Zaidi ya wanafunzi 120 wa kidato cha pili wakijiandaa kufanya mitihani ya majaribio katika shule ya sekondari huko Mwanza, Kaskazini-Magharibi mwa Tanzania.

Zaidi ya wanafunzi 120 wa kidato cha pili wakijiandaa kufanya mitihani ya majaribio katika shule ya sekondari huko Mwanza, Kaskazini-Magharibi mwa Tanzania. © 2016 Elin Martínez/Human Rights Watch

Muhtasari

Napenda kusoma ili niwe na mawazo mapana. Hakuna ambacho sikupenda kusoma. Nilikuwa na ndoto ya kumaliza shule niende chuo nihitimu, na nifanye kazi kama muhasibu.

Kama ilivyo kwa vijana mamilioni wa Tanzania, Imani, 20, kutoka Mwanza, mkoa wa Kaskazini Magharibi uliyopakana na Ziwa Victoria, alitaka kusoma kadri awezavyo ili aweze kuhitimu, kupata kazi, na aweze kujikimu na kusaidia familia yake. Kuanzia miaka 14, wakati alipojiunga na sekondari, alitembea zaidi ya saa moja na nusu kila siku asubui kufika shule:

Nilikua nafika shule nikiwa nimechoka sana, nikaanza kuchelewa kila wakati. Ninapofika nimechelewa naadhibiwa.

Matarajio ya Imani yalibadilika alipofikia umri wa miaka 16. Alinyanyaswa kingono na mwalimu wake wa mafunzo ya ziada, ambaye alikuwa mwalimu wa shule ya sekondari ambaye wazazi wake walimwajiri ili kumfundisha siku za mapumziko mwishoni mwa wiki. Imani alipogundua kwamba ana mimba, alimtaarifu mwalimu wake. Mwalimu akatokomea pasipo julikana.

Muuguzi aliwapima mimba wasichana wote shuleni, ila Imani aliweza kukwepa kwenda shule nyakati zote mbili ambazo muuguzi alifanya uchunguzi huo. Mwezi wa tatu katika ujauzito wake, viongozi wa shule waligundua kwamba ni mjamzito. “Ndoto yangu ilisambaratika,” aliwambia shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch. “Nilifukuzwa shule, na pia nilifukuzwa kutoka nyumbani nilipokua naishi [kwa dada yangu].

Kama wengi wa vijana wasichana nchini Tanzania, Imani alijaribu njia mbalimbali za kurudi masomoni baada ya kujifungua mtoto wake, ambae alikua na umri wa miaka mitatu wakati Imani alizungumza na shirika la Human Rights Watch.

Nilijaribu[kurudi shule]. Nilienda kwenye vituo vingi binafsi ili niweze kufanya mtihani wa kitaifa wa kidato cha pili. Nililipia ada ya mtihani kwa walimu, ila walimu walitokomea na fedha zangu[hawakumsajili kufanya mtihani,] hivyo sikuweza kufanya mtihani. Huu ulikua ni mwaka 2015.

Wakati Human Rights Watch walivyofanya mahojiano naye mwezi wa kwanza 2016, Imani alikua kaanza mafunzo ya kompyuta ambayo yanaendeshwa na shirika dogo ambalo siyo la kiserikali lililoko Mwanza kuhakisha mabinti wengi kama yeye wanapata fursa ya kupata elimu kwa mara nyingine.

****

Elimu imekua kipaumbele kitaifa kwa serikali zilizoingia madarakani tangu uhuru. Tanzania ni kati ya nchi dunia yenye idadi kubwa ya vijana, na vijana wake ndiyo ni matarajio makubwa katika kufikia malengo ya nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Uchumi wa nchi, maendeleo ya jamii na ya binadamu yanategemea, kwa sehemu, katika uwezeshwaji na elimu; hii ikiwa ni rasilimali ya kipekee pamoja na ujuzi unaotakiwa ili kupeleka mbele malengo ya kitaifa. Elimu bora inaweza kuinua familia na jamii kutoka kwenye umaskini na kuongeza ukuaji wa uchumi wa nchi. Kuhitimu elimu ya sekondari imeonyesha faida kubwa kwa afya ya mtu binafsi, ajira, na kujipatia mapato katika maisha yao yote. Elimu ya sekondari, pamoja na mafunzo ya ufundi stadi, yanaweza kuwawezesha vijana kupata ujuzi laini unaohitajika katika maendeleo endelevu, pamoja na uraia na haki za binadamu, na kuhakikisha upatikanaji wa taarifa kulinda afya zao na ustawi. Kwa wasichana, usalama na usawa kwa upatikanaji wa elimu ya sekondari yaweza kuwa na nguvu kuweka usawa, kuhakikisha wasichana na wavulana kupata masomo sawa, shughuli mbalimbali na uchaguzi wa kazi.

Hata hivyo, mamilioni ya watoto wa kitanzania na vijana hawapati elimu ya sekondari na mafunzo ya ufundi stadi. Inakadiriwa kwamba jumla ya watoto milioni 5.1 wenye umri kati ya miaka 7 hadi 17 hawako mashuleni, ikiwa ni pamoja na karibu milioni 1.5 walio katika umri wa kwenda shule ya sekondari ngazi ya chini. Watoto wengi wanaishia elimu ya msingi: ni vijana watatu pekee kati ya watano Tanzania au asilimia 52 ya idadi ya wanaopaswa kuwa shule, wameandikishwa elimu ya sekondari ngazi ya chini, na wachache wanamaliza  elimu ya sekondari. Elimu rasmi ya mafunzo ya ufundi stadi haipatikani kwa watoto wengi wanaohitaji.

Badala ya kujiunga na shule, watoto wengi wanaishia kwenye ajira za utotoni, mara nyingi ni za unyonyaji, unyanyasaji, au katika mazingira hatarishi na katika ukiukwaji wa sheria za Tanzania, ili kuongeza kipato cha familia. Wasichana pia wanakumbana na changamoto kutokana na jinsia yao. Karibu wasichana wawili kati ya watano wanaolewa kabla ya kufikia miaka 18, na maelfu ya vijana wasichana wanaacha shule kwa sababu ya kupata mimba.

Mpaka hivi karibuni, familia nyingi zimeshindwa kupeleka watoto katika shule za sekondari kwa sababu ya kushindwa kulipa ada na kukimu mahitaji mengine, mara nyingi gharama ni zaidi ya shilingi za kitanzania 100,000 (dola 50) kwa mwaka.

Lakini mwezi wa kumi na mbili mwaka 2015, serikali mpya ya Tanzania ilichukua hatua muhimu: ilifuta ada zote za shule na “michango” – ada ya ziada kwa ajili ya gharama za uendeshaji wa shule. Awali, ada hii ya ziada ilikua kigezo cha kujiunga na elimu ya sekondari ya kidato cha nne nchini. Kwa mujibu wa serikali, uandikishaji katika shule ya sekondari umeongezeka baada ya kufuta ada.

Kufutwa kwa ada ni moja ya hatua muhimu sana kuchukuliwa na serikali ili kutekeleza adhima yake katika malengo ya elimu. Sera ya Tanzania ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi inalenga kuongeza upatikanaji wa elimu ya msingi na sekondari, na kuongeza ubora wa elimu. Malengo haya yanaendana na malengo ya maendeleo endelevu (SDGs), mpango wa shirika la umoja wa mataifa wenye lengo la kuhakikisha nchi zote zinatoa elimu bure kwa watoto, kwa usawa, na elimu bora ya msingi na sekondari ifikapo mwaka 2030. Malengo haya yanaendana na majukumu ya kimataifa na kitaifa ya haki za binadamu kwa Tanzania katika kutekeleza haki ya elimu ya msingi na sekondari kwa wote.

Lakini ni kati ya baadhi ya hatua za muda mfupi hadi mrefu zinazohitajika ili kutekeleza haki ya kupata elimu ya sekondari kwa watoto wote Tanzania. Ripoti hii imehusisha mahojiano zaidi ya 220 yaliyofanywa kwa wanafunzi wa sekondari, kati ya vijana wa shule, wazazi na wadau mbalimbali wa elimu kutoka kwenye jamii na serikali katika kanda nne za Tanzania bara. Utafiti wa ripoti hii ulifanyika mwaka 2016, ukiambatana na mwaka muhimu kwa nchi ya Tanzania baada ya kuchukua hatua ya kutoa elimu ya bure kwa elimu ya kidato cha nne na mipango madhubuti kwa ajili ya elimu ya sekondari. Hii inaongezea kwenye tafiti mbili za awali kuhusu unyanyasaji wa watoto na athari zake kwenye elimu ya sekondari na ustawi zilizofanywa na shirika la Human Rights Watch kwa mwaka 2012 na 2014; kazi ya sumu utotoni na athari za zebaki kwa wachimbaji wadogo Tanzania na hakuna njia mbadala. Ndoa za utotoni na ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Tanzania.

Ripoti imeangazia vikwazo muhimu kwenye elimu ya sekondari zinazozuia vijana wengi kushindwa kuhitimu elimu ya sekondari, na imetambua maeneo mengi ambayo yanahitaji utekelezaji wa serikali kuhakikisha usawa katika upatikanaji wa elimu ya sekondari kwa watoto wote. Haswa, ripoti imeangazia sera za serikali ambazo kwa sana zina bagua wasichana, kuwezesha kufukuzwa shule wasichana wajawazito na waliyo olewa, kuwapokonya elimu pamoja na sera zinazoruhusu viongozi wa shule kuwaadhibisha wanafunzi kikatili na katika hali ya kufedhehesha. Sera hizi kwa makusudi kabisa zinaendeleza ubaguzi na unyanyasaji, na kwenda kinyume na juhudi za serikali kutoa elimu kwa wote.

Muhtasari wa matokeo ya utafiti wa Human Rights Watch:

  • Wanafunzi wengi bado wanapata changamoto ya kifedha: Ingawa ada imetolewa mashuleni, wanafunzi maskini wa kitanzania bado hawana uwezo wa kuenda shule kwa sababu ya gharama zingine za kielimu. Wazazi wao au walezi hawana uwezo wa kuwalipia nauli ya kwenda shule, sare na mahitaji mengine kama vitabu. Endapo shule za sekondari zinapokua mbali, wanafunzi wakati mwingine ina wabidi wapange kwenye hosteli binafsi au wakae mabwenini karibu na shuleni; familia nyingi maskini haziwezi kumudu hili. Hii inakua changamoto kubwa kwa watoto kutoka familia maskini.
  • Kufutwa kwa ada za shule kumeacha upungufu mkubwa sana katika bajeti za shule: Shule zinashindwa kufadhili mahitaji ya muhimu ambayo awali waliweza kulipia kutokana na michango ya wazazi (ongezeko la ada lililo lipishwa mashuleni kwa ajili kukidhi gharama za uendeshaji), ilihusisha ujenzi wa shule na ukarabati, manunuzi ya vifaa vya kufundishia na kuajiri walimu wa ziada.
  • Mtihani wa kitaifa kwa shule ya msingi unazuia upatikanaji wa elimu ya sekondari: Serikali inadhibiti idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari kwa kutegemea ufaulu wa mtihani wa kitaifa unaofanyika ili kuhitimu shule ya msingi. Serikali inaruhusu wanafunzi waliyofaulu tu kuendelea na elimu ya sekondari na hakuna nafasi ya kurudia mtihani huo, hii ni kumaanisha kwamba watoto wanaoshindwa kufaulu hawaweze kuendelea na masomo hivyo wanakomea darasa la saba. Tangu mwaka 2012, zaidi ya vijana milioni 1.6 walikataliwa kujiunga na elimu ya sekondari kwa sababu ya matokeo yao ya mtihani.
  • Miundombinu mibaya na uhaba wa usafiri mashuleni: Wanafunzi vijijini wanalazimika kusafiri mwendo mrefu kwenda shule, na wengi katika maeneo wanayoishi hakuna shule za kata. Shule nyingi za sekondari zinaukosefu wa miundombinu, vifaa vya ufundushaji na wafanyazi waliohitimu. Serikali haijatimiza malengo yake ya kujenga hosteli kutoa malazi salama kwa wasichana karibu na shule.
  • Adhabu kali [viboko] ni tatizo sugu katika shule za sekondari: Viongozi na walimu katika shule nyingi mara kwa mara huishia kutoa adhabu kali sana, mazoea ambayo bado ni halali Tanzania ila ni ukiukwaji wa wajibu wao kimataifa. Wanafunzi wengi wanakabiliwa na ukatili unyanyasaji wa kisaikolojia inayopelekea kufedheheshwa na udhalilishaji. Baadhi ya walimu wanawachapa wanafunzi kwa kutumia fimbo za miti, mikono yao na vitu vingine.
  • Mabinti wanakumbana na unyanyasaji wa kijinsia, ubaguzi na kufukuzwa shule kwa sababu ya mimba au kuolewa: Chini ya robo tatu ya wasichana wanaingia shule ya secondary huitimu. Wasichana wengi wanakumbwa na unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa walimu wao. Wengine hunyanyaswa kijinsia na madereva wa mabasi ya shule na watu wazima ambao hutaka ngono baada ya kuwapa zawadi, lifti au pesa wakati wakiwa njiani kuelekea shule. Baadhi ya shule, viongozi huwa hawatoi ripoti ya kesi za unyanyasaji wa kijinsia polisi na shule nyingi zinakosa mwongozo madhubuti wa kuripoti manyanyaso ya kijinsia. Baadhi au shule nyingi wanalazimisha wasichana kufanyiwa upimaji wa mimba kisha kuwafukuza shule wale ambao watakutwa wana ujauzito. Wasichana ambao wameolewa pia ufukuzwa shule kutokana na mwongozo wa serikali.  Baada ya kuacha shule, wasichana wanapata ugumu sana kurudi kupata elimu kwa sababu ya ubaguzi uliopo juu ya wasichana waliyojifungua, matatizo ya kifedha na kutokuwepo na sera ya kuwasaidia wasichana hao kurudi katika mfumo wa elimu. Wasichana pia wanaukosefu wa mazingira safi ya kiafya, ambayo huleta ukosefu wa usafi kipindi cha hedhi na kuwafanya kukosa kwenda shule wakiwa kwenye hedhi.
  • Elimu ya sekondari bado haipatikani kwa wanafunzi wengi wenye ulemavu: Watoto wenye ulemavu wanakumbana na changamoto nyingi na ubaguzi kwenye shule za msingi, na ni vijana wachache sana wenye ulemavu ambao wanahudhuria shule za sekondari nchini. Shule nyingi za secondary nchini Tanzania hazifikiki na vijana ambao ni viwete au wenye ulemavu mwingine, na kuna upungufu wa miundombinu ya kuwawezesha wanafunzi wenye aina mbalimbali za ulemavu. Wengi wanakosa mahitaji ya shule ikiwemo vifaa na walimu waliyohitimu vyema.
  • Ubora wa elimu ya sekondari upo chini ya kiwango: Shule nyingi zinaukosefu wa walimu wa masomo yote, na ukosefu mkubwa ni katika masomo ya hesabu na sayansi. Wanafunzi wakati mwingine huendelea na masomo bila walimu wa masomo haya kwa muda wa kipindi kirefu na inawabidi watafute njia mbadala wa kujifunza au kulipia mafunzo binasfi ya ziada bila hivyo ni kushindwa kufanya vizuri kwenye mitihani. Madarasa ni makubwa sana yenye wastani wa wanafunzi 70. Pia, shule nyingi za sekondari zinaukosefu wa madarasa, vifaa vya kufundishia, maabara, na maktaba. Ma milioni ya wanafunzi wa sekondari wanatakiwa kufanya mitihani miwili ya lazima hata kama hawakua na walimu au vifaa vya kusomea mitihani hiyo. Wanafunzi wengi wanashindwa kufaulu mitihani, na mara nyingi huacha shule bila kuhitimu. Nje ya shule, vijana wengi wanakosa nafasi za kuhitimu masomo au kuendelea na mafunzo ya ufundi stadi.
  • Vijana ambao hawapo mashuleni wanakosa nafasi mbadala kuhitimu elimu ya sekondari ya kidato cha nne:Serikali inatoa fursa chache mbadala kwa mamilioni ya wanafunzi ambao wanashindwa kufaulu mtihani wa kuhitimu shule ya msingi au wanashindwa kuendelea na masomo ya elimu ya kidato cha nne. Nafasi ya kurudia elimu ya sekondari inawezekana kwa wanafunzi wanaojiunga kwenye vituo binafsi, ila wanafunzi wengi hawana uwezo wa kifedha na taarifa za fursa hii. Mafunzo ya ufundi stadi yanahitaji uhitimu wa ufaulu wa elimu ya kidato cha nne na pia ni gharama. Kozi za mafunzo ya ufundi stadi yanatofautiana ubora, wigo na matumizi.

Malengo ya serikali kwa sasa ni kuhakikisha upatikanaji wa elimu bure ya sekondari kutoa matumaini kwa ma mia elfu ya vijana ambao wamekosa elimu ya sekondari kwa sababu za kifedha na changamoto zingine za kiutaratibu.

Ufumbuzi wa matatizo mengi na changamoto zilizo orodheshwa katika ripoti hii zinahitaji kiwango kikubwa cha rasilimali, na pia uwepo wa malengo ya rasilimali za kitaifa kwa ajili ya elimu ya sekondari. Muongo kumi uliyopita, serikali ya Tanzania imepongezwa kwa kuonyesha azimio la utekelezaji wa malengo ya elimu mbali na changamoto za rasilimali.  Hata hivyo, serikali inatakiwa kupanga mikakati ya kukabiliana na changamoto zilizobakia kwa kulingana na rasilimali za kitaifa kupata msaada wa kifedha kimataifa ili kuhakikisha upatikanaji wa elimu ya bure ya sekondari kwa vijana.

Kufuatana na malengo ya maendeleo endelevu [SDGs], serikali inatakiwa kuweka mkazo katika kupanua wigo wa upatikanaji wa elimu ya sekondari, wakati huo kuhakikisha ubora wa elimu kwa wanafunzi wote, kuangalia kwamba wanafunzi wote wanawezeshwa, wanapata ujuzi na kujenga maarifa maalumu ili kupeleka Tanzania mbele. Ili kuhakikisha vijana wote wanapata ujuzi, hatua zinatakiwa kuchukuliwa kuwawezesha vijana ambao hawapo shuleni kupata elimu ya sekondari na mafunzo bora ya ufundi stadi.

Kwa upande mkubwa wa upatikanaji wa rasilimali, na uwepo wa msaada wa kifedha kutoka kwa wadau wa maendeleo, serikali inatakiwa kuharakisha ujenzi na ukarabati wa shule za sekondari na kuhakikisha ubora wa elimu kwa kuajiri walimu waliyohitimu vyema na kuongeza vifaa vya mafunzo kwa wanafunzi wote.

Serikali inatakiwa kutumia kasi hii haraka ili kupitia upya sera zilizopo ambazo zinagongana na wajibu wa kuhakikisha haki ya elimu ya sekondari, isiyo na ubaguzi na wala aina yoyote ya ukatili.

Tanzania inatakiwa kuchukua hatua maalumu kulinda haki za wasichana na haki za wanafunzi wenye ulemavu kuhakikisha wanaingizwa katika shule za sekondari. Serikali inatakiwa kupitisha kanuni kuzuia ukaguzi wa mimba wa lazima kwa wasichana ili kutoa fursa kwa wajawazito au wasichana waliyoolewa kuendelea na masomo. Inatakiwa kuunga mkono kufutwa kwa adhabu kali (viboko) na kuhakikisha wanafunzi wapo samala bila unyanyasaji wa kijinsia na uonevu mashuleni.

Mapendekezo Muhimu

Kwa Serikali ya Tanzania

Kuhakikisha upatikanaji wa elimu bure ya sekondari kwa vijana wote

  • Kuhakikisha kwamba shule zote zinatekeleza nyaraka ya elimu No. 5 ya 2015, sera ya serikali ya kufuta ada na michango na kufuatilia unatekelezwaji wake.
  • Kuendelea kuongeza bajeti na kuhakikisha kwamba shule zinapokea fedha ya kutosha kwa ajili ya maswala yote ya elimu, pamoja na ujenzi au ukarabati wa majengo, nyumba za walimu na vifaa vya ufundishaji.
  • Kuendelea kuongeza bajeti inayopatikana kwa ajili ya shule za sekondari kuhakikisha uwezo wa shule kukimu mahitaji yake ambayo awali yalilipiwa kutokana na michango ya wazazi na kufikia kiwango cha chini cha fedha kwa ajili ya uendeshaji wa shule zote za sekondari.

Kufutulia mbali utumiaji wa mitihani kama kigezo cha kuteua wanafunzi kujiunga na elimu ya sekondari

  • Kutafuta namna mbalimbali za kuongeza kasi ya kufuta matumizi ya mtihani wa kitaifa kwa shule za msingi kama kigezo cha kuwazuia wanafunzi wanaoshindwa kufaulu kupata elimu ya sekondari kabla ya muda uliyopangwa 2021.
  • Kubadilisha mara moja sera zilizopo ili kuhakikisha wanafunzi ambao wanashindwa mtihani wa kitaifa wa shule ya msingi kupata mafunzo ya ufundi ustadi na maarifa kabla ya kujiunga na kidato cha kwanza.
  • Kuongeza upatikanaji wa shule za sekondari na hosteli.

Kuongeza upatikanaji wa shule za sekondari na hosteli

  • Kwa kiwango kikubwa cha upatikanaji wa rasilimali zilizopo
  • Ujenzi wa shule mpya za sekondari ili kuhakikisha kuna madarasa ya kutosha na vyoo. Kuchukua hatua za kuhakikisha majengo yote mapya pamoja na vyoo vinafikiwa kwa urahisi na wanafunzi na walimu wenye ulemavu.
  • Kuharakisha majengo salama ya hosteli kwa ajili ya wanafunzi wa kike.

Kusisitisha matumizi na kukubaliana kwa adhabu kali na unyanyasaji wa kijinsia mashuleni

  • Kutokomeza sera ya adhabu kali na matumizi pamoja na kurekebisha sheria ya elimu kitaifa ya mwaka 1979 na kupitisha sera na sheria ambazo zinaendana na wajibu wa Tanzania wa haki za kibinadamu kimataifa na kikanda.
  • Kuhakikisha kesi za unyanyasaji wa kijinsia na ukatili pamoja na madereva wa mabasi ya shule, walimu, viongozi wa shule, zinaripotiwa kwa mamlaka husika ikiwemo polisis, na kesi hizo zichunguzwe na hukumu itolewe. Walimu na madreva ambao wanafanyia uchunguzi wasimamishwe kazi.

Kumaliza changamoto za kiubaguzi na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wasichana mashuleni

  • Kuacha kufukuza shule wasichana wajawazito na wale waliyo olewa na kupitia upya sheria No. 4 ya elimu (kufukuzwa na kutengwa kwa wanafunzi mashuleni) ya mwaka 2002 kwa kuondoa “makosa dhidi ya maadili” na “ndoa” kama vigezo vya kufukuzwa.
  • Kusisitisha mara moja upimaji wa mimba mashuleni, na kutoa tangazo rasmi kutoka serikalini kuhakikisha kwamba walimu na viongozi wa utawala wanaufahamu kuhusu kuzuiwa upimaji wa mimba.
  • Kuharakisha sheria ambayo itawakubalia wasichana wajawazito na mabinti wenye watoto wakingali na umri wa kwenda shule kurudi katika shule ya sekondari kufuatana na sera ya elimu na mfunzo ya 2014.

Kuhakikisha elimu shirikishi kwa wanafunzi wote wenye ulemavu

  • Kuhakikisha wanafunzi wenye ulemavu wanapata vifaa vya kuwasaidia bure au kwa bei pungufu, pamoja na baiskeli za miguu, fimbo au miwani ya macho, kuwezesha harakati zao, ushiriki na shuleni. 
  • Kuchukua hatua kuhakikisha shule za sekondari zenye wanafunzi walemavu wana kiwango cha chini kinachokubalika cha vitabu, vifaa vya kufundishia pamoja na vifaa vingine kwa wanafunzi na walimu wenye ulemavu.
  • Kuchukua hatua kuhakikisha walimu wana mafunzo ya kutosha katika elimu shirikishi. Kutoa mafunzo ya ushauri kwa walimu kuwawezesha kutoa msaada kwa watoto wenye ulemavu aina mbalimbali na kwa familia zao.

Kuimarisha ubora wa elimu katika shule za sekondari

  • Kwa kiwango kikubwa cha upatikanaji wa rasilimali zilizopo.
  • Kuhakikisha walimu wanapewa fidia ya kutosha, inayoendana na majukumu yao. Kutoa motisha kwa walimu wanaopangiwa kazi vijijini
  • Au maeneo ya nchi yaliyosahaulika na kutoa nyumba za kutosha kwa walimu.
  • Kuhakikisha wanafunzi wote wanapata vitabu and vifaa vya kujifunzia.

Kwa wafadhili wa kimataifa na mashirika ya umoja wa mataifa

  • Kusihi serikali kukomesha sheria ya adhabu kali [viboko] mashuleni na kutoa fedha na msaada mbadala kwa mafunzo katika madarasa makubwa usimamizi wa walimu wote na viongozi wa shule.
  • Kusihi serikali kusisitisha kufukuzwa shule kwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba, na kuharakisha urasimilishaji wa sera ambayo itatoa nafasi ya kurudia masomo kwa wazazi wenye umri wa shule.

Mbinu za Utafiti

Ripoti hii inatokana na utafiti uliofanyika mwezi Januari, Mei na Novemba 2016 katika Wilaya sita za Mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Tabora zilizopo Tanzania bara pamoja na Wilaya mbili za jiji la Dar es Salaam.[1] Kwa kushauriana na Asasi Zisizokuwa za Kiserikali(NGOs) katika ngazi ya Taifa na Mitaa, Human Rights Watch ilichagua mikoa hii kutokana na utofauti mkubwa katika uandikishwaji wa shule, kiwango cha kuendelea na elimu ya sekondari,umbali kuelekea shule, matukio mengi ya ajira za utotoni,ndoa za utotoni na mimba za utotoni na utofauti wa upatikanaji elimu kati ya watu wanoishi maeneo ya mijini na vijijini. Utafiti huu ni muendelezo wa uchunguzi uliofanyika katika nyakati mbili tofauti juu ya ajira na ndoa za utotoni uliofanywa na Human Rights Watch katika mikoa hii mwaka 2012 na 2014, ambao ulionyesha athari ya matendo haya yenye madhara juu ya upatikanaji wa elimu ya sekondari.

Human Rights Watch ilifanya mahojiano binafsi na watoto 40 na vijana 45. Umri wao ni kati ya miaka 11 hadi 23. Sitini na tano kati yao walikuwa ni watoto na vijana wakike; 20 kati yao walikuwa watoto na vijana wakiume. Kati ya waliohojiwa, saba walikuwa na ulemavu wa viungo, hisia na akili. Kwa ujumla, shule za msingi 14 na sekondari 30 katika mikoa tofauti zilitembelewa.   

Vile vile tulifanya majadiliano na vikundi nane vilivyojumuisha wanafunzi 88 kutoka shule nne za sekondari zinazomilikiwa na Serikali, na vijana 53 walioacha shule. Vijana wenye ulemavu walishiriki katika vikundi vya majadiliano. Wengi walioshiriki katika majadiliano ya vikundi walikuwa na umri chini ya miaka 18. Kwa kuongezea tulifanya mahojiano na wazazi au walezi 12.

Katika ripoti hii, neno “Mtoto” limetumika kumuelezea mtu yeyote chini ya umri wa miaka 18, sambamba na linavyotumika katika sheria za Tanzania na Kimataifa. Neno “Kijana” limetumika kumuelezea mtoto na kijana kati ya miaka 10 hadi 19, kwa kutambua wanafunzi wenye umri zaidi ya miaka 18 na bado wanaandikishwa elimu ya sekondari.[2] Mahojiano yalifanyika katika lugha ya Kiswahili, Kiingereza na Ishara. Mahojiano yalitafsiriwa katika lugha ya Kiingereza na wanaharakati na wawakilishi wa Asasi Zisizokuwa za Kiserikali ambao waliambatana na watafiti wa Human Rights Watch. Katika kila mahojiano, Human Rights Watch walieleza madhumuni ya utafiti, namna utakavyotumika na kusambazwa na kuomba ridhaa ya washiriki kujumuisha uzoefu wao pamoja na mapendekezo yao katika ripoti hii. Washiriki waliridhia kushiriki baada ya kuelewa madhumuni ya utafiti.

Kwa uangalifu mkubwa tulihakikisha mahojiano na vijana yanafanyika kwa kuzingatia unyeti wa mada na kuahidi kutotaja majina yao. Wote waliohojiwa walielezwa kuwa wanaweza kusitisha mahojiano muda wowote au kukataa kujibu swali lolote. Majina yote ya vijana yaliyotumika katika ripoti hii si halisi. Ushahidi wa wanafunzi umewekwa kwa maeneo na sio shule nia ikiwa ni kuhakikisha utambulisho wao unalindwa.     

Human Rights Watch ilirudisha gharama za usafiri kwa baadhi ya washiriki waliosafiri mwendo mrefu kwa ajili ya mahojiano. 

Watafiti walitembelea shule tano za sekondari za Serikali na kituo kimoja cha ufundi stadi kufanya mahojiano na maofisa waandamizi na walimu 20. Vile vile tulifanya mahojiano na maofisa waandamizi na viongozi nane wa Chama cha Walimu Tanzania. Kuepuka aina yoyote ya madhara kwa washiriki hawa, majina ya baadhi ya walimu na maofisa waandamizi yamefichwa kulinda utambulisho wao pale ambapo taarifa iliyotolewa inaweza kupelekea kulipiza kisasi kutoka shule nyingine au viongozi wa Serikali za Mitaa.

Zaidi ya hapo, Human Rights Watch ilifanya mahojiano na maofisa wa Serikali za Mtaa na Serikali Kuu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto; na Ofisi ya Rais ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, na kuwasiliana kwa barua pepe na maofisa wa Serikali.[3]

Human Rights Watch pia ilifanya mahojiano na wawakilishi 24 wa NGOs, ikiwa ni pamoja na mashirika yanayolenga elimu na haki za mtoto, mashirika yanayoongozwa na vijana, mashirika ya watu wenye ulemavu, wataalamu na watendaji wawili wa elimu na wawakilishi saba wa washirika wa maendeleo.  

Tumepitia sheria za Tanzania, sera za Serikali na ripoti, matamko ya bajeti na ripoti za maendeleo, mawasilisho ya Serikali kwa taasisi za Umoja wa Mataifa, ripoti za UN, ripoti za NGO, makala za kitaaluma, makala za magazeti na mijadala katika mitandao ya kijamii miongoni mwa mengine. NGO tatu zilishiriki kwa kutoa takwimu, tafiti zilizokwisha fanyika na tathmini kutokana na tafiti zao pamoja na shughuli za uhamasishaji katika shule za sekondari.

Kiwango cha kubadilisha fedha za kigeni wakati utafiti unafanyika kilikua ni Dola ya Kimarekani $1= Shilingi za Kitanzania (Tsh.)  2,200; kiwango hiki ndicho kilichotumika katika ripoti hii.

I.      Historia: Elimu ya Sekondari Tanzania

Elimu imekua ni kipaumbele cha Taifa katika awamu zote za Serikali za Tanzania toka kupata uhuru.[4] Nia ya Serikali kuhakikisha elimu ya msingi inatolewa bure kwa watoto wote ilipelekea zaidi ya asilimia 97 ya watoto kuandikishwa katika shule za msingi mwishoni mwa miaka ya 2000.[5] Ikiwa ni moja kati ya nchi duniani yenye idadi kubwa ya vijana chini ya umri wa miaka 25, na asilimia 43 ya idadi ya watu wake chini ya umri wa miaka 15, Tanzania, nchi ya kipato cha chini, ina changamoto kubwa katika kuhakikisha elimu ya msingi kwa wote.[6]

Ikiwa ni moja kati ya nchi duniani yenye idadi kubwa ya vijana chini ya umri wa miaka 25, na asilimia 43 ya idadi ya watu wake chini ya umri wa miaka 15, Tanzania, nchi ya kipato cha chini, ina changamoto kubwa katika kuhakikisha elimu ya msingi kwa wote.

Ikiwa ni zaidi ya muongo mmoja tangu kuzindua mpango wa elimu bure na lazima, takribani watoto milioni 8.5 wameandikishwa katika elimu ya msingi ya miaka sita, ikiwakilisha karibu asilimia 77 ya watoto walio katika umri wa kwenda shule ya msingi na vijana milioni 1.87 au asilimia 52 ya idadi ya wanaopaswa kuwa shule wameandikishwa elimu ya sekondari ngazi ya chini.[7] Kati ya watoto milioni 5.1 ambao hawako katika mfumo wa elimu ya msingi, karibu milioni mbili au mmoja kati ya watoto watano hawako mashuleni.[8] Inakadiriwa kuwa vijana milioni 1.5 au vijana wawili kati ya watano wa Kitanzania walio katika umri wa elimu ya sekondari katika ngazi ya chini wako nje ya shule; na wako hawako shuleni.[9] Mwaka 2013, Tanzania ilishika nafasi ya 187 katika viashiria vya Umoja wa Mataifa vya elimu duniani, kipimo hiki hupima wastani wa miaka ya kupata elimu na miaka inayotarajiwa mtu kupata elimu.[10]

Tanzania imekuwa na matumizi yanayofanana katika sekta ya elimu tangu mwaka 2010. Kulingana na viwango vya kimataifa, serikali hutakiwa kutumia angalau asilimia 20 ya bajeti kuu katika elimu.[11] Mwaka 2015-2016, Serikali ilitumia asilimia 16 na zaidi ya bajeti kuu katika elimu na mwaka 2016-2017 imetenga asilimia 22 ya bajeti kuu kwa ajili ya elimu.[12] Sehemu kubwa ya bajeti ya Serikali katika elimu hutumika kugharamia matumizi makubwa na yale ya kawaida, ikiwa ni pamoja na mishahara ya walimu na watumishi wa umma.[13] Serikali imewekeza zaidi katika elimu ya juu na mikopo kwa wanafunzi kuliko katika elimu ya sekondari, ijapokuwa hii inaweza kubadilika baada ya uzinduzi wa elimu bure kwa sekondari ngazi ya chini.[14]

Ingawa fedha kutoka nje zimepungua katika miaka ya karibuni, michango ya wafadhili imeendelea kuwa chanzo kikubwa cha fedha: mwaka 2014 misaada kutoka nje ilifikia zaidi ya asilimia 46 ya bajeti ya serikali katika elimu.[15]

Mwaka 2016,baada ya kutangaza mpango wa elimu bure kwa sekondari ngazi ya chini, Serikali ilitenga shilingi za kitanzania trilioni 4.77 (US$ 2.1 bilioni) kwa ajili ya sekta ya elimu, sawa na zaidi ya asilimia 22 ya bajeti kuu ya Taifa.[16] Kugharamia gharama za ziada zilizotokana na mpango wa elimu ya sekondari bure kwa mwaka wa masomo 2016-2017, Serikali ilitenga ziada ya shilingi za kitanzania bilioni 137 (US$ 62 milioni), zilizookolewa kutoka katika hatua za kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ndani ya Serikali na Wizara.[17]

Hata hivyo, kutokana na uchambuzi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa unaoshughulikia masuala ya watoto (UNICEF), Serikali itahitaji kuendelea kuongeza mgao katika bajeti ya elimu ya sekondari ili kuweza kuigharamia kikamilifu.[18] Kutokana na asasi ya Policy Forum, mtandao wa kitaifa wa mashirika unaoshughulika na uwazi katika bajeti, Serikali inapaswa kutenga ziada ya shilingi za kitanzania bilioni 852 (US$387 milioni) kwa mwaka kuhakikisha inakidhi gharama zote za elimu ya sekondari bure sambamba na makadirio ya kuongezeka kwa wanafunzi, idadi ya kutosha ya walimu na miundombinu. Ongezeko hili la fedha litakidhi “gharama za kutoa elimu bila utaratibu wa wanafunzi kulipa ada au michango ya wazazi, kutenga fedha kwa ajili ya ukaguzi na kuongeza bajeti ya maendeleo.”[19]

Mfumo wa Elimu ya Tanzania

Katika Katiba ya Tanzania, Serikali inajukumu la kuhakikisha upatikanaji wa “fursa sawa na za kutosha” kumuwezesha kila mtu “kupata elimu na mafunzo ya ufundi stadi katika ngazi zote za shule na taasisi nyingine za kujifunza.”[20]

Kwa mujibu wa Sheria ya Elimu Tanzania, watoto wote walio na umri zaidi ya miaka saba lazima wahudhurie na kumaliza elimu ya msingi.[21] Katika kanuni za sasa, mzazi au mlezi yeyote anaeshindwa kuhakikisha mtoto anaandikishwa elimu ya msingi atakua amefanya kosa kisheria na atatozwa faini au kifungo cha hadi miezi sita.[22] Katika Sheria ya Mtoto, watoto wana haki ya kupata elimu, ikiwa ni pamoja na haki ya kupata elimu ya ufundi stadi na wazazi wana wajibu wa kuhakikisha watoto wanapata haki hii.[23]

Sera ya Tanzania ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 iliyozinduliwa rasmi mwezi Februari 2015 imetangaza miaka 10 ya elimu bure na ya lazima: miaka sita ya elimu ya msingi na miaka minne ya elimu ya sekondari ngazi ya chini.[24] Sera pia imeruhusu matumizi ya lugha mbili za Kiswahili na Kiingereza kama lugha za kufundishia katika shule za sekondari, ambayo imeondoa sera ya awali ya kufundisha elimu ya sekondari katika lugha ya Kiingereza.[25]Hata hivyo mitihani ya shule za sekondari itaendelea kufanywa kwa Kiingereza. 

Katika sera hii, watoto walioandikishwa elimu ya msingi mwaka 2016 watapata miaka 10 ya elimu ya msingi ya bure na lazima. Hata hivyo, watoto wengine wote walioandikishwa shule ya msingi lazima wafanye mtihani wa mwisho wa darasa la saba, mwaka wa mwisho wa elimu ya msingi kwa wanafunzi wa sasa ili waweze kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya chini.

Wakiwa katika shule za sekondari, wanafunzi wanatakiwa kufanya mitihani miwili ya Taifa wanapomaliza kidato cha pili na kidato cha nne. Zaidi ya elimu ya sekondari, vyuo vya elimu ya watu wazima (FDCs) na vituo vya mafunzo ya ufundi stadi (VTCs) vinatoa mafunzo kwa vijana na watu wazima wa umri wa kati.

Kuanzia Machi 2016, kulikuwa na shule 3,601 za sekondari zinazomilikiwa na Serikali Tanzania bara kulinganisha na shule 16,087 za msingi zinazomilikiwa na Serikali.[26] Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi inamiliki na kusimamia vituo 28 vya mafunzo na vituo 10 vya mafunzo ya ufundi stadi ambavyo vipo katika miji mikubwa nchini.[27]

Taasisi nne za Serikali ndizo zinazowajibika zaidi na utekelezaji wa mipango mbalimbali ya elimu na malengo ya Taifa:[28] Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (W-ELT), Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (W-AMJWW), Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) na Tume ya Utumishi wa Umma.[29] TAMISEMI inasimamia utekelezaji wa elimu ya msingi, mishahara ya walimu na maafisa wa elimu na kuratibu shughuli za serikali za mitaa. Wizara ya Elimu inaongoza uundwaji wa sera na vipengele vya kimkakati katika sekta ya elimu.[30]

Jitihada za Serikali kuharakisha maendeleo katika Elimu ya Sekondari

Katika miaka ya hivi karibuni Serikali imechukua hatua muhimu kuboresha upatikanaji wa elimu ya sekondari na mwaka 2015 imeweka nia kuelekea lengo la kuhakikisha miaka 12 ya elimu bure ya sekondari ifikapo 2030.[31]Katika kufikia lengo, mwaka 2016 Serikali imechukua hatua muhimu kwa kufuta ada na michango yote ya shule ambayo ilikua inagharamia gharama za uendeshaji kwa shule za sekondari ngazi ya chini, hii ikiwa ni jitihada za kuhakikisha vijana wote Tanzania wanamaliza elimu ya msingi.

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari na Matokeo Makubwa Sasa

Serikali imefanya upanuzi wa elimu ya sekondari ikiwa ni pamoja na elimu ya mafunzo na ufundi stadi toka mwaka 2000. Katika mpango wa sasa wa elimu ya sekondari uliozinduliwa mwaka 2005, Seikali imesema itajenga angalau shule moja ya sekondari katika kila kata ili kupanua upatikanaji wa elimu ya sekondari na kuhakikisha wanafunzi wanasoma karibu na makazi yao.[32]

Benki ya Dunia ambayo ni moja ya washirika wakubwa wa maendeleo ilitoa zaidi ya dola za kimarekani milioni 300 kusaidia utekelezaji wa sera ya Serikali ya elimu ya sekondari.[33] Katika miaka 10 Serikali imeongeza idadi ya shule za sekondari mara kumi kukiwa na ongezeko la wazi katika uandikishwaji wa elimu ya sekondari: kutoka wanafunzi 524,325 mwaka 2005 kufikia wanafunzi milioni 1.8 mwaka 2015.[34]

Mwaka 2013,Tanzania ilipitisha mkakati wa kukuza uchumi na maendeleo, mpango wa Matokeo Makubwa Sasa ambao umelenga kuifanya Tanzania kua nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.[35] Moja ya vipaumbele vya Mpango huu unalenga elimu na umeanza kutekelezwa kupitia mpango wa dola za kimarekani milioni 416, milioni 252 kati ya hizo zitatolewa na Benki ya Dunia na washirika wengine wa maendeleo kupitia mpango wa kutoa fedha kwa matokeo ambapo fedha zitatolewa pale Serikali inapokua imefikia idadi iliyokubalika ya matokeo.[36] Kwa mujibu wa Serikali ya Tanzania, nia ni “kuharakisha uboreshaji wa ufanisi kwa elimu ya msingi na sekondari ili kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapata elimu na sio kuhudhuria shule pekee.”[37]

Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Elimu ya Sekondari unaofanywa na Serikali umeathiriwa na ucheleweshaji ambao ni zaidi ya miundombinu ya utekelezaji kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha zilizotengwa kwa ajili ya shule na kukosekana kwa utekelezaji wa uhakika nchi kote.[38]

Mwaka 2016, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Tanzania alitangaza mipango ya Serikali kuharakisha ujenzi wa shule mpya na ukarabati wa shule za zamani za sekondari nchini kote.[39] Serikali pia imeanza kugawa fedha za ruzuku kwa mwezi zinazolenga kuzipatia shule fedha za ziada kugharamia uendeshaji kwa kila mwanafunzi alieandikishwa, fedha hizi zinalipwa moja kwa moja katika akaunti za benki za shule za sekondari za Serikali. Hatua hii inalenga kupunguza vitendo vya rushwa katika Serikali za Mtaa ambapo hapo awali ndizo zilizokuwa zinasimamia ugawaji wa fedha hizi kwa shule ambazo ziko katika maeneo yao ya utawala.[40] Uchambuzi uliofanywa na Policy Forum umeonyesha kwamba shule za sekondari zilikua zinapokea shilini za kitanzania 12,000-15,000 (dola za kimarekani $5.5-7) kati ya shilingi za kitanzania 25,000 (dola za kimarekani $11) zilizokuwa zinatakiwa katika ruzuku. Pia imeripotiwa kwamba Serikali haikutoa fedha kwa ajili ya gharama za miundombinu.[41]

Elimu Bure Tanzania

Mpaka kufikia Desemba 2015, Serikali ilikua inategemea ada za shule na michango ya wazazi kugharamia gharama za uendeshaji, mishahara ya walimu wa kujitolea na wa muda mfupi, ukarabati wa majengo, ufundishaji na vitabu kwa ajili ya walimu na wanafunzi. Ada kwa shule za sekondari ilikua Tshs. 20,000 ($10) kwa mwaka.[42]

Desemba 2015, mara baada ya kuingia ofisini Rais John Magufuli alitangaza maamuzi ya Serikali kusitisha malipo ya ada na michango mingine yote hadi kufikia kidato cha nne, mwaka wa mwisho wa elimu ya sekondari ngazi ya chini na kusisitiza: “Ninaposema elimu bure kwa hakika ninamaanisha bure.”[43] Hatua hii ilitanguliwa na Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo inatoa muongozo wa miaka 10 ya elimu bure na lazima kwa ngazi ya elimu ya msingi na sekondari ngazi ya chini.[44]

Kabla ya kuanza kwa mwaka wa shule 2016, Serikali ilitoa waraka wa elimu ulioelekeza maafisa wa shule zote za msingi na sekondari kutokudai ada au michango kwa mwaka mpya wa shule.[45]Hata hivyo kusitishwa huku kwa ada hakuhusishi elimu ya watu wazima au mipango mingine ya elimu isiyokuwa rasmi kwa vijana walio katika umri wa kwenda shule lakini waliacha shule kabla ya wakati.[46]

Dhamira ya Maendeleo ya Kimataifa

Mwaka 2015 Tanzania iliidhinisha Malengo ya Maendeleo Endelevu ikiwa ni pamoja na dhamira ya miaka 15 ya:

Kuhakikisha watoto wa kike na kiume wanamaliza elimu ya bure ya msingi na sekondari yenye usawa na ubora ambayo itapelekea matokeo yenye ufanisi na uhalisia katika kujifunza...

Kujenga na kuboresha vifaa vya elimu ambavyo vinazingatia mahitaji maalumu ya watoto, walemavu na utofauti wa jinsia na kuhakikisha mazingira yenye ufanisi, salama, yasiyo na vurugu na yenye kujumuisha wote. [47]

Kufikia 2030, Serikali pia imelenga kuhakikisha usawa katika upatikanaji nafuu na bora wa elimu ya ufundi na ufundi stadi.[48] Katika wakati huo huo vijana wote na idadi kubwa ya watu wazima watatakiwa kuwa wamejua kusoma na kuhesabu.[49]

Vikwazo vya Kijamii na Kiuchumi Vinavyowafanya Watoto Kukosa Shule

Watoto wengi walio katika umri wa kwenda shule wanakabiliwa na vikwazo vya kijamii na kiuchumi vinavyowazuia kupata elimu, vikwazo hivi ni pamoja na masuala ya jinsia, ulemavu au kipato. Watoto na vijana wengi pia wanakabiliwa na ukiukwaji wa haki za kibinadamu na vitendo vyenye madhara ikiwa ni pamoja na ajira za watoto na ndoa za utotoni ambavyo vyote vinapelekea suala la kupata elimu kuwa gumu au kushindakana kabisa.[50]

Mwaka 2015 na 2016, Tanzania ilikua nchi waanzilishi wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kukomesha Ukatili dhidi ya Watoto ambao unatokana na dhamira ya kumaliza suala la ukatili dhidi ya watoto ifikapo mwaka 2030.[51] Serikali ilikubali kutekeleza mpango madhubuti wa Taifa kupambana na aina zote za ukatili na tabia zenye madhara kwa watoto na wanawake ikiwa ni pamoja na yale yanayowadhuru kwa kiasi kikubwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wameorodheshwa hapa chini.[52]

Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Magumu

Serikali inakadiria kwamba asilimia 74 ya watoto wote wa Tanzania wanaishi katika “umasikini wa aina mbalimbali”, na kwamba asilimia 29 wanaishi katika kaya zilizo chini ya kipimo cha umasikini wa fedha.[53] Kati ya mwaka 2008 na 2012, mahudhurio ya shule za msingi miongoni mwa asilimia 20 ya idadi ya watu masikini kupindukia ilikua asilimia 67.5 kulinganisha na asilimia 98 ya idadi ya walio katika umri wa kwenda shule ya msingi.[54]

Watoto wengi wanaotoka katika familia masikini wanakabiliwa na changamoto za utofauti wa kiuchumi ambao kwa kiasi kikubwa una athiri elimu yao.[55] Hali ngumu ya kiuchumi na ukosefu wa mahitaji ya msingi unawalazimu watoto wengi kuingia katika ajira za utotoni ambazo mara nyingi ni za unyonyaji, manyanyaso au zenye kufanyika katika hali hatarishi kama vile katika migodi ya dhahabu, uvuvi, mashamba ya tumbaku au kazi za ndani.[56] Mazingira mengi kama haya yanakiuka sheria za Tanzania.[57] Kwa ujumla, watoto milioni 4.2 au asilimia 29 wenye umri kati ya miaka 5-17 wanajihusisha katika ajira za utotoni.[58] Miongoni mwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu inakadiriwa kuwa ni yatima milioni 3 ambao kati yao milioni 1.2 wamepoteza wazazi kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.[59]

Ndoa za Utotoni

Tanzania ina kiwango kikubwa cha matukio ya ndoa za utotoni ambapo katika watoto wa kike watano, wawili wameolewa kabla ya miaka 18.[60] Zaidi ya asilimia 37 ya watoto wa kike wanaolewa katika umri wa miaka 18 na asilimia 7 wanaolewa katika umri wa miaka 15.[61] Shinyanga na Tabora, mikoa miwili yenye matukio mengi ya ndoa za utotoni na mimba za utotoni, takribani asilimia 60 ya wanawake walio katika umri wa miaka 20 hadi 24 waliolewa wakiwa na umri wa miaka 18.[62] Katika mikoa hii, asilimia 23 ya watoto wa kike wenye umri wa miaka 15-19 ni wajawazito au tayari wana watoto.[63]

Ndoa za utotoni zina athari ya moja kwa moja kwa elimu ya mtoto wa kike. Utafiti mmoja unakadiria kwamba asilimia 97 ya wasichana walioolewa katika umri wa shule za sekondari wameacha shule kulinganisha na asilimia 50 ya wasichana ambao hawajaolewa.[64] Sio kwamba wasichana hulazimishwa kuacha shule na familia zao pekee; Kanuni za kufukuzwa shule kwa Tanzania pia zinamfukuzisha shule moja kwa moja msichana alieolewa katika umri wa kwenda shule.[65] 

Sheria za Tanzania zinavumilia ndoa za utotoni. Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inaruhusu wasichana kuolewa katika umri wa miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi au miaka 14 kwa ridhaa ya mahakama. Mapema mwaka 1994, Tume ya Kurekebisha Sheria ya Tanzania ilishauri marekebisho ya Sheria kuongeza umri wa kuolewa kuwa miaka 21 kwa watoto wa kike na kiume.[66]

Januari 2016, Msichana Initiative, asasi isiyokuwa ya kiserikali inayosimamia haki za watoto wa kike ilipeleka Sheria hii Mahakamani kuipinga.[67] Katika maamuzi ya kihistoria, Mahakama Kuu ya Tanzania ilitoa hukumu juu ya kifungu cha 13 na 17 cha Sheria ya Ndoa kuwa kinyume na katiba na kumuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kurekebisha sheria na kuongeza umri unaofaa kwa ndoa kwa wanaume na wanawake kuwa miaka 18. [68] Agosti 2016, Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju katika hali isiyotarajiwa alikata rufaa dhidi ya maamuzi ya Mahakama Kuu.[69]

II.  Wajibu wa Tanzania kwa Sheria za Kimataifa

Haki ya Kupata Elimu ya Sekondari

Elimu ni haki ya msingi inayotajwa katika makubaliano mbalimbali ya kimataifa yiliyoridhiwa na Tanzania, ikiwa ni pamoja na Mkataba ya Umoja wa Mataifa Juu ya Haki za Mtoto, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (ICESCR), Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto na Azimio la Vijana wa Afrika.[70]

Serikali huongozwa na vigezo muhimu vinne katika kutekeleza majukumu yake katika elimu: kupatikana, kufikiwa, kukubalika na kuendana na mazingira. Ni lazima elimu ipatikane nchini kote ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miundombinu bora na ya kutosha inawafikia watu wote kwa usawa. Mfumo na maudhui ya elimu ni lazima viwe katika ubora unaokubalika na kukidhi viwango, na elimu iendane na mahitaji ya wanafunzi kwa kuzingatia utofauti wa kijamii na kiutamaduni.[71]

Katika sheria ya haki za binadamu za kimataifa na kikanda, watu wote wana haki ya kupata elimu ya msingi na ya lazima bure bila ubaguzi.[72] Vile vile watu wote wana haki ya kupata elimu ya sekondari ambayo inajumuisha kumaliza elimu ya sekondari na kuweka msingi wa kujifunza katika safari ya maisha na maendeleo ya mwanadamu.”[73] Haki ya kupata elimu ya sekondari inajumuisha pia haki ya kupata mafunzo ya ufundi stadi.[74]

Serikali inawajibu wa kuhakikisha aina mbalimbali za elimu ya sekondari zinapatikana na kufikiwa huku ikichukua hatua thabiti katika kufikia lengo la kutoa elimu ya sekondari bure. Jitihada zaidi kama vile kutoa misaada ya kifedha kwa wale wenye mahitaji zinahitajika kuhakikisha elimu inapatikana kwa wote.[75] Serikali pia zinapaswa kuhimiza elimu ya msingi kwa wale ambao hawakupata au kumaliza elimu ya msingi.[76] Haki ya kupata elimu ya msingi inahusisha wale wote ambao “hawajakidhi mahitaji yao ya elimu ya msingi”, hii ni kwa mujibu wa Kamati ya Umoja wa Mataifa (UN) inayoshughulika na Haki za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni ambayo ni chombo cha kitaalam kufafanua Mkataba wa ICESCR na kutoa muongozo kwa mataifa katika juhudi za kuutekeleza.”[77]

Haki ya kupata elimu ni wajibu wa Serikali ambao unahitaji utekelezaji wa haraka na wenye muendelezo.  Kwa mujibu wa Kamati ya Haki za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni, katika kutekeleza malengo ya ICESCR, “hatua za makusudi, thabiti na zenye kulenga kufikia lengo lazima zichukuliwe”. Kamati hii pia inasisitiza kwamba ICESCR inaelekeza “utekelezaji wa haraka wenye ufanisi katika kufikia lengo.”[78]

Kamati hii pia inasisitiza kwamba upatikanaji wa elimu ya sekondari hautakiwi kutegemea uwezo wa mwanafunzi bali elimu lazima isambazwe maeneo yote ya nchi ili ipatikane kwa wote katika misingi ya usawa.[79] Kuna wengi wanaounga mkono dhana ya Mataifa kufanya tathmini kuonyesha utekelezaji wa jukumu la kuhakikisha watoto wote wanapata elimu bora ya msingi na kuwa na fursa ya kupata elimu bora ya sekondari.[80]

Lazima Serikali zihakikishe usawa katika upatikanaji wa elimu isiyokuwa na ubaguzi. Kwa mujibu wa Kamati ya Haki za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni, “ubaguzi unajumuisha tofauti yoyote, kutengwa, vizuizi, au aina yoyote ya upendeleo ambayo kwa namna moja au nyingine inalenga kubagua, kukataza, kushindwa kutambua au kuzuia utekelezaji wa haki na usawa.”[81]

Pamoja na kuondoa aina zote za ubaguzi wa moja kwa moja, Serikali lazima ihakikishe aina nyingine za ubaguzi zinazotokana na utekelezaji wa sheria, sera au utamaduni na kuathiri haki ya kupata elimu kwa watoto wenye mahitaji maalumu au wenye mazingira tofauti na walio wengi mashuleni hautokei.[82]

Mkataba dhidi ya ubaguzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Elimu, Sayansi na Utamaduni ambao uliidhinishwa na Tanzania mwaka 1979 unatoa muongozo kwa serikali kuhakikisha inatokomeza aina zote za ubaguzi wenye kuathiri haki ya kupata elimu iwe ni kwenye sheria, sera au utamaduni. Mkataba huu unazitaka serikali “kutengeneza sera ambazo zinalenga kukuza usawa wa fursa na huduma katika kutoa elimu na hususani kuhakikisha kwamba viwango vya elimu viko sawa katika taasisi zote za elimu za umma zilizo katika ngazi sawa na usawa kuhusiana na ubora wa elimu inayotolewa.”[83]

Hatua maalumu zimechukuliwa kulinda haki za wanawake na watoto wa kike kupata elimu kwa viwango vya haki za binadamu kwa Kanda ya Afrika. Itifaki ya Maputo juu ya Haki za Wanawake Afrika imeipa jukumu serikali kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake huku ikiwahakikishia fursa sawa na upatikanaji wa elimu na mafunzo na kuwalinda wanawake na watoto wa kike na aina zote za manyanyaso ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia mashuleni.[84]

Azimio la Vijana wa Afrika lililoridhiwa na Tanzania mwaka 2012 unajumuisha wajibu wa kuhakikisha wasichana wanaopata mimba au kuolewa kabla ya kumaliza shule wanapata fursa ya kuendelea na masomo yao.[85]

Ubora wa Elimu

Ni jambo linaloeleweka kwamba juhudi yoyote ya msingi kuhakikisha haki ya kupata elimu inafikiwa ni lazima itoe kipaumbele katika ubora wa elimu hiyo. Kamati ya Haki za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni inasisitiza kwamba pamoja na jukumu la serikali kuhakikisha elimu inapatikana, ni lazima pia zihakikishe mfumo na maudhui ya elimu ikiwa ni pamoja na mitaala na mbinu za ufundishaji “zinakubalika” na wanafunzi. Kamati inaeleza kwamba kukubalika kwa elimu kunategemea mambo kadhaa ikiwemo dhana kuwa elimu lazima “iwe na ubora.”[86] Lengo ni kuhakikisha kuwa “hakuna mtoto anaemaliza shule bila kuwezeshwa kukabiliana na changamoto ambazo anaweza kukutana nazo katika maisha.”[87] Kwa mujibu wa Kamati ya UN juu ya Haki za Mtoto, elimu bora “inahitaji uangalizi katika ubora wa mazingira ya kujifunzia, mfumo wa kufundisha na kujifunzia, vifaa na matokeo bora ya kujifunza.”[88]

Katika Mkataba Dhidi ya Ubaguzi katika Elimu, nchi wanachama zinawajibika “kuhakikisha viwango vya elimu viko sawa katika taasisi zote za elimu za umma za ngazi sawa na usawa kuhusiana na ubora wa elimu inayotolewa.”[89]

Haki ya Elimu Jumuishi na yenye kuzingatia Watu Wenye Mahitaji Maalum

Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu (MHWU) umelenga kuongeza ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika kila ngazi ya elimu na kuzitaka Nchi wanachama kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanajumuishwa katika elimu na wanawekewa mazingira kuwawezesha kupata elimu kwa usawa kama wengine katika jamii.[90] Watoto wenye ulemavu wanapaswa kuwekewa mipango maalumu ya kuwasaidia kupata elimu kwa ufanisi.”[91]

MHWU inazitaka Serikali kuhakikisha “watu wenye ulemavu wanawekewa mazingira wezeshi katika mfumo mzima wa elimu kwa kuzingatia mahitaji binafsi kuwawezesha kupata elimu kwa ufanisi.”[92] MHWU inafafanua mazingira wezeshi kama “aina yoyote ya uboreshaji wa miundombinu ambayo itamsadia mtu mwenye mahitaji maalumu kufurahia haki zake za kibinadamu na uhuru kama watu wengine katika jamii.”[93]

Katika MHWU, Tanzania inawajibu wa kuhakikisha mazingira wezeshi kwa wanafunzi wenye ulemavu yanawekwa katika shule.[94] Hii inajumuisha wajibu wa kuhakikisha miundombinu ikiwa ni pamoja na shule vinafikika na wanafunzi. Kuhakikisha kwa mfano shule zinakuwa na vifaa na mbinu za kufundishia wanafunzi wenye ulemavu wa kuona au kusikia.[95] Tanzania pia inawajibu wa kuweka viwango vya mazingira wezeshi ili kutoa muongozo wa ubunifu wa huduma na vifaa na kuchukua hatua stahiki katika kuweka miundombinu hiyo.[96]

Ulinzi dhidi ya Vitendo vya Ukatili ikiwa ni pamoja na Ukatili wa Kijinsia, Adhabu za Viboko na Aina ya Adhabu za Kudhalilisha

Serikali inapaswa kuchukua hatua za kisheria, kiutawala, kijamii na kutoa elimu juu ya ulinzi wa watoto dhidi ya vitendo vya kikatili vya kimwili au kiakili, kuumizwa, kutelekezwa, vitendo viovu au unyonyaji pamoja na unyanyasaji wa kijinsia.[97]

CRC inazitaka Serikali kuchukua “hatua madhubuti kuhakikisha nidhamu shuleni zinasimamiwa katika namna ambayo inazingatia utu wa mtoto.”[98] Kamati ya Haki za Mtoto inafafanua adhabu ya viboko kama “adhabu yoyote ambapo nguvu hutumika kwa nia ya kuleta maumivu au usumbufu hata uwe mdogo kiasi gani.”[99]

Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto unazitaka Serikali kuchukua hatua stahiki kuhakikisha “hatua za kinidhamu zinazochukuliwa dhidi ya watoto na shule au wazazi zinazingatia na kuheshimu utu wa mtoto.”[100]

Mwandishi maalumu wa UN anaeandika juu ya mateso na adhabu za kikatili na zile za kudhalilisha alitoa angalizo kwa Serikali kuhusu adhabu za viboko kwamba haiendani na jukumu la Serikali kulinda wananchi dhidi ya adhabu za kikatili.[101] Katazo la Kimataifa juu ya mateso na aina nyingine za adhabu za kikatili na udhalilishaji kwa binadamu linalenga vitendo vyote vinavyopelekea maumivu na mateso ya mwili na akili kwa muathirika.[102] Watoto na wanafunzi waliopo katika taasisi za kujifunzia ni lazima walindwe dhidi ya adhabu za viboko “ikiwa ni pamoja na adhabu zinazotolewa kama hatua za kufundisha au za kinidhamu.”[103]

Mwaka 2011, Kamati ya Wataalamu wa Afrika juu ya Haki na Ustawi wa Mtoto ilizitaka Nchi za Afrika kuchukua hatua thabiti kuondoa ukatili mashuleni.[104] Mwaka 2015, Kamati ya Haki za Mtoto na Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki walizitaka Serikali kufuta adhabu za viboko mashuleni na kurekebisha sheria ili kuzuia adhabu za viboko na aina nyingine za adhabu za kimwili katika nyanja zote.[105] 

Ulinzi dhidi ya Ndoa za Utotoni na Ajira za Watoto

Azimio la Afrika juu ya Haki na Ustawi wa Mtoto linasema, “Ndoa za watoto, wa kike au wa kiume ni lazima zipigwe marufuku.”[106] Azimio hili linazitaka Serikali kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kuweka sheria zinazoeleza umri wa kuoa au kuolewa kuwa zaidi ya miaka 18.[107]

Kamati ya Haki za Watoto (KHW) imekua na msimamo mmoja juu ya miaka 18 kuwa umri wa chini kwa ndoa bila kujali ridhaa ya wazazi na mara kadhaa kuzitaka nchi wanachama kutoa ufafanuzi rasmi wa mtoto katika sheria ambao utaendana na maazimio ya KHW.[108]

Sheria za Tanzania zinavumilia ndoa za utotoni. Watoto wa kike wanaweza kuolewa katika umri wa miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi au miaka 14 kwa ridhaa ya mahakama. Mwaka 1994, Tume ya Kurekebisha Sheria ya Tanzania ilishauri urekebishaji wa Sheria kuongeza umri wa chini wa ndoa kuwa miaka 21 kwa wanawake na wanaume.[109]

KHW pia inazitaka Serikali kuwalinda watoto dhidi ya unyonyaji wa kiuchumi, utendaji wa kazi zenye madhara, zenye kuingilia elimu ya mtoto au zenye athari kwa maendeleo ya afya ya mwili, akili, roho, maadili au kijamii.[110] Mkataba wa Umri wa Chini na ule wa Aina Mbaya za Ajira za Watoto zinaeleza aina za kazi ambazo zinahesabika kama ajira za watoto kutokana na umri wa mtoto, aina na saa za kazi iliyofanyika, athari yake kwa elimu na mambo mengine.[111] Sheria za Tanzania zinakataza aina zote za kazi na ajira za unyonyaji na zenye madhara ambazo zinaingilia elimu kwa watoto. Watoto walio chini ya umri wa miaka 14 hawawezi kuajiriwa.[112]

III.     Vikwazo vya kupata Elimu ya Sekondari  

Maamuzi ya Serikali ya Tanzania kufuta ada za shule yameondoa moja ya vikwazo vikubwa kwa watoto kupata elimu ya sekondari. Bado vikwazo vingine vimeendelea kuzuia wanafunzi wengi kupata elimu ya sekondari au kuzuia uwezo wao kufanya hivyo. Vikwazo kama vile vya kifedha vinaathiri watoto wanaotoka katika familia masikini, umbali wa shule ambao huwalazimu watoto kutembea umbali mrefu kufika shule pamoja na mitihani ambayo inapelekea watoto wengi kuacha shule. Serikali ya Tanzania inabidi iweke mikakati kabambe kuharakisha mipango yake kupambana na vikwazo hivi.

Gharama za Elimu ya Sekondari

Matokeo ya Kufuta Ada za Shule

Kabla ya mwaka 2016, ada ya shule ilikua moja ya kikwazo kikubwa kwa elimu ya sekondari kulingana na mahojiano yaliyofanywa na Human Rights Watch kwa vijana wengi. Utafiti uliofanywa nchi nzima na Twaweza ambayo ni asasi isiyokuwa ya kiserikali na kuhusisha watu 1,900 iligundua kuwa asilimia 89 ya wazazi huchangia fedha kwa elimu ya umma.[113] Kumekuwa na matukio mengi ya wazazi kushindwa kulipa ada ambayo yalipelekea walimu kurudisha wanafunzi nyumbani mpaka pale shule itakapoweza kukusanya fedha za kutosha kukidhi gharama za shule.

Vijana arobaini na nane waliohojiwa na Human Rights Watch waliacha shule moja kwa moja kutokana na gharama za elimu ya sekondari. Vijana kutoka kaya masikini, wale wenye ndugu wagonjwa au waliofiwa na ndugu na wasichana ndio wameathirika zaidi. Abasi, kijana wa miaka 17 kutoka Nzega aliwaambia Human Rights Watch:

Kuanzia kidato cha kwanza wazazi wangu walijitahidi kulipa ada na michango mingine ya shule lakini ilikua ni mzigo mzito wa kiuchumi kwa familia. Hali hii ilizidi kidato cha pili. Hatimaye walishindwa kulipa ada ya shule na ya mitihani. Walimu walinifukuza nirudi nyumbani. Kwa wiki nzima kila siku asubuhi walimu walinifukuza na hivyo nikaamua kuacha shule na kutafuta maisha mengine.[114]

Kabla ya mwaka 2016, ada rasmi za shule za sekondari za umma ilikuwa shilingi za kitanzania (Tsh.) 20,000 (US$9) na zile za shule za bweni shilingi 40,000 ($18).[115] Vile vile wakati mwingine familia za wanafunzi zilitakiwa kulipa shilingi 5,000-10,000 ($2-5) kama malipo ya ulinzi, shilingi 50,000 ($23) kwa ajili ya madawati pamoja na malipo mengine madogo madogo ya sare za shule, kalamu, madaftari, chakula, mitihani na usafiri.[116]

Wanafunzi wengine walieleza Human Rights Watch kwamba wakati mwingine walimu waliwachapa waliposhindwa kulipa michango ambayo walihitajika kulipa au kuzuiwa kuingia darasani mpaka watakapolipa ada. [117]Theodora mwenye umri wa miaka 17 kutoka Nzega aliacha shule aliposhindwa kuendelea kulipa michango:

Walimu walituambia turudi nyumbani… mara nyingi ilikua ni asubuhi. Nilikosa siku nyingi kwa sababu hiyo. Iliathiri masomo yangu kwasababu unaporudishwa nyumbani kwa kushindwa kulipa michango masomo yalikuwa yanaendelea. Nilikosa masomo mengi… walimu walitutukana kwa kushindwa kulipa michango na kusema ni jukumu la mzazi kulipa.[118]

Vivyo hivyo wanafunzi walioshindwa kumudu ada za mitihani hawakuruhusiwa kufanya mitihani na maafisa waliwazuia kuendelea na elimu ya sekondari.[119]

Zaidi ya hayo pia wazazi walichangia mishahara midogo ya walimu kwa kugharamia, mara nyingi kwa lazima, gharama za masomo ya ziada yanayotolewa na walimu. Waliohojiwa walisema kwamba walikuwa wakilipa kati ya shilingi 10,000 na 20,000 ($5 na 9) kwa somo linalofundishwa baada ya muda wa shule. Aina hii ya masomo yanayotolewa baada ya muda wa masomo na walimu imekua ni jambo la kawaida na wakati mwingine la lazima kutokana na mahojiano na wanafunzi yaliyofanya na Human Rights Watch.[120]

Uamuzi wa Serikali kusitisha aina zote za ada na michango ya ziada ya kifedha ikiwa ni pamoja na masomo ya ziada kuanzia Januari 2016 umefungua milango kwa vijana wengi ambao wazazi au walezi wao hawawezi kumudu kulipa ada kwa shule za sekondari. Hivyo uamuzi huu umetatua moja ya kikwazo kikubwa kinachowafanya watoto kuacha shule za sekondari. 

Maafisa wa shule waliohojiwa na Human Rights Watch wametoa taarifa kwamba kumekua na ongezeko kubwa la uandikishwaji wa kidato cha kwanza kutokana na kuondolewa kwa ada katika elimu ya sekondari.[121] Katika shule moja Mwanza, kaimu mkuu wa shule alibainisha kuongezeka kwa mahudhurio: “kwa sababu ya sera hii, wanafunzi wengi wanakuja shule, hapo awali wanafunzi wengi walikua na matatizo ya ada na sare.”[122]

Maafisa waandamizi wa Serikali kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST) walitoa taarifa za kuongezeka maradufu uandikishwaji katika baadhi ya shule ijapokuwa kwa kiasi kikubwa ongezeko kubwa limeonekana katika shule za msingi.[123] Idadi halisi haikuweza kupatikana wakati wa uandishi. Mwezi Agosti 2016, Serikali ilitoa onyo kwa maafisa wa shule kutokudanganya idadi ya waliojindikisha kwa nia ya kujipatia fedha nyingi zaidi kwa shule zao.[124]

Agnes mwenye umri wa miaka 16 ambaye aliwahi kuwa mfanyakazi wa ndani Mwanza anaifurahia sera mpya:

Namshukuru rais kwa kufanya elimu ya sekondari bure, hata hivyo mbali na kutoa vifaa, serikali inabidi itoe elimu (uhamasishaji) kuhimiza wazazi kuwapeleka watoto hasa wa kike shule.[125]

Vikwazo vya Kifedha Vinavyowaathiri Wanafunzi Masikini

Elimu ni bure lakini sio bure kabisa … kwa sasa hakuna shida ya kulipa ada ya shule bali kuwasaidia wale wasioweza kumudu kitu chochote kabisa?

Sandra, 19, ambae kwa sasa anahudhuria kituo cha ushonaji wilaya ya Kahama na ameacha shule akiwa kidato cha pili, Kahama, Januari 2016

Hata baada ya kuondoa ada za shule, gharama za vitu vingine kama vile sare, vifaa vya kujifunzia au chakula vinawakosesha wanafunzi wengi masikini nafasi ya kupata elimu. Ndugu au walezi wenye kipato cha chini wakati mwingine wanashindwa kumudu gharama hizo.[126]Familia nyingi haziwezi kupata fedha za hifadhi ya jamii kuwawezesha kumudu gharama hizo.[127] Serikali haina budi kujitahidi kutumia rasilimali zilizopo kuweka mipango ya muda mfupi na ya kati kuhakikisha vijana walio katika mazingira magumu wanaenda shule ikiwa ni pamoja na kutoa misaada ya kifedha kwa kaya masikini zenye vijana walio katika umri wa kwenda shule.

Emmanuel Samara, mwakilishi wa chama cha walimu kutoka mkoani Mara, moja ya mikoa masikini na yenye idadi ndogo ya wanaoandikishwa shule za sekondari anasema:

Elimu bure ni katika ada pekee lakini kuna michango mingi ambayo wazazi wanatakiwa kuitoa. Kwa kiwango cha umasikini hususani katika mkoa wangu, sidhani kama wazazi wengi wataweza. Tunaongelea wazazi ambao wanaishi chini ya dola $1 ya kimarekani kwa siku na ambao hawana uwezo wa kununua chakula. Wanaishi kwa mlo mmoja kwa siku na wana watoto wengi wasioweza kuwapatia chakula.[128]

Dar es Salaam, Khadija, 16, ameshindwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa sababu ya gharama nyingine. Aliwaeleza watafiti wa Human Rights Watch:

Shule imeanza toka Januari 11 lakini mimi bado sijaanza kwa sababu wazazi wangu hawana uwezo wa kununua sare za shule, begi na vifaa vingine. Wameniambia nisubiri mpaka watakapopata fedha … tunahitaji shilingi 75,000 (US$34).[129]

Saida, 14, ambaye alikua anajiandaa kuingia kidato cha pili huko Kahama alisema: “Nahitaji msaada wa kulipia vifaa vya shule ili niweze kuendelea na shule ya sekondari.”[130]

Benard Makachia, ambaye anaongoza shirika linalotoa ujuzi wa maisha kwa wamama wadogo anaeleza namna gani wakati mwingine wasichana hufanya biashara ya ngono ili kumudu gharama za shule:

Zaidi ya asilimia 20 ya wasichana wanasema umasikini ndio uliowapelekea kufanya ngono. Lakini umasikini kwa upande wao unamaanisha kukosa pesa ya usafiri, chakula, matumizi madogo madogo, sare, viatu, na kumudu gharama za mahitaji mengine ya elimu.[131]

Wanafunzi Wengi Wanaacha Shule

Agizo la Serikali la Januari 2016 kuzuia ulipaji wa ada za shule linamaanisha kwamba wengi ambao walishindwa kupata elimu ya sekondari hapo awali sasa wanaweza kwenda shule. Hata hivyo, mamia kwa maelfu ya wanafunzi wa Kitanzania ambao waliacha shule kabla ya mwaka 2016 kwa sababu walishindwa kumudu ada hawana njia ya kuwasaidia kurudi katika mfumo wa shule. Serikali haina budi kuweka mkakati wa kutoa elimu ya msingi kwa wanafunzi hawa kwa kuwafanya kuwa na vigezo vya kurudi shule za sekondari ili kuendelea na kumaliza elimu hii ya msingi. 

Mitihani-Kikwazo cha Kufikia Elimu ya Sekondari

Kila mwaka, mamia kwa maelfu ya wanafunzi wa darasa la 7 hufanya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi, mtihani ambao ni lazima kufaulu ili kuweza kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya chini.[132] Wataalamu wa elimu wanasema kwa kiasi kikubwa maandalizi duni ya wanafunzi kufanya mitihani hii ya Taifa husababishwa sio na uwezo wa wanafunzi bali na uduni wa ubora wa elimu katika shule nyingi za msingi, uwiano mbovu wa wanafunzi kwa walimu pamoja na msaada duni unaotolewa kwa wanafunzi wenye ulemavu au wale wenye mahitaji maalumu.[133]

Kila mwaka wanafunzi mamia kwa maelfu hufeli mitihani ya darasa la saba. Toka mwaka 2012, zaidi ya vijana milioni 1.6 wamezuiwa kuendelea na elimu ya sekondari kutokana na matokeo yao.[134] Elimu rasmi huishia hapa kwa watoto ambao hufeli mtihani huu kwa sababu fursa ya kurudia mtihani au kurudia darasa la saba haipo.[135] Serikali hutumia mtihani wa darasa la 7 kama chombo cha kuchagua wanafunzi wanaoruhusiwa kuendelea na elimu ya sekondari badala ya kuitumia kama chombo cha kutathmini utendaji wa wanafunzi na kukabiliana na vikwazo vya kujifunza na ubora duni wa elimu unaoathiri wanafunzi.[136]

Utafiti uliofanywa na Human Rights Watch mwaka 2013 na 2014 ulionyesha kwamba watoto wengi wanaofeli mtihani wa darasa la 7 wako katika hatari ya kufanya kazi katika mazingira ya kinyonyaji migodini na wengi walikua wanaozeshwa katika umri mdogo.[137]

Mwaka 2016, Human Rights Watch ilikutana na vijana saba ambao walikua wanafanya kazi kama watumishi wa ndani, wachimbaji wa dhahabu, wakulima na wengine wajawazito baada ya kufeli mtihani wa darasa la 7. Walinyimwa nafasi ya kujiandikisha shule kwa mara nyingine ili kurudia mtihani huo.

Adelina, 17, mtihani wa darasa la 7 ulikuwa mgumu kwake na hakufaulu mtihani huo mwaka 2013, hii ilipelekea kuacha shule na kuanza kufanya kazi katika migodi ya dhahabu akiwa na umri wa miaka 15:

Baada ya kufeli mtihani wa darasa la 7 nilianza kulima, nikafanya kazi katika hoteli na kisha nikaenda mgodini kufanya kazi ya kupasua mawe.[138]

Mtihani wa darasa la saba umekua na changamoto nyingi na uzingatiaji hafifu katika ngazi ya shule. Tathmini ya mwaka 2009 iligundua kwamba mitihani hii ilikua hatarini kutokana na uwizi, matukio kadhaa ya udanganyifu unaofanywa na wasimamizi wa mitihani, walimu na wazazi na changamoto katika usahihishaji wa mitihani.[139] Wanafunzi waliripotiwa kufanya udanganyifu katika mitihani kutokana na ufinyu wa nafasi katika elimu ya sekondari, uoga wa kupewa adhabu kwa matokeo mabovu na maandalizi duni.[140]

Kulingana na Richard Temu, ambae ni afisa mradi-Uwezo, asasi ya elimu isiyokuwa ya kiserikali inayoshugulika na tathmini ya elimu Afrika Mashariki, uduni wa ubora wa elimu ni tatizo kubwa: “Asilimia arobaini [ya wanafunzi] hawako tayari kujiunga na elimu ya sekondari-hawajifunzi chochote-hawafundishwi kusoma wala kuandika [shule za msingi].”[141]

Serikali imepanga kuachana na mitihani ya darasa la saba ifikapo mwaka 2021 wakati ambapo kizazi cha watoto walioko darasa la kwanza sasa hivi watakua wamefika darasa la 7.[142] Kizazi hiki kitakuwa cha kwanza kujiunga moja kwa moja na elimu ya sekondari bila kujali alama au ufaulu wao. Hata hivyo, kwa miaka mitano ijayo wanafunzi wataendelea na mfumo wa mtihani wa darasa la saba na wale watakaofeli hawatoweza kuendelea na elimu ya sekondari.

Clarence Mwinuka, afisa wa WEST anaeleza kuwa mfumo wa mtihani wa darasa la saba unaondolewa katika kipindi cha miaka mitano badala ya kuuondoa mara moja ili kuepuka uwingi wa wanafunzi: “Nia ni kutekeleza taratibu- je tuna madarasa ya kutosha? Walimu wa kutosha? Nia ipo ila hatuwezi kwenda moja kwa moja.”[143]

Mwandishi maalumu wa UN juu ya elimu anashauri Serikali kutumia tathmini ya Kitaifa kuonyesha kwamba wametekeleza majukumu yao ya kuhakikisha watoto wote wanamaliza elimu bora ya msingi na wanapewa nafasi ya kujiunga na elimu bora ya sekondari.[144]

Kama tulivyojadili hapo juu, Serikali ya Tanzania imedhamiria kuondokana na mfumo wa mtihani wa darasa la saba kama kigezo cha kujiunga na elimu ya sekondari ifikapo mwaka 2021. Kwa sasa Serikali haina budi kuchukua hatua stahiki kuhakikisha kwamba wanafunzi wanaofeli mtihani huu hawafukuzwi shule. Wanafunzi wanaofeli mtihani wa darasa la saba wanapaswa kuruhusiwa kujiunga na shule binafsi kurudia darasa na kuruhusiwa kurudia mtihani. Serikali pia itumie mtihani wa darasa la saba kufanya tathmini kuhakikisha wanafunzi wamepata ujuzi na maarifa ya awali na kwamba wameandaliwa vyema kuingia elimu ya sekondari.

Miundombinu Duni ya Shule

Shule zilizotembelewa na Human Rights Watch zilikuwa katika hali mbaya na hazikuwa na madarasa ya kutosha, maktaba na zilikua na miundombinu hafifu ya usafi hususani zile za wasichana na watoto wenye ulemavu. Shule hizi pia hazikuwa na maabara zinazofanya kazi kwa ajili ya masomo ya sayansi na zilikosa vifaa maalumu kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu. Hivi ndivyo hali ilivyo pamoja na dhamira ya Serikali kuziwezesha shule 2,500 kuwa na maabara zinazofanya kazi na kurekebisha nusu ya shule za sekondari kuweza kuwahudumia wanafunzi wenye ulemavu pamoja na kuweka miundombinu ya kutosha ya usafi kwa shule 500.[145]

Kabla ya mwaka 2016, shule za serikali zilikuwa zinategemea angalau asilimia 20 ya michango ya jamii katika kufanya upanuzi wa shule za sekondari.[146] Kufuatia kusitishwa kwa malipo ya ada, shule zimepewa maagizo kuacha kuchangisha wazazi kugharamia maboresho ya miundombinu, vifaa vipya vya kufundishia na kuajiri walimu wa ziada kama ilivyokuwa hapo mwanzo. 

Watafiti wa Human Rights Watch waliona katika shule nne majengo ya maabara za sayansi ambayo hayajamaliziwa yakiwa karibu na majengo ya zamani ya shule. Maafisa wa shule waliwaambia Human Rights Watch kwamba ujenzi ulianza kwa fedha zilizotokana na michango ya wazazi. Hata hivyo ujenzi ulisimama Desemba 2015 baada ya serikali kutangaza kuondoa ada na michango ya wazazi na mpaka sasa shule hazijapokea fedha kwa ajili ya kumalizia miradi hiyo.[147]

Maafisa waandamizi katika shule tatu waliwaambia Human Rights Watch kuwa fedha za ruzuku hazijumuishi bajeti kwa ajili ya kugharamia matumizi kama haya. Hali hii imeziacha shule bila rasilimali zinazohitajika kununua bidhaa au kujenga miundombinu inayohitajika na shule. Huko Mwanza, kaimu mwalimu mkuu aliwaambia Human Rights Watch:

Kuna uhaba … tunashindwa kuhakikisha mazingira mazuri ya kujifunzia. Kwa mfano hakuna meza na viti vya kutosha, ubao … tuna uhaba wa madarasa.[148]

Mei 2016, WEST ilitangaza mipango zaidi ya kukarabati wa shule kadhaa za sekondari na kutoa vifaa vya maabara.[149] Ili kutekeleza dhamira ya serikali ya elimu bure, serikali haina budi kubuni mbinu kadhaa kuhakikisha inapeleka rasilimali zaidi katika ujenzi wa shule mpya na kuboresha miundombinu ya shule. Serikali haina budi pia kutambua hizi gharama za ziada katika mipango yake ya muda mfupi na wa kati na katika bajeti ili kuhakikisha sera ya elimu ya sekondari inatekelezwa kwa ufanisi na bure.

Usafiri Duni

Wanafunzi wengi husafiri umbali mrefu kwenda shule kitu ambacho kinaathiri mahudhurio pamoja na utendaji wao shuleni.[150] Wanafunzi kumi na tatu waliohojiwa na Human Rights Watch hutembea zaidi ya saa moja kwenda shule; wengine hutembea hadi kilometa 20 au kuendesha baiskeli kati ya kilometa 20-25 ambapo huondoka nyumbani asubuhi na mapema.[151] Wanafunzi wengi waliohojiwa na Human Rights Watch walisema huwa wamechoka siku nzima shuleni kutokana na kutembea mwendo mrefu.[152]

Kwa mfano katika kisiwa cha Ukerewe na visiwa vya jirani kuna shule za sekondari za umma 22 pekee ambazo zinahudumia kata 26. Kata nne hazina shule za sekondari za umma.[153] Kwa mujibu wa mwanaharakati wa ndani wa elimu aliehojiwa na Human Rights Watch karibu na Nansio, Ukerewe mjini anasema mwendo mrefu kwenda shule na utegemezi wa vivuko ambavyo wakati mwingine havitabiriki ndio moja ya sababu kwa nini vijana wanaacha shule mara kwa mara.[154]

Katika maeneo ya vijijini na mikoa ya ndani kama Shinyanga ambapo wanafunzi wameripotiwa kusafiri kilometa hadi 25 kwa baiskeli, umbali ni moja ya kikwazo ambacho kinaondoa motisha kwa baadhi ya wanafunzi.[155] Martin Mwenza, kaimu mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Shinyanga anasema wanafunzi wengi shuleni kwake wanatembea hadi kilometa 10 kitu ambacho ni kikwazo kikubwa kwa wengi.[156]

Wanafunzi wanaochelewa shule walituambia hupewa adhabu na walimu kwa kushindwa kufuata kanuni za shule.[157] Elsa, 18, hutembea kilometa 18 kwenda shule: “Natembea kwa saa mbili kwa mwendo wa haraka. Mara nyingi huchelewa … wakati mwingine napewa adhabu. Huchapwa au kuambiwa nikate majani.”[158]

Katika hatua ya Serikali kuboresha usafiri kwa wanafunzi, madereva wa magari binafsi hutakiwa kuwatoza wanafunzi nauli ya chini. Hata hivyo wamiliki wa mabasi hawapati ruzuku au fidia kwa kupunguza nauli kwa wanafunzi.[159] Wanafunzi wengine waliiambia Huma Rights Watch kwamba kutokana na hali hiyo, madereva wakati mwingine hukataa kusimama kubeba wanafunzi.[160]

Kwa mfano, wanafunzi wengi Dar es Salaam wanalalamikia madereva wa mabasi na abiria kuwanyanyasa kwa kuwasukuma na kuwapiga na wakati mwingine kuwatukana.[161] Kiwango cha unyanyasaji dhidi ya wanafunzi wanaotumia mabasi katika jiji ulipelekea Modesta Joseph ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari kuanzisha tovuti ya “Kilio Chetu” ambapo wanafunzi wanaweza kutoa taarifa ya aina yoyote ya unyanyasaji na kisha kutuma malalamiko ya wanafunzi kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi kavu na Majini.[162]

 

IV.   Adhabu za Viboko na Kufedhehesha 

Tunapigwa sana. Wakikupiga leo basi utapata nafuu ndani ya siku mbili. Kila mwalimu anapiga wanafunzi kadri anavyojisikia. Mwalimu mmoja anaweza kukuchapa hadi mara 15 kama anajisikia.

—Rashidi, 18, Mwanza, Januari 21, 2016

Matumizi ya adhabu za viboko na wakati mwingine ukatili ni jambo la mara kwa mara kwa maisha ya kila siku ya wanafunzi katika shule za Tanzania. Ripoti iliyotolewa na Jukwaa la Sera ya Mtoto wa Afrika inaonyesha kwamba nusu ya wasichana na wavulana wa Tanzania waliopitia unyanyasaji wa kimwili wameadhibiwa na walimu.[163] Serikali ya Tanzania haina budi kuchukua hatua za haraka kuondoa au kupambana na aina zote za ukatili mashuleni. 

Adhabu za Viboko kama Utamaduni uliozoeleka Nchini

Maafisa wa shule mara nyingi hutumia adhabu za viboko – hii ikiwa ni pamoja na adhabu zote ambazo zinahusisha matumizi ya nguvu na kupelekea kusababisha maumivu au hali ya usumbufu hata kama ni kidogo namna gani.[164] Viongozi waandamizi wa kisiasa ikiwa ni pamoja na Rais John Magufuli na aliekuwa naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi mara kadhaa wamekua wakihamasisha matumizi ya adhabu za viboko mashuleni.[165] Machi 2016, akihutubiwa umati mkubwa wa watu, Rais Magufuli alisema: “Ninashangaa kwanini wameacha kuchapa shuleni. Mimi mwenyewe nilichapwa na ndio maana nimesimama hapa leo.”[166]

Kinyume na wajibu wake wa haki za binadamu kimataifa, Tanzania ina kanuni za kitaifa juu ya adhabu za viboko ikiwa ni pamoja na muongozo wa matumizi ya fimbo mashuleni.[167] Kanuni hizi zinatoa kibali cha matumizi ya adhabu za viboko kwa “utovu wa nidhamu shuleni,” na makosa makubwa… yanayofanyika ndani au nje ya shule … ambayo uongozi wa shule unaona yanaharibu sifa ya shule.”[168]

Maafisa wa shule wanaruhusiwa kutoa adhabu “kwa kumchapa mwanafunzi mkononi au katika makalio akiwa amevaa nguo kwa fimbo nyepesi na kuepuka kumchapa mtoto kwa kutumia kitu kingine au katika sehemu nyingine ya mwili.”[169]

Walimu wakuu wa shule ndio wenye mamlaka ya kusimamia utoaji wa adhabu. Adhabu haitakiwi izide viboko vine. Pale mkuu wa shule anapokaimisha mamlaka kwa mwalimu mwingine ni lazima afanye hivyo kwa maandishi.[170] Kanuni hizi pia zinaelekeza kwamba ni lazima mwanafunzi wa kike achapwe na mwalimu wa kike na ikishindikana basi mwalimu mkuu.[171] Pamoja na yote, shule ni lazima ziweke kumbukumbu kwa kila adhabu ya viboko inayotolewa.[172]

Kwa mujibu wa kanuni hizo, hatua za kinidhamu pia zinaweza kuchukuliwa kwa mwanafunzi anaekataa adhabu ya viboko- anaweza kufukuzwa shule – au mwalimu mkuu au mamlaka ya shule inayovunja kanuni hizi.[173] 

Matukio ya adhabu za viboko yaliyoripotiwa kwa Human Rights Watch yameonyesha kuenea kwa matumizi ya adhabu za viboko yanayopitiliza kikomo cha kishera cha kanuni za sasa za serikali.

Maafisa waandamizi au walimu waliulizwa na Human Rights Watch iwapo walitoa taarifa ya idadi ya matukio yaliyopelekea kutumia fimbo darasani. Mwalimu mmoja (jina limehifadhiwa) alisema: “Tunashauriwa kwamba pale wanafunzi wanapochapwa zaidi ya mara mbili inapaswa kutoa taarifa kwa mwalimu mkuu. Imeandikwa kwamba inapaswa kufanya hivyo, lakini … ninaweza … kuchapa zaidi ya mara nne na nisitoe taarifa.”[174] Mmoja ya afisa mwandamizi wa shule alisema kwamba shule yake haifuati kanuni: “Kusema ukweli hatuweki kumbukumbu ya adhabu za viboko.”[175]

Katika ripoti yake ya mwaka 2015 kwa Kamati ya Haki za Watoto, serikali “ilionesha kuwa ni halali kutumia fimbo kwa wanafunzi watukutu shuleni na kudai iko nje ya wigo wa adhabu kali.”[176] Katika majibu yake, Kamati ilitoa wito kwa serikali kufuta au kurekebisha sheria ili kuzuia adhabu za viboko na za mwili katika mazingira yote na kueleza wasiwasi wake juu ya matumizi ya adhabu kali ikiwa ni pamoja na matumizi ya fimbo kuendelea kutumia kwa wingi.”[177]

Mwaka 2015, Bunge la Afrika Mashariki lilitoa wito kwa Tanzania kupiga marufuku adhabu za viboko mashuleni.[178]

Kuenea kwa Matumizi ya Adhabu za Viboko

Watoto wanaacha shule kutokana na fimbo.

—Sandra, 19, Wilaya ya Kahama, Januari 2016.

Karibu vijana na wanafunzi wote waliohojiwa na Human Rights Watch wameshapitia adhabu za viboko wakati fulani katika maisha yao ya shule na wanafunzi wengi wa shule za sekondari waliripoti uzoefu wao juu ya adhabu za viboko. Matumizi ya mara kwa mara ya adhabu za viboko yameelezwa katika utafiti wa mwaka 2011 juu ya ukatili dhidi ya watoto uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshugulikia Watoto (UNICEF). Ripoti hii inaonyesha kwamba watoto wa kike na wa kiume wa Tanzania mara kwa mara huchapwa, kupigwa mateke, ngumi au hata kutishwa kwa silaha na walimu.[179]

Kwa mujibu wa Jukwaa la Sera ya Mtoto wa Afrika, “Idadi ya matukio ya unyanyasaji unaofanywa na walimu Tanzania ni wa kiwango cha juu: asilimia 78 ya wanafunzi wa kike na asilimia 67 ya wanafunzi wa kiume waliotoa taarifa ya kunyanyaswa na walimu walisema walikua wanapigwa ngumi, mateke au kuchapwa zaidi ya mara tano.”[180]Wanafunzi wa shule za sekondari na walimu walioongea na Human Rights Watch walisema katika shule zao watoto huchapwa mara kwa mara kwa fimbo – za mianzi au miti ambazo mara nyingi huonekana darasanai. Katika matukio mengine, wanafunzi waliripoti kupigwa na walimu kwa kutumia mikono yao au vitu vingine. Walimu wa kike na wa kiume wameripotiwa kuwapiga wanafunzi bila kujali jinsia au ulemavu wao.

Baadhi ya wanafunzi waliripoti kupigwa katika makalio wakati wanafunzi wa kike wakiripoti kupigwa katika makalio na matiti.[181] Lewis, mwanafunzi mwenye umri wa miaka 20 na mwenye ulemavu wa ngozi yuko kidato cha III katika shule ya sekondari Shinyanga, aliwaambia Human Rights Watch, “Walimu wanakupia na fimbo katika makalio. Unalala chini na wanakuchapa mbele ya darasa. Kwa mfano, kama hujamaliza kuandika notisi darasani.”[182]

Fatma, 16, alisema: “Walimu wanapiga wanafunzi … ukishindwa kujielezea katika somo flani, wanakupiga … kwa fimbo na wakati mwingine hata kukupiga vibao.”[183] Wiki tatu katika mwaka wake mpya wa shule, Aisha, 15, anaripoti kuchapwa fimbo “mara moja katika wiki chache zilizopita.”[184] Sandra, 19, ambae aliacha shule akiwa kidato cha II mwaka 2014 aliwaambia Human Rights Watch: “Nilipopigwa kibao, nilijiskia kama nina alama za mkono wa mwalimu usoni kwangu.”[185]

Watoto wengi huchapwa au kupigwa kwa kuchelewa shule na hii ni baada ya kuwa wametembea takribani kwa saa mbili kufika shule iliyo karibu na wanapoishi.[186] Ana, 17, aliacha shule akiwa kidato cha I baada ya kukata tamaa kutokana na mwendo mrefu kuelekea shule na matokeo ya kuchelewa: “Unapata zaidi ya viboko 16 kwa kuchelewa. Nilikua naogopa kupigwa lakini ukikosa kufika shule pia utapigwa.”[187]

Jaclen, 17, aliwaambia Human Rights Watch:

Adhabu hutolewa ukichelewa. Unaweza kupewa adhabu ya viboko au kukata majani wakati wengine wakiwa darasani. Au kusafisha vyoo bila vifaa vya kusafishia … tunatumia majani kama madekio [kusafisha sakafu za vyoo].[188]

Leocadia Vedasius, mwalimu wa shule ya sekondari katika shule iliyotembelewa na Human Rights Watch katika Kisiwa cha Ukerewe, anasema mara nyingi hutumia adhabu za viboko kuonyesha mamlaka kwenye darasa lenye wanafunzi zaidi ya 60: “Unawajengea hofu-wakikuona wanakua na wasiwasi darasani. Wanafunzi wengine ni wakorofi darasani- inabidi kufanya kitu ili waweze kufanya vizuri darasani. Lakini kama wakifeli lazima tutoe maelezo. Wakati mwingine tuna wanafunzi wengi sana … njia rahisi na ya haraka ni kutumia adhabu ya viboko.”[189]

Baadhi ya walimu waliokubali kuongea kwa kuficha majina yao walieleza sababu zinazowapelekea kutumia adhabu za viboko. Mwalimu mmoja anasema: “Wakati mwingine inabidi utumie fimbo kuwanyoosha.” Mwalimu mwingine aliwaambia Human Rights Watch anawapiga “ watoto katika makalio-natumia fimbo kuwapa maumivu katika miili yao-napendelea kutumia fimbo pale ninapomuita mwanafunzi na kisha anakukimbia.” Mwalimu mwingine, “Unaweza kuongea na wasikusikilize- hivyo natumia fimbo.”[190]

Mwalimu mmoja anahusisha matumizi ya adhabu za viboko na mazingira duni ya kujifunzi:

Mazingira ya kufundisha ni mabovu mno-natumia chaki kufundisha. Inabidi nilazimishe wanafunzi kusoma. Ninachomaanisha ni kwamba hatuna michezo au burudani. Mwalimu mkuu anasema hakuna pesa kwa matumizi hayo … shule hii haina maktaba, hakuna vitabu. Mahusiano ya mwanafunzi na mwalimu si mazuri.[191]

Wakati wengi kati ya maafisa wa shule na serikali waliohojiwa na Human Rights Watch wanapuuzia matumizi ya adhabu za viboko, mwalimu mmoja alipinga matumizi ya adhabu za viboko, alisema: “Sidhani kama hizi adhabu zinasaidia. Utovu wa nidhamu umeongezeka licha ya adhabu hizi. Matokeo ya kumchapa mtoto … ukiwa na hasira unapitiliza kiwango na mtoto anateseka zaidi. Tunapowachapa tuwasababishia wasiwasi.”[192] Ushahidi wa kisayansi unaonyesha kuwa ubongo wa mtoto huathirikia sana kwa kufanyiwa vitendo vya ukatili wakati wa utoto wake, na katika miaka ya awali mtoto hupata kiwewe pamoja na kipindi cha ujana ambapo anakua amepevuka kihisia na amepata ujuzi wa juu.[193]

Kulingana na Eric Guga, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Child Rights Forum, adhabu za viboko na za kikatili zimeota mizizi katika utamaduni wa shule na “kila mmoja anajaribu kutetea [unyanyasaji],” na hakuna jitihada za kutosha zilizochukuliwa kuwapatia walimu njia mbadala ya kusimamia darasa au aina tofauti ya kufundisha kwa kuwashirikisha wanafunzi. Kutokana na Guga, tatizo ni kwamba kanuni nyingi za shule zinaeleza namna mwanafunzi anavyotakiwa kuwa lakini hakuna maelezo ya namna mwalimu anatakiwa kuwa.[194]

Katika shule moja ya sekondari Mwanza, wanafunzi nane wa kike waliwaonyesha Human Rights Watch alama za mikwaruzo na michubuko miguuni na mapajani. Salma, 15, aliwaambia Human Rights Watch kwamba wasichana hudhalilika zaidi wanapopigwa wakiwa katika hedhi:

Wanatumia vimbo kama adhabu, kwenye makalio na mgongoni. Inabidi tuiname kama hivi. … wakati wa hedhi hali ni mbaya zaidi … wakati wanatuchapa na fimbo, huendelea kutuchapa na wakati mwingine pedi zinadondoka na damu kuchafua nguo zetu.[195]

Katika shule hiyo hiyo, wanafunzi wa kike wanasema wamekuwa wakipigwa mara kwa mara katika matiti na walimu wa kike. “Hawathamini wasichana na wanatudhalilisha,” anasema Renata, 15, ambae ni muathirika wa adhabu hizi.[196]

Kwa mujibu wa wanafunzi wengine, walimu pia hutumia vitendo vya kufedhehesha na matusi.[197] Martha, 15, and Jacklen, 17, waliwaambia Human Rights Watch mara nyingine wanafunzi hulazimishwa kuruka kichura au kutembea kwa magoti huku mikono ikiwa nyuma. “Ninajiskia vibaya. Hii hutokea pia nikifeli jaribio,” anasema Jacklen.[198]

V. Vikwazo, Ubaguzi na Unyanyasaji dhidi ya Wanafunzi wa Kike

Juhudi za Serikali ya Tanzania kuhakikisha elimu bure ya sekondari kwa watoto wote zinapingana na kushindwa kwake kubadili sera zinazoruhusu na kuhamasisha ubaguzi dhidi ya wanafunzi wa kike na kuvumilia unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya wanafunzi wa kike.

Wasichana mara nyingi ndio hupata matatizo: wengi wao hutegemewa kulea wagonjwa nyumbani au kuacha shule na kufanya kazi za ndani na familia nyingine zinatoa vipaumbele kwa watoto wa kiume kusoma.[199]

Viwango vya mahudhurio ya wasichana hupungua kwa kiasi kikubwa kati ya umri wa miaka 13 hadi 14 umri ambao wengi wao huingia kidato cha I au cha II.[200] Ingawa kuna usawa wa kijinsia katika uandikishaji wa kidato cha I, chini ya theluthi moja ya wasichana wanaomaliza elimu ya msingi wanamaliza elimu ya sekondari ngazi ya chini.[201]

Shule nyingi hulazimisha wasichana kupima mimba mara kwa mara na kufukuza wale wanaokutwa na mimba, wanaojifungua au kuolewa, jambo ambalo mara nyingi hupelekea juhudi za wasichana kupata elimu kuzimwa. Mwezi Machi 2016, Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kuondoa Ubaguzi Dhidi ya Wanawake ilisema hatua nyingi kama hizi ni za kibaguzi na kuitaka Serikali ya Tanzania kuchukua hatua kuondoa vitendo hivi.[202]

Wanafunzi wa kike katika shule nyingi wanashindana na unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa walimu wa kiume, kushambuliwa au kulazimishwa katika mahusiano ya kingono kwa nguvu-tatizo ambalo limeendelea kuwepo kutokana na mamlaka za shule na serikali kushindwa kuwawajibisha walimu.

Kufukuzwa kwa Wasichana Wajawazito na Wenye Watoto

Shuleni alikuwa anakuja muuguzi (nesi) kutoka hospitali kwa ajili ya kupima mimba. Walinipima na kunikuta na ujauzito. Wanashika tumbo lako. Hufanya hivyo kwa kila msichana kila mwezi. Kisha waliandika barua kwenda kwa wazazi kuwaeleza kuwa nilikua mjamzito na kuwaita shule. Wazazi walipokuja shule walipewa barua ya kufukuzwa kwangu shule. Nilikua na ujauzito wa miezi mitatu.

—Imani, 20, Mwanza, Januari 21, 2016

Wasichana wakipata mimba mara nyingi hufukuzwa shule au kuacha kwa sababu wao au wazazi wao huhisi kwamba inabidi waache kwenda shule.[203]

Katika kijiji cha Igombe kilichopo mkoani Mwanza, Mercy, 20, alieleza kwamba, “Huwapeleka wasichana wote hospitali na kuwapima mimba mmoja baada ya mwingine. Ikigundulika kama msichana ana mimba hufukuzwa shule.”[204] Sophia, 20, aliacha shule akiwa kidato cha III alipopata mimba, “Kwa sababu kulikua na sheria shuleni kama ukijigundua una mimba inabidi auche kwenda shule.”[205]

Kufukuzwa shule kwa wasichana wanaopata mimba ni jambo ambalo linakubalika katika kanuni za kufukuzwa shule za Tanzania ambazo zinasema “Mwanafunzi anaweza kufukuzwa shule kama … mwanafunzi ame … amefanya kosa kinyume na maadili” au “amefunga ndoa.”[206] Sera haifafanui makosa ya kimaadili lakini viongozi wa shule mara nyingi hutafsiri mimba kama moja ya kosa la kimaadili.[207]

Maafisa wa elimu waandamizi wa serikali wanatetea mtazamo kwamba wanafunzi wajawazito hawatakiwi shule kwani wanaweza kuwashawishi vibaya wasichana wengine, lakini wanaongeza kwamba kuna mipango ya elimu isiyo rasmi kwa ajili ya kina mama vijana.[208] Kwa mujibu wa Dkt. Leonard Akwilapo, naibu katibu mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), “Sheria zetu hazikubali wasichana wajawazito kuwa shule … ni sheria zetu za kimila.[209]

Mimba za utotoni ni kawaida sana Tanzania.Kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2015-2016 wa Idadi ya watu na Afya, mmoja kati ya wasichana wanne wenye umri kati ya miaka 15-19 tayari ni mama.[210] Wasichana wengi waliohojiwa na Human Rights Watch wanafahamu wasichana walioacha shule kutokana na mimba. Kwa mfano, Eileen, ambaye ni mama tayari anakadiria kwamba angalau wasichana 20 aliokuwa nao kidato cha II walikuwa na watoto.[211] Jessica, 19, kutoka Igombe anakumbuka:

Kutoka kidato cha I hadi kidato cha III wasichana wengi waliacha shule kutokana na mimba. Nakumbuka wasichana nane ambao waliacha shule kwa sababu ya mimba au kuolewa na wengine sita wako nyumbani na watoto.[212]

Leocadia Vedastus, mwalimu wa shule ya sekondari Kisiwa cha Ukerewe anaeleza namna ambavyo wasichana walio wengi wanakubali kushiriki ngono ili kupata usafiri wa kwenda shule na kisha kuacha shule wanapopata mimba. Anasema:

Wasichana wanaotoka mbali hukutana na wanaume wenye magari au pikipiki kisha kuwapa lifti na kuomba kufanya nao [wasichana] mapenzi. Mimba za utotoni ni tatizo kubwa. Ninapofundisha mimi takribani wasichana watano waliacha kuja shule kutokana na mimba.[213]

Kituo cha Haki za Uzazi, asasi ya kimataifa isiyokuwa ya serikali inakadiria kwamba shule za Tanzania hufukuza zaidi ya wasichana 8,000 kila mwaka kutokana na kuwa na mimba.[214] Shule nyingi haziweki sababu ya mwanafunzi kufukuzwa katika kitabu cha mahudhurio, kutokana na mahojiano ya Human Rights Watch na viongozi wa shule.[215]

Rita mwenye miaka kumi na tisa kutoka wilaya ya Kahama aliwaambia Huma Rights Watch kwamba uoga wa kufukuzwa shule ulimfanya aache shule alipopata mimba:

Nilipata mimba nikiwa kidato cha II. Nilikua na miaka 17. Walimu waligundua nina mimba, hawakunifukuza lakini niliamua kuacha shule. Nilikua najua kwamba hakuna mwanafunzi anaruhusiwa shule akiwa na mimba … niliacha shule kutokana na sera hiyo.[216]

Mwaka 2015, Kamati ya haki za Mtoto ilieleza wasiwasi wake kwa kutokuwepo kwa sheria madhubuti zinazokataza wasichana kufukuzwa shule wanapopata mimba. Kamati ilitoa wito kwa serikali kuchukua hatua za haraka kuhakikisha wasichana wenye mimba wanaendelea kuandikishwa shule na kuwasaidia kujiunga na kuendelea na masomo katika shule za umma.[217]

Vipimo vya lazima vya mimba Shuleni

Shule za sekondari Tanzania mara kwa mara huwapima wasichana mimba kwa lazima ikiwa ni hatua ya kinidhamu kufukuza shule wale wenye mimba.[218] Wasichana wengi waliohojiwa na Human Rights Watch mara kwa mara walipimwa mimba wakiwa shule au saa nyingine kupelekwa katika zahanati ya karibu kupimwa na wauguzi.[219] Wakati mwingine viongozi wa shule hufanya vipimo wenyewe kwa kushika matumbo ya wasichana kuangalia kama wana mimba.[220]

Wanafunzi wa sasa na wale waliomaliza waliwaambia Human Rights Watch kwamba shule inapopata matokeo inawajulisha wazazi kwa barua au kwa ujumbe wa simu na kisha kuwafukuza.[221] Imani, 21, ambae ni mama wa mtoto wa miaka 3 sasa alifukuzwa shule alipokua anakaribia kumaliza Kidato cha II: “Walinipima na kugundua ni mjamzito. […] Kisha wakaandika barua kwa wazazi wangu kuwaleza kwamba nilikua na mimba … ilibidi wazazi waende shule. Wazazi walipokuja shule walipewa barua ya kufukuzwa kwangu shule. Nilikua na mimba ya miezi mitatu.” ”[222]

Upimaji wa mimba unahusisha ukiukwaji mkubwa wa haki ya faragha kwa wasichana, usawa, uhuru na kuwazuia wasichana kuendelea na masomo. Upimaji wa lazima mara nyingi hupelekea wasichana kuacha shule kwa kuepuka aibu au kutengwa.[223] Wakati mwingine wazazi huwafukuza watoto wenye mimba nyumbani. Jessica, 19, alipoteza marafiki wengi wa shule ambao waliacha shule kati ya Kidato cha I na cha III kwa sababu walikua na mimba: “Shule ziliwafukuza, wengine walifukuzwa na wazazi … waliishia mitaani.”[224]

Ugumu wa Kurudi Shule baada ya Mimba

Wasichana wengi wanaopata mimba hawarudi shule baada ya kujifungua au hata mimba kuharibika kwa sababu wanaogopa kutengwa au wanakataliwa kujiunga upya na shule.[225] Kama Sera ya WEST ya kuruhusu wasichana kujiandikisha upya shule itatekelezwa itasaidia kuhakikisha viongozi wa shule hawakatai kuwapokea wasichana wenye watoto na wanaotaka kurudi shule.

Utafiti wa kitaifa uliofanywa Novemba 2016 unaonyesha kwamba jamii inaunga mkono suala la wasichana kurudi shule: asilimia 62 ya wananchi waliohojiwa wanaamini kwamba wasichana waliopata mimba wakiwa shule wanatakiwa wakubaliwe kurudi shule baada ya kujifungua.[226] Lakini hata wakikubaliwa kurudi shule, wasichana wengi wenye watoto wanakosa msaada nyumbani au mipango ya kulea watoto kuhakikisha watoto wanalelewa vyema ili kuhamasisha wasichana kurudi shule.[227]

Sawadee aliacha shule alipopata mimba akiwa Kidato cha III. Bila ya msaada wa familia yake anahangaika kutafuta namna ya kurudi shule:

Ndani ya miezi mitatu, wazazi wangu waligundua nina mimba. … walinifukuza nyumbani. Nilikua na miaka 16 wakati huo. Shuleni nilifukuzwa kwa kuwa nilikuwa na mimba. Ndoto zangu zilipotea-nitaenda wapi? Niko njia panda sasa-niende wapi?[228]

Maafisa wa serikali waliwaambia Human Rights Watch kwamba wizara iko katika mchakato wa kuandaa “rasimu ya muongozo wa kujiunga upya” ambao utaruhusu wasichana waliopata watoto kabla ya kumaliza shule kurudi shule katika kipindi kisichopungua miaka miwili toka kujifungua na kuwaruhusu kuchagua shule watakazotaka kwenda.[229] Rasimu ya sera hii ilikamilika mwezi Juni 2015 na sasa inasubiri kupitishwa na maafisa waandamizi wa WEST.[230] Haya hivyo, asasi zisizo za kiserikali zinaonyesha wasiwasi kwamba muongozo huo umekua katika majadiliano tangu mwaka 2013.

Eileen, 21, ambae ana mtoto wa miaka mitatu, aliambiwa atakubaliwa kurudi shule lakini wakati wa mahojiano alikuwa bado anasubiri maombi yake yafanyiwe kazi. Januari 2016, mwalimu mkuu wa shule Kisiwa cha Ukerewe alimwambia ampe pesa ili kumuandikisha shule:

Nimekua nikifuatilia shule [sekondari] nyingine lakini sijapata taarifa yoyote kutoka kwao. Ukiwa na pesa unakuwa na nafasi. Inabidi umlipe mwalimu mkuu shilingi 40,000-50,000 ($US18-23), lakini bado utaratibu ni mrefu. Inabidi utafute mtu [afisa elimu] kwa ajili ya kusaini barua. Mwalimu mkuu ameendelea kunipa ahadi.[231]

Agnes Mollel, anaesimamia makazi ya wasichana waliofukuzwa au kukimbia nyumbani huko Arusha kutokana na unyanyasaji ilimbidi kupitia matabaka mengi ya viongozi ili kuhakikisha msichana ambae alikua na ulemavu wa kusikia na ambae alibakwa shuleni na kupata mimba anapewa nafasi ya kurudi shule baada ya kujifungua: “Ilinibidi kuwapigia simu [mara nyingi]. Nilipiga simu shule na kuongea na mwalimu mkuu na pia Wizara ya Elimu.”[232]

Unyanyasaji wa Kijinsia dhidi ya Wasichana Shuleni

Kuna walimu wanaojihusisha na masuala ya ngono na wanafunzi-Najua [wasichana] wengi ambao hii imeshawatokea … mwanafunzi anaekataa hupewa adhabu. Wakati mwingine walimu wanaowatongoza wanafunzi na kukataliwa huuliza maswali tofauti darasani na mwanafunzi anaposhindwa kujibu hupewa adhabu. Najisikia vibaya … hata kama ukiripoti suala kama hili halichukuliwi uzito. Inatufanya tujisikie hatuko salama. Wasichana watatu waliacha shule kutokana na walimu na ngono mwaka 2015.

Joyce, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016

Unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wasichana umetapakaa katika shule za Tanzania na wakiwa njiani kuelekea shule.[233]

Human Rights Watch ilifanya mahojiano na baadhi wa wasichana na wanawake ambao wamepitia unyanyasaji wa aina hii au kutongozwa na walimu wa kiume au kuwalazimisha wao au marafiki zao kushiriki vitendo vya ngono. Wengi wao walisema hawaripoti matukio haya kwa kuwa hawajui namna ya kuyaripoti, hawaamini kama madai yao yatafanyiwa kazi au wanaogopa visasi na walimu.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa linashughulikia masuala ya Watoto (UNICEF) juu ya ukatili dhidi ya watoto uligundua kwamba 1 kati ya wasichana 10 wamepitia ukatili wa kijinsia wakiwa watoto uliofanywa na walimu wakati asilimi ndogo ya watoto wa kiume waliripoti juu ya ukatili wa kijinsia shuleni kutoka kwa marafiki au wanafunzi wenzao.[234]

Ubakaji ni kosa la jinai kwa sheria za Tanzania na unahusisha mtu yeyote mwenye mamlaka na anaetumia nafasi yake kutishia au kushinikiza wasichana au wanawake kujihusisha na vitendo vya ngono.[235] Unyanyasaji wa kijinsia unafafanuliwa kama “ maneno au vitendo vya kingono ambavyo hufanywa bila ridhaa na watu wenye madaraka katika maeneo ya kazi au maeneo mengine”, wakati unyonyaji wa kingono unahusisha mtu kutumia nafasi yake ya ushawishi au mahusiano na mtoto kushawishi vitendo vya ngono au aina zingine za unyanyasaji wa kijinsia.[236]

Beatrice, 17, ambae sasa yupo Kidato cha II Sinyanga, aliwaambia Human Rights Watch:

Wasichana wanapatia mimba shuleni … nyingine za walimu nyingine za wanakijiji. Mwaka jana mmoja wa marafiki zangu alipewa mimba. Mwalimu bado yupo hapa. Anafanya hivyo kwa wasichana wengine.[237]

Lucia, 17, ambae aliacha shule kabla ya kuingia Kidato cha II na sasa anafanya kazi za ndani Mwanza, anasema:

Mwalimu mmoja alikua anajaribu kunishawishi kufanya mapenzi hivyo sikutaka kwenda Kidato cha I kwa ajili hiyo … Nilijiskia vibaya … Niliamua kuacha shule kuepuka kuchezea pesa za wazazi wangu.[238]

Sada, 16, aliwaambia Human Rights Watch kwamba baadhi ya walimu katika shule yake ya sekondari Mwanza waliwaomba yeye pamoja na rafiki zake kuwa na mahusiano ya kimapenzi: “Nilichanganyikiwa mwalimu alivyofanya hivyo. Tunaogopa, tuna hofu-tunaambiana pale inapotokea.”[239]

Kwa mujibu wa Richard Mabala, mkurugenzi mtendaji wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya vijana, kuna utamaduni ulioenea wa unyanyasaji wa kijinsia na ukatili wa kijinsia katika shule, utamaduni huu unakua kwa kukosekana kwa sera zinazojitosheleza juu ya unyanyasaji wa kijinsia.[240] Walimu, wakiwa kama watumishi wa umma lazima waheshimu muongozo wa utendaji wa Watumishi wa Umma na kujiepusha na vitendo vyote ambavyo vitapelekea unyanyasaji wa kijinsia ikiwa ni pamoja na ubakaji, udhalilishaji au ukatili wa kijinsia.[241] Mwaka 2015, Kamati ya Haki za Watoto ilieleza wasiwasi wake kwa kutokuepo kwa uchunguzi wa nidhamu au tuhuma za walimu wanaokiuka miiko ya kazi zao.[242]

Mpango wa Kitaifa wa serikali wa mwaka 2017/18-2021/22 juu ya Ulinzi wa Watoto na Wanawake unatambua ukatili uliokithiri dhidi ya watoto mashuleni pamoja na “Ulafi wa ngono” katika shule;[243] na inatanabaisha kwamba “kila mtoto na mtu mzima katika mazingira ya elimu lazima awe na uwezo wa kushiriki katika elimu bila uoga wa ukatili.”[244] Sambamba na hiyo, Tume ya Huduma za Walimu ya Tanzania imepanga kuzindua muongozo wa kitaifa wa maadili kuhakikisha walimu wanaheshimu viwango vya ulinzi wa mtoto.[245]

Unyanyasaji wa Kijinsia njiani Kuelekea Shule

Shule iko mbali, na tunahitaji kuwa na pesa ili kutumia basi la shule ili kufika shule mapema. Lakini wazazi hawana pesa za kutumia kila siku. Tunatembea kwenda shule. Tunapochelewa shule tunaadhibiwa. Ndio maana ni rahisi kushawishiwa na wengine [wanaume] tukiwa njiani kuelekea shule-kwa pesa, usafiri. Pia [kuna] umasikini: Tunaondoka nyumbani lakini hakuna kifungua kinywa au chakula cha mchana. Hivyo wanaume wanatushawishi kwamba watatupa pesa na chakula na wao wanafanya mapenzi na sisi kisha tunapata mimba.

-Jane, 17, aliacha shule Kidato cha II alipopata mimba, Mwanza mjini, Januari 2016.

Wanafunzi wengi wanakabiliwa na mwendo mrefu kwenda shule bila kuwa na usafiri salama na uhakika. Hali hii inawaweka wasichana katika hatari ya unyonyaji wa kijinsia na unyanyasaji kutoka kwa madereva, wauza maduka na watu wengine ambao hutumia pesa, bidhaa au huduma kuwashawishi kufanya nao mapenzi.[246]

Renata, 15, aliwaambia Human Rights Watch:

Madereva wa usafiri wa umma hawapendi kubeba wanafunzi [kwa sababu] tunalipa nauli tofauti [nauli ndogo]-hivyo madereva wanapenda watu wazima. Makondakta hujenga mahusiano [ya ngono] na wanafunzi ili [kutupatia] unafuu wa nauli- kama [hatuna] mahusiano na dereva basi tunachelewa shule.[247]

Richard Mabala, mkurugenzi wa Tamasha, asasi ya vijana isiyokuwa ya kiserikali anasema: “Wasichana wanaishia kuwa marafiki na madereva nah ii inapelekea unyanyasaji wa kijinsia. Wasichana wanatafuta lifti na wanakuwa na mahusiano ya kimapenzi na madereva.”[248]

Wakati mwingine wazazi huchagua kuwalipia wanafunzi mabweni ya watu binafsi au nyumba za watu binafsi ambazo zipo karibu na shule katika kata yao ambapo wanakodisha kwa bei nafuu. Bado huu utaratibu unaendelea kuwaweka wanafunzi wa kike katika hatari ya unyonyaji wa kijinsia na unyanyasaji.[249]

Wengi waliohojiwa na Human Rights Watch kuanzia wanafunzi wa kike na wa kiume, walimu na wazazi wanakubali kwamba wasichana inabidi waishi katika mabweni yaliyo salama ili kupunguza hatari zinazohusiana na kutembea mwendo mrefu kwenda shule na hususani unyanyasaji wa kijinsia na mimba za utotoni.[250] Serikai imetangaza mipango ya ujenzi wa mabweni zaidi kwa ajili ya kuwapatia makazi wasichana karibu na shule kuepuka hatari na gharama za usafiri.[251]

Ukosefu wa Taarifa na Uwajibikaji

Walimu wa kike wakati mwingine wanatuambia: ‘Wewe ndie ulimfuata mwalimu!’

Sada, 15, Mwanza, Januari 21, 2016

Serikali ya Tanzania inakosa sera za uhakika na taratibu za utoaji taarifa, uchunguzi na kutoa adhabu kwa matukio ya unyanyasaji wa kijinsia, unyonyaji au ubakaji shuleni.[252]

Kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Ubakaji, malalamiko ya unyanyasaji wa kijinsia lazima yafanyike na muathirika ndani ya siku 60 tangu kosa lifanyike.[253] Bado utoaji taarifa juu ya unyanyasaji wa kijinsia sio jambo rahisi kwa wasichana. Wasichana wengi waliwaambia Human Rights Watch kwamba hawajisikii kama wanaweza kutoa taarifa juu ya unyanyasaji shuleni. Mariamu, 20, aliemaliza Kidato cha IV Dar es Salaam anasema:

Kuna mwalimu mmoja kila wakati alikua akijaribu kuwa na mahusiano na wasichana … kama ukikataa, anakua mkali na anaweza kulipiza kisasi … Nilikua nawaogopa walimu … Nilikuwa naogopa kuwaambia uongozi wa shule … pengine wasingemfukuza kazi, wangesema ilikua kosa letu … wasichana wanapata matatizo shule lakini hawana sehemu ya kutoa taarifa au mtu wa kumuelezea matatizo yao.[254]

Walimu na wakufunzi wanawajibika kutoa taarifa au ushahidi wa unyanyasaji kwa afisa wa ustawi wa jamii.[255] Kwa kawaida shule huchagua walimu kuwa ‘walezi,’ ambapo kazi yao ni kusikiliza malalamiko na taarifa za unyanyasaji ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia au utovu wa nidhamu unaotokea shule.

Mifumo ya shule ya kutoa taarifa kwa sasa haina ufanisi, kwa mujibu wa Ayoub Kafyulilo, afisa elimu UNICEF, hususani pale ambapo mlezi wa shule anapokua anafanya unyanyasaji kwa watoto au kupuuza malalamiko yao.[256] Eric Guga, mkurugenzi wa Tanzania Child Rights Forum anasisitiza kwamba shule hazihitaji kusubiri muongozo wa serikali kuchunguza tuhuma za ubakaji. Lazima wazingatie Kanuni za Adhabu na Sheria ya Mtoto na “mwalimu anaembaka au kumshambulia mtoto lazima ahukumiwe sio kufukuzwa kazi pekee.”[257] Wawakilishi wa Mtandao wa Elimu Tanzania, mtandao wa kitaifa wa utetezi unaowakilisha wadau wa elimu, pia wanashauri kurejesha muongozo wa zamani na mpango wa ushauri nasaha shuleni wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), mpango mpana ambao pia ulipata kuungwa mkono na taaisi nyingi za UN kuchagua washauri wenye ujuzi katika shule zote nchi nzima.[258]

Ukosefu wa Vifaa vya Kutosha vya Usafi na Usimamizi wa Usafi wa Hedhi

Tulikua na vyoo vya wasichana lakini vilikua vimechakaa na sio visafi. Hakukuwa na maji hivyo tulikua tunatumia karatasi. Hakuna mfumo wa kusukuma uchafu wala kusafisha mikono. Wengine [wasichana] walikuwa hawatumii vyoo na badala yake wanatumia maeneo mengine. Kulikuwa na jengo ambalo halijakamilika ambapo wasichana wengi walikuwa wanakwenda kubadili pedi huko na kutupa zilizotumika. Wakati mwingine nilipokuwa katika hedhi nilikaa nyumbani.

Sophia, 20, aliacha shule akiwa Kidato cha III mwaka 2015, Mwanza, Januari 21, 2016

Uwepo wa vifaa vya usafi na vyoo salama na vya kutosha ni sehemu ya msingi ya mazingira ya kujifunzia yanayokubalika, lakini katika shule nyingi za sekondari vyoo havikidhi viwango.[259] Vifaa vya kutosha vya usafi na kusafisha mikono vinapunguza hatari ya magonjwa kama vile kuharisha na magonjwa ya kuambikiza.[260] Uwepo wa vifaa vya kutosha vya usafi kipindi cha hedhi pia unaongeza mahudhurio ya wasichana shuleni.[261]

Mwaka 2012, Serikali ilipitisha mpango mkakati wa miaka mitano kuboresha maji na usafi katika shule kwa kubaini kuwa kuboresha upatikanaji wa maji safi ya kutosha, vifaa vya usafi na mazingira kutaboresha utendaji wa kitaaluma, mahudhurio shuleni na kwa ujumla afya ya watoto shuleni.[262] Mwaka 2016 ilitoa muongozo wa kitaifa kuhakikisha kiwango cha chini cha upatikanaji wa maji na vifaa vya usafi mashuleni. Venance Manori, afisa mwandamizi WEST, anakiri uwepo wa mahitaji ya kutoa vifaa vya usafi vya kutosha mashuleni lakini anaweka bayana kwamba “usimamizi wa usafi wa hedhi unategemea fedha za nje … hatuna bajeti hiyo.”[263]

Wanafunzi wengi waliohojiwa na Human Rights Watch waliripoti kuwa wanatumia vyoo vichafu na kwa msongamano.[264] Katika shule moja nje kidogo ya Nansio, Ukerewe mjini, wasichana na wavulana iliwabidi kutumia choo kimoja. Mwalimu aliwaambia Human Rights Watch: “Tuna choo kimoja. Ni jambo lisilokubalika kwa msichana na mvulana kutumia choo kimoja. Ni jambo la kizamani kuwalazimisha kushirikiana kwenye matumizi ya choo. Hatuna nafasi kwa mahitaji ya kila mwezi ya wasichana.”[265]

Kusitishwa kwa ada za shule na michango ya wazazi pia kumeathiri juhudi za kuboresha miundombinu ya usafi. Huko Mwanza, wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari walichanga fedha kujenga vyoo vipya kwa ajili ya wasichana ambavyo viko mbali na vile vya wavulana kabla ya Januari 2016. Hata hivyo baada ya michango ya wazazi kusitishwa pamoja na agizo la kufuta ada na kukosekana kwa fedha za ziada kutoka serikalini, vyoo vipya vilifunikwa na kuacha kutumika wakati Human Rights Watch walipotembelea shule hiyo Januari na Mei 2016.

Usimamizi mzuri wa usafi wa hedhi unahitaji upatikanaji wa kutosha wa maji, uwepo wa mazingira safi, yenye faragha ili kuruhusu wasichana kubadili au kutupa kwa ustaarabu vifaa vya usafi, utaratibu mzuri wa kusimamia taka na upatikanaji wa taarifa za usafi kwa kuzingatia watoto wenye mahitaji maalumu.[266]

Wanafunzi wa kike waliripoti changamoto kadhaa wanapokwenda shule kipindi cha hedhi. Wasichana wengi waliwaambia Human Rights Watch kwamba huwapasa kutumia vitambaa ambavyo vinaweza kuvuja au kuwa ngumu kuwaweka wasafi wakati wote kwa sababu hawana pesa ya kununua pedi na wakati mwingine hukosa kwenda shule kwa kuwa hakuna vifaa vya kutosha kutumia wakati wa hedhi wakiwa shule.

Rebeca, 17, ambaye kwa sasa yuko Kidato cha IV katika shule ya sekondari Ukerewe, aliwaambia Human Rights Watch:

Wakati mwingine [kuwa katika siku zako] ni changamoto na inazuia wasichana kwenda shule. Ukikaa muda mrefu unaweza kukuta damu imechafua sketi yako. Wavulana wanakucheka. Tunajadili haya na marafiki. Wanaweza kukupa sweta ukafunika sketi yako; kisha unamuomba mwalimu uende nyumbani.[267] 

Katika kuwezesha usafi wa hedhi inahitajika upatikanaji wa taarifa kwa wasichana, lakini wasichana wengi waliohojiwa na Human Rights Watch hawakua na maafisa wa shule wanaowaamini au walimu wa kuongea nao. Ukosefu wa taarifa kuhusu hedhi unaweza kupelekea unyanyapaaji na miiko juu ya hedhi. Sada, 15, aliwaambia Human Rights Watch:

Sikujifunza kuhusu hedhi katika somo la biolojia au sayanzi, nategemea kujifunza mwaka huu lakini sio kwa undani. Hakuna muuguzi shuleni … hakuna wa kuongea nae kuhusu hedhi. Wasichana wengine hawaji shule … wavulana wanatucheka ila wakati mwingine nikijiskia vibaya namuambia mwalimu.[268]

Unyanyapaaji juu ya hedhi unaweza kumfanya msichana kujiskia aibu au mnyonge shuleni. Tabia za walimu kwa wasichana walio katika hedhi wakati mwingine sio za kujali. Salma, mwanafunzi wa Kidato cha II, Mwanza anasema: “[kama]tukiomba ruksa ya kuondoka [darasani], hutangaza [kuwa tuko kwenye hedhi] kwa darasa zima.”[269] Matokeo yake, mara nyingi walimu hawaambiwi kwa nini tunakaa nyumbani: “hatuna uwazi kwenye suala hili, tukiwaambia walimu tunawadanganya … nitasema naumwa,” anasema Rebeca.[270]

Kuhakikisha kwamba hedhi haiwi kipingamizi kwa wasichana kupata elimu kunahitaji zaidi ya uwekezaji wa miundombinu au utoaji wa vifaa vya usafi. Wasichana wanahitaji taarifa za kutosha kuhusu mfumo mzima wa hedhi na uchaguzi wa namna bora ya kuhakikisha usafi kipindi cha hedhi.

Ukosefu wa Upatikanaji wa Elimu ya Kina ya Uzazi na Kujamiiana

Utoaji wa taarifa za kina za uzazi kwa wanafunzi na vijana walio nje ya shule unawawezesha kulinda afya zao, ustawi na heshima.[271] Mwaka 2013, Tanzania ilipitisha dhamira ya kikanda kuhakikisha elimu bora ya kina na huduma za uzazi na na masuala ya kujamiiana ambayo ni rafiki kwa vijana ifikapo mwisho wa mwaka 2015.[272]

Wasichana na vijana wa kike wengi waliohojiwa na Human Rights Watch walieleza kwamba wanapata elimu finyu juu ya masuala ya kujamiiana na afya ya uzazi shuleni. [273] Rita, alienukuliwa hapo juu, anaongeza: “Sikuwa na taarifa [elimu ya kujamiiana] kuhusu mimba na nini kitatokea.”[274]

Mara nyingi wasichana wanakosa taarifa na rasilimali zinazowawezesha kujifunza na kuelewa kuhusu masuala ya kujamiiana na uzazi. Wasichana wenye watoto walioongea na Human Rights Watch wanakubali kwamba hawakujua wanaweza kupata mimba kwa kujamiiana kwa mara ya kwanza. Katika matukio yasiyopungua matatu, wasichana wanasema walipata taarifa za uzazi kupitia vituo vya afya au asasi zisizokuwa za kiserikali pale walipokuwa wajawazito tayari.[275]

Kwa mujibu wa Theresa, 19:

Hawakutufundisha elimu ya kujamiiana tukiwa Kidato cha I na Kidato cha II … afya ya uzazi ilifundishwa tulivyokuwa Kidato cha III, hivyo kabla ya hapo hujui chochote. Lakini hata wale wanaofundishwa wakiwa Kidato cha III na cha IV bado wanapata mimba, hivyo ni somo au mada lakini sio kwa kina.[276]

Elimu ya afya ya uzazi na kujamiiana sio somo linalojitegemea katika mtaala wa shule za sekondari wa mwaka 2010, na ulipendekezwa kama mada mtambuka kwa huduma za ushauri katika mtaala wa 2007. [277] Walimu wana hiari ya kufundisha vipengele kadhaa katika somo la sayansi, kwa mfano maambukizo ya UKIMWI au vipengele vya msingi ya uzazi, lakini wanafunzi wengine wanasema kwamba wanafundishwa wakifika Kidato cha III wakati ambapo idadi kubwa ya wanafunzi wanakuwa wameshaacha shule kutokana na mimba.[278]

Serikali haina budi, kwa kuzingatia umri, kutoa elimu ya kina na yenye kujumuisha elimu ya kujamiiana na afya ya uzazi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha inapatikana katika miundo inayozingatia wanafunzi wenye mahitaji maalumu kama vile kutumia vifaa maalumu vya kufundishia au miundo ambayo ni rahisi kusoma katika mitaala ya shule za msingi na sekondari kwa wanafunzi wote.[279] Kulingana na Kamati ya Haki za Mtoto, maudhui lazima “yalingane na ushahidi wa kisayansi na viwango vya haki za binadamu na yafanyiwe kazi na vijana.”[280] Shule lazima ziwe na programu za elimu zinazotoa taarifa za kutosha juu ya masuala ya kujamiiana na afya ya uzazi. Pia lazima waweke mazingira salama ambapo wasichana wanaweza kujadili masuala ya kujamiiana na afya za uzazi ikiwa ni pamoja na mimba na hili lifanywe na watumishi waliopata mafunzo ya ushauri kwa wasichana

VI. Vikwazo Vinavyowakabili Wanafunzi wenye Ulemavu

Sheria ya Tanzania ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010 inawapa watu wenye ulemavu haki sawa ya kupata elimu na mafunzo katika mazingira ya umoja kama raia wengine, na kuweka ulinzi mkali dhidi ya ubaguzi katika taaisisi za elimu.[281] Aidha, sheria inasema kuwa watoto wenye ulemavu wanapaswa kuhudhuria shule za kawaida za umma na wanapaswa kupatiwa msaada sahihi au huduma muhimu za kujifunza.[282]

Hata hivyo, kiuhalisia, watoto wenye ulemavu wanakabiliana na kiwango kikubwa cha ubaguzi katika shule za msingi na sekondari na katika jamii kwa ujumla.[283]

Nchini kote, watoto wenye ulemavu wana uwezekano mara mbili zaidi wa kutohudhuria shule kamwe kama watoto wasio na ulemavu na huendelea ngazi za juu za elimu nusu ya kiwango cha watoto wasio na ulemavu.[284] Vijana wachache sana wenye ulemavu wanahudhuria shule za sekondari. Mwaka 2011, Shirika la Umoja wa Mataifa linashughulika na Watoto (UNICEF) linakadiria kuwa asilimia 0.3 ya watoto wa kiume na asilimia 0.25 ya watoto wa kike ambao ni walemavu wameandikishwa shule za sekondari.[285] Takwimu za karibuni za serikali zinaonyesha mwaka 2012 wanafunzi 5,495 pekee wenye ulemavu waliandikishwa shule za sekondari; na mwaka 2013 idadi ya walioandikishwa ilipungua hadi 5,328.[286] Katika miaka yote hii, kulikuwa na idadi ndogo sana ya wanafunzi wa kike wenye ulemavu walioandikishwa elimu ya sekondari.[287]

Elimu jumuishi inalenga kuhakikisha mazingira yote ya shule yanatengenezwa kuendeleza ushirikishwaji na sio ubaguzi au ushirikiano. Katika mazingira jumuishi, watoto wenye ulemavu lazima wahakikishiwe usawa katika mfumo mzima wa elimu yao ikiwa ni pamoja na kuwa na fursa na uwezo wa kuchagua kwenda shule za kawaida kama wakitaka, na kupata elimu bora katika misingi ya usawa sambamba na watoto wasio na ulemavu.[288]

Wanafunzi saba wenye ulemavu waliohojiwa na Human Rights Watch walipata elimu ya msingi katika shule maalumu ambapo walikuwa wakisoma na wanafunzi wengine wenye ulemavu.[289] Watoto wengi wenye ulemavu wanaopata elimu ya msingi huandikishwa katika shule maalumu za msingi ambazo ziko chache nchini. Shule kadhaa za kawaida za msingi na sekondari zimetenga vitengo vya mahitaji maalumu kuhudumia watoto wenye ulemavu.[290] 

Wanafunzi wanaoandikishwa katika shule maalumu ambazo kwa kawaida uhudumia watoto wenye ulemavu wa mwili na hisia hufuata mtaala wa kitaifa, na kufanya mtihani wa kumaliza darasa la 7 katika misingi sawa na wanafunzi wasio na ulemavu walioandikishwa katika shule za kawaida za umma.[291] Kwa mujibu wa maafisa wenye wajibu wa elimu ya mahitaji maalumu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), watoto wachache sana wenye ulemavu wa akili wa kati au uliokomaa wanafaulu elimu ya msingi, moja ya sababu ni kutokana na kuandikishwa katika shule maalumu ambapo mitala hulenga kufundisha stadi za maisha na ufundi stadi. Grayson Mlanga kutoka WEST aliwaambia Human Rights Watch: “Wengi wao sio sehemu ya maisha ya kielimu … wengi wanaitwa wanaojifunza polepole.”[292]

Shule za sekondari Tanzania zinakosa vifaa vya kujitosheleza au rasilimali zingine kwa ajili ya kuhudumia watoto wenye aina zote za ulemavu, mbali na mpango wa kina wa serikali wa elimu jumuishi.[293] Ni asilimia 75 kati ya shule za sekondari za umma 3,601 zenye vitengo vya mahitaji maalumu na walimu wenye sifa, kutokana na idara ya Mahitaji Maalumu ya Elimu ya WEST.[294]

Katika shule moja Kisiwa cha Ukerewe, Sigareti Lugangika, mwalimu mkuu aliwaambia Human Rights Watch: “Kamwe katika miaka yangu mitatu [katika hii shule], na hapo awali miaka saba katika shule nyingine Mwanza … hatukuwahi kuwa na watoto wenye ulemavu. Kwa kawaida, watoto wenye ulemavu wanakwenda shule maalumu [za msingi] pekee. Hawawezi kuja katika shule ya sekondari ya kawaida.”[295]

Kwa sasa kuna shule 27 pekee za sekondari ambazo zina uwezo wa kujumuisha wanafunzi wenye ulemavu kwa sababu shule hizi zina vitengo maalumu pamoja na walimu na nyingi zinatoa huduma ya bweni kwa wanafunzi wenye ulemavu. Shule hizi zinahudumia wanafunzi wenye ulemavu wa viungo, wa ngozi, pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa kuona au kusikia na wale walio na upungufu kiasi wa ulemavu wa kiakili ambao wamefuzu kuendelea na shule za sekondari.

Wanafunzi kutoka mikoa yote nchini hupelekwa katika shule hizi. Hii hupelekea watoto kuishi mbali na familia zao na mara nyingi masaa mengi mbali na familia na jamii zao. Oscar, 18, mwanafunzi wa Kidato cha III mwenye ulemavu anaesoma shule ya bweni Shinyanga ambayo iko takribani kilometa 500 mbali na mkoa wake aliwaambia Human Rights Watch:

 Wazazi wengi hawafiki kuchukua wanafunzi. Wazazi hawajafika kututembelea. Unaona wazazi ukienda likizo nyumbani … sio zaidi ya mara nne kwa mwaka, au Juni na Desemba.[296]

Ukosefu wa Shule zinazoweza kuhudumia Wanafunzi wenye Ulemavu

Hakuna shule iliyotembelewa na Human Rights Watch ilikuwa na miundombinu ya kuwezesha wanafunzi wenye ulemavu; na mara nyingi, ardhi yenye mabonde na milima inamaanisha wanafunzi walio katika baiskeli ya kusukuma hawawezi kutembea na wanafunzi wenye ulemavu wa macho au wanaona kwa tabu wanaweza kuumia. Shule pia zinakosa vifaa vya kujifunzia kwa ajili ya walemavu kuhakikisha wanafunzi walemavu wanahudumiwa inavyopaswa darasani.

Shule moja ya sekondari Mwanza ambayo ina wanafunzi ambao wana ulemavu wa macho au wanaona kwa tabu pamoja na idadi ndogo ya wanafunzi wenye ulemavu wa viungo iko katika eneo lenye vilima na mabonde kadhaa. Wanafunzi wa bweni lazima wapande na kushuka vilima kutoka shuleni kwenda bwenini. Wanafunzi wenye ulemavu wameripoti kuanguka na kuumia mara kwa mara. Wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi lazima wasindikizwe na walimu au maofisa wa shule kuwalinda na mashambulizi yoyote.[297]

Shule ya sekondari ya bweni Shinyanga imeandikisha wanafunzi 99 walio na ulemavu kati ya 1,035 mwanzoni mwa mwaka wa masomo. Marxon Paul, ambaye ni mwalimu mkuu, aliwaambia Human Rights Watch: “Shule haikujengwa kwa madhumuni ya kuhudumia wanafunzi wenye ulemavu. Majengo sio mazuri kwa ajili yao.”[298]

Oscar, 18, alienukuliwa awali, anapata tabu kutumia choo au kwenda darasani akiwa shule na hata bweni akiwa ni mwanafunzi mwenye miguu ya bandia na anaetumia magongo:

Vyoo ni tatizo. Kuna vyoo vya shimo. Naweza kuvitumia [kwa kutoa miguu ya bandia na kuweka mikono katika viatu kuepuka kushika sakafu] lakini ni vigumu sana … wanafunzi wengine wenye ulemavu wa viungo wanajisaidia vichakani-wanatumia vichaka kunapokuwa hakuna mwalimu. Vyoo vya shule ni vichafu mno [lakini] watapata magonjwa mengi wakienda vichakani.[299]

Kwa kuongeza, shule nyingi zinakosa vifaa au msaada wa ufundishaji kufanya elimu ipatikane kwa wanafunzi wote katika misingi ya usawa. Hii inatolewa mfano kutokana na hali za wanafunzi waliohojiwa na Human Rights Watch ambao wana ulemavu wa macho au wanaona kwa tabu ikiwa ni pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi. Nasser, 18, mwanafunzi wa Kidato cha IV ambae ni mlemavu wa macho anaesoma shule ya bweni Shinyanga, anaelezea matatizo yake: 

Hakuna mashine maalumu za kusomea (Perkins brailler) wala vitabu vya kiada. Mashine tunazotakiwa kuzitumia … hazifanyi kazi. Inatuzuia kufanya kazi za darasani na mazoezi vizuri. Napata notisi kila baada ya wiki mbili au mwezi mmoja baadae [ukilinganisha na wengine darasani]. Inanifanya niwe nyuma kiutendaji darasani-wakati Napata notisi, tayari niko nyuma vipindi viwili au vitatu.[300]

Lewis, mwanafunzi wa Kidato cha III mwenye ulemavu wa ngozi, ameandikishwa katika shule hiyo hiyo ya bweni kama Nasser, aliwaambia Human Rights Watch:

Wakati mwingine walimu hawajali hususani unaposema unahitaji msaada … kwa mfano, unaenda kwa mwalimu kuomba daftari kunakili naotisi vizuri au kupata ufafanuzi … na wanakataa … wakati mwingine unajiskia kubaguliwa … wakati mwingine maisha ya shule ni magumu sana.[301]

Kwa mujibu wa Alfred Kapole, mwenyekiti wa shirika linalowakilisha watu wenye ulemavu mkoani hapa: “Walimu wanadai kwamba kwasababu kuna wanafunzi wenye ulemavu … wanahitaji vifaa maalumu … lakini hakuna fedha. Shule hazina fedha za ziada kugharamia vitu hivi.”[302] 

Katika shule ya bweni Shinyanga, Human Rights Watch walijifunza kwamba walimu wanafanya kazi na vifaa vichache mno vya kusaidia wanafunzi wenye ulemavu, na walimu wengine wanaona wanafunzi wenye ulemavu wa hisia wanakosa kujifunza. Marxon Paul, mwalimu mkuu, anasema serikali haitoi fedha za ziada kwa wanafunzi wenye ulemavu.[303]

VII.     Ukosefu wa Elimu Bora katika Shule za Sekondari

Kutokana na ongezeko kubwa la uandikishaji, mfumo wa elimu ya umma unashindwa kutoa elimu bora kwa ngazi ya msingi na sekondari.[304] Katika miaka ya karibuni, serikali imetambua changamoto hii na kuweka dhamira ya kuboresha elimu hususani kwa shule za msingi.[305] Mamia kwa maelfu ya wanafunzi sasa wanasoma katika mfumo duni na wanapimwa katika masomo ambayo mara kadhaa hayafundishwi mara kwa mara katika shule zao.[306]

Shule za sekondari Tanzania-hasa zile zilizoko maeneo ya vijijini zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu wenye sifa na ujira mzuri.[307]

Matokeo yake, masomo kama vile hisabati na sayansi wakati mwingine hayafundishwi kabisa na idadi ya wanafunzi darasani ni kubwa. Wanafunzi pia wanakosa vifaa vya kujifunzia vya kutosha na msaada wa kubadili lugha ya kujifunzia kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza.[308]

Vipengele muhimu vya mazingira mazuri ya kujifunzia- idadi ya kutosha ya walimu wenye sifa na motisha, upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia, vyumba vya kutosha vya madarasa na vifaa vya usafi na elimu jumuishi-vilikua adimu katika shule nyingi zilizotembelewa na Human Rights Watch.[309]

Viwango vya ufaulu kwa mwaka kwa mtihani wa sekondari Kidato cha IV unaonyesha idadi ndogo ya wanafunzi wanafikia alama zinazoridhisha ambazo zinawaruhusu kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya juu au mafunzo ya ufundi stadi.[310] Mwaka 2010, karibu ya asilimia 50 ya wanafunzi walifaulu mtihani wa Kidato cha IV au Cheti cha Elimu ya Sekondari.[311] Mwaka 2015, asilimia 25 pekee ya wanafunzi waliohitimu ndiyo waliofikisha alama za kutosha kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya juu; asilimia 26 ya wanafunzi waliohitimu ambao ni jumla ya zaidi ya vijana 175,000 walifeli mtihani wa Kidato cha IV.[312]

Umahiri Duni wa Kufundisha

Tuna uhaba wa walimu wa hisabati. Inatuathiri kwa sababu tuko hapa kujifunza. Mwaka huu tuna mtihani wa majaribio wa Kidato cha III, hivyo kama mwalimu hatokuja kutufundisha tutafeli.

Farida, 17, Shinyanga, Januari 2016

Ukosefu wa Walimu Waliohitimu

Moja ya sababu kubwa inayoathiri ubora wa elimu ni uhaba mkubwa wa walimu wenye sifa.[313] Kwa mujibu wa Chama cha Walimu Tanzania, zaidi ya walimu 50,000 wanahitajika kujaza nafasi katika shule za sekondari.[314] Matokeo yake wanafunzi wengi hususani wale walioko maeneo ya vijijini wanajifunza katika mazingira magumu. Hawana walimu waliohitimu katika baadhi ya masomo ya msingi kama hisabati, sayansi na Kiingereza.[315] Utoro wa walimu nao ni tatizo kwa shule nyingi: Wanafunzi wasiopungua 20 kutoka Kidato cha I hadi cha IV wamesema baadhi ya walimu hukosa vipindi mara kwa mara.[316]

Walimu wengi waliohojiwa na Human Rights Watch hawajapata mafunzo wakiwa kazini na hivyo hawajajifunza mbinu mpya za ufundishaji, maarifa mapya au mbadala ya masomo sambamba na mabadiliko ya mitaala. Mwalimu mmoja wa historia hajapata mafunzo katika miaka yake 11 ya kufundisha.[317] Katika shule ya sekondari jijini Mwanza, ambayo inahudumia wanafunzi wenye ulemavu, walimu 2 kati ya 13 wanaofundisha watoto wenye mahitaji maalumu ndio wamepata mafunzo ya lugha ya ishara na hakuna mwalimu mwingine aliepata mafunzo ya ziada juu ya elimu jumuishi au lugha ya ishara.[318]

Ukubwa wa darasa

Mwaka 2010, shule za sekondari zilikua na wastani wa zaidi ya wanafunzi 70 kwa darasa, idadi ambao ni kubwa kuliko wanafunzi 40, kiwango kilichowekwa na serikali.[319] Wanafunzi wengi waliohojiwa na Human Rights Watch wamesoma katika madarasa yenye msongamano. Kwa mfano katika kijiji cha Igombe, Caroline, 15, aliwaambia Human Rights Watch alisoma Kidato cha II na wanafunzi 78 wakati John, 14, anasoma Kidato cha III na wanafunzi 80 katika darasa moja.[320]

Kutokana na ukubwa wa darasa, walimu waliwaambia Human Rights Watch inakuwa vigumu kwa wao kutoa msaada kwa mwanafunzi mmoja mmoja.[321] Wanafunzi wengi pia walieleza kutopewa vitabu na vifaa vya kujifunzia ili kuhakikisha wanaelewa na kukumbuka kile wanachojifunza.[322] Ripoti wa Benki ya Dunia inahusisha ukosefu wa umakini wa kutosha na msaada kwa ajili ya wanafunzi na kushindwa kutambua mapema wanafunzi wenye mahitaji ya kujifunza na kiwango kikubwa cha kufeli katika ngazi zote za elimu ya msingi na sekondari ngazi ya chini.[323]

Ukosefu wa walimu wa hisabati na sayansi

Agosti 2016, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia alitangaza kwamba masomo ya sayansi yatakua ni lazima kwa wanafunzi wote wa Kidato cha I hadi Kidato cha IV.[324] Bado shule zilizotembelewa na Human Rights Watch zilishindwa kuhakikisha hata kiwango cha chini cha ufundishaji wa masomo haya. 

Shule sita zilizotembelewa hazikuwa na walimu wa kudumu wa hisabati na sayansi. Shule ya sekondari iliyoko Mwanza mjini, yenye wanafunzi 569 walioandikishwa Januari 2016, ina walimu wa kudumu 29. Miongoni mwao, wanne wanafundisha Kiingereza, 10 wanafundisha historia, watano wanafundisha sayansi; na mwalimu mmoja anafundisha hisabati shule nzima, isipokuwa pale shule inapomlipa mwalimu wa mkatana kuja kusaidia. Shule haina mwalimu wa fizikia. Na bado shule haipati bajeti ya ziada kuajiri walimu wa sayansi.[325]

Kabla ya 2016, shule nyingi zilikua zinategemea michango ya wazazi kuajiri au kulipa walimu wa kujitolea, mara nyingi wanafunzi waliomaliza Kidato cha VI, kufundisha masomo haya.[326] Kutoka na sera ya kufuta ada, shule hizi hazina tena uwezo wa kuchangisha wazazi. Tangu Januari 2016, serikali haija ajiri walimu zaidi wa kudumu au kuongeza fungu la bajeti katika fedha za ruzuku za mwezi za shule kuwezesha shule kuajiri walimu wa muda mfupi.[327] Katika shule iliyoko kijijini, Shinyanga, Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, aliwaambia Human Rights Watch Januari 2016 kuwa:

Kutokana na sera ya elimu bure, hatuwezi kulipa walimu tena-ilikuwa ni walimu wa sayansi. Wiki iliyopita tulikuwa na mkutano wa wazazi-tuliongea nao kuhusu upungufu wa walimu wa hisabati lakini hatukupata suluhisho. Hivyo hisabati haifundishwi kwa sasa hapa shuleni.[328]

Victoria, 18, Kidato cha IV, aliamua kumlipa mwalimu binafsi ili amfundishe masomo ya sayansi. Analipa shilingi 15,000 za kitanzania (US$7) kwa mwezi.[329] Lakini wanafunzi wengi waliohojiwa hawana uwezo kumudu gharama za msingi za elimu.[330]

Beatrice, 17, alihamishwa kwenda kwenye mkondo tofauti wa masomo mwaka 2016 kutokana na ukosefu wa walimu wa sayansi wenye sifa: “Ndoto zangu zilikuwa kusoma masomo ya sayansi lakini hakuna walimu wa sayansi, nilihamishiwa darasa la masomo ya sanaa, nasoma historia, uraia na jiografia. Sijisiki vema kutokuwa na masomo ya sayansi.”[331]

Wanafunzi na vijana wengi waliwaambia Human Rights Watch kuwa wanafanya mitihani bila kuwa na uelewa wa kutosha wa masomo. Prosper, 15, alieingia Kidato cha II hakumaliza mtaala wa fizikia na kemia kwa sababu hakukuwa na mwalimu.[332]

Eva, 18, aliechukua masomo ya sayansi Kidato cha III na Kidato cha IV pamoja na wanafunzi wengine 42 na kufeli mitihani yake anasema: “Wakati huo, hawakuwa na mwalimu yeyote wa sayansi … walikuja mwishoni karibu na mitihani. Eva amesubiria zaidi ya miaka miwili kwa familia yake kukusanya pesa ili aweze kurudia elimu ya sekondari.[333]

Kukosekana kwa msaada kwa wanafunzi kuanza kutumia Kiingereza kama Lugha ya Kufundishia.

Wanafunzi wote wa shule za sekondari waliohojiwa na Human Rights Watch walifundishwa kwa Kiingereza, lugha ambayo ni mpya kwa walio wengi. Shule zinasisitiza matumizi ya Kiingereza kama lugha pekee ya kufundishia bila kutoa msaada wowote kwa wanafunzi ambao wanabadilika kutoka kutumia Kiswahili kwenda Kiingereza.

Caroline, 15, katika kijiji cha Igombe, anahangaika na mabadiliko ya kutumia Kiingereza kama lugha pekee ya kufundishia shuleni kwake:

Ilikua ngumu sana kwa sababu mar azote nilikuwa naongea Kiswahili na ilikuwa ngumu kubadilika. Ningependa serikali itumie lugha ya Kiingereza shule za msingi kuondoa ugumu tunaopata Kidato cha I.[334]

Kama wanafunzi wengi waliohojiwa na Human Rights Watch, Joseph, 14, waliona ugumu wa mabadiliko ya lugha katika shule za sekondari:

Kutoka shule ya msingi masomo yote ni kwa Kiswahili kisha sekondari, ilikua ngumu … Ingekuwa vizuri kama watu wangejifunza kwa Kiswahili kwa sababu sina hakika kama wanafunzi wanafeli kwa sababu hawajui lakini kwa sababu hawana misamiati ya kutosha kuelewa swali.[335]

Wanafunzi wengine wanasema walikuwa wakipewa adhabu wanapotumia Kiswahili. Katika kesi ya Jumla,

Niliongea Kiswahili kwa mwalimu wa Kiswahili. Kwa mujibu wa shule haturuhusiwi kuongea Kiswahili shuleni. Nilikutana na mwalimu wangu nje ya darasa nikaongea nae. Alinichapa kwenye makalio. Inatokea kila siku, sio kwangu kwa sababu sasa najaribu kuongea Kiingereza kila wakati kukwepa adhabu.[336]

Hata walimu wenyewe wakati mwingine hawajui Kiingereza fasaha. Kwa mujibu wa Prospro Lubuva, mkuu wa Mafunzo ya Elimu katika Chama cha Walimu Tanzania:

Tunahitaji mafunzo zaidi ya kiingereza kwa shule za sekondari, hata vyuo vikuu inahitajika. Wakati mwingine walimu hawajui lugha vizuri na wanafundisha katika lugha wasioijua vema … kuna haja kubwa kabisa ya walimu wa shule za sekondari kupatiwa mafunzo ya Kiingereza wakiwa kazini.[337]

Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), walimu 2,485 wa shule za sekondari wamepatiwa mafunzo kuwawezesha kufundisha Kiingereza, hii ikiwa ni asilimia 2.8 pekee ya walimu wa shule za sekondari za umma.[338]

Upungufu wa Vitabu vya Kiada na Vifaa Shule

Kuna upungufu mkubwa wa vitabu vya kiada na vifaa vya kujifunzia na kufundishia katika shule za sekondari Tanzania.[339] Katika kesi ya Esther, mwalimu wake wa kidato cha II katika shule iliyopo wilaya ya kijijini mkoani Shinyanga, ana vitabu lakini hana vitabu vya kiada: “Darasani kwangu hakuna mwenye kitabu. Niliona watu wenye vitabu nikiwa Kidato cha I pekee.”[340]

Walimu na wawakilishi kutoka chama cha Walimu Tanzania wanalalamika juu ya ukosefu wa vifaa vya kufundishia, vitabu vya kiada na teknolojia za msingi.[341] Katika shule ya sekondari Mwanza, Human Rights Watch waliambiwa: “Kuna upungufu wa vifaa vya kufundishia kama vile “overhead projector”, tarakilishi mpakato (laptop) … tunategemea makaratasi.”[342] Shule pia zina upungufu wa vifaa vya maabara kwa masomo ya sayansi.[343]

VIII. Ukosefu wa Njia Mbadala za Kupata Elimu kwa Watoto Wanaoacha Shule

Kama ningepata msaada ningefurahi kurudi shule-lakini hakuna wa kunisaidia.

Felicity, 18, aliacha shule Kidato cha I mwaka 2014, Igombe, Januari 23, 2016

Mfumo wa elimu unatoa njia mbadala chache za uhakika kwa wanafunzi wengi ambao waliacha shule kwa sababu ya ada, kufeli mtihani wa Darasa la Saba, au sababu nyinginezo.

Wanafunzi wanaotaka kumaliza elimu ya sekondari licha ya kuwa wamefeli mtihani wa darasa la saba, wasichana wanaofukuzwa shule kutokana na kupata mimba au wale wanaoacha shule ili wafanye kazi inabidi wajisomee wenyewe au kujiandikisha na kulipa ada ambayo inafikia karibu shilingi 500,000 za kitanzania (US$227) kwa mwaka ili wasome vyuo binafsi. Wanafunzi wanaopitia njia hii wanamaliza kozi ambayo inajumuisha mtaala mzima wa elimu ya sekondari ngazi ya chini katika kipindi cha miaka miwili.[344]

Kupata mafunzo mazuri ya ufundi stadi ni vigumu na gharama vile vile.[345] Vijana wanaoacha elimu ya sekondari mapema wanakosa vigezo na masomo yanayohitajika kusoma elimu ya ufundi stadi na ujuzi.

Badala yake, vijana walioacha shule wanaweza kujiunga kwa kozi fupi za ufundi stadi na kupata cheti cha msingi cha ujuzi. Wakati vituo vya elimu ya watu wazima vinatoa elimu ya msingi na ujuzi wa kiufundi kwa wanafunzi kuwawezesha kujiajiri na kujitegemea, bado sio sawa na shahada ya ufundi na mafunzo ambayo inatolewa katika vituo vilivyothibitishwa vya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).[346] Lakini pia kujiunga na elimu ya watu wazima sio jambo la moja kwa moja kwa walio wengi. Wanafunzi lazima wajue Kiingereza na lazima walipe ada kiasi cha shilingi 60,000 za kitanzania ($27) kwa vyuo rasmi vya serikali ambayo bado kuna gharama nyingine za ziada au kulipa ada kiasi cha shilingi 600,000 za kitanzania ($273) kwa vyuo visivyokuwa vya serikali.[347]

Vijana wengine waliohojiwa na Human Rights Watch waliweza kujiunga na program za mafunzo na ufundi stadi kupitia asasi zisizokuwa za kiserikali ambazo zinatoa udhamini na kusaidia wanafunzi na vikwazo vya kiutawala. Human Rights Watch ilifanya mahojiano na vijana 11 ambao walikua katika ajira za utotoni na sasa wamejiunga na vyuo vya elimu ya watu wazima kupitia Rafiki SDO, asasi isiyokuwa ya kiserikali mkoani Tabora.[348]

Hali hii ni tofauti kabisa na madai ya serikali kwamba “wale wanaofeli wanajiunga na shule za mafunzo na ufundi stadi.”[349] Kwa mujibu wa Venance Manori, afisa mwandamizi katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST) kitengo cha elimu ya sekondari, “Ni sera ya nchi-kila wilaya iwe na angalau shule moja ya mafunzo na ufundi stadi.”[350]

Vijana wengi hawana taarifa ya namna ya kufikia elimu ya mafunzo na ufundi stadi. Aprili, ambae ana miaka 21, aliacha shule akiwa na miaka 15 kwa sababu baba yake “anaamini katika kusomesha watoto wa kiume kuliko wa kike” na kuanzisha biashara ya kuuza bidhaa ndogo ndogo lakini hana taarifa ya namna ya kujiendeleza kielimu:

Sijui nitaanzia wapi-kama ni Kidato cha I na Kidato cha II … hakuna mtu katika familia yangu anaweza kunipatia taarifa ninazohitaji,” anasema. “Hata kama sitaanza Kidato cha I … ningependa shule yoyote ambayo nitapata ujuzi.[351]

Shule nyingi za mafunzo na ufundi stadi pia hazijumuishi wanafunzi wenye ulemamvu, kwa mujibu wa Alfred Kapole, mwakilishi wa Shivyawata Mwanza.[352] Kwa mujibu wa Mr. Adamson Shimbatano kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, idara ya Mahitaji Maalumu ya Elimu, kuna vyuo viwili pekee vya serikali ambavyo vinaweza kuhudumia watu wenye ulemavu, Temeke, wilaya ya Dar es Salaam na Mtwara, mji mashuhuri wa kanda ya kusinimashariki mwa Tanzania.[353]

Mapendekezo

Kuhakikisha Upatikanaji wa Elimu ya Sekondari Bure kwa Vijana Wote

Serikali ya Tanzania

  • Kuendelea kuongeza bajeti kuhakikisha shule zinapata fedha za kutosha kutoka serikalini wa ajili ya mahitaji yote ya elimu, ikiwa ni pamoja na ujenzi au ukarabati wa majengo, nyumba za walimu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia.
  • Kuendelea kuongeza bajeti kwa shule za sekondari ili kuhakikisha shule zinaweza kuziba mapengo ya kifedha yaliyokuwa yanagharamiwa kupitia michango ya wazazi na kufikia kiwango cha chini cha kutoa fedha kwa shule zote za sekondari.
  • Kuhakikisha vyuo vya elimu ya watu wazima navyo vinaondolewa ada na michango
  • Kuunda program za bure kwa vijana walioacha shule ili waweze kumaliza elimu ya sekondari ngazi ya chini na kuweza kujiunga na program rasmi za mafunzo na ufundi stadi.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kuhakikisha shule zote zinatekeleza Waraka wa Elimu Na. 5 wa mwaka 2015, sera ya serikali kufuta ada na michango na kufuatilia uzingatiaji.
  • Kuweka utaratibu imara wa kuripoti kuhakikisha shule zote za sekondari wakati wote zinafuatilia wanafunzi walio nje ya shule kwa muda au kuacha shule kabisa na kutoa ripoti ya sababu za utoro.
  • Kutekeleza mpango wa kutoa chakula shuleni kwa shule zenye idadi kubwa ya uandikishaji wa wanafunzi kutoka kaya zenye kipato cha chini.

Kufuta kwa Awamu Matumizi ya Mitihani kama Kigezo cha Kuchagua Wanafunzi kwa Elimu ya Sekondari

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kuchanganua njia zote zinazowezekana kuharakisha mipango ya kuondoa matumizi ya Mtihani wa Kumaliza Darasa la Saba kuzuia wanafunzi ambao hawafaulu mtihani kuendelea na elimu ya sekondari kabla ya kikomo cha 2021.
  • Kubadili sera iliyopo mara moja ili kuhakikisha wanafunzi ambao hawafaulu mtihani wa darasa la saba wanaweza kurudia Darasa la 7 na kupata ujuzi na maarifa ya msingi kabla ya kuendelea Kidato cha I.

Kuongeza Upatikanaji wa Shule za Sekondari

Serikali ya Tanzania

Kwa kadiri iwezekanavyo kutokana na upatikanaji wa rasilimali:

  • Kuharakisha maendeleo kufikia malengo ya msingi ya Programu ya II ya Maendeleo ya Elimu, ikiwa ni pamoja na kujenga shule mpya za sekondari na kuhakikisha shule zote za sekondari zina vyumba vya kusomea na vifaa vya usafi vya kutosha. Kuchukua hatua kuhakikisha maeneo yote ya majengo mapya ikiwa ni pamoja na vyoo yanafikika na wanafunzi na walimu wenye ulemavu.
  • Kuharakisha ujenzi wa mabweni salama kwa wanafunzi wa kike.  

Kuhakikisha Usafiri Salama na Nafuu

Waziri wa Ujenzi, Usafiri na Mawasiliano

  • Kuandaa mpango mzuri wa usafiri kwa wanafunzi wanaosafiri zaidi ya saa moja kufika shule, kwa kushauriana na maafisa wa shule, wanafunzi, jamii na maafisa husika wa serikali za mitaa. 
  • Kuanzisha mafunzo ya lazima na programu za kuelimisha juu ya ulinzi dhidi ya unyonyaji wa kingono na unyanyasaji kwa madereva wa mabasi au pikipiki kudumisha leseni za kuendesha. Kushirikiana na vikundi vya kijamii, asasi zisizokuwa za kiserikali, wanafunzi na maofisa wa wilaya katika kutengeneza program hizi.
  • Kwa kadiri iwezekanavyo kutokana na upatikanaji wa rasilimali:
    • Kuanzisha mpango wa ruzuku ya usafiri kwa kutoa ruzuku kamili au kiasi kwa wanafunzi wanaoishi maeneo ya mijini na kuhakikisha madereva wa basi wanafidiwa au kupewa motisha kwa kubeba abiria wanafunzi.
    • Hatua kwa hatua kuanzisha mpango wa ruzuku ya usafiri kwa walimu, kama mpango wa pamoja wa mamlaka ya serikali za mtaa na chama cha wamiliki wa mabasi Dar es Salaam, katika miji na majiji mengine Tanzania bara.

Kuondoa Adhabu za Viboko na Unyanyasaji wa kijinsia katika Shule

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kuondoa adhabu za viboko katika sera na mienendo ikiwa ni pamoja na kubadilisha Kanuni za Adhabu za Elimu Kitaifa (1979) na kupitisha sera na kanuni ambazo zinazingatia wajibu wa Tanzania kimataifa na kikanda juu ya haki za binadamu.
  • Kutoa ujumbe wenye nguvu kwa umma juu ya kupiga marufuku adhabu za viboko.
  • Kuchukua hatua kusaidia kuhakikisha kesi za unyanyasaji wa kijinsia zinaripotiwa kwa mamlaka zinazohusika kusimamia ikiwa ni pamoja na polisi na kwamba kesi zinachunguzwa na hukumu kutolewa.
  • Kuhakikisha shule zote zina sera za kutosha za ulinzi wa mtoto ikiwa ni pamoja na itifaki na kanuni za shule kwa walimu na wanafunzi.
  • Kuhakikisha shule zote zina utaratibu uliojitosheleza wa ulinzi kama vile itifaki za ulinzi na kanuni za maadili kwa walimu na wanafunzi. Kuhakikisha wanafunzi wanaweza kutoa taarifa bila kujulikana, juu ya adhabu za viboko, unyanyasaji wa kijinsia, udhalilishaji au aina yoyote ya vitisho vinavyofanywa na mwanafunzi na mwalimu; na mwalimu mkuu au afisa mwandamizi wa shule anaripoti kesi yoyote kwa uongozi wa mtaa pamoja na polisi.
  • Kutoa mafunzo ya ulinzi wa mtoto kwa walimu wakuu na maafisa waandamizi wa shule.
  • Kuruhusu klabu za wanafunzi au vijana za shule za sekondari kupendekeza utaratibu mzuri wa kushughulikia masuala ya ulinzi wa mtoto shuleni.
  • Kupitisha kanuni za maadili kitaifa kwa walimu na maafisa wa shule.
  • Kuongeza mafunzo ya lazima ya aina mbadala wa kuongoza darasa na nidhamu ya mwalimu katika mafunzo yote ya walimu. Kuhakikisha walimu wanapata mafunzo ya kutosha ya aina mbadala wa kusimamia darasa na kuhakikisha walimu wanapewa vifaa vya kutosha kuongoza darasa kubwa.

Kuondoa Vikwazo vya Kibaguzi na Unyanyasaji wa Kijinsia dhidi ya Wasichana katika Shule

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kuacha kufukuza shule wasichana wenye mimba na walioolewa na kurekebisha Kanuni Na. 4 ya Kanuni za Elimu (Kufukuzwa na Kutengwa kwa wanafunzi wa Shule) ya 2002 kwa kuondoa “makosa dhidi ya maadili” na “ndoa” kama sababu za kufukuzwa shule.
  • Kuondoa mara moja upimaji wa mimba shuleni na kutoa Waraka wa Serikali kuhakikisha kwamba walimu na maafisa wa uongozi wa shule wanafahamu kwamba kitendo hicho kimepigwa marufuku.
  • Kuongeza elimu ya afya ya uzazi na kujamiiana kama somo linalojitegemea katika mtaala wa shule za sekondari na kutoa mafunzo ya kutosha kwa walimu kufundisha bila upendeleo na kuhakikisha wanafunzi wanapata taarifa bila upendeleo shuleni. Kuhakikisha pia kuwa elimu na taarifa za afya ya uzazi na kujamiiana zinapatikana kwa wanafunzi wenye ulemavu katika mifumo ambayo itakua rahisi kwao kuelewa na kujifunza.
  • Kuharakisha kanuni ambazo zinamruhusu msichana mwenye mimba na wamama vijana walio katika umri wa kwenda shule wanarudi shule za sekondari sambamba na Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014. Kuhakikisha kwamba wanafunzi wenye mimba na walioolewa ambao wanataka kuendelea na shule wanaweza kufanya hivyo katika mazingira ambayo hayana ubaguzi na unyanyapaaji kwa kuruhusu wanafunzi wa kike kuchagua shule mbadala na kufuatilia utekelezaji wake.
  • Kuongeza machaguo kwa huduma za mtoto na vituo vya maendeleo ya watoto wadogo kwa watoto waliozaliwa kutokana na mimba za utotoni ili kuruhusu kina mama kurudi shule kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
  • Kuongeza upatikanaji wa fursa za mafunzo na ufundi stadi kwa wanawake walioolewa na wasichana katika wilaya zote na kujulisha umma kuhusu uwepo wa programu hizo.
  • Kwa kushirikiana na wizara husika kuandaa mada na vifaa vya kufundishia kwa walimu kujifunza namna ya kufundisha masuala ya hedhi darasani katika namna ambayo inaheshimu faragha ya msichana na maendeleo yake.
  • Kuwalazimu maafisa wa shule kuripoti kesi za wanafunzi ambao wako katika hatari ya kuolewa kwa mamlaka husika zinazosimamia.
  • Kuendeleza mafunzo ya ulinzi wa mtoto kwa walezi wa shule, hususani juu ya namna ya kuripoti unyanyasaji wa kijinsia na udhalilishaji shuleni na muongozo sahihi na msaada kwa wanafunzi waliothirika na vitendo hivi.
  • Kupitisha miongozo ya kina ya kuripoti, uchunguzi na kutoa adhabu kwa unyanyasaji wa kijinsia shuleni. Kuzitaka shule zote kuweka takwimu ya ripoti za matukio ya unyanyasaji wa kijinsia na ukatili. Takwimu hizi ni lazima ziwe zinakusanywa kitaifa na kuchapishwa kila mwaka.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

  • Kupanua wigo wa upatikanaji na kuhakikisha ubora wa taarifa za afya ya uzazi ambazo ni rafiki kwa vijana na zinapatikana katika mifumo ambayo itaruhusu watu wenye ulemavu kuweza kuzisoma na upatikanaji wa huduma katika wilaya zote.
  • Kuzuia watoa huduma za afya kushiriki katika upimaji mimba wa lazima kwa wasichana katika shule au katika mazingira mengine.
  • Kusaidia juhudi za kuondoa upimaji mimba wa lazima kwa wasichana wa shule na kufukuzwa kwao shule.
  • Kuimarisha uwezo wa jamii na watendaji wa serikali za mitaa kulinda watoto walio katika mazingira magumu ikiwa ni pamoja na watoto walio katika hatari ya ndoa za utotoni na ajira za utotoni na kuhakikisha wanapata huduma ya ulinzi wa mtoto.

Kuhakikisha Elimu Jumuishi kwa Watoto wote wenye Ulemavu

Serikali ya Tanzania

  • Kuhakikisha bajeti ya mwaka inaakisi dhamira ya serikali ya elimu jumuishi.
  • Kuhakikisha shule za sekondari zenye idadi kubwa ya wanafunzi wenye ulemavu zinapata bajeti ya ziada kununua vifaa vinavyohitajika kuhakikisha elimu inapatikana kwa wanafunzi hawa katika misingi ya usawa na wengine.
  • Kuhakikisha majengo mapya yanajengwa kwa kuzingatia hatua za ubunifu zinazowezesha walimu na wanafunzi wenye ulemavu kuyatumia bila shida.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kukabiliana na vikwazo vya kijamii na kifedha vinavyoathiri unadikishwaji wa watoto wenye ulemavu katika elimu ya awali na ya msingi.
  • Kuchukua hatua kuhakikisha shule za sekondari zilizo na wanafunzi wenye ulemavu zina idadi inayokubalika ya vitabu, vifaa vya kufundishia na vifaa ambavyo vinatumika na wanafunzi na walimu wenye ulemavu.
  • Kuchukua hatua kuhakikisha walimu wengi zaidi wana mafunzo ya kutosha ya elimu jumuishi. Kutoa mafunzo ya ushauri kwa walimu kuwawezesha kuwasaidia watoto wenye ulemavu mbalimbali na familia zao.
  • Kuchukua hatua kuongeza idadi ya walimu wenye ujuzi wa lugha ya ishara.
  • Kuhakikisha wanafunzi wenye ulemavu wanapata vifaa vya usaidizi kwa ruzuku au bure ikiwa ni pamoja na baiskeli ya kutembelea, fimbo au miwani zinazohitajika kuwezesha mizunguko yao na ushiriki na ushirikishwaji kamili shuleni.
  • Kukusanya takwimu za uandikishwaji, kuacha shule na viwango vya ufaulu kwa wanafunzi wenye ulemavu na kugawa takwimu kwa aina ya ulemavu na jinsia.

Kuimarisha Ubora wa Elimu katika Shule zote za Sekondari

Kwa kadiri iwezekanavyo kutokana na upatikanaji wa rasilimali:

Serikali ya Tanzania

  • Kuongeza fedha za ruzuku ili kuwezesha utoaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia na vifaa muhimu katika shule zote za sekondari.
  • Kuhakikisha walimu wanafidiwa vya kutosha kulingana na majukumu yao na kutoa motisha ya fedha kwa walimu wanaopangiwa maeneo ya vijijini au maeneo ambayo yako nyuma kwa maendeleo nchini. Kutoa nyumba za kutosha za walimu.
  • Kutekeleza mkakati wa serikali wa kuounguza umasikini, MKUKUTA II, ukilenga kuhakikisha shule zinapata vifaa vya usafi vya kutosha na hususani vifaa salama vya usafi na usimamizi wa usafi wa hedhi.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

  • Kuweka kipaumbele katika kupanga walimu wa masomo yote katika shule zilizo vijijini na kuchukua hatua za haraka kuhakikisha shule zote zinaweza kufundisha Kiingereza, masomo ya sayansi na hisabati mbali na masomo mengine ya msingi.
  • Kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi wanafundishwa vema na wanajifunza lugha ya kufundishia ambayo watakutana nayo wakifika shule za sekondari; iwapo hii haitowezekana basi kuhakikisha shule za sekondari zinatoa msaada wa ziada kwa wanafunzi ambao ujuzi wao wa lugha ya Kiingereza ni wa chini. 
  • Shule za sekondari zinachagua kufundisha kwa Kiingereza zichukue hatua za haraka kuhakikisha walimu wote wana vigezo vinavyokubalika vya uelewa wa Kiingereza na wana sifa za kufundisha kwa Kiingereza.
  • Kuhakikisha walimu wanapata mafunzo ya mara kwa mara wakiwa kazini na kuwapatia fursa rasmi za kuongeza au kupata ujuzi wa somo fulani.

Kusaidia Serikali ya Tanzania katika Jitihada zake za Kutambua Haki ya Elimu ya Sekondari

Kwa Wafadhili wa Kimataifa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa

  • Kusaidia juhudi za serikali kutoa elimu ya sekondari bure na jumuishi kwa wote. 
  • Kusaidia kipaumbele cha serikali cha usafi na usimamizi wa usafi wa hedhi.
  • Kusaidia mpango wa serikali wa kutoa takwimu kuhakikisha uwazi na uwajibikaji katika takwimu za uandikishwaji wa elimu ya sekondari kitaifa, matokeo na viashiria vya ubora.
  • Kufikiria kuchukua hatua kusaidia mipango iliyowekwa kuongeza upatikanaji wa elimu kwa wasichana ikiwa ni pamoja na hatua za kifedha kuongeza upatikanaji wa mabweni salama kwa wanafunzi wa kike na kutoa ruzuku ya usafiri kwa wanafunzi wa kike wanaosafiri umbali mrefu.
  • Kusaidia wigo mpana wa utoaji wa elimu jumuishi. Kufikiria kutoa fedha kwa mipango ya serikali, mashirika wa watu walemavu na asasi zisizokuwa za kiserikali kusaidia watoto wenye ulemavu kupata haki yao ya elimu jumuishi. 

Kuomba Serikali Kufuta Sheria na Sera ambazo Zinakiuka Haki ya Elimu ya Sekondari na Haki nyingine za Mtoto

Kwa Wafadhili wa Kimataifa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa

  • Kuiomba serikali kufuta kanuni ya adhabu za viboko na kuondoa mwenendo huu katika shule na kutoa fedha kusaidia mafunzo ya aina mbadala ya kuongoza darasa kwa walimu wote na maafisa wa shule.
  • Kuiomba serikali kusitisha ufukuzaji wa wanafunzi wa kike wanaopata mimba na kuharakisha upitishaji wa sera imara zinazoruhusu kujiunga upya kwa wazazi walio katika umri wa kwenda shule.
  • Kuiomba na kuisadia serikali ya Tanzania kutambulisha elimu ya afya ya uzazi na kujamiiana katika mitaala ya elimu ya shule za msingi na sekondari kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu; kutekeleza mtaala huu kama somo linalojitegemea na kuwa na mtihani.

Kuiomba Serikali ya Tanzania Kuzingatia Wajibu wake wa kimataifa na Kikanda

Umoja wa Afrika

  • Kuitaka Tanzania:
    • Kuondoa matumizi na kupuuzia adhabu za viboko mashuleni ikiwa ni pamoja na kuchukua mifano ya kupiga marufuku na hatua zilizochukuliwa na mataifa mengine ya Afrika.
    • Kumaliza ubaguzi kwa wanafunzi wenye mimba, walioolewa na ambao ni wazazi wakiwa shule na kuhimiza serikali kuhakikisha wasichana wote na wanawake vijana wanaweza kwenda shule.

Shukrani

Ripoti hii imefanyiwa utafiti na kuandikwa na Elin Martínez, mtafiti wa Human Rights Watch katika idara ya haki za watoto;na utafiti wa ziada uliofanywa na Zama Coursen-Neff, mkurugenzi mtendaji wa haki za watoto. Sarah Crowe, Esther Phillips, Sahar McTough, Langley King na Elena Bagnera walisaidia katika utafiti.

Ripoti imehaririwa na Juliane Kippenberg, mkurugenzi msaidizi wa haki za watoto. Chris Albin-Lackey, mshauri mwandamizi wa sheria na Babatunde Olugboji, naibu mkurugenzi wa programu walitoa ushauri wao wa kisheria katika programu. Agnes Odhiambo na Amanda Klasing, watafiti waandamizi wa haki za wanawak; Leslie Lefkow, naibu mkurugenzi Afrika; na Kriti Sharma, mtafiti wa haki za walemavu, walitoa ushauri wao wa kitaalamu. Shughuli za uzalishaji zilifanywa na Helen Griffiths, mratibu wa haki za watoto; Grace Choi, mkurugenzi wa machapisho; Olivia Hunter, mshirika wa picha na machapisho; na Fitzroy Hepkins, meneja utawala.  

Human Rights Watch inapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa watoto wote, vijana, wazazi, walimu, walimu wakuu, maafisa wa elimu, watetezi wa elimu na wataalamu ambao walitoa uzoefu wao na michango ya kitaalamu. Shukrani za kipekee zienda kwa Angel Benedict, mkurugenzi mtendaji wa Wotesawa, Gerald Ng’ong’a na Naomi Goodwin wa Rafiki SDO na John Mayola na timu ya mpango wa kudhibiti UKIMWI wa Agape.

Tunapenda kuyashukuru mashirika yote, wataalamu, na wanaharakati ambao wametusaidia katika kufanya utafiti wa ripoti hii na kushiriki kwa kutoa takwimu na taarifa nyingine. Watafiti hawa na wataalamu ni pamoja na: Alfred Kiwuyo, Lightness Kweka, na waliojitolea kutoka Tanzania Youth Vision Association; Eric Guga na Jones John wa Tanzania Child Rights Forum; Boniventura Godfrey na John Kalage wa Haki Elimu; Richard Temu wa Uwezo Tanzania; Richard Mabala wa Tamasha; Ayoub Kafyulilo na Pedro Guerra wa UNICEF Tanzania; Professor Mkhumbo Kitila wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; Ezekiah Oluoch na Gratian Mkoba wa Chama cha Walimu Tanzania; Margaret Mliwa, Philippo Paul na waliojitolea kutoka Restless Development Tanzania; Rebeca Gyumi wa Msichana Initiative; Cathleen Sekwao na Nicodemus Eatlawe wa TEN/MET; Jennifer Kotta na Faith Shayo wa UNESCO Tanzania; Charlotte Goemans wa Shirika la Kazi Duniani (ILO); Fredrick Msigallah na Gisela Berger wa CCBRT; Anke Groot wa Terre des Hommes Netherlands; Petrider Paul wa Youth for Change Tanzania; Koshuma Mtengeti wa Children’s Dignity Forum Tanzania; Theresia Moyo wa CAMFED Tanzania; Gwynneth Wong, Jane Mrema, na Emmanuel Mang’ana wa Plan International Tanzania; Barbara Ammirati wa the Global Partnership to End Violence Against Children; Nafisa Baboo wa Light for the World International; Given Edward wa MyElimu; na Felician Mkude na Alfred Kapole wa Shivyawata.

Pia tunapenda kuwashukuru wawakilishi wa Global Partnership for Education, Shirika la Swiss la Maendeleo na Ushirikiano, Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID), Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani na Benki ya Dunia, ambao waliongea nasi. 

Human Rights Watch pia inatambua ushirikiano wa maafisa wa serikali katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

 

[1] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar. Ina Mikoa 30 ya kiutawala. Mikoa ina ngazi mbalimbali za utawala kuanzia wilaya, kata, tarafa na vijiji. Ripoti hii imejikita katika sheria, kanuni, sera na mienendo ya Tanzania Bara. Katika ripoti hii neno Tanzania linamaanisha Tanzania Bara.

[2] Ujana ni kipindi katika ukuaji wa binadamu ambapo ni baada ya utoto na kabla ya utu-uzima. Shirika la Afya Duniani, “Maternal, newborn, child and adolescent health: Adolescent development,” http://www.who.int/maternal_child_adolescent/topics/adolescence/dev/en/ (imepitiwa Septemba 27, 2016).

[3] Kabla ya mwaka 2016, Wizara hizi zilikua zinatambulika kama; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto; na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

[4] Yusuf Kassam, United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO), International Bureau of Education, “Julius Kambarage Nyerere (1922 -),” Prospects: the quarterly review of comparative education, vol. XXIV, no. 1/2, (1994), pp. 247–259, http://www.ibe.unesco.org/sites/default/files/nyereree.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[5] Margaret Simwanza Sitta, then-minister for community development, gender and children of the United Republic of Tanzania, “Towards Universal Primary Education: The Experience of Tanzania,” UN Chronicle, vol. XLIV No. 4, (December 2007), https://unchronicle.un.org/article/towards-universal-primary-education-experience-tanzania (imepitiwa Septemba 22, 2016); United Republic of Tanzania, Ministry of Education and Vocational Training, “Education for All (EFA) Report for Tanzania Mainland,” November 2014, http://unesdoc.unesco.org/images/0023/002314/231484e.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[6] United Republic of Tanzania, National Bureau of Statistics, “2015: Tanzania in Figures,” June 2016, http://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/references/Tanzania_in_Figures_2015.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), pp. 20 – 21.

[7] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Uandikishwaji Shule za Msingi kwa Jinsia na Umri 2016,” Julai 30, 2016, http://opendata.go.tz/dataset/uandikishaji-katika-shule-za-msingi-kwa-jinsi-na-umri-2016 (imepitiwa Septemba 22, 2016), “Uandikishwaji Shule za Sekondari kwa Jinsia na Umri 2016,” Julai 30, 2016, http://opendata.go.tz/dataset/uandikishaji-katika-shule-za-sekondari-kwa-jinsi-na-umri-2016 (imepitiwa Septemba 22, 2016); UNESCO na Timu ya Kitaifa ya Tanzania, “Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya ELimu 2016/17 – 2020/21 Tanzania Bara, Pendekezo la Kiufundi (Rasimu ya Mwisho, Januari 2017),” June 2016, nakala iko kwenye faili na Human Rights Watch.

[8] Ibid.

[9] Ibid.

[10] Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), “Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu, viashiria vya Elimu,” Novemba 15, 2013, http://hdr.undp.org/en/content/education-index (imepitiwa Agosti 26, 2016); Angalia Kipengele cha VII: ‘Ukosefu wa Elimu Bora kwa Shule za Sekondari.”

[11] UNICEF, “Ufafanuzi wa Bajeti ya Elimu FY 2011/12 – FY 2015/16,” Novemba 24, 2016, https://www.unicef.org/tanzania/UNICEF-TZ-BB-Education-WEB(1).PDF (imepitiwa Desemba 12, 2016).

[12] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (MB), kutambulisha kwa Bunge, makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17,” Juni 8, 2016, http://www.mof.go.tz/mofdocs/msemaji/BUDGET%20SPEECH%20FINAL%202016.pdf (imepitiwa Oktoba 31, 2015), para. 55.

[13] Ibid.

[14] UNICEF, “Ufafanuzi wa Bajeti ya Elimu FY2011/12 – FY2015/16;” UNESCO, “Education: Funding,” isiyo na tarehe, http://www.unesco.org/new/en/education/themes/leading-the-international-agenda/education-for-all/funding/ (imepitiwa Oktoba 31, 2015).

[15] Policy Forum, “The Paradox of Financing Education in Tanzania, ’The 2014/15 Post Budget Brief,’” Policy Brief 03, (2014), http://www.policyforum-tz.org/sites/default/files/BriefEducation.pdf (imepitiwa Desemba 4, 2016).

[16] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (MB), kutambulisha kwa Bunge, makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17,” para. 55.

[17]“Waraka wa elimu bure watolewa,” Daily News, December 14, 2015, http://dailynews.co.tz/index.php/home-news/45072-free-education-circular-issued (imepitiwa Mei 3, 2016); Arthur Chatora, “Tanzania allocates US $62 million towards free education Magufuli says,” This is Africa, February 15, 2016, http://thisisafrica.me/tanzania-allocates-us-62-million-towards-free-education-magufuli-says/ (imepitiwa Mei 3, 2016). Agosti 2016, serikali ilitangaza kuongezeka kwa fedha za serikali kwa ajili ya “elimu bure”, zaidi ya shilingi za Kitanzania billion 2 ([US$909 milioni) kwa mwezi. Pius Rugonzibwa, “Tanzania: More ‘Boom’ for Free Education, Tanzania Daily News, August 19, 2016, http://allafrica.com/stories/201608190137.html (imepitiwa Septemba 20, 2016).

[18] UNICEF, “Ufafanuzi wa Bajeti ya Elimu FY 2011/12 – FY 2015/16.”

[19] Policy Forum, “Position Statement: Budget 2016/2017,” April 19, 2016, http://www.policyforum-tz.org/position-statement-budget-20162017 (imepitiwa Septemba 3, 2016).

[20] Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, http://www.agctz.go.tz/index.php/download-documents/constitutions#, art. 11 (3). Rasimu ya Katiba ambayo itajumuisha haki ya elimu ya msingi, elimu ya sekondari na mafunzo na ufundi stadi imekua ikijadiliwa tangu 2014. Kura ya maoni iliyokuwa imepangwa kupigwa mwezi Aprili 2015 iliahirishwa kwa muda usiojulikana. Adjoa Anyimadu (Chatham House), “Research Paper: Politics and Development in Tanzania: Shifting the Status Quo,” March 2016, https://www.chathamhouse.org/sites/files/chathamhouse/publications/research/2016-03-18-politics-development-tanzania-anyimadu_1.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016), pp. 3–6; Voice of America (Reuters), “Tanzania Delays Referendum on Constitution,” April 2, 2015, http://www.voanews.com/a/tanzania-delays-constitution-referendum/2705034.html (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[21] Sheria ya Elimu (Marekebisho), Bunge, Na. 10 ya 1995, http://www.unesco.org/education/edurights/media/docs/29595900c1028686edf504060e6a17df3eaeea8d.pdf, s. 25(1).

[22] Shule za Msingi (Ulazima wa kujiandikisha na Kuhudhuria) Rules, G.N. No. 280 of 2002, s. 4 (1)-(2).

[23] Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsi na Watoto, Na. 21 ya 2009, http://www.mcdgc.go.tz/data/Law_of_the_Child_Act_2009.pdf, arts. 9(1), 87.

[24] Sera pia inajumuisha uzinduzi wa hatua kwa hatua wa mwaka mmoja wa kuhudhuria shule ya awali. Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Wizara Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi (United Republic of Tanzania, Ministry of Education and Vocational Training), “Sera Ya Elimu Na Mafunzo (Education and Training Policy), 2014 http://www.tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/SERA_ya_Elimu_2_sw.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), pp. 23–24. Translated by Human Rights Watch.

[25] Sera ya 2014 pia inatambulisha lugha ya ishara kama lugha inayofundishwa shuleni. Ibid., pp. 36–38.

[26] Kuna shule 1,078 zaidi za msingi ambazo ni binafsi, na shule binafsi za sekondari 1,172. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tovuti ya Takwimu za Serikali kwa Umma, “Orodha ya Shule za Msingi zilizosajiliwa 2016,” Julai 2016, http://opendata.go.tz/dataset/orodha-ya-shule-za-msingi-zilizosajiliwa-2016, na “Orodha ya Shule za Sekondari zilizosajiliwa 2016,” Julai 2016, http://opendata.go.tz/dataset/orodha-ya-shule-za-sekondari-2016 (aimepitiwa Septemba 22, 2016).

[27] Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Vituo vya mafunzo vya VETA,” http://www.veta.go.tz/index.php/en/training (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[28] Hii ni pamoja na “Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025,” http://www.unesco.org/education/edurights/media/docs/061eb2eed52b8f11b09b25a8845436f19d5ae0ad.pdf; Sera ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo 1996, 1996, http://planipolis.iiep.unesco.org/upload/Tanzania%20UR/Tanzania_technical_education_policy_1996.pdf; “Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu 2008-2017,” Agosti 2008, http://www.globalpartnership.org/content/tanzania-education-sector-development-programme-2008-17; “Mkakati wa Taifa wa Kukuza na Kuondoa Umaskini (MKUKUTA),” Juni 2005, http://www.povertymonitoring.go.tz/Mkukuta/MKUKUTA_MAIN_ENGLISH.pdf; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari I (2004 – 2009),” April 2004, http://www.tamisemi.go.tz/menu_data/Programmes/SEDP/SEDP.pdf, and “II” (July 2010 – June 2015), June 2010, http://planipolis.iiep.unesco.org/upload/Tanzania%20UR/Tanzania_SEDP_2010_2015.pdf, (imepitiwa Januari 16, 2017).

[29] Mwemezi Makumba (Haki Elimu), “Je tunawekeza kwa ufanisi kwenye elimu? Ufuatiliaji wa mwenendo wa utoaji fedha kwa Sekta ya Elimu ‘A 2014/2015 post budget analysis Report,’” August 2014, http://hakielimu.org/files/publications/The%202014%20POST%20BUDGET%20Analysis.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), p. 2.

[30] Ibid., p. 2; UNICEF, “Ufafanuzi wa Bajeti ya Elimu FY 2011/12 – FY 2015/16.”

[31] UNESCO et al, “Education 2030, Incheon Declaration and Framework for Action – Towards inclusive and equitable quality education and lifelong learning for all,” ED-2016/WS/2, May 2015, http://www.uis.unesco.org/Education/Documents/incheon-framework-for-action-en.pdf (imepitiwa Agosti 30, 2016).

[32] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (2008–17), August 2008, http://www.globalpartnership.org/content/tanzania-education-sector-development-programme-2008-17 (imepitiwa Agosti 20, 2016); Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari II (July 2010 – June 2015), June 2010, http://planipolis.iiep.unesco.org/upload/Tanzania%20UR/Tanzania_SEDP_2010_2015.pdf (imepitiwa Agosti 20, 2016).

[33] Serikali ya Tanzania, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mpango Unaopendekezwa wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari II (SEDP II) 2010-2014,” March 2010, http://planipolis.iiep.unesco.org/upload/Tanzania%20UR/Tanzania_SEDP_II_Environmental_Social_Managt_Framework.pdf; “Environmental and Social Management Framework (ESMF),” March 2010, http://www.unesco.org/education/edurights/media/docs/3e1b3c4a9ac660e5c3528470d366bc316b1591c9.pdf (imepitiwa Agosti 20, 2016), p. 2.

[34] Haki Elimu, “Miaka Kumi ya Urais wa Jakaya Kikwete: Ahadi, Mafanikio na Changamoto katika Elimu,” Novemba 2015, http://hakielimu.org/files/publications/Ten%20Years%20of%20Jakaya%20Kikwetes%20Presidency-Final%20%20Report.pdf (imepitiwa Desemba, 2016).

[35] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, “Matokeo Makubwa Sasa – BRN,” isiyo na tarehe, http://www.pmoralg.go.tz/quick-menu/brn/ (imepitiwa Septemba 3, 2016).

[36] World Bank, “Namna Tanzania Ilivyojipanga Kufanikisha “Matokeo Makubwa Sasa” katika Elimu,” Julai 14, 2014, http://www.worldbank.org/en/news/feature/2014/07/10/how-tanzania-plans-to-achieve-big-reforms-now-in-education (imepitiwa Septemba 3, 2016).

[37] Ibid.

[38] UNICEF, “Ufafanuzi wa Bajeti ya Elimu FY 2011/12 – FY 2015/16;” Mahojiano ya Human Rights Watch na John Kalage na Boniventura Godfrey, meneja, Haki Elimu, Dar es Salaam, Januari 18, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Professor Kitila Mkumbo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dar es Salaam, Mei 25, 2016.

[39] Wizara ya ELimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Hotuba Ya Waziri Wa Elimu, Sayansi, Teknolojia Na Ufundi Mheshimiwa Prof. Joyce Lazaro Ndalichako (MB.) Akiwasilisha Bungeni Makadirio Ya Matumzi Ya Fedha Kwa Mwaka 2016/2017,” (Speech by the Minister of Education, Science, Technology and Vocational Training, Honorable Joyce Lazaro Ndalichako Introducing the National Assembly of Estimates Budget for The Year 2016/2017), Dodoma, May 2016, http://www.parliament.go.tz/uploads/budgetspeeches/1464680317-HOTUBA_WEST_2016_FINAL%20-%2023-05-2016.pdf (imepitiwa Desemba 6, 2016), paras. 50, 99.

[40] “Fedha za ruzuku za shule kulipwa katika akaunti za shule,” Daily News, December 31, 2015,  http://dailynews.co.tz/index.php/home-news/45594-capitation-grants-to-be-routed-via-school-accounts (imepitiwa Mei 30, 2016); Ben Taylor, “Free basic education, Education, Issue 113,” Tanzanian Affairs, January 1, 2016, https://www.tzaffairs.org/2016/01/education-11/comment-page-1/ (imepitiwa Januari 16, 2017); Twaweza East Africa, “A New Dawn? Citizens’ views on new developments in education,” Sauti za Wananchi, Brief No. 30, February 2016, http://www.twaweza.org/uploads/files/SzW-Education-Feb2016-EN-FINAL.pdf (imepitiwa Mai 30, 2016), p. 4; Jessica Mahoney, “Sending Money Directly to School Accounts in Tanzania: Using Experience to Inform Policy,” December 20, 2016, https://www.poverty-action.org/blog/sending-money-directly-school-accounts-tanzania-using-experience-inform-policy (imepitiwa Januari 9, 2017).

[41] Policy Forum, “Taarifa ya Msimamo: Bajeti 2016/2017,” http://www.policyforum-tz.org/position-statement-budget-20162017 (imepitiwa Desemba 4, 2016).

[42] Jamuhuri ya Muungano wa Tanznaia, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Waraka Wa Elimu Namba 11” (2004) (Education Circular Number 11), imenakiliwa kutoka “Waraka Wa Elimu Namba 3 Wa Mwaka 206 Kuhusu Utekelezaji Wa Elimu ya MSingi Bila Malipo,” (Education Circular No. 3 of 2016 on the implementation of abolition of school fee charges), May 2016, http://www.moe.go.tz/en/publications/send/44-circulars-nyaraka/270-waraka-namba-3-wa-mwaka-2016-elimu-bure (imepitiwa Septemba 22, 2016), p. 2.

[43] Ben Taylor, “Elimu ya msingi bure, Elimu, Toleo 113,” Tanzanian Affairs, January 1, 2016.

[44] Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Wizara Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi (United Republic of Tanzania, Ministry of Education and Vocational Training), “Sera Ya Elimu Na Mafunzo (Education and Training Policy), 2014 http://www.tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/SERA_ya_Elimu_2_sw.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), pp. 23–24. Imetafsriwa na Human Rights Watch.

[45]“Waraka wa Elimu bure umetolewa,” Daily News, December 15, 2015, http://dailynews.co.tz/index.php/home-news/45072-free-education-circular-issued(imepitiwa Septemba 3, 2016).

[46] Mahojiano ya Human Rights Watch na Ms. Paulina Mkonongo, mkurugenzi, elimu ya sekondari, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[47] Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, “Kubadilisha Dunia Yetu: Ajenda za 2030 kwa Maendeleo Endelevu,” (2015) A/RES/70/1, http://www.un.org/ga/search/view_doc.asp?symbol=A/RES/70/1&Lang=E (imepitiwa Desemba 9, 2015), Goal 4.1 and 4.4.a. Serikali lazima ihakikishe miaka 12 ya kutoa fedha za umma na ujumuishi na usawa katika elimu ya msingi na sekondari. UNESCO et al, “Education 2030, Incheon Declaration and Framework for Action – Towards inclusive and equitable quality education and lifelong learning for all,” ED-2016/WS/2, May 2015, http://www.uis.unesco.org/Education/Documents/incheon-framework-for-action-en.pdf (imepitiwa Agosti 30, 2016), p. 8, “Target 4.1,” and “Target 4.4.a,” p. 12.

[48] Ibid., Goal 4.3.

[49] UNESCO et al, “Education 2030, Incheon Declaration and Framework for Action – Towards inclusive and equitable quality education and lifelong learning for all,” Target 4.6,” p. 19.

[50] Human Rights Watch, Toxic Toil: Child Labor and Mercury Exposure in Tanzania’s Small-Scale Gold Mines, August 2013, https://www.hrw.org/report/2013/08/28/toxic-toil/child-labor-and-mercury-exposure-tanzanias-small-scale-gold-mines; No Way Out: Child Marriage and Human Rights Abuses in Tanzania, October 2014, https://www.hrw.org/report/2014/10/29/no-way-out/child-marriage-and-human-rights-abuses-tanzania#78bac8.

[51] Ushirikiano wa Dunia Kuondoa Ukatili Dhidi ya Watoto, “Utekelezaji katika Ngazi ya Nchi,” http://www.end-violence.org/countries.html (imepitiwa Desemba 5, 2016).

[52] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Mpango Kazi wa Taifa Kuondoa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto, 2017/18 – 2021/2022,” December 2016, http://www.mcdgc.go.tz/data/NPA_VAWC.pdf (imepitiwa Januari 9, 2016).

[53] Umasikini wa aina mbalimbali ni mchanganyiko wa viashiria vya uwezo wa kifedha, ustawi wa watoto, na kiwango cha maisha. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Taifa ya takwimu, na Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF), “Umasikini wa Mtoto Tanzania,” June 2016, http://www.nbs.go.tz/nbstz/index.php/english/statistics-by-subject/panel-survey-statistics/762-child-poverty-report-2016 (imepitiwa Januari 9, 2016), p. 2.

[54] Mahudhurio ya shule za msingi kati ya asilimia 20 wenye uwezo ilikua ni 93.4. Tangu 2012, mahudhurio yameshuka kiasi kikubwa. Wakati wa kuandika, takwimu zinazoonyesha utajiri hazikuwepo kwa elimu ya sekondari. UNICEF, “Takwimu: Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania,” takwimu za 2013, http://www.unicef.org/infobycountry/tanzania_statistics.html (imepitiwa Septemba 5, 2016).

[55] FHI360 and Education Policy and Data Center, “Watoto walio katika Mazingira magumu Tanzania: Kupata elimu na mwenendo wa kutohudhuria,” 2012, https://www.fhi360.org/sites/default/files/media/documents/Tanzania_Vulnerability.pdf, (imepitiwa Septemba 22, 2016); Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Taifa ya Takwimu, na UNICEF, “Umasikini wa Mtoto Tanzania,” p. 55.

[56] Idara ya Kazi Marekani, Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya Kazi, “Tanzania: 2015 Matokeo ya Aina mbaya za Ajira za Watoto,” 2015, https://www.dol.gov/agencies/ilab/resources/reports/child-labor/tanzania (imepitiwa Januari 9, 2016); Human Rights Watch, Toxic Toil.

[57] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Sheria ya Mtoto (Ajira kwa Mtoto) Kanuni,” G.N. No. 196 of 2012, http://www.ilo.org/dyn/natlex/docs/SERIAL/96139/113528/F1782966342/TZA96139.pdf.

[58] Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Ofisi ya Takwimu Tanzania, “Utafiti wa Ajira kwa Watoto Tanzania 2014, Analytical Report,” February 2016, http://www.ilo.org/wcmsp5/groups/public/---africa/---ro-addis_ababa/---ilo-dar_es_salaam/documents/publication/wcms_502726.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[59] UNICEF, “Statistics: United Republic of Tanzania,” data as of 2013, http://www.unicef.org/infobycountry/tanzania_statistics.html (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[60] Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), et al, “Ukweli kuhusu ndoa za utotoni (Child Marriage Fact Sheet),” August 2014, http://tanzania.unfpa.org/sites/default/files/resource-pdf/Child%20Marriagge%20fact%20sheet%20English%202014_0.pdf (imepitiwa January 16, 2017).

[61] Wasichana sio Wanaharusi, “Ndoa za Utotoni Duniani: Tanzania,” isiyo na tarehe, http://www.girlsnotbrides.org/child-marriage/tanzania/ (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[62] UNFPA et al, “Ukweli kuhusu ndoa za utotoni (Child Marriage Fact Sheet),” Agosti 2014.

[63] Ibid.

[64] FHI 360 and Education Policy and Data Center, “Watoto walio katika Mazingira Magumu Tanzania: Kupata elimu na mwenendo wa kutohudhuria,” p. 11.

[65] Serikali ya Jamhuri ya Tanzania, Kanuni za Elimu (Kufukuza na Kutenga wanafunzi shule), G.N. No. 295 of 2002, art. 4(c).

[66] Mapendekezo ya Tume yalipigwa chini na Waziri wa wakati huo wa Sheria na Katiba. USAID Health Policy Initiative, “Kutetea Mabadiliko ya Kisheria kwa Umri wa Ndoa Tanzania: Juhudi chni ya Sera ya Afya,” June 2013, http://www.healthpolicyinitiative.com/Publications/Documents/1534_1_Law_of_Marriage_Report.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016), p. 3.

[67] Wasichana sio Wanaharusi, “Mahakama Kuu ya Tanzania yatoa hukumu juu ya sheria ya umri wa ndoa kuwa ya kibaguzi na inakiuka Katiba,” Julai 13, 2016, http://www.girlsnotbrides.org/high-court-tanzania-child-marriage/ (imepitiwa Septemba 5, 2016); Sheria ya Mtoto 2009, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamiii, Jinsia, Wazee na Watoto, http://www.mcdgc.go.tz/data/Law_of_the_Child_Act_2009.pdf (imepitiwa Septemba 5, 2016), arts. 161–162.

[68] Rebeca Z. Gyumi v The Attorney General, Mahakama Kuu ya Tanzania, Miscellaneous Civil Cause No. 5 of 2016, Judgment, July 08, 2016, http://las.or.tz/wp-content/uploads/2016/07/REBECA-Z.-GYUMI-vs-A.G_Misc-Civil-Cause-No.5-of-2016.compressed.pdf (imepitiwa Septemba 5, 2016).

[69] Rosina John, “Serikali kukata rufaa dhidi ya hukumu ya umri wa chini wa ndoa,” The Citizen, August 3, 2016, http://www.thecitizen.co.tz/News/Govt-to-appeal-against-rulling-on-minimum-age-of-marriage/1840340-3328348-4kns7pz/index.html (imepitiwa Septemba 5, 2016).

[70] Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni (ICESCR), imepitishwa Desemba 16, 1966, G.A. Res. 2200A (XXI), 21 U.N. GAOR Supp. (No. 16) at 49, U.N. Doc. A/6316 (1966), 993 U.N.T.S. 3, utekelezaji ulianza Januari 3, 1976, acceded to by Tanzania on June 11, 1976, art. 13; Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC), imepitishwa Novemba 20, 1989, G.A. Res. 44/25, annex, 44 U.N. GAOR Supp. (No. 49) at 167, U.N. Doc. A/44/49 (1989), utekelezaji ulianza Septemba 2, 1990, ilipitishwa na Tanzania Juni 10, 1991, art. 28; Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto (ACRWC), OAU Doc. CAB/LEG/24.9/49 (1990), utekelezaji ulianza Novemba 29, 1999, ilipitishwa na Tanzania Machi 16, 2003, art. 11; Azimio la Vijana wa Afrika (AYC), (2006), ilianza kutumika Agosti 8, 2009, ilipitishwa na Tanzania Desemba 20, 2012, art. 13.

[71] Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla Na. 13, “Haki ya ELimu (Art. 13),” E/C.12/1999/10 (1999), http://www.ohchr.org/EN/Issues/Education/Training/Compilation/Pages/d)General Comment No13 The right to education (article13)(1999).aspx (imepitiwa Agosti 10, 2016), para. 6 (a)–(d).

[72] ICESCR, arts. 13 and 2; Angalia pia Baraza la Umoja wa Mataifa la Uchumu na Jamii, “Ripoti ya awali ya Mwandishi maalumu wa haki ya kupata elimu, Ms. Katarina Tomasevski, imewasilishwa kwa mujibu wa Tume ya azimio la Haki za Binadamu 1998/33,” E/CN.4/1999/49, January 13, 1999, https://documents-dds-ny.un.org/doc/UNDOC/GEN/G99/101/34/PDF/G9910134.pdf?OpenElement (imepitiwa Mei 11, 2016).

[73] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla No. 13, “Haki ya Elimu (Art. 13),” E/C.12/1999/10 (1999), http://www.ohchr.org/EN/Issues/Education/Training/Compilation/Pages/d)GeneralCommentNo13Therighttoeducation(article13)(1999).aspx (imepitiwa Agosti 10, 2016), para. 11–12.

[74] Azimio la Haki za Binadamu (UDHR), imepitishwa Desemba 10, 1948, G.A. Res. 217A(III), U.N. Doc. A/810 at 71 (1948), art. 26; ICESCR, art. 13(2)(b); CRC, art. 28. Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi ni pamoja na aina na ngazi zote za mfumo wa elimu unaojumuisha, mbali na maarifa ya ujumla, mafunzo ya teknolojia na sayansi zinazohusika na kupata ujuzi wa vitendo, ufahamu, mtazamo na uelewa kuhusiana na fani fulani katika sekta mbalimbali za uchumi na jamii. Mkataba wa Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi 1989, imepitishwa Novemba 10, 1989, No. 28352, art. 1 (a). kwa taarifa zaidi, see also: Mkataba wa Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi, November 10, 1989, art. 3.

[75] ICESCR, art. 13(2) (b); CRC, art. 28(1)(b); Azimio la Afrika juu ya Haki na Ustawi wa Mtoto, art. 11(3) (b); Azimio la Vijana wa Afrika, art. 13 (1) na art. 13 (4) (b).

[76] ICESCR art. 13 (d). Kwa mujibu wa Makubaliano ya Dunia ya 1990 juu ya Elimu kwa wote, “elimu ya msingi na yenye kueleweka ni muhimu katika kuboresha ngazi za juu za elimu na uelewa wa sayansi na teknolojia na uwezo na hivyo maendeleo ya kujitegemea.” Elimu ya msingi “lazima itolewe kwa watoto wote, vijana na watu wazima … [and] lazima itanuliwe na hatua za uhakika zichukuliwe kuondoa utofauti.” Kongamano la Dunia la Elimu kwa Wote, Makubaliano ya Dunia juu ya Elimu kwa Wote na Mipango ya Utekelezaji kufikia Mahitaji ya Msingi ya Elimu, Jomtien, Thailand, March 1990, http://unesdoc.unesco.org/images/0012/001275/127583e.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016), art. 3 (1)-(2).

[77] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla No. 13, “Haki ya Elimu (Art. 13),” para. 23.

[78] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla 3, Majukumu ya Nchi Wanachama (Fifth session, 1990),” U.N. Doc. E/1991/23, para. 2 and 9.

[79] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla No. 13, “Haki ya Elimu (Art. 13),” para. 13.

[80] Mkutano Mkuu wa UN, Ripoti ya Mwandishi Maalumu wa haki za elimu, Kishore Singh, “Tathmini ya upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi na utekelezaji wa haki ya elimu,” A/HRC/26/27, May 2, 2014, http://ap.ohchr.org/documents/dpage_e.aspx?si=A/HRC/26/27 (imepitiwa Agosti 10, 2016), paras. 79, 81.

[81] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla No. 20, “Kutokuepo kwa ubaguzi katika haki za uchumi, jamii na utamaduni (art. 2, para. 2, of the Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni),” E/C.12/GC/20 (2009), http://www.refworld.org/docid/4a60961f2.html (imepitiwa Mei 20, 2016), para. 10 (b).

[82] Ibid.

[83] Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Makubaliano Dhidi ya Ubaguzi katika Elimu yaliyopitishwa Desemba 14, 1960, na kuanza kutumika Mei 22, 1962, na kuridhiwa na Tanzania Januari 3, 1979, art. 4.

[84] Itifaki ya Azimio la Afrika la Haki za Binadamu na Haki za Wanawake Afrika, imepitishwa na Kikao cha Pili cha Kawaida cha Umoja wa Afrika, Maputo, September 13, 2000, CAB/LEG/66.6, entered into force November 25, 2005, ratified by Tanzania on March 3, 2007, art. 12 (1) (a) and (c).

[85] Azimio la Vijana wa Afrika (2006), imeanza kutumika Agosti 8, 2009, art. 13 (1) and art. 13 (4) (b).

[86] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Maoni ya jumla No. 13, “Haki ya Elimu (Art. 13),” para. 6 (c).

[87] Kamati ya UN ya Haki za Mtoto, “Maoni ya jumla No. 1, “Lengo la ELimu (article 29),” CRC/GC/2001/1 (2001), http://www2.ohchr.org/english/bodies/crc/docs/GC1_en.doc (imepitiwa Agosti 18, 2016), para. 9.

[88] Ibid., para. 22.

[89] UNESCO Mkataba dhidi ya Ubaguzi wa Elimu, art. 4(b).

[90] Mkataba wa Haki ya Watu wenye Ulemavu (MHWU), imepitishwa Desemba 13, 2006, G.A. Res 61/106, U.N. Doc A/RES/61/106, kuanza kutumika Mei 3, 2008, kuridhiwa na Tanzania Novemba 10, 2009, art. 24.

[91] MHWU, art. 24(2) (d), (e).

[92] Ibid., arts. 24(c) and (d) respectively.

[93] Ibid., art. 2.

[94] Ibid., art. 9.

[95] Kamati ya UN ya Haki za Watu wenye Ulemavu, “Maoni ya jumla No. 4 (2016) Article 24: Haki ya Elimu Jumuishi,”, CRPD/C/GC/4 (2016), http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRPD/C/GC/4&Lang=en (imepitiwa Januari 16, 2017), paras. 13-26.

[96] Ibid., para. 24.

[97] CRC, art. 19 (1). Angalia Mipango ya Dunia Kuondoa Adhabu zote za Viboko kwa Watoto na Kuwaokoa Watoto, “Kuelekea shule zisizokuwa na vurugu: kupiga marufuku adhabu zote za viboko, Ripoti ya Dunia 2015,” Mei 2015, http://www.endcorporalpunishment.org/assets/pdfs/reports-thematic/Schools%20Report%202015-EN.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016), pp. 4–5.

[98] CRC, art. 28 (2).

[99] Kamati ya UN ya Haki za Mtoto, Maoni ya jumla No. 8 (2006): Haki ya mtoto kulindwa na adhabu ya viboko na adhabu nyingine za kikatili au za kudhalilisha (arts.19; 28, para. 2; and 37, inter alia),” CRC/C/GC/8 (2007), http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fGC%2f8&Lang=en (imepitiwa Septemba 28, 2016), para. 11.

[100] Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto, art. 11 (5).

[101] UN, Tume ya Haki za Binadamu, “Ripoti ya Mwandishi Maalumu, Mr. Nigel S. Rodley, imewasilishwa kwa mujibu wa maazimio ya Tume ya Haki za Binadamu 1995/37 B,” E/CN.4/1997/7, January 10, 1997, https://daccess-ods.un.org/TMP/5068366.52755737.html (imepitiwa Septemba 28, 2016), para. 6.

[102] UN, Kamati ya Haki za Binadamu, “Maoni ya jumla No. 20: Article 7 (Kuzuia mateso au aina nyingine za adhabu za kikatili, zisizokuwa za kibinadamu na za kudhalilisha),” A/44/40, (1992), http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=INT%2fCCPR%2fGEC%2f6621&Lang=en (imepitiwa Septemba 28, 2016), para. 5

[103] Ibid., para. 5.

[104] Umoja wa Afrika, Kamati ya Afrika ya Wataalamu wa Haki na Ustawi wa Mtoto, “Taarifa ya juu ya Ukatili dhidi ya Watoto,” 2011, http://www.endcorporalpunishment.org/assets/pdfs/reference-documents/ACERWC-statement-on-VAC-2011-EN.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[105] Kamati ya Haki za Mtoto, “Maoni ya kuhitimisha ya ripoti za pamoja za kipindi cha tatu hadi tano cha upimaji Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” CRC/C/TZA/CO/3-5, March 3, 2015, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fTZA%2fCO%2f3-5&Lang=en (imepitiwa Septemba 28, 2016), pp. 7–8; Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, “Ripoti ya Kamati juu ya Malengo ya shughuli za Usimamizi wa Mfumo wa Kisheria na Utekelezaji wa Sera ya Haki za Mtoto kwa Nchi Wanachama wa EAC, 22nd – 26th February 2015,” August 2015, http://www.eala.org/uploads/Report%20of%20the%20oversight%20activity%20of%20rights%20of%20the%20child%20%20fin%2019%2008%2015.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016), p. 13.

[106] Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto, art. 21(2). Kuzuia ndoa za utotoni na kuondoa ubaguzi, vyote vimejumuishwa katika itifaki ya Maputo. Angalua vyombo 13 vya kimataifa na kikanda vinatoa ulinzi dhidi ya ndoa za utotoni. African Child Policy Forum, “Kuwepo kwa vyombo vya Kimatifa na Kikanda kutoa Ulinzi dhidi ya Ndoa za Utotoni,” May 2013, http://www.girlsnotbrides.org/wp-content/uploads/2013/06/International-and-Regional-Standards-for-Protection-from-Child-Marriage-June-2013.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[107] Azimio la Afrika la Haki na Ustawi wa Mtoto, art. 21 (2).

[108] Kamati ya Haki za Mtoto, “Maoni ya jumla No. 4, Afya ya Vijana na Maendeleo katika Mazingira ya Mkataba wa Haki za Mtoto,” CRC/GC/2003/4, (2003), http://www.ohchr.org/Documents/Issues/Women/WRGS/Health/GC4.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016), paras. 16, 20, and 35 (g).

[109] Mapendekezo ya Tume yalitupwa mbali na aliekuwa Waziri wa Sheria na Katiba. USAID Health Policy Initiative, “Kutetea Mabadiliko katika umri wa ndoa Kisheria Tanzania: Juhudi Chini ya Mipango ya Sera ya Afya,” June 2013, http://www.healthpolicyinitiative.com/Publications/Documents/1534_1_Law_of_Marriage_Report.pdf (imepitiwa Septemba 22, 2016), p. 3.

[110] CRC, art. 32.

[111] Shirika la Kazi Duniani, “Mkataba na Mapendekezo ya ILO ya ajira kwa mtoto,” http://www.ilo.org/ipec/facts/ILOconventionsonchildlabour/lang--en/index.htm (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[112] Sheria ya Mtoto (Ajira kwa Mtoto) Kanuni, G.N. No. 196 of 2012, http://www.ilo.org/dyn/natlex/docs/SERIAL/96139/113528/F1782966342/TZA96139.pdf.

[113] Twaweza East Africa, “A New Dawn? Maoni ya wananchi juu ya maendeleo mapya katika elimu,” Sauti za Wananchi, Brief No. 30, Februari 2016, http://www.twaweza.org/uploads/files/SzW-Education-Feb2016-EN-FINAL.pdf (imepitiwa Mei 30, 2016), p. 3.

[114] Mahojiano ya Human Rights Watch na Abasi, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[115] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Waraka Wa Elimu Namba 11” (2004) (Education Circular Number 11), quoted in “Waraka Wa Elimu Namba 3 Wa Mwaka 206 Kuhusu Utekelezaji Wa Elimu ya Msingi Bila Malipo,” (Education Circular No. 3 of 2016 on the implementation of abolition of school fee charges), May 2016, http://www.moe.go.tz/en/publications/send/44-circulars-nyaraka/270-waraka-namba-3-wa-mwaka-2016-elimu-bure (imepitiwa Septemba 22, 2016), p. 2.

[116] Mahojiano ya Human Rights Watch na Imani, 20, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Juma, 22, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Zahra, 19, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Sophia, 20, Mwanza, Januari 21, 2016 ; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mercy, 20, Igombe, Mwanza, January 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Sarah, 20, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Paulina, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Abasi, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[117] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Busara, 17, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[118] Mahojianoa ya Human Rights Watch na Theodora, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[119] Mahojiano ya Human Rights Watch na Imani, 20, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Emmanuel, 23, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mariamu, 20, Dar es Salaam, Januari 30, 2016.

[120] Wanafunzi wengi ambao hapo awali walikuwa wakilipa ada ya masomo ya muda wa ziada waliwaambia Human Rights Watch kwamba hawapati tena hiyo huduma kwa mwaka 2016, isipokuwa kama wakipata mwalimu binafsi kwa kujitegemea. Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Bernard, 19, Shinyanga, Januari 26,2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Fatma, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[121] Mahojiano ya Human Rights Watch na naibu mwalimu mkuu, shule ya msingi, Mwanza, Januari 20, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na mwalimu mkuu, shule ya sekondari, Ukerewe, Januari 22, 2016. 

[122] Mahojiano ya Human Rights Watch na kaimu mwalimu mkuu, Mwanza, Mei 26, 2016.

[123] Ada zilikuwa zimeshafutwa hapo awali kwa shule za msingi, lakini wazazi bado walikuwa wanalipa michango mingi ya shule mpaka Desemba 2015. Mahojiano ya Human Rights Watch na Venance Manori, mkurugenzi msaidizi, masuala mtambuka, na Mr. Salum Salum, afisa mwandamizi wa elimu (sekondari), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[124] Shule zinapata ruzuku za kila mwezi ambayo inajumuisha kiasi kamili cha fedha kwa kila mwanafunzi alieandikishwa katika shule husika.“Tanzania: Wacheni Kudanganya, Shule zapewa onyo,” The Citizen, August 26, 2016, http://allafrica.com/stories/201608260117.html (imepitiwa Septemba 20, 2016).

[125] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wafanyakazi wa ndani 28 ambao ni watoto, Mwanza, Januari 23, 2016.

[126] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rachel, 17, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Sandra, 19, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[127] Mahojiano ya simu ya Human Rights Watch na Pedro Guerra, mtaalamu wa ulinzi wa mtoto, Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF), Dar es Salaam, Oktoba 28, 2016.

[128] Mahojiano ya Human Rights Watch na Emmanuel Samara, mwakilishi wa mkoa wa Mara, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016.

[129] Mahojiano ya Human Rights Watch na Khadija, 16, Dar es Salaam, Januari 30, 2016.

[130] MAhojiano ya Human Rights Watch na Saida, 14, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[131] Mahojiano ya Human Rights Watch na Bernard Makachia, mkurugenzi mtendaji, Elimu kwa Maisha Bora (Education for Better Living), Mwanza, Januari 21, 2016.

[132] Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania linafafanua Mtihani wa Kumaliza Darasa la Saba (PSLE) kama, “jaribio la uteuzi ambalo linaiwezesha serikali kuchagua wanafunzi watakaojiunga Kidato cha kwanza katika shule zake. Wanafunzi wanaochaguliwa na wale wasiochaguliwa wote wanapewa vyeti.” Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania, “Mtihani wa Kumaliza Darasa la Saba,” http://www.necta.go.tz/psle (imepitiwa Septemba 22, 2016).

[133] Prof. Suleman Sumra na Dr. Joviter K. Katabaro (The Economic and Social Research Foundation), “Kushuka kwa Ubora wa Elimu: Mapendekezo ya Kusitisha na Kugeuza Mwenendo,” Background Paper No. 9, ESRF Discussion Paper 63, 2014, http://www.thdr.or.tz/docs/THDR-BP-9.pdf (imepitiwa Septemba 5, 2016), pp. 3-14; Arun R. Joshi and Isis Gaddis (World Bank Group), “Kuandaa Kizazi Kijacho cha Tanzania: Changamoto na Fursa katika ELimu,” 2015, http://documents.worldbank.org/curated/en/531071468187781204/pdf/97256-PUB-PUBLIC-Box391441B-9781464805905.pdf (imepitiwa Septemba 5, 2016), p. 5; Jussi Karakoski na Kristina Ström, “Mahitaji Maalumu ya Elimu Tanzania, Ripoti ya Mwisho ya Kutafuta Ukweli 10.1.2005, Imefanywa na Kuwasilishwa kwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland,” Januari 2005, http://formin.finland.fi/Public/download.aspx?ID=14227&GUID=%7B536C2E76-0615-4771-A230-6066422D44EE%7D (imepitiwa Novemba 30, 2016), p. 19. Mahojiano ya Human Rights Watch na Fredrick Msigallah, Kitengo cha Utetezi CCBRT, Dar es Salaam, Januari 18, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Sr. Sylvia Emanuel, Mhadhiri, Kituo cha Haki za Binadamu, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine Tanzania, Mwanza, Mei 27, 2016.

[134] Asilimia imewekwa katika namba ya karibu kupata namba kamili. Takwimu zilichambuliwa kwa kiasi kidogo na Human Rights Watch, kulingana na takwimu za serikali. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tovuti ya Serikali ya Takwimu kwa Umma, “Upangaji Shule za Msingi kutokana na Ufaulu,” August 23, 2015, http://opendata.go.tz/dataset/upangaji-shule-za-msingi-kutokana-na-ufaulu (imepitiwa Septemba 28, 2016); Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania, “Matokeo ya Taifa kwa ujumla katika PSLE - 2012 Examination,” http://41.188.136.75/BRN/PSLE/PSLE%20PERFORMANCE/2012/PSLE2012_PERFORMANCE.pdf,  “PSLE Performance 2013,” http://41.188.136.75/BRN/PSLE/PSLE%20PERFORMANCE/2013/PSLE2013_PERFORMANCE.pdf and “PSLE Performance 2014,” http://41.188.136.75/BRN/PSLE/PSLE%20PERFORMANCE/2014/PSLE2014_PERFORMANCE.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016); Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania, “Upangaji wa Shule za Msingi kwa ufaulu 2015,” http://www.necta.go.tz/brn and “PSLE Performance 2015,” http://41.188.136.75/BRN/PSLE/PSLE%20SCHOOLS%20RANKING/2015/PSLE2015_RANKING.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[135] Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Temu, afisa mipango, Uwezo, Dar es Salaam, Januari 19, 2016.

[136] Haki Elimu, “Elimu Bora ni nini? Ripoti ya Utafiti wa Mtazamao wa Wananchi na Ujuzi wa Msingi wa Watoto,” May 2008, http://hakielimu.org/files/publications/What%20is%20Quality%20Education.pdf (imepitiwa Agosti 30, 2016); Tanzanian Child Rights Forum na Human Rights Watch, “Barua ya HRW na TCRF kwa Waziri wa Elimu Tanzania, Upatikanaji wa Elimu ya Sekondari,” March 28, 2014, https://www.hrw.org/news/2014/03/28/letter-hrw-and-tcrf-tanzania-minister-education.

[137] Human Rights Watch, Toxic Toil: Child Labor and Mercury Exposure in Tanzania’s Small-Scale Gold Mines, August 2013, https://www.hrw.org/report/2013/08/28/toxic-toil/child-labor-and-mercury-exposure-tanzanias-small-scale-gold-mines; No Way Out: Child Marriage and Human Rights Abuses in Tanzania, October 2014, https://www.hrw.org/report/2014/10/29/no-way-out/child-marriage-and-human-rights-abuses-tanzania#78bac8.

[138] Mahojiano ya Human Rights Watch na Adelina, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[139] Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania na UNICEF, “Tathmini ya Maadili katika Mtihani wa Kumaliza Darasa za Saba Tanzania Bara,” March 2009, http://www.unicef.org/evaldatabase/files/NECTA_(2009_03_xx)_-_Evaluation_of_the_conduct_of_Primary_School_Leaving_Examination_(PSLE)_in_Tanzania_Mainland.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[140] Ibid., p. 23.

[141] Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Temu, afisa mipango, Uwezo, Dar es Salaam, Januari 19, 2016. Kwa mujibu wa uchambuzi wa Uwezo, wanafunzi hawapati ujuzi wa msingi wa kusoma na kuhesabu kama mtaala wa shule za msingi unavyoeleza. Uwezo, “Watoto wetu wanajifunza? Kujua kusoma na kuhesabu Afrika Mashariki,” 2013, http://www.uwezo.net/wp-content/uploads/2012/08/2013-Annual-Report-Final-Web-version.pdf (imepitiwa Oktoba 31, 2016).

[142] Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Wizara Ya Elimu Na Mafunzo Ya Ufundi (United Republic of Tanzania, Ministry of Education and Vocational Training), “Sera Ya Elimu Na Mafunzo (Education and Training Policy), 2014 http://www.tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/SERA_ya_Elimu_2_sw.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), pp. 23–24. Translated by Human Rights Watch.

[143] Mahojiano ya Human Rights Watch na Clarence Mwinuka, afisa mwandamizi wa elimu ya msingi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[144] Mkutano Mkuu wa UN, Ripoti ya Mwandishi Maalumu wa haki ya elimu, Kishore Singh, Tathmini ya kiwango cha elimu ya wanafunzi na utekelezaji wa haki ya kupata elimu, A/HRC/26/27, May 2, 2014, http://ap.ohchr.org/documents/dpage_e.aspx?si=A/HRC/26/27 (imepitiwa Agosti 10, 2016), paras. 79 and 81.

[145] Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari II (Julai 2010 – Juni 2015), Juni 2010, http://planipolis.iiep.unesco.org/upload/Tanzania%20UR/Tanzania_SEDP_2010_2015.pdf (imepitiwa Agosti 20, 2016).

[146] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (2008–2017),” August 2008, http://www.globalpartnership.org/content/tanzania-education-sector-development-programme-2008-17 (imepitiwa Oktoba 10, 2016).

[147] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sigareti Lugangika, mwalimu mkuu, Shule ya Sekondari Nyakurunduma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Marxon Paul, mwalimu mkuu, Shule ya Sekondari Shinyanga, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[148] Mahojiano ya Human Rights Watch na maafisa waandamizi wa shule, Mwanza, Mei 27, 2016.

[149] Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, “Hotuba Ya Waziri Wa Elimu, Sayansi, Teknolojia Na Ufundi Mheshimiwa Prof. Joyce Lazaro Ndalichako (MB.) Akiwasilisha Bungeni Makadirio Ya Matumzi Ya Fedha Kwa Mwaka 2016/2017,” (Speech by the Minister of Education, Science, Technology and Vocational Training, Honorable Joyce Lazaro Ndalichako Introducing the National Assembly of Estimates Budget for The Year 2016/2017), Dodoma, May 2016, http://www.parliament.go.tz/uploads/budgetspeeches/1464680317-HOTUBA_WEST_2016_FINAL%20-%2023-05-2016.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016), paras. 50, 99.

[150] Arun R. Joshi na Isis Gaddis (World Bank Group), “Kuandaa Kizazi Kijacho cha Tanzania: Changamoto na Fursa katika Elimu,” 2015, http://documents.worldbank.org/curated/en/531071468187781204/pdf/97256-PUB-PUBLIC-Box391441B-9781464805905.pdf (imepitiwa Desemba 5, 2016), pp. 39–46; Gervas Machimu na Josephine Joseph Minde, “Wasichana wa Vijijini’ Changamoto za Elimu Tanzania: Utafiti uliofanyika katika Jamii inayofuata upande wa Mwanamke (Matrilineal Society),” The Social Sciences, vol. 5, issue 1 (2010), http://www.medwelljournals.com/fulltext/?doi=sscience.2010.10.15 (imepitiwa Desemba 5, 2016), pp. 10–15; Deogratias Mushi, “Tanzania: Ward Schools Need Better Ways to Address Pregnancy,” Tanzania Daily News, August 8, 2015, http://allafrica.com/stories/201508100438.html (imepitiwa Desemba 5, 2016).

[151] Mahojiano ya Human Rights Watch na Yasinta, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Fatma, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Beatrice, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mercy, 20, Igombe, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Bernard, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Gerald, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[152] Chakula kinachotolewa mashuleni kilikua kinagharamiwa na michango. Shule ziliacha kutoa chakula Januari 2016 kutokana na agizo la serikali la kusitisha ada. Mei 2016, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ufundi Stadi, ilitoa maelekezo rasmi kwa shule kurejesha huduma ya chakula na migahawa shuleni. Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[153] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wazazi nane, wanachama wa Marafiki wa Elimu (Haki Elimu), Ukerewe, Januari 22, 2016.

[154] Ibid.

[155] Mahojiano ya Human Rights Watch na Fatma, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Aisha, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[156] Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[157] Angalia Kifungu cha IV: “Adhabu za Viboko na za Kudhalilisha.”

[158] Mahojiano ya Human Rights Watch na Elsa, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[159] Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Mabala, mkurugenzi mtendaji, TAMASHA, Dar es Salaam, Januari 20, 2016; Kizito Makoye, Thomson Reuters Foundation, “Sikia kilio Chetu”: app mpya ya kuwasaidia wanafunzi Tanzani kupambana na unyanyasaji katika usafiri,” Februari 12, 2016, http://news.trust.org/item/20160212140343-adjhd (imepitiwa Agosti 30, 2016).

[160] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 2016.

[161] Abraham Ntambara, “Usafiri Usio wa Uhakika Tatizo kwa Wanafunzi Dar es Salaam”, Agosti 23, 2013, https://wewriteforrights.wordpress.com/2013/08/22/unreliable-transport-a-problem-for-students-in-dar-es-salaam/ (imepitiwa Desemba 5, 2016); Johanes Mugoro, “Matatizo ya usafiri kwa wanafunzi na madhara yake kwa mahudhurio ya shule katika shule za sekondari za umma jijini Dar es Salaam, Tanzania,” (Masters thesis, Open University of Tanzania, 2014), http://repository.out.ac.tz/757/ (imepitiwa Desemba 5, 2016).

[162] Kilio Chetu, “Vilio vilivyoripotiwa” http://www.ourcries.com/ViewCries.php (imepitiwa Agosti 30, 2016).

[163] Jukwaa la Sera ya Mtoto wa Afrika, “Ripoti ya Afrika juu ya Ukatili dhidi ya Watoto,” 2014, http://africanchildforum.org/files/AfricanReprotVAC.pdf (imepitiwa Desemba 3, 2016), p. 21.

[164]  Kamati ya Haki za Mtoto, “Maoni ya ujumla  Na. 8 (2006): Haki ya mtoto kulindwa dhidi ya adhabu za viboko na aina nyingine za adhabu za ukatili au kufedhehesha (arts. 19; 28, para. 2; and 37, inter alia),” CRC/C/GC/8 (2007) http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fGC%2f8&Lang=en (imepitiwa Septemba 21, 2016).

[165] Mwaka 2013, aliekua Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Philipo Mulugo alihusisha kutokuwepo kwa adhabu za viboko na kudorora kwa nidhamu mashuleni kama alivyoripotiwa akitetea matumizi ya viboko. “Tanzania: Public Schools to Continue Using Corporal Punishment,” Tanzania Daily News, April 9, 2013, http://allafrica.com/stories/201304090024.html (imepitiwa Mai 3, 2016); Henry Lyimo, “Tanzania: Ministry Sets Guidelines on Corporal Punishment,” Tanzania Daily News, June 14, 2014, http://allafrica.com/stories/201406161113.html (imepitiwa Mai, 3 2016); Elisha Magolanga, “Abolish the cane in schools, activists urge govt,” The Citizen, June 13, 2013, http://www.thecitizen.co.tz/Business/Abolish-the-cane-in-schools--activists-urge-govt/-/1840434/1882514/-/view/printVersion/-/qt74oj/-/index.html (imepitiwa Mai 3, 2016); “Rais Magufu Ashangaa Viboko Kufutwa Shuleni,” March 29, 2016, video clip, YouTube, https://www.youtube.com/watch?v=AsQq56-KiiM (imepitiwa Juni 6, 2016). Video imetafsiriwa na Human Rights Watch.

[166] Ibid.

[167] Kwa mujibu wa kifungu cha 60, Sheria ya Taifa ya Elimu ya 1978, Kanuni za Elimu (Adhabu za Viboko), G.N. No. 294 2002. Nakala iko na Human Rights Watch.

[168] Kanuni ya Sheria ya Elimu (Adhabu za Viboko), reg. 3 (1).

[169] Ibid., reg. 2.

[170] Ibid., reg. 4(1).

[171] Ibid., reg. 4 (2).

[172] Ibid., reg. 5 (1).

[173] Ibid., regs. 6 and 7; hatua zinaweza kuchukuliwa chini ya Kanuni za Kusimamisha na Kufukuza Shule Wanafunzi (2002) na Sheria ya Tume ya Huduma za Walimu (1989).

[174] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwalimu wa shule ya sekondari, Mwanza, Mei 26, 2016.

[175] Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa mwandamizi wa shule, Mwanza, Mei 26, 2016.

[176] Kamati ya Haki za Mtoto, “Kupitia ripoti zinazowasilishwa na Nchi wanachama chini ya kifungu cha 44 cha Mkataba. Third to fifth periodic reports of States parties due in 2012. United Republic of Tanzania,” CRC/C/TZA/2-5, November 4, 2013, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2FC%2FTZA%2F3-5&Lang=en (imepitiwa Aprili 28, 2016).

[177] Committee on the Rights of the Child, “Concluding observations on the combined third to fifth periodic reports of the United Republic of Tanzania,” CRC/C/TZA/CO/3-5, March 3, 2015, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fTZA%2fCO%2f3-5&Lang=en (imepitiwa Mai 3, 2016), pp. 7–8.

[178] Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki, “Report of the Committee on General Purposes on the Oversight Activity on the Legal Framework and Implementation of Policies on the Rights of the Child in the EAC Partner States, 22nd – 26th February 2015,” August 2015, http://www.eala.org/uploads/Report%20of%20the%20oversight%20activity%20of%20rights%20of%20the%20child%20%20fin%2019%2008%2015.pdf (imepitiwa Mai 3, 2016), p. 13.

[179] United Nations Children’s Fund (UNICEF), U.S. Centers for Disease Control and Prevention, and Muhimbili University of Health and Allied Sciences, “Violence Against Children in Tanzania: Findings from a National Survey 2009,” August 2011, http://www.unicef.org/media/files/VIOLENCE_AGAINST_CHILDREN_IN_TANZANIA_REPORT.pdf (imepitiwa Mai 3, 2016), p. 109.

[180] African Child Policy Forum, “The African Report on Violence Against Children,” 2014, http://africanchildforum.org/files/AfricanReprotVAC.pdf (imepitiwa Desemba 3, 2016), p. 21.

[181] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi wa kike 12, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi wa kiume 15, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[182] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lewis, 20, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[183] Mahojiano ya Human Rights Watch na Fatma, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[184] Mahojiano ya Human Rights Watch na Aisha, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[185] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sandra, 19, Wailaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[186] Tazama sehemu ya III: “Vikwazo vya Kupata Elimu ya Sekondari: Mindombinu Duni ya Shule.”

[187] Mahojiano ya Human Rights Watch na Ana, 17, Mwanza, Januari 23, 2016.

[188] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jacklen, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[189] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leocadia Vedasius, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[190] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na walimu wa shule za sekondari, Mwanza, Mei 27, 2016.

[191] Mahojiano ya Human Rights Watch na walimu wa shule za sekondari, Mwanza, Mei 27, 2016.

[192] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwalimu wa shule ya sekondari, Mwanza, Mei 27, 2016.

[193] Hilary K. Mead, Theodore P. Beauchaine, and Katherine E. Shannon, “Neurobiological Adaptations to Violence Across Development,” Development and Psychopathology, 22(1) (2010), https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC2813461/pdf/nihms114576.pdf (imepitiwa Januari 16, 2017), p. 19. 

[194] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eric Guga, mkurugenzi mtendaji, Tanzania Child Rights Forum, Dar es Salaam, Januari 29, 2016.

[195] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[196] Ibid.

[197] Mahojiano ya Human Rights Watch na Editha, 16, Mwanza, Januari 22, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 15 wa kike, shule za sekondari za umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Felicity, 18, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Theodora, 17, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[198] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 15 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Jacklen, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[199] Oyin Shyllon (World Bank Group), “Addressing Tanzania’s Gender Inequality Challenge in Secondary Schools,” June 2015, http://elibrary.worldbank.org/doi/abs/10.1596/978-1-4648-0590-5_ch3 (imepitiwa Januari 17, 2017), pp. 27–31; Mahojiano ya Human Rights Watch na Florence, 18, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na April, 21, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Petra, 23, Wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[200] Oyin Shyllon (World Bank Group), “Kushughulikia Changamoto ya Kukosekana kwa Usawa wa Jinsia katika Shule za Sekondari,” p. 31.

[201] Ibid., p. 32.

[202] Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kuondoa Ubaguzi dhidi ya Wanawake, “Concluding observations of the combined seventh and eighth periodic reports of the United Republic of Tanzania,” March 9, 2016, CEDAW/C/TZA/CO/7-8, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CEDAW%2fC%2fTZA%2fCO%2f7-8&Lang=en  (imepitiwa Januari 17, 2017), para. 31.

[203] Center for Reproductive Rights, “Forced Out: Mandatory Pregnancy Testing and the Expulsion of Pregnant Students in Tanzanian Schools,” September 2013, https://www.reproductiverights.org/document/tanzania-report-forced-out-mandatory-pregnancy-testing-expulsion (imepitiwa Mai 20, 2016); Human Rights Watch, No Way Out: Child Marriage and Human Rights Abuses in Tanzania, October 2014, https://www.hrw.org/report/2014/10/29/no-way-out/child-marriage-and-human-rights-abuses-tanzania.

[204] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mercy, 20, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[205] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sophia, 20, Mwanza, Januari 21, 2016.

[206] Education (Expulsion and Exclusion of Pupils from Schools) Regulations, art.4 (b)-(c).  

[207] Human Rights Watch, No Way Out.

[208] Mahojiano ya Human Rights Watch na Venance Manori, mkurugenzi msaidizi, masuala mtambuka, na Mr. Salum Salum, afisa elimu mkuu (sekondari), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[209] Mahojiano ya Human Rights Watch na Dr. Leonard D. Akwilapo, naibu katibu mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[210] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto et al, “Tanzania Demographic and Health Survey and Malaria Indicator Survey 2015-2016,” December 2016, https://www.dhsprogram.com/pubs/pdf/FR321/FR321.pdf, pp. 10–11.

[211] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[212] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Igombe, Mwanza, Januari 21, 2016.

[213] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leocadia Vedastus, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[214] Kizito Makoye, “Tanzania yaanza kutoa elimu ya kujamiiana kudhibiti mimba za utotoni,” Thomson Reuters Foundation, November 4, 2015, http://uk.reuters.com/article/uk-tanzania-sex-education-idUKKCN0ST1OO20151104 (imepitiwa Aprili 4, 2016); Kituo cha Haki ya Afya ya Uzazi, “Kuadhibu Mimba: Kufukuza, Kulazimishwa kuacha shule, na Kutengwa kwa Wanafunzi wenye mimba, Kipengele cha 4 “Kulazimishwa kutoka: Upimaji mimba wa lazima  na Kufukuzwa kwa Wanafunzi wenye Mimba katika Shule za Tanzania,” September 2013,  http://www.reproductiverights.org/sites/crr.civicactions.net/files/documents/crr_Tanzania_Report_Part2.pdf (imepitiwa Mei 20, 2016), p. 80.

[215] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sigareti Lugangika, mwalimu mkuu, shule ya sekondari Nyakurunduma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mercy, 20, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[216] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rita, 19, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 25, 2016.

[217] Kamati ya UN ya Haki za Mtoto, “Concluding observations on the combined third to fifth periodic reports of the United Republic of Tanzania,” CRC/C/TZA/CO/3-5, March 3, 2015, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fTZA%2fCO%2f3-5&Lang=en, (imepitiwa Mei 21, 2016), paras. 62-63.

[218] Ijapokuwa sheria au sera za Tanzania hazielezi matumizi ya vipimo vya mimba shule, matokeo ya utafiti wa Human Rights Watch ya 2014 yanaonyesha kwamba muongozo wa uboreshaji wa shule wa 2013 wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, unatoa hamasa kwa shule kufanya vipimo vya mimba mara kwa mara. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Muongozo wa Uboreshaji Shule, Muongozo kwa Walimu Wakuu wa Shule,” Julai 2013. Nakala kwa Human Rights Watch. Human Rights Watch, No Way Out; Center for Reproductive Rights, “Forced Out: Mandatory Pregnancy Testing and the Expulsion of Pregnant Students in Tanzanian Schools,” p. 56.

[219] Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mercy, 20, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[220] Mahojiano ya Human Rights Watch na Faraidi Mebua, mkuu wa kituo cha mafunzo Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[221] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Imani, 20, Mwanza, Januari 21, 2016.

[222] Mahojiano ya Human Rights Watch na Imani, 21, Mwanza, Januari 21, 2016.

[223] Onyema Afulukwe (Kituo cha Haki ya Afya ya Uzazi), “RH Reality Check: Forced Pregnancy Testing: Blatant Discrimination and a Gross Violation of Human Rights,” August 2012, http://www.reproductiverights.org/press-room/louisiana-africa-pregnancy-test-teens-girls-schools (imepitiwa Machi 6, 2016).

[224] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[225] Center for Reproductive Rights, “Forced Out: Mandatory Pregnancy Testing and the Expulsion of Pregnant Students in Tanzanian Schools,”; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na mahojiano binafsi na wasichana 25, Elimu kwa Maisha Bora, Mwanza, Januari 21, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano Human Rights Watch na Imani, 20, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Juma, 22, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Angela, 17, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[226] Twaweza East Africa, “Reality Check – Maoni ya Wananchi ya elimu katika nyakati za bure,” Sauti za Wananchi, Brief No. 37, November 2016, http://www.twaweza.org/uploads/files/SzW2016-TZ-Education-EN-FINAL.pdf (imepitiwa Novemba 30, 2016).

[227] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sawadee, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Helen, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Bernard Makachia, mkurugenzi mtendaji, Education for Better Living, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Rebeca Gyumi, mkurugenzi mtendaji, Msichana Initiative, Dar es Salaam, Januari 29, 2016.

[228] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sawadee, Mwanza, Januari 21, 2016.

[229] Mahojiano ya Human Rights Watch na Venance Manori, mkurugenzi msaidizi, masuala mtambuka, na Mr. Salum Salum, afisa elimu mkuu (sekondari), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Dr. Leonard D. Akwilapo, naibu katibu mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Ms. Paulina Mkonongo, mkurugenzi, elimu ya sekondari, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[230] Mahojiano ya Human Rights Watch na Margaret Mliwa, mkurugenzi, Restless Development Tanzania, Dar es Salaam, Januari 18, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na John Kalage and Boniventura Godfrey, meneja, Haki Elimu, Dar es Salaam, Januari 18, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Eric Guga, mkurugenzi mtendaji, Tanzania Child Rights Forum, Dar es Salaam, Januari 29, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Ms. Paulina Mkonongo, mkurugenzi, elimu ya sekondari, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[231] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[232] Mahojiano ya Human Rights Watch na Agnes Mollel, mkurugenzi na muanzilishi, Huruma Care Development Arusha, Dar es Salaam, Januari 18, 2016.

[233] African Child Policy Forum, “The African Report on Violence Against Children,” 2014, http://africanchildforum.org/files/AfricanReprotVAC.pdf (imepitiwa Desemba 3, 2016), pp. 28 -29; United Nations Children’s Fund (UNICEF), U.S. Centers for Disease Control and Prevention, and Muhimbili University of Health and Allied Sciences, “Violence against Children in Tanzania: Findings from a National Survey 2009,” August 2011, https://www.unicef.org/media/files/VIOLENCE_AGAINST_CHILDREN_IN_TANZANIA_REPORT.pdf (imepitiwa Desemba 3, 2016).

[234] UNICEF, “Ujana Tanzania,” September 2011, http://www.unicef.org/tanzania/TANZANIA_ADOLESCENT_REPORT_Final.pdf (imepitiwa Mei 3, 2016), p. 44.

[235] Sheria ya Makosa ya Ubakaji, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1998, http://parliament.go.tz/polis/uploads/bills/acts/1457516075-ActNo-4-1998.pdf, kifungu cha 130. Chini ya kifungu cha 131 (2) mtu atakuwa amefanya ubakaji kama atakua ameonesha nia yake pamoja na mambo mengine kwa (a) kumtisha msichana au mwanamke kwa madhumuni ya ngono, (b) kuwa mtu wa mamlaka au ushawishi juu ya msichana au mwanamke na kutoa vitisho kwa madhumuni ya ngono, na (c) kusema uwongo kwa mwanamke kwa nia ya kupata ridhaa yake. Iko kwenye faili na Human Rights Watch. Mtu yeyote anaepatikana na hatia ya ubakaji anawajibika kufungwa kwa miaka si chini ya 30, wakati mtu yeyote anaepatikana na hatia ya unyanyasaji wa kijinsia uliopitiliza anawajibika kufungwa si chini ya miaka 15, au isiyozidi miaka 20 kama kosa la unyanyasaji wa kijinsia limefanywa dhidi ya mtu mwenye umri chini ya miaka 15. Sheria ya Makosa ya Ubakaji, 1998, kifungu cha 131 (1) na (2) (a)–(b).

[236] Ibid., section 138 (3), 138B (I) (d).

[237] Mahojiano ya Human Rights Watch na Beatrice, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[238] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lucia, 17, Mwanza, Januari 23, 2016.

[239] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 8 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[240] Vijana walioongea na utafiti wa TAMASHA walishauri kushughulikia unyanyasaji wa kijinsia katika shule kama suala la kipaumbele na kuchukua hatua dhidi ya walimu wanaokiuka kanuni za maadili. Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Mabala, mkurugenzi mtendaji, TAMASHA, Dar es Salaam, Januari 20, 2016; TAMASHA, “Youth consultations for DFID,” August 2015, pp. 9, 24-28, nakala iko kwenye faili na Human Rights Watch.

[241] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania United Republic of Tanzania, “Kanuni za Maadili na Utendaji kwa Watumishi wa Umma– Tanzania,” 2005, https://www.agidata.org/pam/Legislation.axd/Tnazania(2005)codeofethicsandconductforthepublicservice%5BEN%5D.pdf (imepitiwa Oktoba 31, 2016), para. 6.

[242] UN Committee on the Rights of the Child, “Concluding observations on the combined third to fifth periodic reports of the United Republic of Tanzania,” CRC/C/TZA/CO/3-5, March 3, 2015, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC/C/TZA/CO/3-5&Lang=En (imepitiwa Oktoba 31, 2016), para. 40.

[243] Serikali inafafanua “ulafi wa ngono” kama hali ambayo mtu anadai ngono ili kutoa huduma ya umma.” Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Mpango Kazi wa Taifa Kumaliza Ukatili dhidi Wanawake na Watoto Tanzania, 2017/18 – 2021/2022,” Desemba 2016, http://www.mcdgc.go.tz/data/NPA_VAWC.pdf (imepitiwa Januari 9, 2016), p. 1.

[244] Ibid., p. 28.

[245] Mahojiano ya Human Rights Watch na mshirika wa maendeleo, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[246] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na mahojiano binafsi na wanawake 25, Elimu kwa Maisha Bora, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Joyce, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Margaret Mliwa, mkurugenzi mkazi, Restless Development Tanzania, Dar es Salaam, Januari 18, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Lightness Kweka, Girls Support Girls campaigner, Tanzania Youth Vision Association, Dar es Salaam, Januari 20, 2016.

[247] Majadilano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[248] Mahojiano ya Human Rights Watch na Richard Mabala, mkurugenzi mtendaji, TAMASHA, Dar es Salaam, Januari 20, 2016.

[249] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mandile Kiguhe, mratibu wa jinsia na mkuu wa idara ya jinsia, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016; Majadiliano Kikundi ya Human Rights Watch na wazazi tisa, wanachama wa Marafiki wa Elimu (Haki Elimu), Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Lightness Kweka, Girls Support Girls campaigner, Tanzania Youth Vision Association, Dar es Salaam, Januari 20, 2016.

[250] Mahojiano Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Mwanza, Januari 23, 2016; Majadiliano Kikundi ya Human Rights Watch na mahojiano binafsi na wanafunzi 30 wa kike, Mwanza, Mei 27, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Lightness Kweka, Girls Support Girls campaigner, Tanzania Youth Vision Association, Dar es Salaam, Januari 20 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mwandile Kiguhe, mratibu wa jinsia na mkuu wa idara ya jinsia, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016.

[251] Mahojiano ya Human Rights Watch na Boniventura Godfrey, meneja, Haki Elimu, Mwanza, Mei 25, 2016; Mamlaka ya Elimu Tanzania, “Supported Project: March 2003 – January 2011,” isiyo na tarehe, http://www.tea.or.tz/index.php/afsspro/read (imepitiwa Agosti 30, 2016); Deogratias Mushi, “Tanzania: Need to Address Problems Facing Girls in Ward Schools,” Tanzania Daily News, May 24, 2015, http://allafrica.com/stories/201505251047.html (imepitiwa Agosti 30, 2016); Melanie Lindman, “Dormitory expansion in Tanzania is slow but keeps girls in school,” Global Sisters Report, March 29, 2016, http://globalsistersreport.org/news/ministry/dormitory-expansion-tanzania-slow-keeps-girls-school-38851 (imepitiwa Agosti 30, 2016).

[252] UNICEF, U.S. Centers for Disease Control and Prevention, and Muhimbili University of Health and Allied Sciences, “Violence Against Children in Tanzania: Findings from a National Survey 2009,” August 2011, http://www.unicef.org/media/files/VIOLENCE_AGAINST_CHILDREN_IN_TANZANIA_REPORT.pdf (imepitiwa Oktoba 31, 2016); Dr. Kate McAlpine, “Legislation, responsibilities and procedures for protecting children in Tanzania: What does it mean for people wanting to build safe schools?” May 30, 2015, https://www.academia.edu/14192594/Legislation_responsibilities_and_procedures_for_protecting_children_in_Tanzania_What_does_it_mean_for_people_wanting_to_build_safe_schools (imepitiwa Oktoba 31, 2016); UNICEF and Under The Same Sun, “Sexual abuse cases reported in assessed schools and centres hosting internally displaced children with albinism and other children with disabilities – A report to the Ministry of Education and Vocational Training (MoEVT),” May 26, 2011, http://www.underthesamesun.com/sites/default/files/ABUSE%20AT%20CENTRES%20-TANZANIA%20-%20Text%20and%20Tables%20combined.pdf (imepitiwa Oktoba 31, 2016).

[253] Sheria ya Makosa ya Ubakaji, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1998, http://parliament.go.tz/polis/uploads/bills/acts/1457516075-ActNo-4-1998.pdf, section 138 (5).

[254] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mariamu, Dar es Salaam, Januari 30, 2016.

[255] Sheria ya Elimu, 1995, kifungu cha 59 (A) (1), kilichorekebishwa na Sheria ya Mtoto 2009, ibara. 169.

[256] Mahojiano ya Human Rights Watch na Ayoub Kafyulilo, afisa elimu, UNICEF, Dar es Salaam, Mei 25, 2016.

[257] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eric Guga, mkurugenzi mtendaji, Tanzania Child Rights Forum, Dar es Salaam, Januari 29, 2016.

[258] Mahojiano ya Human Rights Watch na Cathleen Sekwao, mratibu mtendaji, na Nicodemus Eatlawe, meneja mpango, Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET), Dar es Salaam, Novemba 11, 2016.

[259] SNV World, UNICEF, and WaterAid, “School WASH in Tanzania, Improving WASH in Schools: Improving the Quality of Education,” http://www.wateraid.org/~/media/Publications/school-wash.pdf (imepitiwa Septemba 27, 2016).

[260] Haki ya binadamu kupata maji inampa kila mmoja haki ya kupata maji ya kutosha, salama, yanayokubalika na kufikika na kwa gharama nafuu kwa matumizi binafsi na ya kawaida. Haki ya binadamu ya usafi inampa kila mmoja haki ya kupata mazingira safi kwa gharama nafuu katika kila nyanja ya maisha ambayo ni salama, safi, yenye ulinzi na inayokubalika kijamii na kiutamaduni na yenye kuhakikisha faragha na utu. Mkutano Mkuu wa UN, “Haki ya binadamu kupata maji na usafi,” Azimio 64/292 (2010), A/Res/64/292, http://www.un.org/es/comun/docs/?symbol=A/RES/64/292&lang=E (imepitiwa Oktoba 31, 2016).

[261] Arun R. Joshi na Isis Gaddis (World Bank Group), “Kuandaa Kizazi Kijacho Tanzania: Changamoto na Fursa katika Education,” 2015, http://documents.worldbank.org/curated/en/531071468187781204/pdf/97256-PUB-PUBLIC-Box391441B-9781464805905.pdf (imepitiwa Desemba 5, 2016), pp. 39–46.

[262] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “National Strategic Plan for School Water, Sanitation and Hygiene (SWASH) 2012 – 2017,” 2012, http://www.unesco.org/education/edurights/media/docs/39d043c2367b728dd6580cc173bb4ce26e2f80f7.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016). Mpango mkakati wa pili wa Serikali wa ukuaji na kuounguza umasikini unahusisha lengo maalumu kuhakikisha shule zina vifaa vya usafi vya kutosha ifikapo 2015. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Fedha na Uchumi, “Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Awamu ya II,” Julai 2010, http://www.povertymonitoring.go.tz/Mkukuta/Mkukuta%20English.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016), p. 160.

[263] Mahojiano ya Human Rights Watch na Venance Manori, mkurugenzi msaidizi, masuala mtambuka, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[264] Mahojiano ya Human Rights Watch na Beatrice, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Sophia, 20, Mwanza, January 21, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Majadiliano ya Human Rights Watch na Yasinta, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Majadiliano ya Human Rights Watch na Oscar, 18, Shinyanga, Januari 27, 2016. 

[265] Majadiliano ya Human Rights Watch na mwalimu, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[266] Sarah House, Thérese Mahon, na Sue Cavill (Water Aid et al), “Masuala yahusuyo usafi wa Hedhi: Rasilimali kwa ajili ya kuboresha usafi wa hedhi duniani kote,” 2012, http://www.wateraid.org/what-we-do/our-approach/research-and-publications/view-publication?id=02309d73-8e41-4d04-b2ef-6641f6616a4f (imepitiwa Septemba 27, 2016), pp. 48–50.

[267] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[268] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 12 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[269] Ibid.

[270] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016.

[271] Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Idadi ya Watu (UNFPA), “Elimu ya kina ya kujamiina,” imehuishwa Septemba 30, 2016, http://www.unfpa.org/comprehensive-sexuality-education (imepitiwa Desemba 13, 2016).

[272] Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), “Dhamira ya Mawaziri juu ya elimu ya kina ya masuala ya kujamiiana na huduma za afya ya uzazi kwa vijana wa Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESA),” Desemba 7, 2013, http://www.unesco.org/new/fileadmin/MULTIMEDIA/HQ/HIV-AIDS/pdf/ESACommitmentFINALAffirmedon7thDecember.pdf (imepitiwa Desemba 13, 2016).

[273] Mahojiano ya Human Rights Watch na Theresa, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Rita, 19, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 25, 2016; Human Rights Watch, No Way Out.

[274] Mahojiano ya Human Rights Watch na Rita, 19, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 25, 2016.

[275] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eileen, 21, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Rita, 19, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Angela, 17, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 25, 2016.

[276] Mahojiano ya Human Rights Watch na Theresa, 19, Igombe, Mwanza, Januari 21, 2016.

[277] Kitila A. Mkumbo, “Uchambuzi wa maudhui ya hadi na nafasi ya elimu ya kujamiiana katika sera ya taifa ya shule na mtaala nchini Tanzania,” Educational Research and Review , Vol. 4 (12) (2009), http://www.academicjournals.org/journal/ERR/article-full-text-pdf/4B11D834171, pp. 616–625; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Taasisi ya Elimu Tanzania, “Mtaala kwa Elimu ya Sekondari [O-Level] Tanzania,” 2007, http://tie.go.tz/docs/CURRICULUM%20FOR%20SECONDARY%20EDUCATION.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016), pp. 37 – 38; UNESCO, UNFPA , et al, “Vijana Leo. Wakati wa Vitendo Sasa. Kwanini vijana wanahitaji elimu ya kina ya kujamiiana na huduma za afya ya uzazi Mashariki na Kusini mwa Afrika,” 2013, http://unesdoc.unesco.org/images/0022/002234/223447E.pdf (imepitiwa Desemba 12, 2016), pp. 102–103.

[278] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Eva, 18, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[279] Kamati ya UN ya Haki za Uchumi, Jamii na Utamaduni, “Concluding observations on the initial to third reports of the United Republic of Tanzania, adopted by the Committee at its forty-ninth session (12 – 30 November 2012), E/c.12/TZA/CO/1-3, December 13, 2012, http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=E%2fC.12%2fTZA%2fCO%2f1-3&Lang=en (imepitiwa Septemba 27, 2016), para. 24; UNFPA, “Comprehensive Sexuality Education: Advancing Human Rights, Gender Equality and Improved Sexual and Reproductive Health,” December 2010, http://www.unfpa.org/sites/default/files/resource-pdf/Comprehensive%20Sexuality%20Education%20Advancing%20Human%20Rights%20Gender%20Equality%20and%20Improved%20SRH-1.pdf (imepitiwa Desemba 12, 2016).

[280] Kamati ya Haki za Mtoto, “Maoni ya jumla Na. 20 (2016) juu ya utekelezaji wa haki za watoto katika umri wa kupevuka,” CRC/C/GC/20 (2016), http://tbinternet.ohchr.org/_layouts/treatybodyexternal/Download.aspx?symbolno=CRC%2fC%2fGC%2f20&Lang=en (imepitiwa Desemba 12, 2016), para. 61.

[281] Sheria ya Watu wenye Ulemavu, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria Na. 9 ya 2010, http://parliament.go.tz/polis/uploads/bills/acts/1452071737-ActNo-9-2010.pdf, arts. 27 (1), 28.

[282] Ibid., art. 27 (3).

[283] Kwa mujibu wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, “Mtu mwenye ulemavu anaonekana kama mtu asie na msaada kwa jamii na yuko pale kusaidiwa … kanuni za utamaduni na jadi zinaweza kulaumiwa kwa mtazamo huu wa jamii kwani zinaona ulemavu kama aina ya adhabu na laana. Matokeo yake, hata watunga sera wanaathiriwa na mtazamo huu wanapo tunga sera kuhusu ustawi kwa watu wenye ulemavu.” Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, “Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2015: Tanzania Bara,” 2016, http://www.humanrights.or.tz/userfiles/file/TANZANIA%20HUMAN%20RIGHTS%202015.pdf (imepitiwa Septemba 27, 2016), p. 154; Harriet Kiama, “Tanzania: Kuhamasisha Watoto wenye Ulemavu kwa Elimu Jumuishi,” Tanzania Daily News, Februari 3, 2015, http://allafrica.com/stories/201502040373.html (imepitiwa Septemba 28, 2016). Utafiti wa Twaweza wa 2014 juu ya maoni ya wananchi juu walemavu uligundua kwamba mwananchi mmoja kati ya watatu anajua mtoto mwenye ulemavu na alie katika umri wa kwenda shule ya msingi lakini hayupo shule. Twaweza, “Kulinda haki ya kila mmoja- maoni ya wananchi juu ya ulemavu–,” Sauti za Wananchi, Ufafanuzi Na. 17, Novemba 2014, http://www.twaweza.org/uploads/files/PeopleWithDisabilities-EN-FINAL.pdf (imepitiwa Septemba 27, 2016).

[284] Mwanga kwa Dunia, “Mtazamo wa Mahitaji Maalumu ya Elimu na Ulemavu – Elimu Jumuishi kwa Watoto wenye Ulemavu Tanzania,” haina tarehe, nakala iko na Human Rights Watch.

[285] Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF), “Usawa na ubora wa Elimu– Watoto wenye ulemavu,” haina tarehe, http://www.unicef.org/tanzania/6911_10810.html (imepitiwa Septemba 27, 2016).

[286] Takwimu zilichambuliwa na Human Rights Watch na kuthibitishwa na Wizara aya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST) kitengo cha Elimu ya Mahitaji Malumu. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Tovuti ya takwimu za serikali kwa umma, “Idadi ya Wanafunzi wa shule za sekondari wenye ulemavu kwa mikoa, 2012 na 2013,” Agosti 24, 2015, http://opendata.go.tz/dataset/idadi-ya-wanafunzi-wa-shule-za-sekondari-wenye-ulemavu-kwa-mikoa (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[287] Ibid.

[288] Angalia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mkakati wa Taifa wa Elimu Jumuishi 2009 – 2017,” Machi 27 2009, http://www.ttu.or.tz/images/files/INCLUSIVE_EDUCATION_STRATEGY_2009-2017.pdf (imepitiwa Septemba 28, 2016).

[289] Shule maalumu zinahudumia watoto wenye ulemavu pekee, na mara nyingi hujulikana kama “ shule za mahitaji maalumu”. Mara nyingi hupatiwa tiba, huduma na vifaa kwa ajili ya watoto wenye ulemavu au kupatiwa watumishi maalumu ambao husaidia watoto wenye aina fulani ya ulemavu.

[290] Mwanga kwa Dunia, “Mtazamo wa Mahitaji Maalumu ya Elimu na Ulemavu – Elimu Jumuishi kwa Watoto wenye Ulemavu Tanzania,” haina tarehe, nakala ipo na Human Rights Watch; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mr. Adamson Shimbatano, kaimu mkurugenzi, kitengo cha Elimu ya Mahitaji Maalum, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[291] Kwa mujibu wa WEST, mipango inawekwa kwa wanafunzi wenye ulemavu wa macho au upungufu wa kuona, ambao wanapewa dakika 10-20 za ziada katika mtihani. Mitihani inapatikana katika Braille au maandishi makubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa linashughulika na Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Ofisi ya Kimataifa ya Elimu, “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Semina ya Kanda “Kuondoa umasikini, Elimu ya HIV na AIDS na Elimu Jumuishi: Masuala ya Kipaumbele kwa Elimu Bora Jumuishi kwa Afrika Mashariki na Magharibi mwa Jangwa la Sahara,” Julai 2007, http://www.ibe.unesco.org/fileadmin/user_upload/Inclusive_Education/Reports/nairobi_07/tanzania_inclusion_07.pdf (imepitiwa Oktoba 10, 2016).

[292] Mahojiano ya Human Rights Watch na Grayson Mlanga, kitengo cha Mahitaji Maalumu ya Elimu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[293] Serikali inatambua elimu jumuishi kama: “mfumo wa elimu ambapo watoto wote, vijana na watu wazima walioandikishwa, wanashiriki kikamilifu na kufaulu katika program za kawaida za shule na za elimu bila kujali asili mbalimbali na uwezo wao, bila ubaguzi, kupitia kupunguza vikwazo na kuongeza rasilimali.” Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi 2009 – 2017,” Machi 2009.

[294] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mr. Adamson Shimbatano, kaimu mkurugenzi, kitengo cha Mahitaji Maalumu ya Elimu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Novemba 10, 2016.

[295] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sigareti Lugangika, malimu mkuu, shule ya sekondari Nyakurunduma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[296] Mahojiano ya Human Rights Watch na Oscar, 18, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[297] Mahojiano ya Kikundi ya Human Rights Watch na mahojiano binafsi na wanafunzi 30 wa kike, shule ya sekondari wa umma, Mwanza, Mei 27, 2016.

[298] Mahojiano ya Human Rights Watch na Marxon Paul, mwalimu mkuu, Shule ya Sekondari Shinyanga, Januari 27, 2016.

[299] Mahojiano ya Human Rights Watch na Oscar, 18, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[300] Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasser, 18, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[301] Mahojiano ya Human Rights Watch na Lewis, 20, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[302] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alfred Kapole, mwenyekiti, Shivyawata Mwanza, Mwanza, Mei 27, 2016.

[303] Mahojiano ya Human Rights Watch na Marxon Paul, mwalimu mkuu, Shule ya Sekondari Shinyanga, Shinyanga, Januari 27, 2016.

[304] Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF), “Ujana Tanzania,” Septemba 2011, https://www.unicef.org/tanzania/TANZANIA_ADOLESCENT_REPORT_Final.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016), pp. 22, 26; Haki Elimu, “Andiko juu ya Sera ya Elimu na Mafunzo 2014: Je, Sera ya Elimu na Mafunzo (2014) Itawaandaa Watoto wa Tanzania Kukabiliana na Changamoto za Karne ya 21?” October 2015, http://www.hakielimu.org/files/publications/HakiElimu_Education_PostitionPaper_2014.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016), p. 12; Uwezo Tanzania, “Watoto wetu Wanajifunza? Kusoma na Kuhesabu Tanzania 2014,” 2015, http://www.twaweza.org/uploads/files/UwezoTZ-ALA2014-FINAL-EN.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016).

[305] Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu (2008 – 2017),” Agosti 2008, http://www.globalpartnership.org/content/tanzania-education-sector-development-programme-2008-17 (imepitiwa Agosti 23, 2016); World Bank Group, “Program-For-Results Information Document (PID) Concept Stage – Matokeo Makubwa Sasa katika Programu ya Elimu,” 2014, http://documents.worldbank.org/curated/en/130791468309353015/pdf/860910PID0P1474860Box385162B00PUBLIC0.pdf (imepitiwa Desemba 5, 2016).

[306] Haki Elimu, “Andiko juu ya Sera ya Elimu na Mafunzo 2014,” p. 11; TAMASHA, “Mashauriano ya Vijana kwa DFID,” 2015, pp. 24–26, nakala iko na Human Rights Watch. 

[307] Joyce Lazaro Ndalichako na Aneth Anselmo Komba, “Uchaguzi wa Masomo kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Tanzania: Suala la Uwezo wa Mwanafunzi na Kupenda au Kulazimishwa?” Open Journal of Social Sciences, 2 (2014), http://file.scirp.org/pdf/JSS_2014082509082694.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016); Haki Elimu, “Kurejesha Heshima ya Mwalimu, Volume II: Vifaa vya Kufundishia na Makazi,” Novemba 2011, http://hakielimu.org/files/publications/Restoring%20Teacher%20Dignity%20II_1.pdf (imepitiwa Novemba 30, 2016); “Teachers shortage hurting Tanzania,” The Citizen, October 14, 2014, http://www.thecitizen.co.tz/News/national/Teachers-shortage-hurting-Tanzania/1840392-2485582-10oc88lz/index.html (imepitiwa November 30, 2016).

[308] TAMASHA, “Elimu: kujifunza au kujidanganya?” haina tarehe, http://www.twaweza.org/uploads/files/Education%20Tamasha.pdf (imepitiwa Desemba 6, 2016); Twaweza, “Kiswahili na Kiingerza Katika Shule za Tanzania: Kujenga Mgawanyiko wa Darasa na kupunguza Viwango vya Elimu,” Julai 13, 2011, http://www.twaweza.org/go/kiswahili-and-english-in-tanzanian-schools--creating-class-divides-and-decreasing-educational-standards (imepitiwa Desemba 6, 2016).

[309] Vipengele vingi vinawekwa na miongozo ya Serikali, ikiwa ni pamoja na: Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Taasisi ya Elimu Tanzania, “Mtaala kwa Elimu ya Sekondari (O-level) Tanzania,” 2007, http://tie.go.tz/docs/CURRICULUM%20FOR%20SECONDARY%20EDUCATION.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016), p. 27.

[310] Mradi wa Haki ya Elimu, “Tathmini ya Matokeo ya Kujifunza: Mtazamo wa Haki za Binadamu,” Februari 2013, http://www.right-to-education.org/sites/right-to-education.org/files/resource-attachments/RTE_Learning_Outcomes_Assessments_HR_perspective_2013.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016).

[311] UNICEF, “Ujana Tanzania,” Septemba 2011, p. 26.

[312] “Tanzania: Kushuka kwa Matokeo ya Kidato cha Nne,” Tanzania Daily Star, Februari 19, 2016, http://allafrica.com/stories/201602190909.html (imepitiwa Agosti 23, 2016).

[313] Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, “Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2015: Tanzania Bara,” 2016, http://www.humanrights.or.tz/userfiles/file/TANZANIA%20HUMAN%20RIGHTS%202015.pdf (imepitiwa Septemba 27, 2016), p. 96; TAMASHA, “Elimu: kujifunza au kujidanganya?” http://www.twaweza.org/uploads/files/Education%20Tamasha.pdf (imepitiwa Desemba 6, 2016).

[314] Elimu Kimataifa, “Tanzania: Hatua muhimu ili kukabiliana na upungufu wa walimu,” Januari 16, 2013, https://www.ei-ie.org/en/news/news_details/2428 (imepitiwa Desemba 6, 2016).

[315] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016 ; Mahojiano ya Human Rights Watch na Eva, 18, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Jessica, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na James, 20, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Joseph, 14, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Gerald, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Caroline, 15, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Stanley, 20, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Jumla, 17, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mohamed, 22, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Theodora, 17, wilaya ya Nzega, Tabora, Januari 25, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Yasinta, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[316] Utafiti uliofanywa na Uwezo ulionyesha utoro miongoni mwa walimu wa hisabati na kiingereza wa shule za sekondari ulikua katika hali mbaya mwaka 2014. Walimu wengi wa shule za sekondari pia wanashindwa kufundisha vipindi vilivyo katika ratiba wakiwa shuleni. Uwezo, “Jinsi Utoro wa Walimu Unavyoathiri Elimu,” Machi 17, 2014, http://www.uwezo.net/how-teachers-absenteeism-greatly-effects-education/ (imepitiwa Agosti 23, 2016); Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Mariam, 19, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Joyce and Farida, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Prosper, 15, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Fatma, 16, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Leyla, 15, Dar es Salaam, Januari 30, 2016.

[317] Mahojiano ya Human Rights Watch na mwalimu, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Mei 26, 2016.

[318] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na walimu tisa, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Mei 27, 2016.

[319] Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Taasisi ya Elimu Tanzania, “Mtaala kwa Elimu ya Sekondari (O-Level) Tanzania,” 2007, http://tie.go.tz/docs/CURRICULUM%20FOR%20SECONDARY%20EDUCATION.pdf (imepitiwa Agosti 23, 2016), p. 23.

[320] Mahojiano ya Human Rights Watch na Caroline, 15, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Joseph, 14, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[321] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leocadia Vedasius, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na mwalimu, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Mei 26, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na walimu tisa wa shule za sekondari, shule za sekondari za umma, Mwanza, Mei 27, 2016.

[322] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi watano wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Mwanza, Januari 21, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Esther, 14, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Farida, 17, Shinyanga, January 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Lewis, 20, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Nasser, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[323] World Bank Group, “Program-For-Results Information Document (PID), Concept Stage – Matokeo Makubwa Sasa katika Programu ya Elimu,” 2014, http://documents.worldbank.org/curated/en/130791468309353015/pdf/860910PID0P1474860Box385162B00PUBLIC0.pdf (imepitiwa Desemba 5, 2016).

[324] Nestory Ngwega, “Tanzania: Waziri Atangaza Masomo Sayansi Lazima,” Tanzania Daily News, Agosti 7, 2016, http://allafrica.com/stories/201608080145.html (imepitiwa Septemba 27, 2016); Adonis Byemelwa, “Tanzania: Fanya Masomo ya Sayansi Lazima lakini Walimu wapewe motisha,” The Citizen, Agosti 21, 2016, http://allafrica.com/stories/201608220144.html (imepitiwa Septemba 27, 2016).

[325] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sigareti Lugangika, mwalimu mkuu, Shule ya Sekondari Nyakurunduma, Mwanza, Januari 21, 2016.

[326] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kike, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Janeth, 18, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[327] Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na afisa mwandamizi wa shule, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na kaimu Mwalimu mkuu, shule ya sekondari ya Nyakurunduma, Mwanza, Mei 26, 2016.

[328] Mahojiano ya Human Rights Watch na Martin Mweza, kaimu mwalimu mkuu, shule ya sekondari Mwawaza, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[329] Mahojiano ya Human Rights Watch na Victoria, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[330] Angalia Kipengele cha III: “Gharama ya Elimu Shule za Sekondari.”

[331] Mahojiano ya Human Rights Watch na Beatrice, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016. 

[332] Mahojiano ya Human Rights Watch na Prosper, 15, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[333] Mahojiano ya Human Rights Watch na Eva, 18, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[334] Mahojiano ya Human Rights Watch Caroline, 15, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[335] Mahojiano ya Human Rights Watch na Joseph, 14, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[336] Mahojiano ya Human Rights Watch na Jumla, 17, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[337] Mahojiano ya Human Rights Watch na Prospro Lubuva, mkuu wa mafunzo ya elimu, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016.

[338] Mpaka kufikia Machi 2016, takwimu za serikali zinaonyesha walimu 88,695 wanafundisha katika shule za sekondari za serikali. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi Stadi, “Hotuba Ya Waziri Wa Elimu, Sayansi, Teknolojia Na Ufundi Mheshimiwa Prof. Joyce Lazaro Ndalichako (MB.) Akiwasilisha Bungeni Makadirio Ya Matumzi Ya Fedha Kwa Mwaka 2016/2017,” (Speech by the Minister of Education, Science, Technology and Vocational Training, Honorable Joyce Lazaro Ndalichako Introducing the National Assembly of Estimates Budget for The Year 2016/2017), Dodoma, Mei 2016, http://www.parliament.go.tz/uploads/budgetspeeches/1464680317-HOTUBA_WEST_2016_FINAL%20-%2023-05-2016.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016), para. 111; Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tovuti ya Takwimu za Serikali kwa Umma, “Idadi ya Walimu katika Shule za Sekondari 2016,” Julai 30, 2016, http://www.opendata.go.tz/dataset/idadi-ya-walimu-katika-shule-za-sekondari-2016 (imepitiwa Septemba 29, 2016).

[339] UNESCO, Ripoti ya Dunia ya Ufuatiliaji wa Elimu, “Kila mtoto Lazima awe na Kitabu cha Kiada,” andiko la sera 23, Januari 2016, http://unesdoc.unesco.org/images/0024/002433/243321E.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016); Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, “Ripoti ya Haki za Binadamu Tanzania 2014,” 2015, http://www.humanrights.or.tz/downloads/THRR%20REPORT%20-%202014.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016), pp. 122-124; Joyce Lazaro Ndalichako na Aneth Anselmo Komba, “Uchaguzi wa Masomo kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari Tanzania: Suala la Uwezo wa Mwanafunzi na Kupenda au Kulazimishwa?” Open Journal of Social Sciences, 2 (2014), http://file.scirp.org/pdf/JSS_2014082509082694.pdf (imepitiwa Agosti 24, 2016), pp. 53–54; “Spectre of poor quality education stalks Tanzania,” The East African, May 18, 2013, http://www.theeastafrican.co.ke/news/Spectre-of-poor-quality-education-stalks-Tanzania/2558-1856356-ecugcb/index.html (imepitiwa Agosti 24, 2016).

[340] Mahojiano ya Human Rights Watch na Esther, 14, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[341] Mahojiano ya Human Rights Watch na Leonard Haule, idara ya utetezi, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Peter Mpande, mwakilishi kutoka Katani, Chama cha Walimu Tanzania, Morogoro, Januari 20, 2016; Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na walimu tisa wa shule ya sekondari, Mwanza, Mei 27, 2016.

[342] Mahojiano ya Human Rights Watch na Sigareti Lugangika, mwalimu mkuu, shule ya sekondari Nyakurunduna, Mwanza, Januari 21, 2016.

[343] Majadiliano ya Kikundi ya Human Rights Watch na wanafunzi 14 wa kiume, shule ya sekondari ya umma, Ukerewe, Januari 22, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Elsa, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Beatrice, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Prosper, 15, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Yasinta, 17, Shinyanga, Januari 26, 2016; Mahojiano ya Human Rights Watch na Gerald, 18, Shinyanga, Januari 26, 2016.

[344] Mahojiano ya Human Rights Watch na Angel Benedict, mkurugenzi mtendaji, Wotesawa, Mwanza, Mei 27, 2016.

[345] TAMASHA, “Elimu: kujifunza au kujidanganya?” http://www.twaweza.org/uploads/files/Education%20Tamasha.pdf (imepitiwa Desemba 6, 2016); World Bank Group, “Program-For-Results Information Document (PID) Appraisal Stage – Education and Skills for Productive Jobs,” March 22, 2016, http://documents.worldbank.org/curated/en/968821468165276476/pdf/PID35202-PGID-P152810-Initial-Appraisal-Box396254B-PUBLIC-Disclosed-5-17-2016.pdf (imepitiwa Desemba 13, 2016).

[346] Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, “Vyuo vya Elimu ya Watu Wazima,” http://www.mcdgc.go.tz/index.php/colleges/fdc/folk_development_colleges_provision/ (imepitiwa Agosti 17, 2016); Mahojiano ya Human Rights Watch na Fabio Siani, afisa mwandamizi wa programu ya ajira na kipato, Ubalozi wa Swiss, Dar es Salaam, Mei 25, 2016.

[347] Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, “Utaratibu wa Kujiunga na Vituo vya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania,” Novemba 2015, http://www.veta.go.tz/assets/uploads/dc7ae-Brochure-3-Namna-ya-kujiunga-na-vyuo-Kiingereza.doc (imepitiwa Agosti 17, 2016); Mahojiano ya Human Rights Watch na Gerald Ng’ong’a, mkurugenzi mtendaji, Rafiki SDO, wilaya ya Kahama, Shinyanga, Januari 24, 2016.

[348] Mahojiano ya Human Rights Watch na Wendy, 16, Nzega, Tabora, Januari 25, 2016.

[349] Mahojiano ya Human Rights Watch na Venance Manori, mkurugenzi msaidizi, masuala mtambuka, na Mr. Salum Salum, afisa elimu mkuu (sekondari), Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 24, 2016.

[350] Ibid.

[351] Mahojiano ya Human Rights Watch na April, 21, Igombe, Mwanza, Januari 23, 2016.

[352] Mahojiano ya Human Rights Watch na Alfred Kapole, mwenyekiti, Shivyawata Mwanza, Mwanza, Mei 27, 2016.

[353] Mahojiano ya Human Rights Watch na Mr. Adamson Shimbatano, Idara ya Mahitaji Maalumu ya Elimu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam, Mei 29, 2016.

Region / Country