.unaids.org/Publications/Fact-Sheets01/tanzania_en.pdf (ilisomwa Aprili 3, 2013).

[14] “Preliminary Results from MSM Studies in Dar es Salaam,” Joyce Nyoni, Jasmine Shio na Michael W. Ross, onyesho la power point, kwenye faili  ya Human Rights Watch; mahojiano ya Human Rights Watch na Dr. M.T. Leshabari, Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[15]Eric A. Ratliff  et. al., “An Overview of HIV Prevention Interventions for People Who Inject Drugs in Tanzania,” Advances in Preventive Medicine, Juzuu 2012, p. 1.

[16] Tanzania ni muungano kati ya makoloni  mawili  ya  zamani ya Uingereza, Tanganyika na Zanzibar ambayo ilipata uhuru mwaka 1961 na 1963 na ilijiunga kama Tanzania mwaka 1964,  lakini Zanzibar ilibaki na madaraka kidogo.

[17]Tume ya UKIMWI Zanzibar, “UNGASS Country Progress Report, Zanzibar,” Januari 30, 2008, http://www.unaids.org/en/dataanalysis/knowyourresponse/countryprogressreports/2008otherentities/zanzibar_2008_country_progress_report_en.pdf (ilisomwa Mei 9, 2013), na “HIV Prevalence in Zanzibar and Tanzania,” http://www.zac.or.tz/national-hiv-response/hiv-prevalence-in-zanzibar (ilisomwa Mei 9, 2013).

[18]Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, “Mkakati wa Pili wa Taifa wa Ukimwi Zanzibar (ZNSP-II), 2011-2016.” Utafiti mwingine unayojulikana sana kutoka Zanzibar unaripoti maambukizi ya UKIMWI kwa kiwango cha 12.3% kati ya wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume; soma Dahomaet. al., “HIV and Related Risk Behavior Among Men Who Have Sex with Men in Zanzibar, Tanzania: Results of a Behavioral Surveillance Survey,” AIDS and Behavior, Disemba 8, 2009, DOI 10.1007/s10461-009-9646-7, http://www.deepdyve.com/lp/springer-journals/hiv-and-related-risk-behavior-among-men-who-have-sex-with-men-in-NvOUd0vhH7.

[19]Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), “Guidance Note 2012: Key Programmes to Reduce Stigma and Discrimination and Increase Access to Justice in National HIV Responses,” http://www.unaids.org/en/media/unaids/contentassets/documents/document/2012/Key_Human_Rights_Programmes_en_May2012.pdf (ilisomwa Mei 31, 2013), p. 5. Soma pia Benki ya Dunia (The World Bank),

“Increased Targeting of Key Populations Can Accelerate End of Global HIV Epidemic,” Novemba 28, 2012, http://www.worldbank.org/en/news/press-release/2012/11/28/increased-targeting-key-populations-can-accelerate-end-global-hiv-epidemic (ilisomwa May 31, 2013).

[20] Global Commission on HIV and the Law, “HIV and the Law: Risks, Rights & Health,”July 2012, http://www.hivlawcommission.org/resources/report/FinalReport-Risks,Rights&Health-EN.pdf(ilisomwa May 31, 2013).

[21] Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, “Mkakati wa Pili wa Taifa wa Ukimwi Zanzibar (ZNSP-II), 2011-2016,” uk. 27.

[22] Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, kif. 154.

[23] Ibid., kif. 157.

[24]Kanuni ya Adhabu ya Zanzibar, kif. 150, 153.

[25] Ibid., kif. 158.

[26] Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, kif. 176(a).

[27]Kanuni ya Adhabu ya Zanzibar, kif. 140.

[28] Sheria ya Tanzania, Sura 95, Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya, kif. 17; Drugs and Prevention of Illicit Drgus Act, 2009 (Zanzibar), kif. 15(1)(c), 15(2), kif. 16.

[29]Drugs and Prevention of Illicit Drgus Act, 2009 (Zanzibar), kif.16(1)(c).

[30]Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2011 (Zanzibar), “Marekebisho ya Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya, Nambari ya 2009,” kif. 12.

[31] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Waziri mkuu, Mkakati wa Pili wa Taifa  wa Kudhibiti Ukimwi, 2008-2012 (Toleo la Pili), Oktoba, 2007,http://www.entersoftsystems.com/tacaids/documents/MKAKATI%20WA%20UKIMW%202008%20-2012.pdf (ilisomwa Juni 16, 2013), uk. 48, mkakati “10.”

[32]Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Waziri mkuu,The Second National Multi-sectoral Strategic Framework on HIV/AIDS, 2008-2012 (Second Edition), (English version), Oktoba 2007, http://www.entersoftsystems.com/tacaids/documents/NMSF%20%202008%20-2012.pdf (ilisomwa Juni 16, 2013), uk. 57, mkakati “j.”

[33] Mahojiano ya Human Rights Watch na Dkt. Salash Toure, Disemba 4, 2012.

[34] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO na mwakilishi wa shirika linaloshughulika na VVU/UKIMWI, Arusha, Disemba 4, 2013.

[35] Mahojiano ya Human Rights Watch na Umukulthum Ansell, mkurugenzi wa ZAYEDESA, Zanzibar, Septemba 13, 2012.

[36] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO na mwakilishi wa shirika la Tanzania Women Living with HIV/AIDS (TAWLWHIA), Mwanza, Oktoba 25, 2012.

[37] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO na mwakilishi wa shirika la Engender Health, Mwanza, Oktoba 25, 2012.

[38] Mahojiano ya Human Rights Watch na Dkt. Joyce Nyoni, Dar es Salaam, Septemba 14, 2012.

[39] Mahojiano ya Human Rights Watch na viongozi wa CHRAGG, Dar es Salaam, Mei 14, 2012.

[40]Ibid.

[41] Joyce E. Nyoni na Michael W. Ross, “Condom Use and HIV-related behaviors in urban Tanzanian men who have sex with men: A study of beliefs, HIV knowledge sources, partner interactions and risk behaviours,” AIDS Care, 2012, uk. 5.

[42]Mahojiano ya Human Rights Watch na Dr. M.T. Leshabari, Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[43] Mahojiano ya Human Rights Watch na Daudi L., Mwanza, Oktoba 26, 2012.

[44] Mahojiano ya Human Rights Watch na kashif M., Mwanza, Oktoba 27, 2012.

[45]PSI, shirika la kimataifa la afya, lina mpango wa kuanzisha mradi unaolenga kuzuia maambukizi ya VVU miongoni mwa wafanyabiashara wa ngono Arusha. Mahojiano ya Human Rights Watch na wafanyakazi wa PSI, Arusha, Disemba 3, 2012.

[46] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwanaharakati Mtanzania wa haki za binadamu, Kampala, Aprili 17, 2013.

[47] Mfululizo wa hivi karibuni wa mashambulizi dhidi ya makanisa nchini Tanzania yalihoji utamaduni wa nchi wa kuvumiliana kidini. "Religious clashes in Tanzania, problems in government," InformAfrica, Oktoba 18, 2012, http://www.informafrica.com/breaking-news-africa/news-religious-clashes-in-tanzania-problems-in-governnment/ (Ilisomwa 21 Januari 2013).

[48]Mahojiano ya Human Rights Watch na Sabas Masame, mkurugenzi wa Kituo cha Dogodogo, Dar es Salaam, Septemba 3, 2012; na Justa Mwaituka, mkurugenzi wa KIWOHEDE, Dar es Salaam, Septemba 3, 2012; na pamoja na mwakilishi wa shirika la haki za binadamu anayefanya kazi na wakimbizi, Dar es Salaam, Septemba 7, 2012. Kuhusu ulemavu wa ngozi, tazama Under the Same Sun, "Children with Albinism in Africa: Murder Mutilation and Violence – A report on Tanzania, With parallel references to other parts of Sub-Saharan Africa," Juni 19, 2012, http://www.underthesamesun.com/sites/default/files/UTSS%20report%20to%20UN%20-%20REPORT_0.pdf (ilisomwa Mei 9, 2013).

[49] Katrina Manson, "Politics: Young activists bring a belief that things must change," Financial Times, Disemba 6, 2012, http://www.ft.com/intl/cms/s/0/02230122-3bcf-11e2-b45f -00144feabdc0.html (ilisomwa Disemba 8, 2012).

[50] Mahojiano ya Human Rights Watch na Edward Nsajigwa wa Nyerere Centre for Human Rights, Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[51] Mahojiano ya Human Rights Watch na wawakilishi wa balozi Tanzania, Dar es Salaam, Mei 2012.

 

[52] Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, kif.154.

[53]   Human Rights Watch, This Alien Legacy: The Origins of "Sodomy" Laws in British Colonialism, Disemba 17, 2008, http://www.hrw.org/reports/2008/12/17/alien-legacy-0.

[54] UHAI, "A People Condemned: The Human Rights Status of Lesbian, Gay, Bisexual, Transgender and Intersex Persons in East Africa, 2009-2010," 2010, http://www.uhai-eashri.org/ENG/resources (ilisomwa Januari 21, 2013).

[55] Global Gayz, "Gay Tanzania News and Reports," http://archive.globalgayz.com/africa/tanzania/gay-tanzania-news-and-reports/ # article1 (ilisomwa Januari 13, 2013).

[56]  Privatus Lipili, "New turn in homosexuality storm in African church," The Guardian, Machi 2, 2007, http://www.bongo5.com/new-turn-in-homosexuality-storm-in-anglican-church-03-2007 /; "Bishops and Homosexuality," Tanzanian Affairs, Septemba 1, 2008, Toleo 91, Dini, http://www.tzaffairs.org/2008/09/bishops-homosexuality/ (ilisomwa 16 Januari 2013).

[57] Mahojiano ya Human Rights Watch na wafanyakazi wa TGNP pamoja na washiriki wa Tamasha ya Jinsia Dar es Salaam, Mei 2012.

[58] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Saidi W., Dar es Salaam, Juni 30, 2012.

[59] Mahojiano ya Human Rights Watch na wafanyakazi wa TGNP pamoja na Washiriki wa Tamasha ya Jinsia Dar es Salaam, Mei 2012.

[60] Chini ya mchakato huu, rekodi ya haki za binadamu ya kila nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa inatathminiwa kila baada ya miaka minne na nchi nyingine, ambao hutoa mapendekezo ya jinsi gani nchi inayotathminiwa inaweza kufanya marekebisha ili kuboresha rekodi yake za haki za binadamu. Tazama: http://www.ohchr.org/EN/HRBodies/UPR/Pages/UPRMain.aspx.

[61]   UPR-INFO.ORG, "Responses to Recommendations: Tanzania," http://www.upr-info.org/IMG/pdf/recommendations_to_tanzania_2012.pdf (ilisomwa Januari 16, 2012).

[62]  "Homosexuality? Not in Tanzania!" Daily News (Dar es Salaam), Novemba 5, 2011, http://www.dailynews.co.tz/editorial/?n=25180 (ilisomwa Januari 16, 2013).

[63]  Ibid.

[64] Tazama kwa mfano International Gay and Lesbian Human Rights Commission (IGLHRC), "Tanzania: Arbitrary Arrests and Detemtions of Gay and Lesbian Activists," Oktoba 30, 2009, http://www.iglhrc.org/cgi-bin/iowa/article / takeaction/resourcecentre/993.html (ilisomwa Januari 16, 2013).

[65]  Mwanafunzi gay aliyehojiwa kwa ajili ya ripoti hii alifukuzwa kwa muda kutoka Shule ya Sekondari ya Baraa, shule ya umma mjini Arusha, kwa ajili ya kuonekana kama mwanamke, wakati msagaji alisema yeye alifukuzwa kutoka shule ya kibinafsi ya sekondari wakati utambulisho wake wa kijinsia ulipojulikana na mkurugenzi wa shule. 

[66] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Lester F., Arusha, Disemba 3, 2012, pamoja na Rebecca F., Dar es Salaam, Mei 15, 2012. Wasagaji wawili jijini Dar es Salaam waliripoti kufurushwa na wamiliki wa nyumba zao: Mahojiano ya Human Rights Watch mahojiano na Rebecca F., Dar es Salaam, Mei 15, 2012, na kwa Ruqayya V., Dar es Salaam, Julai 24. 2012. Ubaguzi pia unafanyika katika maeneo ya kazi: mtu mmoja shoga alisema alikuwa taarishi katika ofisi ya sheria, lakini "waliniambia nitafute kazi nyingine ya kufanya wakati walipogundua nilikuwa shoga." Mahojiano ya Human Rights Watch na Terence G., Dar es Salaam, Mei 7, 2012.

[67] Mhaojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa mwakilishi wa asasi ya kijamii, Tanga, Septemba 6, 2012.

[68]  Mahojiano ya Human Rights Watch, tarehe na mahali zimewekwa siri.

[69] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ali L., Tanga, Septemba 5, 2012

[70] Mahojiano ya Human Rights Watch na Abdalla J., Dar es Salaam, Mei 8, 2012.

[71] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Nicholas Y., Septemba 6, 2012

[72] Tazama, kwa mfano, Marian Stevens, Gender Dynamix, "Transgender access to sexual health services in South Africa: findings from a key informant survey,” September 2012, http://www.genderdynamix.org.za/wp-content/uploads/2012/10/Transgender-access-to-sexual-health-services-in-South-Africa.pdf (ilisomwa Mei 31, 2013). Utafiti alihitimisha, "Ni dhahiri kwamba huduma za afya zilizopo kwa sasa ni za kibaguzi na wafanyakazi wa afya hutoa huduma duni kwa watu wenye jinsia tofauti na asili."

 

[73] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO na Saidi W., Dar es Salaam, June 30, 2012.

[74] Kerrigan et.al, The Global HIV Epidemics Among Sex Workers, uk. xxvii na xxxiii.

[75]   Ibid. uk. 284 na 285.

[76]   Programu ya Kitaifa ya Kudhibiti UKIMWI (NACP), "HIV Behavioral and Biological Surveillance Survey Among Female Sex Workers in Dar es Salaam, 2010," Julai 2011, uk. 31.

[77] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa AMREF, Mwanza, Oktoba 26, 2012.

[78] Mahojiano ya Human Rights Watch na Dhuriya M., Itumbi (Wilaya ya Chunya), Disemba 9, 2012.

[79] Programu ya Kitaifa ya Kudhibiti UKIMWI, "HIV Behavioral and Biological Surveillance Survey Among Female Sex Workers in Dar es Salaam," Julai 2011, uk. 41.

[80] Ibid. uk. 14.  

[81] Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, "Violence Against Children in Tanzania: Findings from a National Study  2009," http://www.unicef.org/media/files/VIOLENCE_AGAINST_CHILDREN_IN_TANZANIA_REPORT.pdf (ilisomwa Mei 31, 2013), uk 75 na 76. Utafiti haukushirikisha visa vya  kesi za wavulana wanaoshiriki katika kazi ya ngono. Human Rights Watch na WASO wanafahamu kwamba visa kama hivyo vipo, lakini hatukuwahoji watoto wa kiume wanaofanya kazi ya ngono wakati tukifanya utafiti kwa ajili ya ripoti hii.

[82] Tazama Mkataba wa 182 wa Shirika La Kazi Duniani (ILO) wa 1999 kuhusu Mifumo Mibaya ya Ajira ya Watoto (Convention concerning the Prohibition and Immediate Action for the Elimination of the Worst Forms of Child Labour), ulioanza kutekelezwa Novemba 19, 2000, ibara 3; Itifaki ya Hiari ya Mkataba wa Kimataifa juu ya Haki za Mtoto kuhusu Usafirishaji Watoto, Ukahaba wa Watoto na picha za Ngono (Optional Protocol to the Convention on the Rights of the Child on the sale of children, child prostitution, and child pornography), azimio A/RES/54/263, la Mkutano wa Baraza Kuu lililopitishwa Mei 25, 2000, lililoanza kutekelezwa Januari 18, 2002, lililokubaliwa Tanzania mnamo Aprili 24, 2003.

[83] Sheria ya Mtoto Namba 21 ya Novemba 20, 2009, http://www.ilo.org/aids/legislation/WCMS_151287/lang--en/index.htm (ilisomwa Mei 31, 2013), kif. 83.

[84] Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Ofisi ya Demokrasia, Haki za Binadamu na Kazi, "2012 Human Rights Reports: Tanzania," Aprili 19, 2013, http://www.state.gov/j/drl/rls/hrrpt/2012/af / 204176.htm (ilisomwa Mei 9, 2013).

[85] Kidato cha tatu ni sawa na darasa la tisa nchini America.

[86] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rosemary I., Mbeya, Disemba 7, 2012

[87]Médecins du Monde”, "Assessment of risk practices and infectious diseases among drug users in Temeke District, Dar es Salaam, Tanzania," 2011, uk. 17. Kwa mujibu wa shirika la “Médecins du Monde”, "Inakadiriwa kuwa hivi leo, kuna 25,000-50,000 PWID [watu ambao kujidunga dawa] nchini Tanzania, ingawa idadi hii inaweza kuwa hata juu zaidi."Tazama pia Ashery Mkama, “Drug Addiction On Increase Countrywide,” Daily News (Dar es Salaam), Disemba 29, 2012, http://allafrica.com/stories/201212310239.html (ilisomwa Mei 9, 2013), akirejelea Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, anakadiria kuwa watu 150,000 hadi 500,000 ni waraibu wa dawa za kulevya nchini Tanzania

[88]   Shirika la Afya Duniani (WHO), "New treatment gives hope to East Africa’s drug users," Jarida la Shirika la Afya Duniani, Juzuu 91, Namba 2, Februari 2013, uk. 81 mpaka 156, http://www.who.int/bulletin/volumes/ 91/2/13-030213/en/index.html (ilisomwa Aprili 3, 2013).

[89]“Médecins du Monde”, "Assessment of risk practices and infectious diseases among drug users in Temeke District, Dar es Salaam, Tanzania," 2011, uk. 10 na 16.

[90]  Mahojiano ya Human Rights Watch na  Sandrine Pont, mratibu mkuu wa nchi na mwakilishi, “Médecins du Monde”, Dar es Salaam, Disemba 6, 2012.

[91] Tanzania: Tackling Drug Abuse in the Islands,” IRIN, Aprili 9, 2010, http://www.irinnews.org/Report/88757/TANZANIA-Tackling-drug-abuse-in-the-islands (ilisomwa Disemba 19, 2012).

[92] Kwa habari zaidi juu ya matibabu ya methadone, tazama Human Rights Watch, Rehabilitation Required: Russia’s Human Rights Obligation to Provide Evidence-based Drug Dependence Treatment, Juzuu 19, Nambari 7 (D) Novemba 2007, http://www.hrw.org/sites/default/files/reports/russia1107webwcover.pdf, uk 107 na 108.

[93] Shirika la Afya Duniani (World Health Organization), "New treatment gives hope to East Africa’s drug users,” Jarida la Shirika la Afya Duniani, Juzuu 91, Namba 2, Februari 2013, uk. 81 mpaka 156, http://www.who.int/bulletin/volumes/ 91/2/13-030213/en/index.html (ilisomwa Aprili 3, 2013).

[94] Mahojiano ya Human Rights Watch na wawakilishi wa Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Zanzibar, Julai 16, 2012.

[95] Mahojiano ya Human Rights Watch na January H., Dar es Salaam, Juni 26, 2012.

[96] Mahojiano ya Human Rights Watch na Abdul P., Zanzibar, Septemba 13, 2012.

[97] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa wafanyakazi wa ngono wa jinsia ya kike, Arusha, Disemba 4, 2012.

[98]   Kituo cha Kisheria na Haki za Binadamu, 2013, uk 21 na 22.

[99]   Kituo cha Kisheria na Haki za Binadamu, 2013, uk 24 na 25. Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, "LHRC iliripoti mnamo Oktoba kwamba hakuna afisa wa polisi au wafanyakazi wengine rasmi wa usalama walikuwa wamehukumiwa kwa mauaji ya raia yalio kinyume cha sheria tangu mwaka 2002. “Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, “2012 Human Rights Reports: Tanzania,” Aprili 19, 2013.

[100]   Asilimia 92 ya Watanzania inaamini kwamba jeshi la polisi ni fisadi, kulingana na utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Afrobarometer na Utafiti wa Sera ya Maendeleo (REPOA). Washiriki waliipa polisi nambari ya kwanza kama asasi fisadi zaidi ya umma nchini Tanzania. REPOA na Afrobarometer, "PROGRESS ON MKUKUTA *: Results from the Afrobarometer Round 5 Survey in Tanzania," Novemba 21, 2012, http://www.afrobarometer.org/files/documents/media_briefing/tan_r5_presentation1_21nov12.pdf, p. 18, 23 (ilisomwa Mei 9, 2013).

[101] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa shirika la misaada ya kigeni, Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[102] Mahojiano ya Human RIghts Watch na mwakilishi wa shirika la haki za binadamu, Dar es Salaam, Septemba 7, 2012; “MPs Join Public in Uproar Against Alleged Traffic Police Corruption,” Daily News (Dar es Salaam), Juni 30, 2012, http: / / allafrica.com/stories/201207020103.html (ilisomwa Mei 9, 2013).

[103] Mahojiano ya Human Rights Watch na Naibu Kamishna wa Polisi Rashid Ali Omar, Dar es Salaam, Septemba 10, 2012.

[104] Mahojiano ya Human Rights Watch na Suleiman R., Dar es Salaam, Juni 26, 2012.

[105] Maskani ni msimu wa Kiswahili unatumika kuaishiria eneo la nje lililowekwa kwa ajili ya matumizi ya dawa za kulevya.

[106] Mahojiano ya Human Rights Watch na Zeitoun Y., Dar es Salaam, Julai 6, 2012.

[107] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwajuma P., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

[108]   Mahojiano ya Human Rights Watch na Ally H., Dar es Salaam, Septemba 15, 2012.

[109]   Ibid.

[110] Mahojiano ya Human Rights Watch na Fazila Y., Dar es Salaam, Julai 18, 2012.

[111] Ibid.

[112] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mickdad J., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

[113] Ibid.

[114] Mahojiano ya Human Rights Watch na John Elias, Dar es Salaam, Juni 26, 2012.

 

[115] Ibid.

[116] Ibid.

[117] Mahojiano ya Human Rights Watch na Edward Nsajigwa, mkurugenzi wa Nyerere Centre for Human Rights, Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[118] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa wa CHRAGG, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013. Tarehe 25 Juni, 2012, mtafiti wa Human Rights Watch alimtembelea Elias nyumbani kwake kuzungumza naye, na kushtukia kujua kwamba mwakilishi wa CHRAGG alikuwa tu amemchukua kwa gari kumpeleka hospitalini. Walikuwa wamemwachia babake Elias barua iliyoonyesha kisa hicho kilikuwa kinachunguzwa. Human Rights Watch ina nakala ya barua hiyo katika faili yetu, ambayo ina tarehe ya "HB/S/3/11/12/IGP/DSM ya Septemba 7, 2011." CHRAGG hawakujibu barua pepe za kuchunguza kutoka kwa Human Rights Watch zilizotumwa Agosti 28, 2012, na tarehe 28 Machi, 2013, kuhusu hatua mahususi ambazo tume ilikuwa imechukua kushughulikia kisa hicho.

[119] Mahojiano ya Human Rights Watch na Musa E., Mbeya, Disemba 12, 2012.

[120] Mahojiano ya Human Rights Watch na Omary Q., Zanzibar, Mei 17, 2012.

[121] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasir O., Zanzibar, Mei 17, 2012.

[122] Ibid.

[123] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sharifa Z., Zanzibar, Septemba 13, 2012.

[124] Mahojiano ya Human Rights Watch na Collins A., Dar es Salaam, Juni 22, 2012.

[125] Ibid.

[126] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Lester F., Arusha, Disemba 3, 2012.

[127] Ibid.

[128]   Mahojiano ya Human Rights Watch na Mariam H., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[129] Mahojiano ya Human Rights Watch na Walid A., Zanzibar, Septemba 13, 3012.

[130] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alex N, Dar es Salaam, Mei 8, 2012.

[131] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Jessie L., Dar es Salaam, Juni 28, 2012.

[132] Mahojiano ya Human Rights Watch na Halima Y., Dar es Salaam, Aprili 12, 2013.

[133] Mahojiano ya Human Rights Watch na Amanda Z., Dar es Salaam, Aprili 12, 2013.

[134] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ramazani H., Dar es Salaam, Juni 27, 2012  

[135]   Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Wilson N, Dar es Salaam, Juni 30, 2012

[136] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alamisi V Disemba 7, 2012.

[137] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jenifer A., ​​Mbeya, Disemba 7, 2012.

[138] Mahojiano ya Human Rights Watch na Khadija J., Mbeya, Disemba 7, 2012.

[139] Ibid.

[140] Mahojiano ya Human Rights Watch na Adimu S., Mbeya, Disemba 7, 2012.

[141] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rosemary I., Mbeya, Disemba 7, 2012.

[142] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ruby C., Mwanza, Oktoba 25, 2012.

[143] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Bishara A., Mwanza, Oktoba 26, 2012.

[144] Mahojiano ya Human Rights Watch na Harun Z., Dar es Salaam, Juni 26, 2012.

[145] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ilham K., Dar es Salaam, Julai 4, 2012.

[146] Mahojiano ya Human Rights Watch na Evelyn D., Dar es Salaam, Julai 18, 2012.

[147] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Edwin J., Dar es Salaam, Juni 22, 2012.

[148] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Henry O., Mwanza, Oktoba 27, 2012.

[149] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ilham K., Dar es Salaam, Julai 4, 2012.

[150] Tazama François Ayissi et al. v Cameroon, Kundi la Umoja wa Mataifa Kuhusu Kukamatwa Kiholela, Maoni Nambari 22/2006, stakabadhi ya Umoja wa Mataifa A/HRC/4/40/Add.1 at 91 (2006), kwenye faili ya Human Rights Watch.

[151] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Mohammed R., Dar es Salaam Julai 5, 2012.

[152] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Victor G., Dar es Salaam, Mei 8, 2012

[153] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Joseph S., Dar es Salaam Julai 5, 2012.

[154] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Hussein M., Dar es Salaam Julai 5, 2012.

[155] Mahojiano ya Human Rights Watch na Hamisi K., Zanzibar, Septemba 13, 2012.

[156] Mahojiano ya Human Rights Watch na Hayat E., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[157] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwajuma P., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

 

[158] Moja kati ya makundi hayo ya wanamgambo ni kundi la mgambo, wanamgambo waliopewa mafunzo na wanajeshi wa Tanzania. Tulipokea taarifa kidogo sana kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu na kikundi cha mgambo.

[159] “Zanzibar Falls Victim to the International Heroin Trade,” VOA, Machi 4, 2012 (ilisomwa 19 Disemba 2012).

[160] Tazama Horace Campbell, “Popular Resistance in Tanzania: Lessons from the Sungu Sungu,” History research seminar series, 1987, katika faili ya Human Rights Watch.

[161] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria Namba 9 ya 1989, Marekebisho ya Sheria ya Wanamgambo, Na. 9 (kwa Kiingereza), http://www.egov.go.tz/home/pages/61/420 .

[162] Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Ofisi ya Demokrasia, Haki za Binadamu na Kazi, “Country Reports on Human Rights Practices for 2011: Tanzania,” http://www.state.gov/documents/organization/186460.pdf, uk. 7 (ilisomwa Januari 23, 2013).

[163] Mahojiano ya Human Rights Watch na Kamishna wa Polisi Paul Chagonja, kaimu Inspekta Mkuu wa Polisi, Dar es Salaam, Septemba 10, 2012.

[164] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alfie N., Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[165] Mahojiano ya Human Rights Watch, Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[166] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alfie N, Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[167] Mahojiano ya Human Rights Watch na mama mwathirika, Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[168] Ibid.

[169] Mahojiano ya Human Rights Watch na wafanyakazi wa shirika la “Médecins du Monde”, Dar es Salaam na kwa njia ya simu, Disemba 6, 2012.

[170] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rashid E., Dar es Salaam, Juni 26, 2012. Watafiti wa Human Rights Watch waliona kidole cha Rashid E. kilichoharibiwa, na alama pana, nyeusi, kwenye mkono wake, ambazo ziliwiana na kupigwa kwa upanga.

[171] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwanahamisi K., Dar es Salaam, Juni 25, 2012.

[172] Ibid.

[173]   Mahojiano ya Human Rights Watch na Angela G., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[174]   Mahojiano ya Human Rights Watch na Susan N., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[175] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rosemary I., Nadia O., na Asha W., Mbeya, Disemba 7, 2012.

[176] Mahojiano ya Human Rights Watch na John Badia Olwasi, mkurugenzi wa CADAAG, Arusha, Disemba 3, 2012.

[177] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwanaharakati wa eneo hilo, Mwanza, Oktoba 27, 2012.

[178] Mahojiano ya Human Rights Watch na mfanyakazi wa huduma za kusaidia aliyetumwa nje ya kituo, Zanzibar, Mei 17, 2012.

[179] Ibid.

[180] Mahojiano ya Human Rights Watch na Idris Z., Zanzibar, Mei 17, 2012.

[181] Mahojiano ya Human Rights Watch na Abdilah D., Dar es Salaam, Mei 9, 2012.

[182] Ibid.

[183] Mahojiano ya Human Rights Watch na Ally H., Dar es Salaam, Septemba 15, 2012.

[184] Ibid

[185] Mahojiano ya Human Rights Watch na Asha W., Mbeya, Disemba 7, 2012.

[186] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwamini K., Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[187]Mahojiano ya Human Rights Watch na Louisa T., Mwanza, Oktoba 25, 2012.

[188]   Mahojiano ya Human Rights Watch na Mickdad J., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

[189] Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimerekodi visa kadhaa vya vikundi vya watu wanaojichukulia sheria mikononi nchini Tanzania; ripoti ya hivi karibuni iligundua kwamba "watu wengi walioathiriwa na aina hii ya kizamani ya adhabu ya jamii ni wezi wa kuchomoa mifuko ya watu, wezi wadogo wadogo, watu wanaotuhumiwa kuwa wachawi na watu wengine wanaoaminiwa kuwa chanzo cha matatizo kwa jamii." LHRC, 2013, uk 26 mpaka 31. Makala asilia katika lugha ya kingereza ilitafsiriwa kwa Kiswahili na Human Rights Watch.

[190] Mahojiano ya Human Rights Watch na Watende A., Dar es Salaam, Julai 6, 2012.

[191]Mahojiano ya Human Rights Watch na Jamal P., Zanzibar, Mei 17, 2012.

[192]Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Abdalla J., Dar es Salaam, Mei 8, 2012.

[193] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Rahim R., Dar es Salaam, Mei 8, 2012.

[194]Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ramazani H., Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[195] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Wilson N, Dar es Salaam, Juni 30, 2012.

[196] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ismail P., Dar es Salaam, Juni 27, 2012

[197] Kulingana  na afisa katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Madawati 417 ya Jinsia yalikuwa yameanzishwa kote nchini kufikia Aprili 2013. Hata hivyo, afisa huyo alikubali kuwa maafisa ambao walikuwa wamepewa mafunzo ya kuendesha Madawati ya Jinsia hawakuwa wamepokea mafunzo juu ya mahitaji ya wafanyabiashara ya ngono. Mahojiano ya Human Rights Watch na Anna Maembe, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, na Watoto, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013.

 

[198] Mahojiano ya Human Rights Watch na Geoffrey Kiangi, kaimu mkurugenzi wa Huduma ya Kinga, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Septemba 10, 2012.

[199] Mahojiano ya Human Rights Watch na wawakilishi wa Mpango wa Kudhibiti UKIMWI Zanzibar, Zanzibar, Mei 17, 2012.

[200] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwanaharakati wa haki za LGBT, Dar es Salaam, Mei 7, 2012.

[201] Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Killian, Mwakilishi wa Nchi wa Engender Health nchini Tanzania, kupitia kwa simu, Oktoba 25, 2012.

[202]  Mawasiliano ya barua pepe kutoka kwa afisa wa “Médecins du Monde” na Human Rights Watch, Machi 18, 2013.

[203] Mahojiano ya Human Rights Watch na Christian B., Mbeya, Disemba 12. 2012.

[204] Mahojiano ya Human Rights Watch na John Badia Olwasi, Mkurugenzi wa CADAAG, Arusha, Disemba 3, 2012.

[205]  Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa AMREF, Mwanza, Oktoba 26, 2012.

[206] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa MSM, Dar es Salaam, Juni 2012; mahojiano ya Human Rights Watch na Dr. Simon Yohana, mkurugenzi wa PASADA, Dar es Salaam, Julai 6, 2012.

[207]  Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Collins A., Dar es Salaam, Juni 22, 2012.

[208]Mahojiano ya Human Rights Watch na Alex N., Dar es Salaam, Mei 8, 2012

[209]Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Yusuf G., Dar es Salaam, Juni 30, 2012.

[210] Mahojiano ya Human Rights Watch na Ally Semsella na Peter Celestine, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013.

[211]Mahojiano ya Human Rights Watch na Jamal P., Zanzibar, Mei 17, 2012.

[212] Mahojiano ya Human Rights Watch na wawakilishi wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Zanzibar, Mei 16, 2012.

[213] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwanaharakati wa haki za LGBT, Zanzibar, Mei 17, 2012.

[214]Mahojiano ya Human Rights Watch na Dk Ramadhan Issa Hassan, mtaalamu wa makundi maalum katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar, Septemba13, 2012.

[215] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Lester F., Arusha, Disemba 3, 2012.

[216]Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Carlos B., Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[217] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ismail P., Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[218] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Mohammed R., Dar es Salaam Julai 5, 2012.

[219] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Peter E., Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[220] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ismail P., Dar es Salaam, Juni 27, 2012.

[221] Mahojiano ya Human Rights Watch na Hayat E., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[222]  Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwajuma P., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

[223] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mickdad J., Dar es Salaam, Julai 3, 2012.

[224]Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa mwakilishi wa asasi ya kijamii, Tanga, Septemba 6, 2012

[225] Human Rights Watch na WASO hawakuweza kubaini chanzo cha kisheria au kanuni za udhibiti wa uhitaji wa PF3. Afisa wa polisi aliiambia Human Rights Watch kuwa yeye aliamini mahitaji ya fomu ya PF3 ilikitwa katika Kanuni ya Jinai, lakini si hivyo. Wizara ya Ustawi wa Afya na Jamii hawakujibu barua kutoka Human Rights Watch, iliyotumwa kwa njia ya mikononi mnamo Aprili 8, 2013, ikitaka kujua hadhi ya kisheria ya fomu ya PF3.

[226] Mahojiano ya Human Rights Watch na Naibu Kamishna wa Polisi Rashid Ali Omar, Dar es Salaam, Septemba 10, 2012.

[227] Ibid.

 

[228] Mahojiano ya Human Rights Watch na Suleiman R., Dar es Salaam, Juni 26, 2012

[229] Mahojiano ya Human Rights Watch na Susan N., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[230] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Walter S., Mwanza, Oktoba 27, 2012.

[231] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwamini K., Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[232] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Jamila H., Dar es Salaam, Julai 4, 2012.

[233] Mahojiano ya Human Rights Watch na Maureen B., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[234] Mahojiano ya Human Rights Watch na Dalili S., Dar es Salaam, Julai 24, 2012.

[235] Florence Mugarula, "Tanzania: Ministry Moves to Assist Gender Violence Victims," The Citizen (Dar es Salaam), Disemba  18, 2011, http://allafrica.com/stories/201112191419.html (ilisomwa Februari 11, 2013); mawasiliano ya barua pepe kwa Human Rights Watch kutoka kwa mwakilishi wa Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA). Juni 5, 2013.

[236] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwamini K., Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[237]Mahojiano ya Human Rights Watch na Pili M., Dar es Salaam, Mei 15, 2012.

[238] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Melissa L., Arusha, Disemba 4, 2012. 

[239] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwakilishi wa ZASOSE, asasi ya kijamii, na ICAP, shirika la kimataifa lisilo la serikali, Zanzibar, Mei 16, 2012

[240]  Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Lester F., Arusha, Disemba 3, 2012.

[241] Mahojiano ya Human Rights Watch na Christian B., Mbeya, Disemba 12, 2012.

[242] Mahojiano ya Human Rights Watch na WASO kwa Ali L., Tanga, Septemba 5, 2012.

 

[243]Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCPR), uliopitishwa 16 Disemba 1966, G.A. Res. 2200A (XXI), 21 U.N. GAOR Supp. (Nambari. 16) katika 52, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa. A/6316 (1966), 999 U.N.T.S. 171, ulioanza kutekelezwa mnamo Machi 23, 1976, na kukubalika Tanzania mnamo Juni 11, 1986. Ibara ya 2 na 26 ya ICCPR yathibitisha usawa wa watu wote mbele ya sheria na haki ya uhuru dhidi ya ubaguzi. Ibara ya 17 inalinda haki ya faragha. Tazama pia Toonen V. Australia, kongamano la 50, Tamko Nambari 488/1992, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa CCPR/C/50/D/488/1992, Aprili 14, 1994, sehemu ya 8.7.

[244] Tazama François Ayissi et al. v. Cameroon, Kamati ya Utendakazi kuhusu Kukamatwa Kiholela, Maoni Namba 22/2006, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa. A/HRC/4/40/Add.1 katika 91 (2006), kwenye faili ya Human Rights Watch.

[245] Mkataba wa Afrika [Banjul] wa Haki za Binadamu na Haki za Watu, iliyopitishwa Juni 27, 1981, Stakabadhi ya Shirika la Umoja wa Afrika (OAU). CAB/LEG/67/3 rev. 5, 21I.L.M. 58 (1982), ulianza kutekelezwa Oktoba 21, 1986, na kukubaliwa Tanzania, Februari 18, 1984, ibara ya 2. Tazama Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Haki za Watu, Zimbabwe Human Rights NGO Forum v. Zimbabwe, uk. 169 na 128 AHRLR (ACHPR 2006).

[246] Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (ilivyorekebishwa mwisho 1985) [Jamhuri ya Muungano ya Tanzania], Aprili 26, 1977, http://www.unhcr.org/refworld/docid/3ae6b50c4.html, (ilisomwa Januari 21, 2013), ibara 9. Matumizi ya mtaji katika sehemu alinukuliwa ifuatavyo asilia.

[247] Ibid. Ibara 13.

[248] Ibid. Ibara 16.

[249]  ICCPR, ibara ya 17.

[250] ICCPR, ibara ya 9; Mkataba wa Afrika [Banjul] wa Haki za Watu na Binadamu, iliyopitishwa 27 Juni 1981, Stakhabadi ya OAU. CAB/LEG/67/3 rev. 5, 21 I.L.M. 58 (1982), ulianza kutekelezwa Oktoba 21, 1986, ibara ya 4, 6.

[251] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (ilivyorekebishwa mwisho 1985) [Jamhuri ya Muungano wa Tanzania], Aprili 26, 1977, http://www.unhcr.org/refworld/docid/3ae6b50c4.html (ilisomwa Januari 21, 2013), ibara ya 15 (2).

[252] Tazama Sheria ya Mtoto Ibara Namba 21 ya Novemba 20, 2009 (ilisomwa Mei 3, 2013), nakala. 83; Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto, Novemba 20, 1989, Umoja wa Mataifa, Mfululizo wa Mikataba, toleo 1577, uk. 3, http://www.unhcr.org/refworld/docid/3ae6b38f0.html (ilisomwa Mei 31, 2013), ibara ya 34; Shirika la Kazi Duniani (ILO), Mapatano  juu ya aina mbaya zaidi za ajira ya watoto, C182, Juni 17,1999, http://www.antislavery.org/includes/documents/cm_docs/2009/i/iloswa.PDF (ilisomwa May 31, 2013), ibara 3 (b), na Mkataba wa Afrika kuhusu Haki na Ustawi wa Mtoto, Stakabadhi ya Shirika la Umoja wa Afrika (OAU) CAB/LEG/24.9/49 (1990), ulianza kutekelezwa Novemba 29, 1999, ibara ya 27.

[253] Mpango Kazi wa Pili wa Taifa wa Huduma kwa Watoto Walio Katika Mazingira Hatarishi, Oktoba 2012, uk. 2, katika faili ya Human Rights Watch.

[254] ICCPR ibara 9; Mkataba wa Afrika [Banjul] wa Haki za Watu na Binadamu, ibara 4, 6.

[255] ACHPR, ibara 5; ICCPR, ibara 7 na 10.

[256] Mkataba Dhidi ya Mateso na Adhabu au Matendo Mengine ya Kikatili, yasiyo ya Kibinadamu au ya Kiudhalilishaji, uliopitishwa Disemba 10, 1984, GA res. 39/46, kiambatisho, 39 U.N.GAOR Supp. (No. 51) katika 197, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa. A/39/51 (1984), ulioanza kutekelezwa Juni 26, 1987

[257] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (ilivyorekebishwa mwisho 1985) [Jamhuri ya Muungano wa Tanzania], Aprili 26, 1977, http://www.unhcr.org/refworld/docid/3ae6b50c4.html (ilisomwa Mei 31, 2013), ibara 13 (6) e.

[258]Ibid., ibara 13 (6) d.

 

[259] Mkataba wa Afrika [Banjul] wa Haki za Binadamu na Haki za Watu, ibara. 16; Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (ICESCR), uliopitishwa Disemba 16, 1966, GA Res. 2200A (XXI), 21 U.N. GAOR Supp. (Nambari 16) katika 49, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa Nambari 49,  A/6316 (1966), 993 U.N.T.S. 3, alipitishwa Januari 3, 1976, kuridhiwa Tanzania Juni 11, 1976, ibara . 12; CEDAW, uliopitishwa Disemba 18, 1979, G.A. Res. 34/180, Stakabadhi ya Umoja wa Mataifa. A/34/46, ulianza kutekelezwa Septemba 3, 1981 na ilikubaliwa Tanzania mnamo Agosti 20, 1985, ibara  12.

[260] Tazama Kamati ya Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni, General Comment No. 20:Non-discrimination in economic, social and cultural Rights (Tamko la Kijumla Nambari 20: Kutobagua katika haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni), (Ibara 2, aya ya 2, ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, kijamii na kiutamaduni), Julai 2, 2009, aya ya. 32. Huku ibara  ya 12 ikitoa dhamana ya haki ya afya, ibara ya 2 (2) inalinda watu binafsi kutokana na ubaguzi katika matumizi ya haki zote zilizoratibiwa na mkataba. Tamko ya Kijumla ya 20 inafafanua kwamba ni marufuku ubaguzi kwa msingi ya mwelekeo wa kingono na utambulisho wa kijinsia.

[261] Kamati ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni (CESCR), The Right to the Highest Attainable Standard of Health (Ibara  12), E/C.12/2000/4, (Agosti. 11, 2000) Tamko la Kijumla Nambari 14, juu ya maudhui kikanuni ya Ibara 12 ya ICESCR, aya ya 9.

[262] The Beckley Foundation Drug Policy Programme, “Recalibrating the Regime: The Need for a Human Rights-Based Approach to International Drug Policy,” Ripoti ya kumi na tatu, Machi 2008, http://www.hrw.org/legacy/pub/2008/hivaids / beckley0308.pdf (ilisomwa Mei 31, 2013), uk 33 na 34.

[263] Eastern African National Networks of AIDS Service Organizations (Mitandao ya Mashirika ya Huduma za UKIMWI katika Afrika Mashariki, EANNASO), “The East African Legislative Assembly passes the EAC HIV & AIDS Prevention and Management Bill 2012," taarifa ya vyombo vya habari isiyo na tarehe (Aprili 2012), http://www.eannaso.org/index.php?option=com_content&view=article&id=48%3Apress-realease-eac-aids-law&catid=73%3Aeac-hiv-bill&Itemid=56&lang=en (ilisomwa Januari 3, 2013).

[264] Muswada wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kudhibiti na Kuzuia VVU/UKIMWI 2012, http://www.eannaso.org/index.php?option=com_docman&task=cat_view&Itemid=10&gid=74&orderby=dmdate_published&ascdesc=DESC&lang=en (ilisomwa Januari 3, 2013), sehemu ya 7 (h) na 11 (d). Hata hivyo, kuchelea kwa Bunge la Afrika Mashariki katika kushughulikia mahitaji ya makundi maalum, na jinsi suala hili muhimu la afya lilivyopigiwa siasa, zinathibitishwa na ukweli kwamba Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki lilidinda kufafanua kile kinachojumuisha “makundi ya watu walio katika hatari kubwa zaidi” katika nakala ya mswada huo. Pendekezo la baadhi ya waandishi kufafanua kuwa istilahi hiyo ilirejelea hasa wanaume wanaofanya ngono na wanaume, wafanyakazi wa ngono na watumiaji mihadarati kwa kujidunga lilikataliwa na maafisa wa serikali waliohusika katika mchakato wa kuandaa muswada huo, ambao walisema kuwa muswada haupaswi "kutambua au kuhalalisha tabia ambayo imeharamishwa waziwazi" na sheria za kitaifa; tazama “Notes to the Draft East African Community HIV and AIDS Prevention and Management Bill,” 2010, http://www.eannaso.org/index.php?option=com_docman&task=cat_view&Itemid=10&gid=74&orderby=dmdate_published&ascdesc=DESC&lang=en (ilisomwa Januari 3, 2013). Muswada huu hivyo basi ni hafifu katika mtazamo wake wa makundi yaliyo katika hatari kubwa zaidi kuliko sheria ya kitaifa nchini Tanzania, Kenya, Rwanda, na Burundi.

[265] Muswada wa Kudhibiti na Kuzuia VVU/UKIMWI Afrika Mashariki 2012, kif. cha 38 (1).

[266] Ibid., kif. 13(b). Sehemu hii inahusu hasa “ubora wa kondomu za kike na za kiume” hata hivyo, kilainisho cha maji kimekubaliwa pia kama njia ya kujikinga inayo julikana. Tazama kwa mfano Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), The Male Latex Condom: 10 Condom Programming Fact Sheets, http://www.unaids.org/en/media/unaids/contentassets/dataimport/publications/irc-pub01/jc003-malecondom-factsheets_en.pdf (ilisomwa Juni 5, 2013), uk. 7.

[267] Umoja wa Afrika, Itifaki ya Nyongeza ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Haki za Watu kuhusu Haki za Wanawake wa Afrika, Julai 11, 2003, http://www.africa-union.org/root/au/Documents/Treaties/Text/Protocol%20on%20the%20Rights%20of%20Women.pdf (ilisomwa Mei 31, 2013), ibara 14(1)d.

[268]   ICCPR, ibara 2, 7, 17.

[269] Itifaki ya Maputo, ibara 3(4).

[270] Ibid. ibara 4(2).

[271] Ibid ibara. 4(2)e.

[272] Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, ibara 131(1); Sheria ya Jinai ya Zanzibar, Nambari 6 ya 2004, kifungu 126 (1).

[273]Kanuni ya Adhabu ya Tanzania,  ibara 130 (1); Sheria ya Jinai ya Zanzibar, sheria ya bunge Nambari 6 ya 2004, kifungu 125 (1).

[274] Sheria za Tanzania, Sura ya 239, Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Namba 11/2007 (PCCA), sehemu  ya 25.

[275] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa wa TAKUKURU, Dar es Salaam, Septemba 11, 2012; PCCA, sehemu ya 52.

[276] Mahojiano ya Human Rights Watch na Elice Mapunda, Dar es Salaam, Aprili 10, 2013.

[277] Mahojiano ya Human Rights Watch na  William Kafura, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013.

[278] Mahojiano ya Human Rights Watch na Anna Maembe, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013.

[279] REPOA na Afrobarometer, "Progress on Mkukuta* : Results from the Afrobarometer Round 5 Survey inTanzania."

[280] Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Ofisi ya Demokrasia, Haki za Binadamu na Kazi, "2012 Human Rights Reports: Tanzania."

[281] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa wa TAKUKURU, Dar es Salaam, Septemba 11, 2012.

[282] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa wa Umoja wa Mataifa, Dar es Salaam, Aprili 8, 2013.

[283] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa wa Umoja wa Mataifa, Dar es Salaam, Aprili 12, 2013; Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam, “President Kikwete Visits CDC Site,” Machi 26, 2013, http://tanzania.usembassy.gov/ph_03262013. html (ilisomwa Mei 9, 2013).